< Josué 19 >

1 Le deuxième sort sortit pour les enfants de Siméon, selon leur parenté, et l’héritage fut
Upigaji wa pili wa kura uliangukia kwa Simoni na waligawiwa kwa kila ukoo wao. Urithi wao ulikuwa katikati ya urithi ulikuwa ni mali ya kabila la Yuda.
2 Pour eux au milieu de la possession des fils de Juda: Bersabée, Sabée, Molada;
Urithi waliokuwa nao ni Beerisheba, Sheba, Molada,
3 Hasersual, Bala, Asem,
Hazari Shuali, Bala, Ezemu,
4 Eltholad, Bétul, Harma,
Elitoladi, Bethuli na Horma.
5 Sicéleg, Bethmarchaboth, Hasersusa,
Simoni alikuwa pia na Ziklagi, Bethi Markabothi, Hazari Susa,
6 Béthlébaoth et Sarohen: treize villes et leurs villages;
Bethi Lebaothi, na Sharuheni. Kulikuwa na miji kumi na mitatu pamoja na vijiji vyake. Vile vile
7 Aïn, Remmon, Athar et Azan: quatre villes et leurs villages;
Simoni alimiliki Aini, Rimon, Etheri, na Ashani. Hii ilikuwa ni miji minne pamoja na vijiji vyake.
8 Toutes les bourgades autour de ces villes jusqu’à Baalath, Béer, Ramath contre la partie australe. Tel est l’héritage des enfants de Siméon, selon leur parenté,
Miji hii pamoja na vijiji vilivyoizunguka hata kufika Baalathi Beeri (ambao ndio Rama katika Negevu). Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Simoni, waliopewa kwa koo zao.
9 Dans la possession et le partage des enfants de Juda, parce qu’il était trop grand pour eux: et c’est pour cela que les enfants de Siméon eurent leur possession au milieu de leur héritage.
Urithi wa kabila la Simoni ulikuwa sehemu ya himaya ya kabila la Yuda. Hii ni kwasababu nchi waliyopewa kabila la Yuda ilikuwa ni kubwa kwao, na hivyo kabila la Simoni lilipokea urithi wao kutoka katika sehemu yao ya katikati.
10 Le troisième sort échut aux enfants de Zabulon, selon leur parenté; et la frontière de leur possession s’étendait jusqu’à Sarid;
Upigaji wa kura ya tatu uliangukia kwa kabila la Zabuloni, na walipewa kwa koo zao. Mpaka wa urithi wao ulianzia huko Saridi.
11 Elle monte de la mer et de Mérala, et elle parvient à Debbaseth, jusqu’au torrent qui est contre Jéconam;
Mpaka wao ulipanda upande wa magharibi kuelekea Marala na ukaigusa Dabeshethi, na kisha ukasonga kuelekea kijito kilichokuwa mkabala na Yokineamu.
12 Elle retourne de Sared contre l’orient, aux confins de Césélethabor, s’avance près Dabéreth et monte contre Japhié;
Kutoka Saridi mpaka ulizunguka upande wa mashariki kuelekea mashariki na ulienda hadi mpaka wa Kislothi Tabori. Kutoka hapo uliendelea hadi Daberathi na kisha ulipanda hata Yafia.
13 De là, elle passe jusqu’à la partie orientale de Géthhépher et Thacasin, et s’avance vers Remmon, Amthar et Noa.
Kutoka hapo ulipita katika upande wa mashariki mwa Gathi Heferi, na kisha ukafika Ethikazini, baadaye ulienda hadi Rimoni na kisha ukageuka kuelekea Nea.
14 De plus, elle fait, à l’aquilon, le tour d’Hanaton, et elle est terminée par la vallée de Jephtahel,
Mpaka ulizunguka kueleka kaskazini ukafika Hanathoni na ulikomea katika bonde la Ifta Eli.
15 Par Cathed, Naalol, Séméron, Jédala et Bethléem; douze villes et leurs villages.
Mkoa huu ulijumuisha miji ya Katathi, Nahalali, Shimroni, Idala, na Bethlehemu. Kulikuwa na miji kumi na miwili, pamoja na vijiji vyake.
16 C’est là l’héritage de la tribu des enfants de Zabulon, selon leur parenté; ce sont leurs villes et leurs bourgades.
Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Zabuloni, waliopewa kwa kufuatana na koo zao - miji pamoja na vijiji vyake.
