< Jérémie 52 >

1 Sédécias était âgé de vingt et un ans lorsqu’il commença à régner; et il régna onze ans dans Jérusalem; le nom de sa mère était Amital, fille de Jérémie de Lobna.
Sedekia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mmoja alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka kumi na mmoja. Jina la mama yake aliitwa Hamutali binti Yeremia, kutoka Libna.
2 Il fit le mal sous les yeux du Seigneur, selon tout ce qu’avait fait Joakim.
Alifanya maovu machoni pa Bwana, kama alivyofanya Yehoyakimu.
3 Parce que la fureur du Seigneur était sur Jérusalem et sur Juda, jusqu’à ce qu’il les eût rejetés de devant sa face; et Sédécias se révolta contre le roi de Babylone.
Ilikuwa ni kwa sababu ya hasira ya Bwana haya yote yalitokea Yerusalemu na Yuda, naye mwishoni akawaondoa mbele zake. Basi, Sedekia akaasi dhidi ya mfalme wa Babeli.
4 Or il arriva, la neuvième année de son règne, le dixième. jour du dixième mois, que Nabuchodonosor, roi de Babylone, vint, lui et toute son armée, contre Jérusalem; et ils l’assiégèrent, et ils bâtirent des fortifications autour.
Hivyo katika mwaka wa tisa wa utawala wa Sedekia, katika siku ya kumi ya mwezi wa kumi, Nebukadneza mfalme wa Babeli akiwa na jeshi lake lote alifanya vita dhidi ya Yerusalemu. Wakapiga kambi nje ya mji na kuuzunguka mji pande zote.
5 Et la ville fut assiégée jusqu’à la onzième année du règne de Sédécias.
Mji ulizungukwa na jeshi mpaka mwaka wa kumi na moja wa utawala wa Mfalme Sedekia.
6 Mais au quatrième mois, au neuvième jour, la famine gagna la cité; et il n’y avait plus de vivres pour le peuple de la terre.
Ilipowadia siku ya tisa ya mwezi wa nne, njaa ikazidi kuwa kali sana ndani ya mji, hadi hapakuwa na chakula kwa ajili ya watu.
7 Une brèche fut faite à la cité, et tous ses hommes de guerre s’enfuirent, et sortirent de la cité pendant la nuit par la voie de la porte qui est entre les deux murs, et conduit au jardin du roi, les Chaldéens assiégeant la ville tout autour, et ils s’en allèrent par la voie qui conduit au désert.
Kisha ukuta wa mji ukavunjwa na jeshi lote likakimbia. Wakaondoka mjini usiku kupitia lango lililokuwa kati ya kuta mbili karibu na bustani ya mfalme, ingawa Wakaldayo walikuwa wameuzunguka mji. Wakakimbia kuelekea Araba.
8 Mais l’armée des Chaldéens poursuivit le roi, et ils prirent Sédécias dans le désert qui est près de Jéricho; et tous ceux qui l’accompagnaient s’enfuirent çà et là d’auprès de lui.
Lakini jeshi la Wakaldayo likamfuatia Mfalme Sedekia na kumpata katika sehemu tambarare za Yeriko. Askari wake wote wakatengwa naye na kutawanyika,
9 Et lorsqu’ils eurent pris le roi, ils l’amenèrent au roi de Babylone à Réblatha, qui est dans la terre d’Emath; et Nabuchodonosor lui prononça son arrêt.
naye akakamatwa. Akapelekwa kwa mfalme wa Babeli huko Ribla, katika nchi ya Hamathi, mahali ambapo alimtangazia hukumu.
10 Et le roi de Babylone égorgea les deux fils de Sédécias sous ses yeux, et il fit tuer en même temps tous les princes de Juda à Réblatha.
Huko Ribla mfalme wa Babeli aliwachinja wana wa Sedekia mbele ya macho yake. Pia akawaua maafisa wote wa Yuda.
11 Et il arracha les yeux à Sédécias, et le chargea de fers aux pieds, et le roi de Babylone le conduisit à Babylone, et l’enferma dans la maison de la prison jusqu’au jour de sa mort.
Kisha akayangʼoa macho ya Sedekia, akamfunga kwa pingu za shaba na kumpeleka Babeli, alipomweka gerezani mpaka siku ya kifo chake.
12 Mais au cinquième mois, au dixième jour du mois qui est la dix-neuvième année même dit règne de Nabuchodonosor, roi de Babylone, vint Nabuzardan, chef de la milice, lequel était de service auprès du roi de Babylone, dans Jérusalem.
