< Jérémie 48 >

1 À Moab, voici ce que dit le Seigneur des armées, Dieu d’Israël: Malheur à Nabo, parce qu’elle a été dévastée et couverte de confusion; Cariathaïm a été prise; la forte a été couverte de confusion, et elle a tremblé,
Kuhusu Moabu: Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: “Ole wake Nebo, kwa maana utaharibiwa. Kiriathaimu utaaibishwa na kutekwa; Misgabu itaaibishwa na kuvunjavunjwa.
2 Il n’y a plus d’exultation dans Moab contre Hésébon; ses ennemis ont conspiré. Venez, et perdons-la entièrement comme nation; ainsi tu garderas un silence absolu, et le glaive te suivra.
Moabu haitasifiwa tena; huko Heshboni watu watafanya shauri baya la anguko lake: ‘Njooni na tuangamize taifa lile.’ Wewe nawe, ee Madmena, utanyamazishwa; upanga utakufuatia.
3 Voix de clameur qui s’élève d’Oronaïm: dévastation et grande destruction.
Sikiliza kilio kutoka Horonaimu, kilio cha maangamizi makuu na uharibifu.
4 Moab est brisée, annoncez un cri à ses petits enfants.
Moabu utavunjwa, wadogo wake watapiga kelele.
5 Par la montée de Luith, gémissant, elle montera en pleur, parce qu’à la descente d’Oronaïm les ennemis ont entendu un hurlement de destruction:
Wanapanda kwenda njia ya kuelekea Luhithi, wakilia kwa uchungu wanapotembea, kwenye njia inayoshuka kwenda Horonaimu, kilio cha uchungu kwa ajili ya uharibifu kinasikika.
6 Fuyez, sauvez vos âmes; et vous serez comme des bruyères dans le désert.
Kimbieni! Okoeni maisha yenu, kuweni kama kichaka jangwani.
7 Parce que tu as eu confiance dans tes fortifications et dans tes trésors, toi aussi tu seras prise; et Chamos émigrera, et ses prêtres et ses princes en même temps.
Kwa kuwa mmetumainia matendo yenu na mali zenu, ninyi pia mtachukuliwa mateka, naye Kemoshi atakwenda uhamishoni, pamoja na makuhani wake na maafisa wake.
8 Et viendra un spoliateur dans toutes les villes, et nulle ville ne sera sauvée; et les vallées périront, et les campagnes seront ravagées, parce que l’a dit le Seigneur.
Mharabu atakuja dhidi ya kila mji, wala hakuna mji utakaookoka. Bonde litaangamizwa na uwanda utaharibiwa, kwa sababu Bwana amesema.
9 Donnez une fleur à Moab, parce qu’elle sortira florissante, et ses cités seront désertes et inhabitables.
Wekeni chumvi kwa ajili ya Moabu, kwa kuwa ataangamizwa; miji yake itakuwa ukiwa, pasipo kuwa na mtu atakayeishi ndani yake.
10 Maudit celui qui fait l’œuvre du Seigneur frauduleusement; et maudit celui qui empêche son glaive de verser le sang.
“Alaaniwe yeye afanyaye kazi ya Bwana kwa hila! Alaaniwe yeye auzuiaye upanga wake usimwage damu!
11 Moab dès sa jeunesse a été fertile, et il s’est reposé sur sa lie; il n’a pas été versé d’un vase dans un autre vase, et il n’a pas émigré; c’est pour cela que son goût lui est toujours demeuré, et que son parfum n’est point changé.
“Moabu amestarehe tangu ujana wake, kama divai iliyoachwa kwenye machujo yake, haikumiminwa kutoka chombo kimoja hadi kingine, hajaenda uhamishoni. Kwa hiyo ana ladha ile ile kama aliyokuwa nayo, nayo harufu yake haijabadilika.
12 À cause de cela, voici que des jours viennent, dit le Seigneur, et je lui enverrai des hommes qui disposeront et renverseront ses bouteilles, et ils le renverseront lui-même, et videront ses vases, et briseront ses bouteilles.
Lakini siku zinakuja,” asema Bwana, “nitakapotuma watu wamiminao kutoka kwenye magudulia, nao watamimina; wataacha magudulia yake yakiwa matupu na kuvunja mitungi yake.
13 Et Moab sera couvert de confusion, à cause de Chamos, comme a été couverte de confusion la maison d’Israël, à cause de Béthel en qui elle avait confiance.
Kisha Moabu atamwonea aibu mungu wao Kemoshi, kama vile nyumba ya Israeli walivyoona aibu walipotegemea mungu wa Betheli.
14 Comment dites-vous: Nous sommes braves, et des hommes robustes pour combattre?
“Mwawezaje kusema, ‘Sisi ni mashujaa, watu jasiri katika vita’?
15 Moab a été dévastée, ses cités ont été renversées; l’élite de ses jeunes hommes a succombé dans le carnage, dit le roi, dont le nom est le Seigneur des armées.
Moabu ataangamizwa na miji yake itavamiwa, vijana wake waume walio bora sana watachinjwa,” asema Mfalme, ambaye jina lake ni Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote.
16 La destruction de Moab est près d’arriver, et sa ruine accourra extrêmement vite.
“Kuanguka kwa Moabu kumekaribia, janga kubwa litamjia kwa haraka.
17 Consolez-le, vous tous qui êtes autour de lui; et vous tous qui savez son nom, dites: Comment a été brisée une verge puissante, un bâton glorieux?
Ombolezeni kwa ajili yake, ninyi nyote mnaomzunguka, ninyi nyote mnaojua sifa zake, semeni, ‘Tazama jinsi ilivyovunjika fimbo ya kifalme yenye nguvu, tazama jinsi ilivyovunjika fimbo iliyotukuka!’
