< Jean 9 >

1 Et comme il passait, Jésus vit un homme aveugle de naissance;
Wakati, kama Yesu alipokuwa akipita, alimwona mtu kipofu tangu kuzaliwa kwake.
2 Et ses disciples l’interrogèrent: Maître, qui a péché, celui-ci ou ses parents, pour qu’il soit né aveugle?
Wanafunzi wake wakamwuliza, “Rabi, nani aliyetenda dhambi, mtu huyu au wazazi wake, hata azaliwe kipofu?”
3 Jésus répondit: Ni celui-ci n’a péché, ni ses parents, mais c’est pour que les œuvres de Dieu soient manifestées en lui.
Yesu akawajibu, “Siyo huyu mtu wala wazazi wake waliotenda dhambi, bali kazi za Mungu zipate kufunuliwa kupitia kwake.
4 Il faut que j’opère les œuvres de celui qui m’a envoyé, tandis qu’il est jour; la nuit vient, pendant laquelle personne ne peut agir;
Tunapaswa kufanya kazi zake yeye aliyenituma wakati bado ni mchana. Usiku waja wakati ambapo hakuna atakayeweza kufanya kazi.
5 Tant que je suis dans le monde, je suis la lumière du monde.
Wakati niwapo ulimwenguni, mimi ni nuru ya ulimwengu.”
6 Lorsqu’il eut dit cela, il cracha à terre, fit de la boue avec sa salive, et frotta de cette boue les yeux de l’aveugle,
Baada ya Yesu kusema maneno haya, alitema kwenye ardhi, alifanya tope kwa mate, na akampaka yule mtu machoni na lile tope.
7 Et il lui dit: Va, lave-toi dans la piscine de Siloé (ce qu’on interprète par Envoyé). Il s’en alla donc, se lava, et revint voyant clair.
Akamwambia, nenda kaoge katika kisima cha Siloam (Inayotafsiriwa kama 'aliyetumwa').” Kwa hiyo huyo mtu alienda, akanawa, na akarudi, anaona.
8 De sorte que ses voisins et ceux qui l’avaient vu auparavant mendier, disaient: N’est-ce pas celui-là qui était assis et mendiait? D’autres disaient: c’est lui.
Majirani wa yule mtu na wale waliomuona mwanzo kama mwombaji walisema, Je! huyu siye yule mtu aliyekuwa akikaa na kuomba?” wengine walisema, “Ni yeye.”
9 Et d’autres: Point du tout, seulement il lui ressemble. Mais lui disait: C’est moi.
Na wengine walisema, “Hapana, bali anafanana naye.” Lakini alikuwa akisema, “Ni mimi.”
10 Ils lui demandaient donc: Comment tes yeux ont-ils été ouverts?
Wakamwambia, “Sasa macho yako yalifunguliwaje?”
11 Il répondit: Cet homme qu’on appelle Jésus a fait de la boue, il a frotté mes yeux, et m’a dit: Va à la piscine de Siloé, et lave-toi. J’y suis allé, je me suis lavé, et je vois.
Alijibu, mtu aitwaye Yesu alifanya tope na kupaka macho yangu na kuniambia, 'Nenda Siloam ukanawe.' Kwa hiyo nilienda, na nikanawa, na nikapata kuona tena.”
12 Ils lui demandèrent: Où est-il? Il répondit: Je ne sais.
Wakamwambia, “Yuko wapi?” Alijibu, “Sijui.”
13 Alors ils amenèrent aux pharisiens celui qui avait été aveugle.
Wakampeleka yule mtu aliyewahi kuwa kipofu kwa Mafarisayo.
14 Or c’était un jour de sabbat que Jésus fit de la boue et ouvrit ses yeux.
Nayo ilikuwa siku ya Sabato wakati Yesu alipotengeneza tope na kuyafumbua macho yake.
15 Les pharisiens lui demandèrent donc aussi comment il avait vu. Et il leur dit: Il m’a mis de la boue sur les yeux, je me suis lavé, et je vois.
Ndipo tena Mafarisayo wakamwuliza alipataje kuona. Aliwaambia, “Aliweka tope katika macho yangu, nikanawa, na sasa naweza kuona.”