17 C’est pour Issachar, selon sa parenté, que sortit le quatrième sort;
Upigaji kura wa nne uliangukia kwa Isakari, na waligawiwa kufuatana na koo zao.
18 Et son héritage fut Jezraël, Casaloth, Sunem,
Eneo lao lilijumuisha Jezreelli, Kesuloothi, Shunemu,
19 Hapharaïm, Séhon, Anaharat,
Hafaraimu, Shioni, na Anaharathi.
20 Rabboth, Césion, Abès.
Pia ilijumuisha miji ya Rabithi, Kishioni, Ebezi,
21 Rameth, Engannim, Enhadda, et Bethphésès;
Remethi, Enganimu, Enihada, na Bethipazezi.
22 Et sa frontière parvient jusqu’à Thabor, Séhésima et Bethsamès; et se termine au Jourdain: seize villes et leurs villages.
Mpaka wao ulifika Tabor, Shahazuma, na Bethi Shemeshi, na ukakomea katika Yordani. Ilikuwa ni miji kumi na sita, pamoja na vijiji vyake.
23 Telle est la possession des enfants d’Issachar, selon leur parenté; telles sont les villes et leurs bourgades.
Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Isakari, na walipewa kufuatana na koo zao - miji pamoja na vijiji vyake.
24 Le cinquième sort échut aux enfants d’Aser, selon leur parenté;
Upigaji wa kura ya tano uliangukia kwa kabila la Asheri, na walipewa kwa koo zao.
25 Et leur frontière fut Halcath, Chali, Béthen, Axaph,
Eneo lao lilijumuisha miji ya Helikathi, Hali, Beteni, Akashafu,
26 Elmélech, Amaad et Messal; et elle parvient jusqu’au Carmel de la mer, jusqu’à Sihor et Labanath;
Alameleki, Amadi, na Mshali. Mpaka wa magharibi ulitanuka hadi Karmeli na Shihori Libnathi.
27 Et elle retourne contre l’orient à Bethdagon; elle passe jusqu’à Zabulon et à la vallée de Jephthael, contre l’aquilon, jusqu’à Bethémec et Néhiel. Elle s’avance, vers la gauche, vers Cabul,
Kisha ulizunguka upande wa mashariki kueleka Bethi Dagoni na ukaenda hadi Zabuloni, na kisha ukafika katika bonde la ifutaheli, upande wa kaskazini mwa Bethemeki na Neieli. Baadaye uliendelea mbele hata Kabuli kueleka upande wa Kaskazini.
28 Abran, Rohob, Hamon et Cana, jusqu’à Sidon la grande;
Na kisha ulienda hadi Ebroni, Rehobu, Hammoni, na Kana, hata kufika mji mkubwa wa Sidoni.
29 Puis elle retourne vers Horma, jusqu’à la ville très fortifiée de Tyr, et jusqu’à Hosa; et elle est terminée, à la mer, au territoire d’Achziba,
Mpaka ulirudi nyuma kuelekea Rama, na kisha ukafika kwenye mji wa Tiro uliokuwa na ngome. Baada ya hapo mpaka ulizunguka kuelekea Hosa na ulikomea katika bahari, katika mkoa wa Akizibu,
30 Amma, Aphec et Rohob: vingt-deux cités et leurs villages.
Umma, Afeki, na Rehobu. Kulikuwa na miji ishirini na miwili, pamoja na vijiji vyake.
31 Telle est la possession des enfants d’Aser, selon leur parenté; telles sont les villes et leurs bourgades.
Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Asheri, na waliopewa kwa koo zao - miji pamoja na vijiji vyake.
32 Aux enfants de Nephthali échut le sixième sort, selon leurs familles;
Upigaji wa kura wa mara ya sita uliangukia kwa kabila la Nafutali, na walipewa kufuatana na koo zao.
33 Et leur frontière commence à Héleph et Elon, va à Saananim et à Adami, qui est la même que Néceb, et à Jebnaël jusqu’à Lécum, et s’avance jusqu’au Jourdain;
Mpaka wao ulianzia Helefu, kutoka katika mwaloni huko Zaananimu, ulipanda hadi Adaminekebu na Yabneeli, umbali kama Lakumu; na ulikomea katka Yordani.
34 Et la frontière retourne, contre l’occident, à Azanoth-Thabor, et de là s’avance vers Hucuca, et passe à Zabulon, contre le midi, à Aser, contre l’occident, et à Juda, vers le Jourdain, contre le levant.
