< Josué 10 >
1 Lorsque Adonisédec, roi de Jérusalem, eut appris ces choses, savoir, que Josué avait pris Haï et qu’il l’avait détruite (car comme il avait fait à Jéricho et à son roi, ainsi fit-il à Haï et à son roi), et que les Gabaonites avaient passés aux Israélites, et qu’ils étaient leurs alliés,
Baada ya haya Adoni-Sedeki mfalme wa Yerusalemu alisikia kuwa Yoshua alikuwa ameteka mji wa Ai na kuuangamiza kabisa, tena alikuwa ameua mfalme wake, kama alivyofanya huko Yeriko na mfalme wake, tena ya kuwa watu wa Gibeoni walikuwa wamefanya mapatano ya amani na Waisraeli, na walikuwa wakiishi karibu yao.
2 Il en eut une grande crainte; car Gabaon était une grande ville et une des cités royales, et plus grande que la ville de Haï et tous ses guerriers étaient très vaillants.
Yeye na watu wake wakataharuki mno kwa kuwa Gibeoni ulikuwa mji mkubwa kama mmojawapo ya miji ya kifalme; ulikuwa mkubwa kuliko Ai, nao watu wake wote walikuwa mashujaa wa vita.
3 Adonisédec, roi de Jérusalem, envoya donc vers Oham, roi d’Hébron, vers Pharam, roi de Jérimoth, vers Japhia aussi, roi de Lachis, et vers Dabir, roi d’Eglon, disant:
Hivyo Adoni-Sedeki mfalme wa Yerusalemu akaomba msaada kwa Hohamu mfalme wa Hebroni, Piramu mfalme wa Yarmuthi, Yafia mfalme wa Lakishi, na Debiri mfalme wa Egloni.
4 Montez vers moi, et me portez secours, afin que nous réduisions Gabaon, parce qu’elle a passé à Josué et aux enfants d’Israël.
Akawaambia, “Njooni mnisaidie kuipiga Gibeoni, kwa sababu imefanya mapatano ya amani na Yoshua na Waisraeli.”
5 S’étant donc assemblés, les cinq rois des Amorrhéens, le roi de Jérusalem, le roi d’Hébron, le roi de Jérimoth, le roi de Lachis, le roi d’Eglon, montèrent ensemble avec leurs armées, ils campèrent près de Gabaon et l’assiégèrent.
Ndipo hao wafalme watano wa Waamori, ambao ni wafalme wa Yerusalemu, Hebroni, Yarmuthi, Lakishi na Egloni, wakaunganisha majeshi yao. Wakapanda na vikosi vyao vyote, nao wakajipanga dhidi ya Gibeoni na kuishambulia.
6 Mais les habitants de Gabaon, la ville assiégée, envoyèrent à Josué, qui alors était au camp près de Galgala, et lui dirent: Ne retire pas tes mains auxiliaires de tes serviteurs: monte aussitôt, délivre-nous, et porte-nous secours; car tous les rois des Amorrhéens qui habitent dans les montagnes se sont réunis contre nous.
Nao Wagibeoni wakatuma ujumbe kwa Yoshua kwenye kambi ya Gilgali na kumwambia, “Usiwatelekeze watumishi wako. Panda haraka uje kwetu kutuokoa! Tusaidie, kwa sababu wafalme wote wa Waamori wakaao kwenye nchi ya vilima wameunganisha majeshi yao pamoja dhidi yetu.”
7 Et Josué monta de Galgala, et avec lui toute l’armée des combattants, hommes très vaillants.
Basi Yoshua akaondoka Gilgali pamoja na jeshi lake lote, wakiwepo watu wote mashujaa wa vita.
8 Et le Seigneur dit à Josué: Ne les crains point; car je les ai livrés en tes mains: nul d’entre eux ne pourra te résister.
Bwana akamwambia Yoshua, “Usiwaogope watu hao, nimewatia mkononi mwako. Hakuna yeyote atakayeweza kushindana nawe.”
9 C’est pourquoi Josué montant de Galgala pendant toute la nuit, fondit soudainement sur eux;
Baada ya Yoshua kutembea usiku kucha kutoka Gilgali, akawashambulia ghafula.
10 Et le Seigneur les mit en déroute à la face d’Israël; il en fit un grand carnage à Gabaon, il les poursuivit par la voie de la montée de Béthoron, et les tailla en pièces jusqu’à Azéca et à Macéda.