16 Alors quelques-uns d’entre les pharisiens disaient: Cet homme n’est point de Dieu, puisqu’il ne garde point le sabbat. Mais d’autres disaient: Comment un pécheur peut-il faire de tels miracles? Et il y avait division entre eux.
Baadhi ya Mafarisayo wakasema, “Mtu huyu hajatoka kwa Mungu kwa sababu haishiki Sabato.” Wengine walisema, “Inawezekanaje mtu mwenye dhambi kufanya ishara kama hizo?” Kwa hiyo kukawa na mgawanyiko kati yao.
17 Ils dirent donc encore à l’aveugle: Et toi, que dis-tu de celui qui t’a ouvert les yeux? Il répondit: C’est un prophète.
Ndipo walipomwuliza yule kipofu tena, “Unasemaje juu yake kwa sababu aliyafungua macho yako?” Kipofu akasema, “Ni nabii.”
18 Mais les Juifs ne crurent point de lui qu’il eût été aveugle et qu’il eût recouvré la vue, jusqu’à ce qu’ils eussent appelé les parents de celui qui avait recouvré la vue;
Hata wakati huu Wayahudi hawakumwamini kwamba alikuwa kipofu naye amepata kuona mpaka walipowaita wazazi wake yeye aliyepata kuona.
19 Et ils les interrogèrent, disant: Est-ce là votre fils, que vous dites être né aveugle? Comment donc voit-il maintenant?
Waliwauliza wazazi, Je, huyu ni mtoto wenu mnayesema alizaliwa kipofu? amewezaje sasa kuona?”
20 Ses parents leur répondirent et dirent: Nous savons que c’est notre fils et qu’il est né aveugle;
Hivyo wazazi wake wakamjibu, “Tunajua kuwa huyu ni mtoto wetu na kwamba alizaliwa kipofu.
21 Mais comment il voit maintenant, nous ne le savons pas; ou qui lui a ouvert les yeux, nous ne le savons pas; interrogez-le: il a de l’âge, qu’il parle pour lui-même.
Jinsi gani sasa anaona, hatujui, na yeye aliyemfumbua macho yake, hatumjui. Mwulizeni yeye. Ni mtu mzima. Anaweza kujieleza mwenyewe.”
22 Ses parents dirent cela, parce qu’ils craignaient les Juifs; car déjà les Juifs étaient convenus ensemble que si quelqu’un confessait que Jésus était le Christ, il serait chassé de la synagogue.
Wazazi wake walisema mambo haya, kwa sababu waliwaogopa Wayahudi. Kwa vile Wayahudi walikuwa wamekubaliana tayari kuwa, ikiwa yeyote atakiri kuwa Yesu ni Kristo, atatengwa na Sinagogi.
23 C’est pourquoi ses parents dirent: Il a de l’âge, interrogez-le lui-même.
Kwa sababu hii, wazazi wake walisema, “Ni mtu mzima, mwulizeni yeye.”
24 Ils appelèrent donc de nouveau l’homme qui avait été aveugle, et lui dirent: Rends gloire à Dieu; pour nous, nous savons que cet homme est un pécheur.
Kwa hiyo kwa mara ya pili, walimwita yule mtu aliyewahi kuwa kipofu na kumwambia, “Mpe Mungu utukufu. Tunajua kwamba mtu huyu ni mwenye dhambi.”
25 Mais il leur dit: S’il est pécheur, je ne sais; je sais une seule chose, c’est que j’étais aveugle, et qu’à présent je vois.
Ndipo yule mtu alijibu, “Awe ni mwenye dhambi, mimi sijui. Kitu kimoja ninachokijua: nilikuwa kipofu, na sasa ninaona.”
26 Ils lui répliquèrent donc: Que t’a-t-il fait? Comment t’a-t-il ouvert les yeux?
Ndipo walipomwambia, “Amekufanyia nini? Aliyafumbuaje macho yako?”
27 Il leur répondit: Je vous l’ai déjà dit, et vous l’avez entendu, pourquoi voulez-vous l’entendre encore? Est-ce que, vous aussi, vous voulez devenir ses disciples?