Mnamo siku ya kumi ya mwezi wa tano, katika mwaka wa kumi na tisa wa utawala wa Nebukadneza mfalme wa Babeli, Nebuzaradani jemadari wa askari walinzi wa mfalme, aliyemtumikia mfalme wa Babeli, alikuja Yerusalemu.
13 Et il brûla la maison du Seigneur, et la maison du roi; et à toutes les maisons de Jérusalem, et à toute grande maison, il mit le feu.
Alichoma moto Hekalu la Bwana, jumba la kifalme, na nyumba zote za Yerusalemu. Aliteketeza kila jengo muhimu.
14 Et tout le mur autour de Jérusalem, l’armée entière des Chaldéens, qui était avec le chef de la milice, l’abattit.
Jeshi lote la Wakaldayo chini ya jemadari wa askari walinzi wa mfalme walivunja kuta zote zilizoizunguka Yerusalemu.
15 Quant à ce qui était demeuré dans la cité d’entre les pauvres du peuple, et d’entre le reste du commun, et d’entre les transfuges qui avaient passé au roi de Babylone, et quant à tout le reste de la multitude, Nabuzardan, prince de la milice, les transféra à Babylone.
Nebuzaradani, jemadari wa askari walinzi, akawapeleka uhamishoni baadhi ya watu maskini sana na wale waliobaki katika mji, pamoja na mabaki ya watu wa kawaida, na wale waliojisalimisha kwa mfalme wa Babeli.
16 Mais d’entre les pauvres de la terre, Nabuzardan, chef de la milice, laissa des vignerons et des laboureurs.
Lakini Nebuzaradani akawaacha mabaki ya wale watu maskini kabisa ili watunze mashamba ya mizabibu na mashamba mengine.
17 Mais les colonnes d’airain qui étaient dans la maison du Seigneur, et les soubassements, et la mer d’airain, qui était dans la maison du Seigneur, les Chaldéens les brisèrent, et ils en emportèrent tout l’airain à Babylone,
Wakaldayo walivunja vipande zile nguzo za shaba, vile vishikilio vya shaba vilivyohamishika, na ile Bahari ya shaba, ambavyo vyote vilikuwa katika Hekalu la Bwana. Hivyo wakaichukua hiyo shaba yote na kuipeleka Babeli.
18 Et les chaudières, et les grandes fourchettes, et les psaltérions, et les tasses, et les petits mortiers, et tous les vases d’airain qui servaient au ministère, ils les emportèrent; et
Wakachukua pia vyungu, masepetu, mikasi ya kusawazishia tambi, mabakuli ya kunyunyizia, sahani na vyombo vyote vya shaba vilivyotumika katika huduma ya Hekalu.
19 Les urnes, et les encensoirs, et les cruches, et les bassins, et les chandeliers, et les mortiers, et les coupes, et tout ce qui était d’argent pur, et tout ce qui était d’or pur, le chef de la milice les emporta;
Jemadari wa askari walinzi wa mfalme akachukua yale masinia, vile vyetezo, yale mabakuli ya kunyunyizia, zile sufuria, vile vinara vya taa, zile sahani na yale mabakuli yaliyotumika kwa sadaka za vinywaji, vitu vyote vile vilivyokuwa vimetengenezwa kwa dhahabu safi au fedha.
20 Ainsi que les deux colonnes, et la mer unique, et les douze bœufs d’airain qui étaient sous les bases, que le roi Salomon avait faites dans la maison du Seigneur; il n’y avait pas de poids pour l’airain de tous ces vases.
Shaba iliyotokana na zile nguzo mbili, ile Bahari na wale mafahali kumi na mawili wa shaba waliokuwa chini yake, pamoja na vile vishikilio vilivyohamishika, ambavyo Mfalme Solomoni alikuwa ametengeneza kwa ajili ya Hekalu la Bwana, ilikuwa na uzito usioweza kupimika.
21 Or l’une des colonnes avait dix-huit coudées de hauteur, un cordon de douze coudées l’environnait; son épaisseur était de quatre doigts, et en dedans elle était creuse.
Kila nguzo ilikuwa na urefu wa dhiraa kumi na nane, kimo chake na mzunguko dhiraa kumi na mbili, na unene wa nyanda nne, na zote zilikuwa wazi ndani.
22 Et sur l’une et l’autre de ces colonnes était un chapiteau d’airain; la hauteur du chapiteau de l’une était de cinq coudées; et des réseaux de grenades étaient sur le couronnement tout autour; le tout était d’airain. Il en était de même pour la seconde colonne qui avait aussi des grenades.