Bwana akawafadhaisha mbele ya Waisraeli, nao wakawashinda kwa ushindi mkuu huko Gibeoni. Israeli wakawafukuza kuelekea njia iendayo Beth-Horoni wakiwaua mpaka kufikia njia iendayo Azeka na Makeda.
11 Et lorsqu’ils fuyaient les enfants d’Israël, et qu’ils étaient dans la descente de Béthoron, le Seigneur lança du ciel sur eux de grosses pierres jusqu’à Azéca: et il en mourut beaucoup plus par les pierres de grêle, que les enfants d’Israël n’en avaient tués par le glaive.
Walipokuwa wakikimbia mbele ya Israeli kwenye barabara iteremkayo kutoka Beth-Horoni hadi Azeka, Bwana akawavumishia mawe makubwa ya mvua kutoka mbinguni, na wengi wao wakauawa na hayo mawe kuliko wale waliouawa kwa upanga wa Waisraeli.
12 Alors Josué parla au Seigneur, dans le jour qu’il livra l’Amorrhéen en présence des enfants d’Israël, et il dit devant eux: Soleil, ne te meus point contre Gabaon, ni toi, lune, contre la vallée d’Aïalon.
Katika siku ile ambayo Bwana aliwapeana Waamori kwa Israeli, Yoshua akanena na Bwana akiwa mbele ya Waisraeli akasema: “Wewe jua, simama juu ya Gibeoni, wewe mwezi, tulia juu ya Bonde la Aiyaloni.”
13 Et le soleil et la lune s’arrêtèrent, jusqu’à ce qu’une nation se fut vengée de ses ennemis. Cela n’est-ii pas écrit dans le livre des Justes? C’est pourquoi le soleil s’arrêta au milieu du ciel, et ne se hâta point de se coucher durant l’espace d’un jour.
Hivyo jua likasimama, nao mwezi ukatulia, hadi taifa hilo lilipokwisha kujilipizia kisasi kwa adui wake, kama ilivyoandikwa katika Kitabu cha Yashari. Jua likasimama kimya katikati ya mbingu, likachelewa kuzama muda wa siku moja nzima.
14 Il n’y eut point avant ni après un aussi long jour, le Seigneur obéissant à la voix d’un homme et combattant pour israël.
Haijakuwepo siku nyingine kama hiyo kabla au baada, siku ambayo Bwana alimsikiliza mwanadamu. Hakika Bwana alikuwa akiwapigania Israeli.
15 Et Josué retourna avec tout Israël au camp de Galgala.
Ndipo Yoshua akarudi kambini huko Gilgali pamoja na Israeli yote.
16 Car les cinq rois s’étaient enfuis et s’étaient cachés dans la caverne de la ville de Macéda.
Basi wale wafalme watano wakawa wamekimbia kujificha kwenye pango huko Makeda.
17 Et l’on annonça à Josué que les cinq rois avaient été trouvés cachés dans la caverne de la ville de Macéda.
Yoshua alipoambiwa kuwa wafalme hao watano wamekutwa wakiwa wamejificha ndani ya pango huko Makeda,
18 Et Josué ordonna à ceux qui l’accompagnaient, et dit: Roulez de grandes pierres à l’ouverture de la caverne, et placez des hommes intelligents qui gardent ceux qui y sont enfermés.
akasema, “Vingirisheni mawe makubwa kwenye mdomo wa hilo pango, tena wekeni walinzi wa kulilinda.
19 Pour vous, ne vous arrêtez point, mais poursuivez les ennemis, et taillez en pièces tous les derniers des fuyards; et ne les laissez point entrer dans les forteresses de leurs villes, eux que le Seigneur votre Dieu a livrés en vos mains.
Lakini msiwaache! Wafuatieni adui zenu, washambulieni kutoka nyuma, wala msiwaache wafike kwenye miji yao, kwa kuwa Bwana Mungu wenu amewatia mkononi mwenu.”
20 Les ennemis donc ayant été taillés en pièces dans un grand carnage, et presque détruits jusqu’à une entière extermination, ceux qui purent échapper à Israël entrèrent dans les villes fortifiées.
Hivyo Yoshua pamoja na Waisraeli wakawaangamiza kabisa karibu wote, lakini wachache waliosalia walifika kwenye miji yao yenye maboma.
21 Et toute l’armée retourna vers Josué à Macéda, où alors était le camp, saine et sauve, et en nombre complet: et nul n’osa murmurer contre les enfants d’Israël.
Basi jeshi lote likarudi salama kwa Yoshua huko kambini Makeda, na hakuna yeyote aliyetoa neno kinyume cha Waisraeli.
