< Job 31 >

1 J’ai fait un pacte avec mes yeux pour ne pas même penser à une vierge.
“Nimefanya agano na macho yangu yasimtazame msichana kwa kumtamani.
2 Car autrement quelle part d’en haut aurait Dieu pour moi, et quel héritage des cieux, le Tout-Puissant?
Kwa kuwa fungu la mwanadamu ni gani kutoka kwa Mungu juu, urithi wake kutoka kwa Mungu Mwenye Nguvu Aliye juu?
3 Est-ce que la ruine n’est pas pour le méchant, et l’aliénation des héritages pour ceux qui opèrent l’injustice?
Je, si uharibifu kwa watu waovu, maangamizi kwa wale watendao mabaya?
4 Dieu ne considère-t-il pas mes voies, et tous mes pas, ne les compte-t-il point?
Je, yeye hazioni njia zangu na kuihesabu kila hatua yangu?
5 Si j’ai marché dans la vanité; si mon pied s’est hâté dans la ruse;
“Kama nimeishi katika uongo au mguu wangu umekimbilia udanganyifu,
6 Que Dieu me pèse dans une balance juste, et qu’il connaisse ma simplicité.
Mungu na anipime katika mizani za uaminifu, naye atajua kwamba sina hatia:
7 Que si mon pas s’est détourné de la voie, et si mon cœur a suivi mes yeux, et si à mes mains s’est attachée quelque souillure;
kama hatua zangu zimepotoka kutoka kwenye njia, kama moyo wangu umeongozwa na macho yangu, au kama mikono yangu imetiwa unajisi,
8 Que je sème et qu’un autre mange, et que ma race soit arrachée jusqu’à la racine.
basi wengine na wale nilichokipanda, nayo yale yote niliyootesha na yangʼolewe.
9 Si mon cœur a été séduit au sujet d’une femme, et si à la porte de mon ami j’ai dressé des embûches;
“Kama moyo wangu umeshawishiwa na mwanamke, au kama nimevizia mlangoni mwa jirani yangu,
10 Que ma femme soit la prostituée d’un autre, et que d’autres la déshonorent.
basi mke wangu na asage nafaka ya mwanaume mwingine, nao wanaume wengine walale naye.
11 Car l’adultère est un crime énorme, et une iniquité très grande.
Kwa kuwa hilo lingekuwa aibu, naam, dhambi ya kuhukumiwa.
12 C’est un feu qui dévore jusqu’à la perdition, et qui extirpe toutes les productions.
Ni moto uwakao kwa Uharibifu; ungekuwa umengʼoa mavuno yangu.
13 Si j’ai dédaigné d’aller en jugement avec mon serviteur et ma servante, lorsqu’ils disputaient contre moi.
“Kama ningewanyima haki watumishi wangu wanaume au vijakazi wangu, walipokuwa na manungʼuniko dhidi yangu,
14 (Car que ferai-je, lorsque Dieu se lèvera pour me juger? et lorsqu’il m’interrogera, que lui répondrai-je?
nitafanya nini Mungu atakaponikabili? Nitamjibu nini nitakapoitwa kutoa hesabu?
15 N’est-ce pas celui qui m’a fait dans le sein de ma mère, qui l’a fait lui aussi, et le même qui m’a formé en elle?)
Je, yeye aliyeniumba tumboni mwa mama yangu, si ndiye aliwaumba? Je, si ni yeye huyo mmoja aliyetuumba sote ndani ya mama zetu?
16 Si j’ai refusé aux pauvres ce qu’ils voulaient, et si j’ai fait attendre les yeux de la veuve;
“Ikiwa nimewanyima maskini haja zao, au kuyaacha macho ya wajane yadhoofike,
17 Si j’ai mangé seul ma bouchée de pain, et si le pupille n’en a pas mangé aussi:
kama nimekula chakula changu mwenyewe, bila kuwashirikisha yatima;
18 (Car dès mon enfance la compassion a crû avec moi, et du sein de ma mère elle est sortie avec moi.)
lakini tangu ujana wangu nimemlea yatima kama ambavyo baba angefanya, nami tangu kuzaliwa kwangu nimewaongoza wajane:
19 Si j’ai détourné mes yeux de celui qui mourait, parce qu’il n’avait pas de quoi se couvrir, et du pauvre qui était sans vêtement;
kama nilimwona yeyote akiteseka kwa kukosa nguo, au mtu mhitaji asiye na mavazi
20 Si ses flancs ne m’ont pas béni, et s’il n’a pas été réchauffé par les toisons de mes brebis:
ambaye wala moyo wake haukunibariki kwa kumpatia joto kwa mavazi ya manyoya ya kondoo zangu,
21 Si j’ai levé ma main contre un orphelin, même lorsque je me voyais supérieur à la porte de la ville:
na kama nimeinua mkono wangu dhidi ya yatima, nikijua kuwa nina ushawishi mahakamani,
22 Que mon épaule tombe séparée de sa jointure, et que mon bras avec tous mes os soit entièrement brisé:
basi mkono wangu na unyofoke toka begani mwangu, nao na uvunjike kutoka kiungio chake.
