< Jean 1 >
1 Au commencement était le Verbe, et le Verbe était en Dieu, et le Verbe était Dieu.
Hapo mwanzo alikuwako Neno, huyo Neno alikuwa pamoja na Mungu, naye Neno alikuwa Mungu.
2 C’est lui qui au commencement était en Dieu.
Tangu mwanzo huyo Neno alikuwa pamoja na Mungu.
3 Toutes choses ont été faites par lui; et sans lui rien n’a été fait de ce qui a été fait.
Vitu vyote viliumbwa kwa yeye, wala pasipo yeye hakuna chochote kilichoumbwa ambacho kimeumbwa.
4 En lui était la vie, et la vie était la lumière des hommes;
Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima na huo uzima ulikuwa nuru ya watu.
5 Et la lumière luit dans les ténèbres, et les ténèbres ne l’ont pas comprise.
Nuru hungʼaa gizani nalo giza halikuishinda.
6 Il y eut un homme envoyé de Dieu dont le nom était Jean.
Alikuja mtu mmoja aliyetumwa kutoka kwa Mungu, jina lake Yohana.
7 Celui-ci vint comme témoin pour rendre témoignage à la lumière, afin que tous crussent par lui;
Alikuja kama shahidi apate kuishuhudia hiyo nuru, ili kwa kupitia kwake watu wote waweze kuamini.
8 Il n’était pas la lumière, mais il devait rendre témoignage à la lumière.
Yeye mwenyewe hakuwa ile nuru, bali alikuja kuishuhudia hiyo nuru.
9 Celui-là était la vraie lumière, qui illumine tout homme venant en ce monde.
Kwamba nuru halisi, imwangaziayo kila mtu ilikuwa inakuja ulimwenguni.
10 Il était dans le monde, et le monde a été fait par lui, et le monde ne l’a pas connu.
Huyo Neno alikuwako ulimwenguni na ingawa ulimwengu uliumbwa kupitia kwake, haukumtambua.
11 Il est venu chez lui, et les siens ne l’ont pas reçu.
Alikuja kwa walio wake, lakini wao hawakumpokea.
12 Mais à tous ceux qui l’ont reçu, il a donné le pouvoir d’être faits enfants de Dieu; à ceux qui croient en son nom;
Bali wote waliompokea, aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake.
13 Qui ne sont point nés du sang, ni de la volonté de la chair, ni de la volonté de l’homme, mais de Dieu.
Hawa ndio wasiozaliwa kwa damu, wala kwa mapenzi ya mwili au kwa mapenzi ya mtu, bali kwa mapenzi ya Mungu.
14 Et le Verbe a été fait chair, et il a habité parmi nous et nous avons vu sa gloire comme la gloire qu’un fils unique reçoit de son père, plein de grâce et de vérité.
Neno alifanyika mwili, akakaa miongoni mwetu, nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba, amejaa neema na kweli.
15 Jean rend témoignage de lui, et il crie, disant: Voici celui-ci dont j’ai dit: Celui qui doit venir après moi a été fait avant moi, parce qu’il était avant moi.
Yohana alishuhudia habari zake, akapaza sauti, akisema, “Huyu ndiye yule niliyewaambia kwamba, ‘Yeye ajaye baada yangu ni mkuu kuniliko mimi, kwa kuwa alikuwepo kabla yangu.’”
16 Et nous avons tous reçu de sa plénitude, et grâce pour grâce;
Kutokana na ukamilifu wake, sisi sote tumepokea neema juu ya neema.
17 Car la loi a été donnée par Moïse, la grâce et la vérité sont venues par Jésus-Christ.
Kwa kuwa sheria ilitolewa kwa mkono wa Mose, lakini neema na kweli imekuja kupitia Yesu Kristo.
18 Personne n’a jamais vu Dieu: le Fils unique qui est dans le sein du Père est celui qui l’a fait connaître.
Hakuna mtu yeyote aliyemwona Mungu wakati wowote, ila ni Mungu Mwana pekee, aliye kifuani mwa Baba ndiye ambaye amemdhihirisha.
19 Or voici le témoignage de Jean, lorsque les Juifs lui envoyèrent de Jérusalem des prêtres et des lévites pour lui demander: Qui es-tu?
Huu ndio ushuhuda wa Yohana wakati Wayahudi walipowatuma makuhani na Walawi kutoka Yerusalemu kumuuliza, “Wewe ni nani?”
20 Car il confessa, et il ne le nia point; il confessa: Ce n’est pas moi qui suis le Christ.
Yohana alikiri waziwazi pasipo kuficha akasema, “Mimi si Kristo.”