Sehemu ya shaba juu ya ile nguzo moja ilikuwa na urefu wa dhiraa tano, na ilikuwa imepambwa kwa wavu na makomamanga ya shaba kuizunguka kote. Ile nguzo nyingine pamoja na makomamanga yake ilifanana na hiyo ya kwanza.
23 Et quatre-vingt-seize grenades pendaient, et toutes les grenades, au nombre de cent, étaient environnées de réseaux.
Kulikuwa na makomamanga tisini na sita pembeni; jumla ya makomamanga juu ya wavu uliokuwa umezunguka yalikuwa mia moja.
24 Et le maître de la milice prit Saraïas, le premier prêtre, et Sophonias, le second prêtre, et les trois gardiens du vestibule du temple.
Yule jemadari wa askari walinzi akawachukua kama wafungwa Seraya kuhani mkuu, kuhani Sefania aliyefuata kwa cheo, na mabawabu watatu.
25 Et de la cité, il prit un eunuque qui était préposé sur les hommes de guerre, et sept hommes d’entre ceux qui voyaient la face du roi, qui se trouvèrent dans la cité; et le scribe, prince des
Miongoni mwa wale watu waliokuwa wamesalia katika mji, alimchukua afisa kiongozi wa wapiganaji, na washauri saba wa mfalme. Akamchukua pia mwandishi aliyesimamia uandikishaji wa watu wa nchi, pamoja na watu wake sitini waliopatikana ndani ya mji.
26 Or Nabuzardan, chef de la milice, les prit, et les amena au roi de Babylone à Réblatha.
Nebuzaradani jemadari akawachukua hao wote na kuwapeleka kwa mfalme wa Babeli huko Ribla.
27 Et le roi de Babylone les frappa et les tua à Réblatha, dans la terre d’Emath; et Juda fut transféré hors de sa terre.
Huko Ribla, katika nchi ya Hamathi, mfalme wa Babeli akaamuru wanyongwe. Hivyo Yuda wakaenda utumwani, mbali na nchi yao.
28 Voici le peuple que transféra Nabuchodonosor; la septième année de son règne, il transféra trois mille vingt-trois Juifs;
Hii ndiyo hesabu ya watu ambao Nebukadneza aliwachukua kwenda uhamishoni: katika mwaka wa saba, Wayahudi 3,023;
29 La dix-huitième année de son règne, il transféra de Jérusalem huit cent trente-deux âmes.
katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Nebukadneza, watu 832 kutoka Yerusalemu;
30 Et la vingt-troisième année du règne de Nabuchodonosor, Nabuzardan, maître de la milice, transféra sept cent quarante-cinq âmes de Juifs; ainsi toutes les âmes transférées furent au nombre de quatre mille six cents.
katika mwaka wa ishirini na tatu wa utawala wake, Wayahudi 745 walichukuliwa kwenda uhamishoni na Nebuzaradani jemadari wa askari walinzi wa mfalme. Jumla ya watu wote walikuwa 4,600.
31 Et il arriva à la trente-septième année de la transmigration de Joachin, roi de Juda, au douzième mois, au vingt-cinquième jour du mois, qu’Evilmérodach, roi de Babylone, la première année même de son règne, releva la tête de Joachin, roi de Juda, et le fit sortir de la maison de la prison.
Katika mwaka wa thelathini na saba tangu Yehoyakini mfalme wa Yuda apelekwe uhamishoni, katika mwaka ule ambao Evil-Merodaki alifanyika mfalme wa Babeli, alimwacha huru Yehoyakini mfalme wa Yuda, na kumfungua kutoka gerezani siku ya ishirini na tano ya mwezi wa kumi na mbili.
32 Et il lui parla avec bonté, et il mit son trône au-dessus des trônes des rois qui étaient au-dessous de lui à Babylone.
Alizungumza naye kwa upole na kumpa kiti cha heshima zaidi kuliko wale wafalme wengine aliokuwa nao huko Babeli.
33 Et il changea ses vêtements de sa prison, et Joachin mangeait du pain devant lui tous les jours de sa vie.
Hivyo Yehoyakini akayavua mavazi yake ya mfungwa, na siku zote za maisha yake zilizobaki alikula mezani mwa mfalme.
34 Et sa nourriture, nourriture perpétuelle, lui était donnée par le roi de Babylone, déterminée jour par jour, jusqu’au jour de sa mort, tous les jours de sa vie.
Siku kwa siku mfalme wa Babeli alimpa Yehoyakini posho siku zote za maisha yake, hadi siku ya kifo chake.

< Jérémie 52 >