22 Et Josué ordonna disant: Ouvrez l’entrée de la caverne, et amenez-moi les cinq rois qui y sont cachés.
Ndipo Yoshua akasema, “Haya fungueni mdomo wa pango, mniletee hao wafalme watano.”
23 Et les serviteurs firent comme il leur avait été commandé; et ils lui amenèrent de la caverne les cinq rois, le roi de Jérusalem, le roi d’Hébron, le roi de Jérimoth, le roi de Lachis, le roi d’Eglon.
Kwa hiyo wakawatoa hao wafalme watano nje ya pango: wafalme wa Yerusalemu, Hebroni, Yarmuthi, Lakishi na Egloni.
24 Et lorsqu’ils eurent été amenés, il appela tous les hommes d’Israël, et il dit aux princes de l’armée, qui étaient avec lui: Allez, et mettez les pieds sur les cous de ces rois. Lorsque ceux-ci furent allés, et pendant qu’ils foulaient leurs cous aux pieds, après les avoir terrassés,
Walipokuwa wamewaleta hawa wafalme kwa Yoshua, akawaita watu wote wa Israeli, na kuwaambia majemadari wa vita waliokwenda pamoja naye, “Njooni hapa mweke nyayo zenu juu ya shingo za hawa wafalme.” Basi wakaja wakaweka nyayo zao shingoni.
25 Il leur dit de nouveau: Ne craignez point, et ne vous épouvantez pas, prenez courage et soyez forts; car ainsi fera le Seigneur à tous vos ennemis contre lesquels vous combattrez.
Yoshua akawaambia, “Msiogope, wala msivunjike moyo. Kuweni hodari na wenye ushujaa. Hili ndilo Bwana atakalowatendea adui zenu wote mnaokwenda kupigana nao.”
26 Et Josué les frappa et les tua, et les suspendit à cinq poteaux; et ils furent suspendus jusqu’au soir.
Ndipo Yoshua akawapiga na kuwaua wale wafalme na kuwatundika juu ya miti mitano, nao wakaachwa wakiningʼinia juu ya ile miti hadi jioni.
27 Et lorsque le soleil se couchait il ordonna à ceux qui l’accompagnaient de les descendre des poteaux. Ceux-ci les ayant descendus, les jetèrent dans la caverne, dans laquelle ils s’étaient cachés, et mirent à l’entrée de grandes pierres, qui sont demeurées jusqu’à présent.
Wakati wa kuzama jua Yoshua akaamuru, nao wakawashusha kutoka kwenye ile miti na kuwatupa kwenye lile pango ambalo walikuwa wamejificha. Kwenye mdomo wa lile pango wakaweka mawe makubwa, ambayo yapo hadi leo.
28 En ce même jour aussi Josué prit Macéda et la frappa du tranchant du glaive; et il tua son roi et tous ses habitants, et il n’y laissa pas même les moindres restes. Ainsi, il fit au roi de Macéda comme il avait fait au roi de Jéricho.
Siku ile Yoshua akateka Makeda. Akamuua kila mmoja katika ule mji, pamoja na mfalme wake kwa upanga. Hakubakiza mtu yeyote. Akamfanyia mfalme wa Makeda kama vile alivyokuwa amemfanyia mfalme wa Yeriko.
29 Or, il passa avec tout Israël de Macéda à Lebna, et il combattait contre elle.
Ndipo Yoshua akaondoka Makeda akiwa pamoja na Israeli yote mpaka mji wa Libna na kuushambulia.
30 Et le Seigneur la livra avec son roi aux mains d’Israël; ils frappèrent du tranchant du glaive la ville et tous ses habitants; ils n’y laissèrent aucun reste. Ainsi, ils firent au roi de Lebna, comme ils avaient fait au roi de Jéricho.
Bwana pia akautia huo mji wa Libna pamoja na mfalme wake mikononi mwa Israeli. Yoshua akaangamiza ule mji na kila mtu aliyekuwa ndani yake kwa upanga. Hakubakiza huko mtu yeyote. Akamfanyia mfalme wa Libna kama alivyokuwa amemfanyia mfalme wa Yeriko.
31 De Lebna il passa à Lachis avec tout Israël; et, son armée étant rangée tout autour, il l’attaquait.
Kisha Yoshua akaondoka Libna kwenda Lakishi akiwa pamoja na Israeli yote; wakajipanga dhidi yake na kuushambulia.