21 Et ils lui demandèrent: Quoi donc? Es-tu Elie? Et il dit: Non. Es-tu le prophète? Et il répondit: Non.
Wakamuuliza, “Wewe ni nani basi? Je, wewe ni Eliya?” Yeye akajibu, “Hapana, mimi siye.” “Je, wewe ni yule Nabii?” Akajibu, “Hapana.”
22 Ils lui dirent donc: Qui es-tu, afin que nous donnions une réponse à ceux qui nous ont envoyés? Que dis-tu de toi-même?
Ndipo wakasema, “Basi tuambie wewe ni nani ili tupate jibu la kuwapelekea wale waliotutuma. Wewe wasemaje juu yako mwenyewe?”
23 Je suis, répondit-il, la voix de celui qui crie dans le désert: Redressez la voie du Seigneur, comme l’a dit le prophète Isaïe.
Akawajibu kwa maneno ya nabii Isaya, akisema, “Mimi ni sauti ya mtu aliaye nyikani, ‘Yanyoosheni mapito ya Bwana.’”
24 Or ceux qui avaient été envoyés étaient du nombre des pharisiens.
Basi walikuwa wametumwa watu kutoka kwa Mafarisayo
25 Ils l’interrogèrent encore et lui dirent: Pourquoi donc baptises-tu, si tu n’es ni le Christ, ni Élie, ni le prophète?
wakamuuliza, “Kama wewe si Kristo, wala si Eliya na wala si yule Nabii, kwa nini basi unabatiza?”
26 Jean leur répondit, disant: Moi je baptise dans l’eau, mais il y a au milieu de vous quelqu’un que vous ne connaissez point.
Yohana akawajibu, “Mimi ninabatiza kwa maji, lakini katikati yenu yupo mtu msiyemjua.
27 C’est lui qui doit venir après moi, qui a été fait avant moi; je ne suis même pas digne de délier la courroie de sa chaussure.
Yeye ajaye baada yangu, sistahili hata kufungua kamba za viatu vyake.”
28 Ceci se passa en Béthanie, au-delà du Jourdain où Jean baptisait.
Mambo haya yote yalitukia huko Bethania, ngʼambo ya Mto Yordani, mahali Yohana alipokuwa akibatiza.
29 Le jour suivant Jean vit Jésus venant à lui, et il dit: Voici l’agneau de Dieu, voici celui qui ôte le péché du monde.
Siku iliyofuata, Yohana alimwona Yesu akimjia akasema, “Tazama, Mwana-Kondoo wa Mungu aichukuaye dhambi ya ulimwengu!
30 C’est celui de qui j’ai dit: Après moi vient un homme qui a été fait avant moi, parce qu’il était avant moi;
Huyu ndiye yule niliyewaambia kwamba, ‘Mtu anakuja baada yangu ambaye ni mkuu kuniliko mimi, kwa kuwa alikuwepo kabla yangu.’
31 Et moi je ne le connaissais pas; mais c’est pour qu’il fût manifesté en Israël, que je suis venu baptisant dans l’eau.
Mimi mwenyewe sikumfahamu, lakini sababu ya kuja nikibatiza kwa maji ni ili yeye apate kufunuliwa kwa Israeli.”
32 Jean rendit encore témoignage, disant: J’ai vu l’Esprit descendant sur lui en forme de colombe, et il s’est reposé sur lui.
Kisha Yohana akatoa ushuhuda huu: “Nilimwona Roho akishuka kutoka mbinguni kama hua, akakaa juu yake.
33 Et moi je ne le connaissais pas; mais celui qui m’a envoyé baptiser dans l’eau m’a dit: Celui sur qui tu verras l’Esprit descendre et se reposer, c’est celui-là qui baptisera dans l’Esprit-Saint.
Mimi nisingemtambua, lakini yeye aliyenituma nibatize kwa maji alikuwa ameniambia, ‘Yule mtu utakayemwona Roho akimshukia na kukaa juu yake, huyo ndiye atakayebatiza kwa Roho Mtakatifu.’
34 Et je l’ai vu, et j’ai rendu témoignage que c’est lui qui est le Fils de Dieu.
Mimi mwenyewe nimeona jambo hili na ninashuhudia kuwa huyu ndiye Mwana wa Mungu.”
35 Le jour suivant, Jean se trouvait de nouveau avec deux de ses disciples.
Siku iliyofuata, Yohana alikuwa huko tena pamoja na wanafunzi wake wawili.
36 Et regardant Jésus qui se promenait, il dit: Voilà l’agneau de Dieu.
Alipomwona Yesu akipita, akasema, “Tazama, Mwana-Kondoo wa Mungu!”
37 Les deux disciples l’entendirent parler ainsi, et ils suivirent Jésus.
Wale wanafunzi wawili walipomsikia Yohana akisema haya, wakamfuata Yesu.
