< Josué 12 >
1 Voici les rois que battirent les enfants d’Israël, et dont ils possédèrent la terre au-delà du Jourdain, vers le levant, depuis le torrent d’Arnon jusqu’à la montagne d’Hermon, et toute la contrée orientale qui regarde le désert.
Hawa ndio wafalme wa nchi ambao Waisraeli waliwashinda na kuitwaa nchi yao upande wa mashariki mwa Yordani, kuanzia Bonde la Arnoni mpaka Mlima Hermoni, pamoja na eneo lote la upande wa mashariki ya Araba:
2 Séhon, roi des Amorrhéens qui habita à Hésébon, et qui régna depuis Aroer, qui est située sur le bord du torrent d’Arnon, au milieu de la vallée, et dans la moitié de Galaad jusqu’au torrent de Jaboc, qui est la frontière des enfants d’Ammon;
Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala huko Heshboni. Alitawala kuanzia Aroeri kwenye ukingo wa Bonde la Arnoni, kuanzia katikati ya bonde, hadi kwenye Mto Yaboki, ambao ni mpaka wa Waamoni. Hii ilijumlisha nusu ya Gileadi.
3 Et depuis le désert jusqu’à la mer du Cénéroth contre l’οrient, et jusqu’à la mer du désert, qui est la mer très salée, vers le côté oriental, par la voie qui mène à Bethsimoth; et depuis la partie australe qui est au-dessous d’Asédoth, jusqu’à Phasga.
Pia alitawala Araba ya mashariki kuanzia Bahari ya Kinerethi hadi Bahari ya Araba (yaani Bahari ya Chumvi), hadi Beth-Yeshimothi, kisha kuelekea kusini chini ya materemko ya Pisga.
4 Les limites d’Og, roi de Basan, qui était des restes des Raphaïm, et qui habita à Astaroth et à Edraï, et qui régna à la montagne d’Hermon, à Salécha et dans tout le Basan, s’étendaient jusqu’aux frontières
Nayo nchi ya Ogu mfalme wa Bashani, aliyekuwa mmoja wa mabaki ya Warefai, aliyetawala Ashtarothi na Edrei.
5 De Gessuri, de Machati et de la moitié de Galaad: frontières de Séhon, roi d’Hésébon.
Naye alitawala katika Mlima Hermoni, Saleka, Bashani yote hadi mpaka wa watu wa Geshuri, na watu wa Maaka na nusu ya Gileadi, hadi kwenye mpaka wa Sihoni mfalme wa Heshboni.
6 Moïse, serviteur du Seigneur, et les enfants d’Israël battirent ces rois, et Moïse livra leur terre en possession aux Rubénites, aux Gadites et à la demi-tribu de Manassé.
Mose, mtumishi wa Bwana, na Waisraeli wakawashinda. Naye Mose mtumishi wa Bwana akawapa Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase nchi ya hao wafalme ili iwe milki yao.
7 Voici les rois du pays que battirent Josué et les enfants d’Israël au-delà du Jourdain, du côté occidental, depuis Baalgad dans la campagne du Liban jusqu’à la montagne dont une partie s’élève vers Séir: et Josué le donna en possession aux tribus d’Israël, à chacune sa part,
Hawa ndio wafalme wa nchi ambao Yoshua na Waisraeli waliwashinda upande wa magharibi mwa Yordani, kuanzia Baal-Gadi katika Bonde la Lebanoni hadi kufikia Mlima Halaki, unaoinuka ukielekea Seiri. (Yoshua alitoa nchi zao kwa makabila ya Israeli iwe urithi wao sawasawa na mgawanyiko wa makabila yao:
8 Tant au milieu des montagnes, que dans la plaine et la campagne. Dans Asédoth, dans le désert et au midi, étaient l’Héthéen et l’Amorrhéen, le Chananéen et le Phérézéen, l’Hévéen et le Jébuséen:
nchi ya vilima, shefela, upande wa magharibi, Araba, materemko ya milima, jangwa, na Negebu; nchi za Wahiti, Waamori, Wakanaani, Waperizi, Wahivi na Wayebusi):
9 Un roi de Jéricho, un roi de Haï, laquelle est à côté de Béthel,
mfalme wa Yeriko mmoja mfalme wa Ai (karibu na Betheli) mmoja
10 Un roi de Jérusalem, un roi d’Hébron,
mfalme wa Yerusalemu mmoja mfalme wa Hebroni mmoja
11 Un roi de Jérimoth, un roi de Lachis,
mfalme wa Yarmuthi mmoja mfalme wa Lakishi mmoja
12 Un roi d’Eglon, un roi de Gazer,
mfalme wa Egloni mmoja mfalme wa Gezeri mmoja
13 Un roi de Dabir, un roi de Gader,
mfalme wa Debiri mmoja mfalme wa Gederi mmoja
14 Un roi d’Herma, un roi d’Héred,
mfalme wa Horma mmoja mfalme wa Aradi mmoja
15 Un roi de Lebna, un roi d’Odullam,
mfalme wa Libna mmoja mfalme wa Adulamu mmoja
16 Un roi de Macéda, un roi de Béthel,
mfalme wa Makeda mmoja mfalme wa Betheli mmoja
17 Un roi de Taphua, un roi d’Opher,
mfalme wa Tapua mmoja mfalme wa Heferi mmoja
18 Un roi d’Aphec, un roi de Saron,
mfalme wa Afeki mmoja mfalme wa Lasharoni mmoja
19 Un roi de Madon, un roi d’Asor,
mfalme wa Madoni mmoja mfalme wa Hazori mmoja
20 Un roi de Séméron, un roi d’Achsaph,
mfalme wa Shimron-Meroni mmoja mfalme wa Akishafu mmoja
21 Un roi de Thénac, un roi de Mageddo,
mfalme wa Taanaki mmoja mfalme wa Megido mmoja
22 Un roi de Cadès, un roi de Jachanan du Carmel,
mfalme wa Kedeshi mmoja mfalme wa Yokneamu katika Karmeli mmoja
23 Un roi de Dor, et de la province de Dor, un roi des nations de Galgal,
mfalme wa Dori (katika Nafoth-Dori) mmoja mfalme wa Goimu katika Gilgali mmoja
24 Un roi de Thersa: en tout, trente-un rois.
mfalme wa Tirsa mmoja wafalme jumla yao ilikuwa thelathini na mmoja.