32 Et le Seigneur livra Lachis aux mains d’Israël, et il la prit le second jour, et il frappa du tranchant du glaive, toute âme qui avait été en elle, comme il avait fait à Lebna.
Bwana akautia Lakishi mikononi mwa Israeli, Yoshua akauteka siku ya pili. Yoshua akauangamiza mji na kila kilichokuwa ndani yake kwa upanga, kama tu vile alivyokuwa ameufanyia mji wa Libna.
33 En ce temps-là monta Horam, roi de Gazer, pour secourir Lachis. Josué le battit avec son armée jusqu’à une dernière extermination.
Wakati huo huo, Horamu mfalme wa Gezeri alikuwa amepanda ili kusaidia Lakishi, lakini Yoshua akamshinda pamoja na jeshi lake, hadi hapakubakia mtu yeyote.
34 Et il passa de Lachis à Eglon et l’assiégea;
Ndipo Yoshua akaondoka Lakishi kwenda Egloni akiwa pamoja na Israeli yote; wakajipanga dhidi yake na kuushambulia.
35 Et il la prit d’assaut le même jour; et il frappa du tranchant du glaive toutes les âmes qui étaient en elle, selon tout ce qu’il avait fait à Lachis.
Wakauteka mji huo siku ile ile, wakaupiga kwa upanga na kumwangamiza kila mmoja aliyekuwa ndani yake, kama vile walivyokuwa wameufanyia Lakishi.
36 Il monta aussi avec tout Israël d’Eglon à Hébron, et combattit contre elle.
Kisha Yoshua akapanda kutoka Egloni kwenda Hebroni akiwa pamoja na Israeli yote na kuushambulia.
37 Il la prit et la frappa du tranchant du glaive, ainsi que son roi et toutes les autres villes de cette contrée, et toutes les âmes qui y étaient demeurées; il n’y laissa aucuns restes: comme il avait fait à Eglon, ainsi fit-il à Hébron, faisant passer par le glaive tout ce qu’il trouva.
Wakauteka mji na kuupiga kwa upanga, pamoja na mfalme wake, vijiji vyake na kila mmoja aliyekuwa ndani yake. Hawakubakiza mtu yeyote. Kama vile huko Egloni, waliuangamiza kabisa pamoja na kila mmoja aliyekuwa ndani yake.
Ndipo Yoshua na Israeli wote wakageuka na kuushambulia Debiri.
39 Il la prit et la ravagea; il frappa aussi du tranchant du glaive son roi et toutes les villes d’alentour: il n’y laissa aucuns restes: comme il avait fait à Hébron et à Lebna et à leurs rois, ainsi fit-il à Dabir et à son roi.
Wakauteka mji, mfalme wake na vijiji vyake, na kuupiga kwa upanga. Kila mmoja aliyekuwa ndani yake wakamwangamiza kabisa. Hawakubakiza mtu yeyote. Wakaufanyia Debiri na mfalme wake kama vile walivyokuwa wameifanyia miji ya Libna na Hebroni na wafalme wao.
40 C’est pourquoi Josué frappa toute la terre des montagnes, du midi et de la plaine, et Asédoth avec ses rois: il n’y laissa aucuns restes; mais tout ce qui pouvait respirer, il le tua, comme lui avait ordonné le Seigneur Dieu d’Israël,
Hivyo Yoshua akalishinda eneo hilo lote, ikiwa ni pamoja na nchi ya vilima, na Negebu, na sehemu ya magharibi chini ya vilima, materemko ya milima, pamoja na wafalme wake wote. Hakubakiza mtu yeyote. Akaangamiza kabisa kila kitu chenye pumzi, kama vile Bwana, Mungu wa Israeli, alivyokuwa ameamuru.
41 Depuis Cadesbarné jusqu’à Gaza. Toute la terre de Gosen jusqu’à Gabaon,
Yoshua akawashinda kuanzia Kadesh-Barnea hadi Gaza na kutoka eneo lote la Gosheni hadi Gibeoni.
42 Et tous leurs rois et leurs contrées, il les prit et les ravagea d’une seule attaque; car le Seigneur Dieu d’Israël combattit pour lui.
Wafalme hawa wote pamoja na nchi zao Yoshua aliwashinda kwa wakati mmoja, kwa sababu Bwana, Mungu wa Israeli, aliwapigania Israeli.
43 Et il retourna avec tout Israël au lieu du camp, à Galgala.
Ndipo Yoshua akarudi pamoja na Israeli yote kwenye kambi huko Gilgali.