< Josué 19 >
1 Le deuxième sort sortit pour les enfants de Siméon, selon leur parenté, et l’héritage fut
Kura ya pili ikaangukia kabila la Simeoni, ukoo kwa ukoo. Urithi wao ulikuwa ndani ya eneo la Yuda.
2 Pour eux au milieu de la possession des fils de Juda: Bersabée, Sabée, Molada;
Ulijumuisha: Beer-Sheba (au Sheba), Molada,
Hasar-Shuali, Bala, Esemu,
4 Eltholad, Bétul, Harma,
Eltoladi, Bethuli, Horma,
5 Sicéleg, Bethmarchaboth, Hasersusa,
Siklagi, Beth-Markabothi, Hasar-Susa,
6 Béthlébaoth et Sarohen: treize villes et leurs villages;
Beth-Lebaothi na Sharuheni; hii ilikuwa miji kumi na mitatu pamoja na vijiji vyake.
7 Aïn, Remmon, Athar et Azan: quatre villes et leurs villages;
Pia Aini, Rimoni, Etheri, na Ashani; hii ilikuwa miji minne na vijiji vyake,
8 Toutes les bourgades autour de ces villes jusqu’à Baalath, Béer, Ramath contre la partie australe. Tel est l’héritage des enfants de Siméon, selon leur parenté,
pamoja na vijiji vyote vinavyoizunguka miji hii mpaka Baalath-Beeri (ambayo ndiyo Rama iliyo katika Negebu). Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Simeoni ukoo kwa ukoo.
9 Dans la possession et le partage des enfants de Juda, parce qu’il était trop grand pour eux: et c’est pour cela que les enfants de Siméon eurent leur possession au milieu de leur héritage.
Urithi wa Wasimeoni ulitolewa kutoka fungu la Yuda, kwa kuwa fungu la Yuda lilikuwa kubwa kuliko walivyohitaji. Hivyo kabila la Simeoni lilipewa urithi wao ndani ya eneo la Yuda.
10 Le troisième sort échut aux enfants de Zabulon, selon leur parenté; et la frontière de leur possession s’étendait jusqu’à Sarid;
Kura ya tatu ikaangukia kabila la Zabuloni, ukoo kwa ukoo: Mpaka wa urithi wao uliendelea hadi Saridi.
11 Elle monte de la mer et de Mérala, et elle parvient à Debbaseth, jusqu’au torrent qui est contre Jéconam;
Kuelekea upande wa magharibi ukafika Marala, ukagusa Dabeshethi, na kuendelea mpaka kwenye bonde karibu na Yokneamu.
12 Elle retourne de Sared contre l’orient, aux confins de Césélethabor, s’avance près Dabéreth et monte contre Japhié;
Ukageuka mashariki, kuanzia Saridi kuelekea mawio ya jua hadi kwenye nchi ya Kisiloth-Tabori, na kwenda hadi Daberathi, kupanda Yafia.
13 De là, elle passe jusqu’à la partie orientale de Géthhépher et Thacasin, et s’avance vers Remmon, Amthar et Noa.
Kisha ukaendelea mashariki hadi Gath-Heferi na kufika Eth-Kasini, ukatokea Rimoni na kugeuka kuelekea Nea.
14 De plus, elle fait, à l’aquilon, le tour d’Hanaton, et elle est terminée par la vallée de Jephtahel,
Huko mpaka ukazungukia upande wa kaskazini hadi Hanathoni na kuishia katika Bonde la Ifta-Eli.
15 Par Cathed, Naalol, Séméron, Jédala et Bethléem; douze villes et leurs villages.
Miji mingine iliyojumuishwa ni Katathi, Nahalali, Shimroni, Idala na Bethlehemu. Kulikuwa na miji kumi na miwili pamoja na vijiji vyake.
16 C’est là l’héritage de la tribu des enfants de Zabulon, selon leur parenté; ce sont leurs villes et leurs bourgades.
Miji hii na vijiji vyake ilikuwa ndio urithi wa Zabuloni, ukoo kwa ukoo.
17 C’est pour Issachar, selon sa parenté, que sortit le quatrième sort;
Kura ya nne ikamwangukia Isakari, ukoo kwa ukoo.
