< Joël 3 >

1 Parce que voilà qu’en ces jours-là et en ce temps-là, lorsque j’aurai ramené les captifs de Juda et de Jérusalem,
“Katika siku hizo na wakati huo, nitakaporejesha neema ya Yuda na Yerusalemu,
2 J’assemblerai tous les peuples, et je les conduirai dans la vallée de Josaphat, et là, j’entrerai en jugement avec eux touchant mon peuple et mon héritage, Israël, qu’ils ont dispersés parmi les nations; et ma terre, ils l’ont partagée;
nitayakusanya mataifa yote na kuyaleta katika Bonde la Yehoshafati Hapo nitaingia kwenye hukumu dhidi yao kuhusu urithi wangu, watu wangu Israeli, kwa kuwa waliwatawanya watu wangu miongoni mwa mataifa na kuigawa nchi yangu.
3 Et sur mon peuple ils ont jeté le sort; et ils ont exposé le jeune enfant dans un lieu de prostitution, et la jeune fille, ils l’ont vendue pour du vin, afin de boire.
Wanawapigia kura watu wangu na kuwauza wavulana ili kupata makahaba; waliwauza wasichana ili wapate kunywa mvinyo.
4 Mais qu’y a-t-il entre moi et vous, Tyr et Sidon, et toi, terre entière des Philistins? Est-ce que vous tirerez vengeance de moi? Mais si vous vous vengez de moi, je vous rendrai la pareille promptement, tout d’un coup, sur votre propre tête.
“Sasa una nini dhidi yangu, ee Tiro na Sidoni, nanyi nchi zote za Ufilisti? Je, mnanilipiza kwa yale niliyoyafanya? Kama mnalipa, mimi nitalipiza juu ya vichwa vyenu kwa kasi na kwa haraka yale mliyoyatenda.
5 Car vous avez enlevé mon argent et mon or, et toutes mes choses précieuses et très belles, vous les avez emportées dans vos temples.
Kwa kuwa mlichukua fedha na dhahabu yangu pia mkabeba hazina zangu nzuri sana mkapeleka kwenye mahekalu yenu.
6 Et les fils de Juda et les fils de Jérusalem, vous les avez vendus aux fils des Grecs, afin de les éloigner de leurs confins.
Mliwauza watu wa Yuda na Yerusalemu kwa Wayunani, ili kwamba mpate kuwapeleka mbali na nchi yao.
7 Et moi, je les retirerai du lieu dans lequel vous les avez vendus et je ferai retomber ce que vous leur avez fait sur votre tête.
“Tazama nitawaamsha kutoka zile sehemu mlizowauza, nami nitawalipiza juu ya vichwa vyenu kile mlichofanya.
8 Et je vendrai vos fils et vos filles par les mains des fils de Juda; ils les vendront aux Sabéens, à une nation éloignée; parce que c’est le Seigneur qui a parlé.
Nitawauza wana wenu na binti zenu kwa watu wa Yuda, nao watawauza kwa Waseba, taifa lililo mbali.” Bwana amesema.
9 Criez ceci parmi les nations: Consacrez une guerre, réveillez les braves; qu’ils s’approchent, qu’ils montent, tous les hommes de guerre.
Tangazeni hili miongoni mwa mataifa: Jiandaeni kwa vita! Amsha askari! Wanaume wote wapiganaji wasogee karibu na kushambulia.
10 Taillez vos charrues en glaives et vos boyaux en lances. Que le faible dise: Je suis fort, moi.
Majembe yenu yafueni yawe panga na miundu yenu ya kukatia iwe mikuki. Aliye dhaifu na aseme, “Mimi nina nguvu!”
11 Faites une sortie, et venez, vous toutes, nations d’alentour, rassemblez-vous; c’est là que le Seigneur fera tomber tes braves.
Njooni haraka, ninyi mataifa yote kutoka pande zote, kusanyikeni huko. Shusha wapiganaji wako, Ee Bwana!
12 Que les nations se lèvent et montent dans la vallée de Josaphat, parce que c’est là que je serai assis, afin de juger toutes les nations d’alentour.
“Mataifa na yaamshwe; na yasonge mbele kuelekea Bonde la Yehoshafati, kwa kuwa nitaketi mahali pale kuhukumu mataifa yote yaliyoko kila upande.
13 Mettez les faucilles dans le blé, parce que la moisson est mûre; venez, et descendez, parce que le pressoir est plein, que les pressoirs regorgent; parce que leur malice s’est multipliée.
Tia mundu, kwa kuwa mavuno yamekomaa. Njooni, mkanyage zabibu, kwa kuwa shinikizo la kukamua zabibu limejaa na mapipa yanafurika: kwa kuwa uovu wao ni mkubwa!”
14 Peuples, peuples, accourez dans la vallée du carnage; parce qu’est proche le jour du Seigneur, dans la vallée du carnage.
Umati mkubwa, umati mkubwa katika bonde la uamuzi! Kwa kuwa siku ya Bwana ni karibu katika bonde la uamuzi.
15 Le soleil et la lune se sont couverts de ténèbres, et les étoiles ont retiré leur splendeur.
Jua na mwezi vitatiwa giza, na nyota hazitatoa mwanga wake tena.
16 Et le Seigneur rugira de Sion; et de Jérusalem il fera entendre sa voix; et le ciel et la terre seront ébranlés; et le Seigneur sera l’espérance de son peuple, et la force des fils d’Israël.
Bwana atanguruma kutoka Sayuni na mshindo wa ngurumo kutoka Yerusalemu; dunia na mbingu vitatikisika. Lakini Bwana atakuwa kimbilio la watu wake, ngome imara kwa ajili ya watu wa Israeli.
17 Et vous saurez que je suis le Seigneur votre Dieu, habitant dans Sion, ma montagne sainte; et Jérusalem sera sainte, et les étrangers ne la traverseront plus.
“Ndipo mtakapojua kwamba Mimi, Bwana Mungu wenu, nakaa Sayuni, mlima wangu mtakatifu. Yerusalemu utakuwa mtakatifu; kamwe wageni hawatavamia tena.
18 Et il arrivera en ce jour-là que les montagnes distilleront la douceur, et que le lait coulera des collines, et que dans tous les ruisseaux de Juda se répandront les eaux, et qu’une fontaine sortira de la maison du Seigneur, et remplira le torrent des épines.
“Katika siku hiyo milima itadondosha divai mpya, na vilima vitatiririka maziwa; mabonde yote ya Yuda yatatiririka maji. Chemchemi itatiririka kutoka kwenye nyumba ya Bwana na kunywesha Bonde la Shitimu.
19 L’Egypte sera désolée, l’Idumée un désert de perdition, parce qu’elles ont agi iniquement envers les fils de Juda, et qu’elles ont répandu un sang innocent sur leur terre.
Lakini Misri itakuwa ukiwa, Edomu itakuwa jangwa tupu, kwa sababu ya jeuri waliofanya kwa watu wa Yuda, ambao katika nchi yao walimwaga damu isiyo na hatia.
20 Et la Judée sera éternellement habitée, et Jérusalem dans toutes les générations.
Yuda itakaliwa na watu milele na Yerusalemu itadumu vizazi vyote.
21 Et je purifierai leur sang que je n’avais pas encore purifié;
Hatia yao ya damu, ambayo sijasamehe, nitasamehe.”

< Joël 3 >