23 Car j’ai toujours craint Dieu comme des îlots soulevés au-dessus de moi, et je n’ai pu supporter le poids de sa majesté.
Kwa kuwa niliogopa uharibifu kutoka kwa Mungu, nami kwa kuuogopa utukufu wake sikuweza kufanya mambo kama hayo.
24 Si j’ai pris l’or pour ma force, et si j’ai dit à l’or affiné: Tu es ma confiance:
“Kama nimeweka tumaini langu kwenye dhahabu, au kuiambia dhahabu safi, ‘Wewe ndiwe salama yangu,’
25 Si je me suis livré à l’allégresse à cause de mes abondantes richesses, et parce que ma main a trouvé des biens en très grand nombre;
kama nimefurahia wingi wa utajiri wangu, ustawi ambao mikono yangu ilikuwa imepata,
26 Si j’ai vu le soleil, lorsqu’il brillait de son vif éclat, et la lune marchant dans son clair,
kama nimelitazama jua katika kungʼaa kwake au mwezi ukienda kwa fahari yake,
27 Et si mon cœur s’est livré à la joie en secret, et si j’ai baisé ma main de ma bouche;
hivyo moyo wangu kushawishiwa kwa siri, au kubusu mkono wangu kwa kuviheshimu,
28 Ce qui est une iniquité très grande, et nier le Dieu très haut:
basi hiyo pia ingekuwa dhambi ya kuhukumiwa, kwa kuwa ningekuwa si mwaminifu kwa Mungu aishiye juu sana.
29 Si je me suis réjoui de la ruine de celui qui me haïssait, et si j’ai bondi de joie de ce que le malheur l’avait atteint:
“Kama nimeshangilia msiba wa adui yangu, au kutazama kwa furaha taabu iliyomjia,
30 (Car je n’ai pas permis à ma bouche de pécher en cherchant à maudire son âme.)
lakini sikuruhusu kinywa changu kufanya dhambi kwa kuomba laana dhidi ya maisha yake;
31 Si les hommes de ma tente n’ont pas dit: Qui nous donnera de nous rassasier de sa chair?
kama watu wa nyumbani mwangu kamwe hawakusema, ‘Ni nani ambaye hajashibishwa na nyama ya Ayubu?’
32 (L’étranger en effet n’est pas resté dehors; ma porte a toujours été ouverte au voyageur.)
Lakini hakuna mgeni aliyelala njiani, kwa maana mlango wangu ulikuwa wazi kwa msafiri;
33 Si comme homme, j’ai tenu mon péché secret, et si j’ai caché dans mon sein mon iniquité;
kama nimeifunika dhambi yangu kama wanadamu wengine wafanyavyo, kwa kuficha hatia yangu moyoni mwangu,
34 Si j’ai été saisi d’effroi à cause de la grande multitude, et si le mépris de mes reproches m’a épouvanté, et si je ne me suis pas plutôt tenu dans le silence, sans sortir de ma porte:
kwa sababu ya kuogopa umati wa watu, na hivyo kuwa na hofu ya kudharauliwa na jamaa, nikanyamaza kimya nisitoke nje ya mlango:
35 Qui me donnera quelqu’un qui m’entende, afin que le Tout-Puissant écoute mon désir, et que celui qui juge, écrive lui-même un livre,
(“Laiti kama angekuwepo mtu wa kunisikia! Tazama sasa ninatia sahihi kwenye utetezi wangu: Mwenyezi na anijibu; mshtaki wangu na aweke mashtaka yake kwenye maandishi.
36 Afin que sur mon épaule je porte ce livre, et que je le mette comme une couronne autour de ma tête?
Hakika ningeyavaa begani mwangu, ningeyavaa kama taji.
37 À chacun de mes pas j’en prononcerai les paroles, et je le présenterai comme à un prince.
Ningempa hesabu ya kila hatua yangu, ningemwendea kama mwana wa mfalme.)
38 Si la terre qui m’appartient crie contre moi, et que ses sillons pleurent avec elle;
“Kama nchi yangu inalia dhidi yangu, na mifereji yake yote imelowana kwa machozi,
39 Si j’ai mangé ses fruits sans argent, et si j’ai affligé l’âme de ses cultivateurs:
kama nimekula mazao yake bila malipo, au kuvunja mioyo ya wapangaji wake,
40 Qu’au lieu de blé il me naisse des ronces, et au lieu d’orge, des épines.
basi miiba na iote badala ya ngano, na magugu badala ya shayiri.” Mwisho wa maneno ya Ayubu.

< Job 31 >