18 Et son héritage fut Jezraël, Casaloth, Sunem,
Eneo lao lilijumuisha: Yezreeli, Kesulothi, Shunemu,
19 Hapharaïm, Séhon, Anaharat,
Hafaraimu, Shioni, Anaharathi,
20 Rabboth, Césion, Abès.
Rabithi, Kishioni, Ebesi,
21 Rameth, Engannim, Enhadda, et Bethphésès;
Remethi, En-Ganimu, En-Hada na Beth-Pasesi.
22 Et sa frontière parvient jusqu’à Thabor, Séhésima et Bethsamès; et se termine au Jourdain: seize villes et leurs villages.
Mpaka ule ukagusa Tabori, Shahasuma na Beth-Shemeshi, na ukaishia kwenye Yordani. Ilikuwa miji kumi na sita, pamoja na vijiji vyake.
23 Telle est la possession des enfants d’Issachar, selon leur parenté; telles sont les villes et leurs bourgades.
Miji hii pamoja na vijiji vyake ilikuwa urithi wa kabila la Isakari, ukoo kwa ukoo.
24 Le cinquième sort échut aux enfants d’Aser, selon leur parenté;
Kura ya tano ikaangukia kabila la Asheri, ukoo kwa ukoo.
25 Et leur frontière fut Halcath, Chali, Béthen, Axaph,
Eneo lao lilijumuisha: Helkathi, Hali, Beteni, Akishafu,
26 Elmélech, Amaad et Messal; et elle parvient jusqu’au Carmel de la mer, jusqu’à Sihor et Labanath;
Alameleki, Amadi na Mishali. Upande wa magharibi mpaka uligusa Karmeli na Shihor-Libnathi.
27 Et elle retourne contre l’orient à Bethdagon; elle passe jusqu’à Zabulon et à la vallée de Jephthael, contre l’aquilon, jusqu’à Bethémec et Néhiel. Elle s’avance, vers la gauche, vers Cabul,
Tena ukageuka mashariki kuelekea Beth-Dagoni, ukagusa Zabuloni na Bonde la Ifta-Eli, ukaenda upande wa kaskazini hadi Beth-Emeki na Neyeli, ukipitia Kabul upande wa kushoto.
28 Abran, Rohob, Hamon et Cana, jusqu’à Sidon la grande;
Ukaendelea hadi Abdoni, Rehobu, Hamoni na Kana, na kufika Sidoni Kuu.
29 Puis elle retourne vers Horma, jusqu’à la ville très fortifiée de Tyr, et jusqu’à Hosa; et elle est terminée, à la mer, au territoire d’Achziba,
Mpaka huo ukageukia nyuma kuelekea Rama na kwenda hadi kwenye mji wenye ngome wa Tiro, ukageuka kuelekea Hosa na kutokeza baharini katika eneo la Akzibu,
30 Amma, Aphec et Rohob: vingt-deux cités et leurs villages.
Uma, Afeki na Rehobu. Ilikuwepo miji ishirini na miwili, pamoja na vijiji vyake.
31 Telle est la possession des enfants d’Aser, selon leur parenté; telles sont les villes et leurs bourgades.
Miji hii pamoja na vijiji vyake ilikuwa ndio urithi wa kabila la Asheri, ukoo kwa ukoo.
32 Aux enfants de Nephthali échut le sixième sort, selon leurs familles;
Kura ya sita ikaangukia kabila la Naftali, ukoo kwa ukoo:
33 Et leur frontière commence à Héleph et Elon, va à Saananim et à Adami, qui est la même que Néceb, et à Jebnaël jusqu’à Lécum, et s’avance jusqu’au Jourdain;
Mpaka wao uliendelea kutoka Helefi na kwenye mti mkubwa ulio katika Saananimu, ukipitia Adami-Nekebu na Yabineeli hadi Lakumu, na kuishia katika Mto Yordani.
34 Et la frontière retourne, contre l’occident, à Azanoth-Thabor, et de là s’avance vers Hucuca, et passe à Zabulon, contre le midi, à Aser, contre l’occident, et à Juda, vers le Jourdain, contre le levant.