Mpaka ule ulizunguka upande wa magharibi kuelekea Aznothi Tabori na ulipanda hadi Hukoki; uligusa Zabuloni katika upande wa kusini, na ulifika hata Asheri katika upande wa magharibi, na Yuda katika upande wa mashariki huko katika mto Yordani.
35 Les villes très fortifiées sont Assédim, Ser, Emath, Reccath, Cénéreth,
Miji yenye ngome ilikuwa ni Zidimu, Zeri, Hammathi, Rakathi, Kinnerethi,
36 Edéma, Arama, Asor,
Adama, Rama, Hazori,
37 Cédés, Edraï, Enhasor,
Kedeshi, Edrei, na Eni Hazori.
38 Jéron, Magdalel, Horem, Bethanath et Bethsamès: dix-neuf villes et leurs villages.
Pia kulikuwa na miji ya Yironi, Migdaleli, Horemu, Bethi Anathi, na Bethi Shemeshi. Kulikuwa na miji kumi na tisa, pamoja na vijiji vyake.
39 Telle est la possession de la tribu des enfants de Nephthali, selon leur parenté; telles sont les villes et leurs bourgades.
Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Nafutali, na walipewa miji pamoja na vijiji vyake kufuatana na koo zao.
40 C’est pour la tribu des enfants de Dan, selon leurs familles, que sortit le septième sort;
Upigaji wa kura ya saba uliangukia kwa kabila la Dani, na walipewa kufuatana na koo zao.
41 Et la frontière de sa possession fut Saraa, Esthaol et Hirsémès, c’est-à-dire, ville du soleil,
Eneo lao la urithi lilijumuisha miji ya Zora, Eshitaoli, Iri Shemeshi,
42 Sélébin, Aïalon, Jéthéla,
Shaalabini, Aijaloni, na Ithila.
43 Elon, Themna et Acron,
Vile vile lilijumuisha miji ya Eloni, Timna, Ekroni,
44 Elthécé, Gébbéhon et Balaath,
Eliteke, Gibethoni, Baalathi,
45 Jud, Bané, Barach, Gethremmon,
Yehudi, Bene - Beraki, Gathi Rimoni,
46 Méjarchon, et Arecon, avec la frontière qui regarde Joppé,
Me -Yarkoni, na Rakoni sambamba na eneo la karibu na Yopa.
47 Et elle est terminée par cette limite. Mais les enfants de Dan montèrent et combattirent contre Lésem, la prirent, la frappèrent du tranchant du glaive, en prirent possession et habitèrent en elle, lui donnant le nom de Lésem-Dan, du nom de Dan leur père.
Ilitokea wakati mpaka wa kabila la Dani ulipowapotea, kabila la Dani waliishambulia Leshemu, wakapigana nao, na wakauteka. Waliua kila mtu kwa upanga, wakauchukua ukawa mali yao, na wakakaa ndani yake. Wakauita mji ule Dani jina la babu yao badala ya Leshemu.
48 Telle est la possession de la tribu des enfants de Dan, selon leur parenté; telles sont les villes et leurs bourgades.
Huu ulikuwa urithi wa kabila la Dani, waliopewa kufuatana na koo zao - miji pamoja na vijiji vyake.
49 Or, lorsqu’il eut achevé de partager par le sort la terre à chacun, selon sa tribu, les enfants d’Israël donnèrent en possession à Josué, fils de Nun, au milieu d’eux,
Walipomaliza kugawana urithi wa nchi, watu wa Israeli walimpa urithi Yoshua mwana wa Nuni kutoka miongoni mwao.
50 Selon le commandement du Seigneur, la ville qu’il avait demandée, Thamnath-Saraa, sur la montagne d’Ephraïm, et il bâtit la ville et il y habita.
Kwa amri ya Yahweh walimpatia mji wa Timnathi Sera ambao aliuomba, ulikuwa katika nchi ya milima ya Efraimu. Aliujenga mji na akaishi huko.
51 Telles sont les possessions que partagèrent au sort Eléazar, le prêtre, Josué, fils de Nun, et les princes des familles et des tribus des enfants d’Israël, à Silo, devant le Seigneur, à la porte du tabernacle de témoignage. C’est ainsi qu’ils partagèrent la terre.
Na huu ndio urithi ambao Eliazari kuhani, na Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi wa makabila ya familia za mababu zao miongoni mwa watu wa Israeli, waligawa kwa kupiga kura huko Shilo, mbele za Yahweh katika mlango wa hema la kukutania. Na hivyo wakamaliza kuigawa nchi.

< Josué 19 >