< Job 37 >

1 C’est pour cela que mon cœur a été saisi d’effroi, et qu’il est sorti de sa place.
“Kwa hili moyo wangu unatetemeka, nao unaruka kutoka mahali pake.
2 Écoutez très attentivement sa voix terrible, et les sons qui sortent de sa bouche.
Sikiliza! Sikiliza ngurumo ya sauti yake, sauti ya ngurumo itokayo kinywani mwake.
3 Lui-même porte ses regards au-dessous de tous les cieux, et sa lumière se répand sur les confins de la terre.
Huuachilia umeme wake wa radi chini ya mbingu yote na kuupeleka hata miisho ya dunia.
4 Après lui un bruit éclatera comme un rugissement; il tonnera par la voix de sa grandeur, et lorsqu’on aura entendu sa voix, on ne pourra la comprendre.
Baada ya hayo huja sauti ya ngurumo yake; Mungu hunguruma kwa sauti yake ya fahari. Wakati sauti yake ingurumapo tena, huuachilia umeme wake wa radi.
5 Dieu tonnera merveilleusement par sa voix, lui qui fait des choses grandes et impénétrables;
Sauti ya Mungu hunguruma kwa namna za ajabu; yeye hutenda mambo makuu kupita ufahamu wetu.
6 Qui ordonne de descendre sur la terre à la neige et aux pluies de l’hiver, et à ses fortes ondées;
Huiambia theluji, ‘Anguka juu ya dunia,’ nayo manyunyu ya mvua, ‘Uwe mvua ya nguvu.’
7 Qui met un sceau sur la main de tous les hommes, afin qu’ils reconnaissent chacun leurs œuvres.
Ili wanadamu wote aliowaumba wapate kujua kazi zake, yeye humzuilia kila mtu shughuli zake.
8 La bête entrera dans sa tanière, et elle demeurera dans son antre.
Wanyama hujificha; hubakia kwenye mapango yao.
9 Des lieux intérieurs sortira la tempête, et d’Arcturus le froid.
Dhoruba hutoka katika chumba chake, baridi hutoka katika upepo uendao kasi.
10 Au souffle de Dieu, la glace se durcit, et de nouveau les eaux les plus abondantes se répandent.
Pumzi ya Mungu hutoa barafu, eneo kubwa la maji huganda.
11 Le blé désire les nuées, et les nuées répandent leur lumière.
Huyasheheneza mawingu kwa maji, naye husambaza umeme wake wa radi kupitia hayo.
12 Elles parcourent tous les lieux où les conduit la volonté de celui qui les gouverne, et selon ce qu’il leur a ordonné sur la face du globe de la terre,
Nayo mawingu huzungukazunguka pande zote kwa amri yake, juu ya uso wa dunia yote, kufanya lolote ayaamuruyo.
13 Soit dans une tribu, soit dans sa terre, soit en quelque lieu de sa miséricorde que ce soit, où il leur aura commandé de se trouver.
Huleta mawingu ili kuadhibu wanadamu, au kuinyeshea dunia yake na kuonyesha upendo wake.
14 Job, écoute ceci attentivement; arrête-toi, et considère les merveilles de Dieu.
“Ayubu, sikiliza hili; nyamaza na uyafikiri maajabu ya Mungu.
15 Est-ce que tu sais quand Dieu a ordonné aux pluies de faire paraître la lumière des nuées?
Je, unajua jinsi Mungu anavyoyaongoza mawingu, na kufanya umeme wake wa radi utoe mwanga?
16 Est-ce que tu connais les grands sentiers des nuées et les sciences parfaites?
Je, wajua jinsi mawingu yanavyokaa yakiwa yametulia, hayo maajabu yake yeye aliye mkamilifu katika maarifa?
17 Tes vêtements ne sont-ils pas échauffés, lorsque le vent du midi souffle sur la terre?
Wewe unayeshindwa na joto katika nguo zako wakati nchi imenyamazishwa kimya bila upepo wa kusini,
18 Tu as peut-être formé avec lui les cieux qui sont très solides, comme s’ils avaient été coulés en bronze.
je, waweza kuungana naye katika kuzitandaza anga, zilizo ngumu kama kioo cha shaba ya kuyeyushwa?
19 Montre-nous ce que nous pourrons lui dire; car nous, nous sommes enveloppés de ténèbres.
“Tuambieni yatupasayo kumwambia; hatuwezi kutayarisha shauri letu kwa sababu ya ujinga wetu.
20 Qui lui racontera ce que je dis? Que si un homme en parle, il sera absorbé.
Je, aambiwe kwamba nataka kuongea? Je, yuko mtu ambaye angeomba kumezwa?
21 Mais maintenant ils ne voient pas la lumière: soudain l’air s’épaissira en nuées, et le vent, passant, les dissipera.
Basi hakuna awezaye kulitazama jua, jinsi linavyongʼaa angani, upepo ukishafagia mawingu.
22 C’est du côté de l’aquilon que l’or vient, et la louange qu’on donne à Dieu doit être accompagnée de crainte.
Kutoka kaskazini yeye huja na fahari kuu; Mungu huja katika utukufu wa kutisha.
23 Nous ne pouvons le comprendre dignement: il est grand en puissance, en jugement et en justice, et il ne peut être l’objet d’un récit.
Yeye Mwenyezi hatuwezi kumfikia, naye ametukuzwa katika uweza; katika hukumu zake na haki yake kuu, hataonea.
24 C’est pourquoi les hommes le craindront, et aucun de ceux qui croient être sages n’osera le contempler.
Kwa hiyo, wanadamu mheshimuni, kwa kuwa yeye hamstahi yeyote anayejidhania kuwa ana hekima.”

< Job 37 >