Mpaka ukaendelea magharibi kupitia Aznoth-Tabori na kutokea Hukoki. Ukagusa Zabuloni upande wa kusini, Asheri upande wa magharibi, na Yordani upande wa mashariki.
35 Les villes très fortifiées sont Assédim, Ser, Emath, Reccath, Cénéreth,
Miji yenye ngome ilikuwa Sidimu, Seri, Hamathi, Rakathi, Kinerethi,
37 Cédés, Edraï, Enhasor,
Kedeshi, Edrei, na En-Hasori,
38 Jéron, Magdalel, Horem, Bethanath et Bethsamès: dix-neuf villes et leurs villages.
Ironi, Migdal-Eli, Horemu, Beth-Anathi na Beth-Shemeshi. Kulikuwa na miji kumi na tisa na vijiji vyake.
39 Telle est la possession de la tribu des enfants de Nephthali, selon leur parenté; telles sont les villes et leurs bourgades.
Miji hiyo pamoja na vijiji vyake ndio iliyokuwa urithi wa kabila la Naftali, ukoo kwa ukoo.
40 C’est pour la tribu des enfants de Dan, selon leurs familles, que sortit le septième sort;
Kura ya saba ikaangukia kabila la Dani, ukoo kwa ukoo.
41 Et la frontière de sa possession fut Saraa, Esthaol et Hirsémès, c’est-à-dire, ville du soleil,
Eneo la urithi wao lilijumuisha: Sora, Eshtaoli, Iri-Shemeshi,
42 Sélébin, Aïalon, Jéthéla,
Shaalabini, Aiyaloni, Ithla,
43 Elon, Themna et Acron,
Eloni, Timna, Ekroni,
44 Elthécé, Gébbéhon et Balaath,
Elteke, Gibethoni, Baalathi,
45 Jud, Bané, Barach, Gethremmon,
Yehudi, Bene-Beraki, Gath-Rimoni,
46 Méjarchon, et Arecon, avec la frontière qui regarde Joppé,
Me-Yarkoni na Rakoni, pamoja na eneo linalotazamana na Yafa.
47 Et elle est terminée par cette limite. Mais les enfants de Dan montèrent et combattirent contre Lésem, la prirent, la frappèrent du tranchant du glaive, en prirent possession et habitèrent en elle, lui donnant le nom de Lésem-Dan, du nom de Dan leur père.
(Lakini Wadani walipata shida kulimiliki eneo lao; kwa hiyo walipanda kuishambulia Leshemu, wakaitwaa, wakawaua watu wake kwa upanga na kuukalia. Walikaa Leshemu na kuuita Dani kufuatana na jina la baba yao.)
48 Telle est la possession de la tribu des enfants de Dan, selon leur parenté; telles sont les villes et leurs bourgades.
Miji hii na vijiji vyake ndio iliyokuwa urithi wa kabila la Dani, ukoo kwa ukoo.
49 Or, lorsqu’il eut achevé de partager par le sort la terre à chacun, selon sa tribu, les enfants d’Israël donnèrent en possession à Josué, fils de Nun, au milieu d’eux,
Walipomaliza kugawanya nchi katika migawo kulingana na sehemu zao zilizowaangukia, Waisraeli wakampa Yoshua mwana wa Nuni urithi katikati yao,
50 Selon le commandement du Seigneur, la ville qu’il avait demandée, Thamnath-Saraa, sur la montagne d’Ephraïm, et il bâtit la ville et il y habita.
kama vile Bwana alivyokuwa ameamuru. Walimpa mji alioutaka, ambao ni Timnath-Sera ulio katika nchi ya vilima ya Efraimu. Naye akajenga mji, akakaa huko.
51 Telles sont les possessions que partagèrent au sort Eléazar, le prêtre, Josué, fils de Nun, et les princes des familles et des tribus des enfants d’Israël, à Silo, devant le Seigneur, à la porte du tabernacle de témoignage. C’est ainsi qu’ils partagèrent la terre.
Haya ndiyo maeneo ambayo kuhani Eleazari, Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi wa koo za kabila za Israeli waliyoyagawanya kwa kura huko Shilo mbele za Bwana penye ingilio la Hema la Kukutania. Hivyo wakamaliza kuigawanya nchi.