38 Or Jésus s’étant retourné et les voyant qui le suivaient, leur dit: Que cherchez-vous? Ils lui répondirent; Rabbi (ce qui veut dire, par interprétation, Maître), où demeurez-vous?
Yesu akageuka, akawaona wakimfuata akawauliza, “Mnataka nini?” Wakamwambia, “Rabi,” (maana yake Mwalimu), “Unaishi wapi?”
39 Il leur dit: Venez et voyez. Ils vinrent, et virent où il demeurait, et ils restèrent avec lui ce jour-là: or, il était environ la dixième heure,
Yesu akawajibu, “Njooni, nanyi mtapaona!” Hivyo wakaenda na kupaona mahali alipokuwa anaishi, wakakaa naye siku ile, kwa kuwa ilikuwa yapata saa kumi.
40 Or André, frère de Simon-Pierre, était un des deux qui avaient entendu de Jean ce témoignage, et qui avaient suivi Jésus.
Andrea nduguye Simoni Petro, alikuwa mmoja wa wale wawili waliosikia yale Yohana aliyokuwa amesema, naye ndiye alimfuata Yesu.
41 Or il rencontra d’abord son frère Simon, et lui dit: Nous avons trouvé le Messie (ce qu’on interprète par le Christ).
Kitu cha kwanza Andrea alichofanya ni kumtafuta Simoni nduguye na kumwambia, “Tumemwona Masiya” (yaani, Kristo).
42 Et il l’amena à Jésus. Et Jésus l’ayant regardé, dit: Tu es Simon, fils de Jona; tu seras appelé Céphas, ce qu’on interprète par Pierre.
Naye akamleta kwa Yesu. Yesu akamwangalia na kusema, “Wewe ni Simoni mwana wa Yohana. Utaitwa Kefa” (ambalo limetafsiriwa Petro).
43 Le lendemain, Jésus voulut aller en Galilée; il trouva Philippe et lui dit: Suis-moi.
Siku iliyofuata Yesu aliamua kwenda Galilaya. Akamkuta Filipo, akamwambia, “Nifuate.”
44 Or Philippe était de Bethsaïde, de la même ville qu’André et Pierre.
Basi Filipo alikuwa mwenyeji wa Bethsaida, mji alikotoka Andrea na Petro.
45 Philippe trouva Nathanaël, et lui dit: Nous avons trouvé celui de qui Moïse a écrit dans la loi et ensuite les prophètes, Jésus, fils de Joseph de Nazareth.
Filipo naye akamkuta Nathanaeli na kumwambia, “Tumemwona yeye ambaye Mose aliandika habari zake katika Sheria na ambaye pia manabii waliandika kumhusu, yaani, Yesu wa Nazareti, mwana wa Yosefu.”
46 Et Nathanaël lui demanda: Peut-il venir de Nazareth quelque chose de bon? Philippe lui répondit: Viens et vois.
Nathanaeli akauliza, “Nazareti! Je, kitu chochote chema chaweza kutoka Nazareti?” Filipo akamwambia, “Njoo uone.”
47 Jésus vit venir à lui Nathanaël, et il dit de lui: Voici vraiment un Israélite en qui il n’y a point d’artifice.
Yesu alipomwona Nathanaeli anakaribia, akanena habari zake akasema, “Tazama huyu ni Mwisraeli kweli kweli; hana hila ndani yake.”
48 Nathanaël lui demanda: D’où me connaissez-vous? Jésus répondit et lui dit: Avant que Philippe t’appelât, lorsque tu étais sous le figuier, je t’ai vu.
Nathanaeli akamuuliza, “Umenifahamuje?” Yesu akamjibu, “Nilikuona ulipokuwa bado uko chini ya mtini, kabla hata Filipo hajakuita.”
49 Nathanaël lui répondit et dit: Rabbi, vous êtes le Fils de Dieu, vous êtes le roi d’Israël.
Nathanaeli akamwambia, “Rabi, wewe ni Mwana wa Mungu! Wewe ni Mfalme wa Israeli!”
50 Jésus répliqua et lui dit: Parce que je t’ai dit: Je t’ai vu sous le figuier, tu crois; tu verras de plus grandes choses.
Yesu akamwambia, “Unaamini kwa kuwa nilikuambia nilikuona ulipokuwa bado uko chini ya mtini? Basi utaona mambo makuu zaidi kuliko hilo.”
51 Et il ajouta: En vérité, en vérité, je vous le dis, vous verrez le ciel ouvert et les anges de Dieu montant et descendant sur le Fils de l’homme.
Ndipo akawaambia, “Amin, amin nawaambia, ninyi mtaona mbingu ikifunguka na malaika wa Mungu wakipanda na kushuka juu ya Mwana wa Adamu.”