Alijibu, “Nimekwishawaambia tayari, na nyinyi hamkusikiliza! Kwa nini mnataka kusikia tena? Nanyi hamtaki kuwa wanafunzi wake pia, sivyo?
28 Ils le maudirent donc, et dirent: Sois son disciple, toi; mais nous, nous sommes disciples de Moïse.
Walimtukana na kusema, “Wewe ni mwanafunzi wake, lakini sisi ni wanafunzi wa Musa.
29 Nous savons que Dieu a parlé à Moïse; mais celui-ci, nous ne savons d’où il est.
Tunajua kwamba Mungu alizungumza na Musa, lakini kwa huyu mtu, hatujui kule atokako.”
30 Cet homme reprit et leur dit: Mais il y a en cela une chose étonnante, c’est que vous ne sachiez d’où il est, et il a ouvert mes yeux;
Yule mtu akajibu na kuwaambia, “Kwa nini, hili ni jambo la kushangaza, kwamba hamjui anakotoka, na bado ameyafumbua macho yangu.
31 Cependant nous savons que Dieu n’écoute point les pécheurs; mais si quelqu’un honore Dieu et fait sa volonté, c’est celui-là qu’il exauce.
Tunajua kuwa Mungu hawasikilizi wenye dhambi, lakini ikiwa mtu yeyote anamwabudu Mungu na hufanya mapenzi yake, Mungu humsikiliza.
32 Jamais on n’a ouï dire que quelqu’un ait ouvert les yeux d’un aveugle-né. (aiōn g165)
Tangu kuanza kwa Ulimwengu haijawahi kamwe kusikiwa kwamba yeyote ameyafumbua macho ya mtu aliyezaliwa kipofu. (aiōn g165)
33 Si celui-ci n’était pas de Dieu, il ne pourrait rien faire.
Ikiwa mtu huyu hakutoka kwa Mungu, asingelifanya chochote.”
34 Ils répliquèrent et lui dirent: Tu es né tout entier dans le péché, et tu nous enseignes! Et ils le jetèrent dehors.
Walijibu na kumwambia, “Ulizaliwa katika dhambi kabisa, na wewe unatufundisha sisi?” Ndipo walipomfukuza kutoka katika sinagogi.
35 Jésus apprit qu’ils l’avaient jeté dehors; et, l’ayant rencontré, il lui demanda: Crois-tu au Fils de Dieu?
Yesu alisikia kwamba wamemwondoa kwenye sinagogi. Alimpata na kumwambia, “Unamwamini Mwana wa Mtu?”
36 Celui-ci répondit et dit: Qui est-il, Seigneur, afin que je croie en lui?
Alijibu na kusema, “Ni nani, Bwana, ili nami nipate kumwamini?”
37 Et Jésus lui dit: Mais tu l’as vu, et c’est lui-même qui te parle.
Yesu akamwambia, “Umeshamuona, naye unayezungumza naye ndiye.”
38 Et celui-ci reprit: Je crois. Seigneur; et se prosternant, il l’adora.
Yule mtu akasema, “Bwana, Naamini.” Ndipo akamsujudia.
39 Alors Jésus dit: C’est en jugement que je suis venu dans ce monde, afin que ceux qui ne voient pas, voient, et que ceux qui voient, deviennent aveugles.
Yesu akasema, “Kwa hukumu nimekuja katika Ulimwengu huu ili kwamba wale wasioona wapate kuona na wale wanaoona wawe vipofu.”
40 Or quelques-uns d’entre les pharisiens, qui étaient avec lui, l’entendirent et lui demandèrent: Est-ce que nous sommes aveugles, nous aussi?
Baadhi ya Mafarisayo waliokuwa pamoja naye wakasikia maneno hayo na kumwuliza, “Na sisi pia ni vipofu?”
41 Jésus leur répondit: Si vous étiez aveugles, vous n’auriez point de péché. Mais vous dites au contraire: Nous voyons. Ainsi votre péché subsiste.
Yesu akawaambia, “Kama mngelikuwa vipofu, msingelikuwa na dhambi. Hata hivyo, sasa mnasema, 'Tunaona,' dhambi yenu inakaa.”

< Jean 9 >