18 Descends de la gloire, assieds-toi dans la soif, habitante de la fille de Dibon; parce que le dévastateur de Moab monte vers toi, il a détruit tes fortifications.
“Shuka kutoka fahari yako na uketi katika ardhi iliyokauka, enyi wenyeji wa Binti wa Diboni, kwa maana yeye aangamizaye Moabu atakuja dhidi yako, na kuangamiza miji yako iliyozungushiwa maboma.
19 Tiens-toi sur la voie, et fais le guet, habitante d’Aroër; interroge celui qui s’est enfui, et à celui qui s’est sauvé, dis: Qu’est-il arrivé?
Simama kando ya barabara na utazame, wewe unayeishi Aroeri. Muulize mwanaume anayekimbia na mwanamke anayetoroka, waulize, ‘Kumetokea nini?’
20 Moab a été couvert de confusion, parce qu’il a été vaincu; hurlez et criez; annoncez sur l’Arnon que Moab a été dévastée.
Moabu amefedheheshwa, kwa kuwa amevunjavunjwa. Lieni kwa huzuni na kupiga kelele! Tangazeni kando ya Arnoni kwamba Moabu ameangamizwa.
21 Et le jugement du Seigneur est venu jusqu’à la terre de la plaine; sur Hélon, sur Jasa, et sur Méphaath,
Hukumu imefika kwenye uwanda wa juu: katika Holoni, Yahasa na Mefaathi,
22 Et sur Dibon, et sur Nabo, et sur la maison de Déblathaïm,
katika Diboni, Nebo na Beth-Diblathaimu,
23 Et sur Cariathaïm, et sur Bethgamul, et sur Bethmaon.
katika Kiriathaimu, Beth-Gamuli na Beth-Meoni,
24 Et sur Carioth, et sur Bosra, et sur toutes les cités de la terre de Moab qui sont loin et qui sont près.
katika Keriothi na Bosra; kwa miji yote ya Moabu, iliyoko mbali na karibu.
25 La corne de Moab a été arrachée, et son bras a été rompu, dit le Seigneur.
Pembe ya Moabu imekatwa, mkono wake umevunjwa,” asema Bwana.
26 Enivrez-le, parce qu’il s’est élevé contre le Seigneur; Moab se heurtera la main en tombant dans son vomissement, et il sera un objet de dérision, lui aussi.
“Mlevye, kwa kuwa amemdharau Bwana. Moabu na agaegae katika matapishi yake, yeye na awe kitu cha dhihaka.
27 Car Israël a été un objet de dérision pour toi, comme si tu l’avais trouvé parmi des voleurs; à cause donc de tes paroles que tu as dites contre lui, tu seras mené captif.
Je, Israeli hakuwa kitu chako cha kudhihakiwa? Je, alikamatwa miongoni mwa wezi, kiasi cha kutikisa kichwa chako kwa dharau kila mara unapozungumza juu yake?
28 Abandonnez les cités, et habitez dans la pierre, habitants de Moab; et soyez comme la colombe qui fait son nid dans la plus haute ouverture d’un rocher.
Ondokeni kwenye miji yenu, mkaishi katikati ya miamba, enyi mnaoishi Moabu. Kuweni kama huwa ambaye hutengeneza kiota chake kwenye mdomo wa pango.
29 Nous avons appris l’orgueil de Moab (il est superbe à l’excès), sa hauteur et son arrogance, et son orgueil, et la fierté de son cœur.
“Tumesikia juu ya kiburi cha Moabu: kutakabari kwake kwa kiburi na majivuno, kiburi chake na ufidhuli wake, na kujivuna kwa moyo wake.
30 Moi, je sais, dit le Seigneur, sa jactance, et que sa force n’y répond pas, et que ce qui n’était pas selon son pouvoir, elle s’est efforcée de le faire.
Ninaujua ujeuri wake, lakini ni bure,” asema Bwana, “nako kujisifu kwake hakumsaidii chochote.
31 C’est pour cela que sur Moab je pleurerai, et que j’adresserai mes cris à Moab tout entière, et aux hommes de mur de briques qui se lamentent.
Kwa hiyo namlilia Moabu, kwa ajili ya Moabu yote ninalia, ninaomboleza kwa ajili ya watu wa Kir-Haresethi.
32 Du pleur de Jazer, je te pleurerai, vigne de Sabama; tes rejetons ont passé la mer, et ils sont parvenus jusqu’à la mer de Jazer; sur ta moisson et sur ta vendange un voleur s’est précipité.
Ninalia machozi kwa ajili yenu, kama Yazeri aliavyo, enyi mizabibu ya Sibma. Matawi yako yameenea hadi baharini; yamefika hadi bahari ya Yazeri. Mharabu ameyaangukia matunda yako yaliyoiva na mizabibu yako iliyoiva.
33 L’allégresse et l’exultation ont été enlevées au Carmel et à la terre de Moab, et j’ai emporté le vin des pressoirs; et le pressureur du raisin ne chantera plus sa chanson accoutumée.
Shangwe na furaha vimetoweka kutoka bustani na mashamba ya Moabu. Nimekomesha kutiririka kwa divai kutoka mashinikizo; hakuna hata mmoja ayakanyagaye kwa kelele za shangwe. Ingawa kuna kelele, sio kelele za shangwe.
34 Par un cri qui a retenti depuis Hésébon jusqu’à Eléalé et jusqu’à Jasa, ils ont fait entendre leur voix de Ségor, génisse de trois ans, à Oronaïm; les eaux même de Nemrim seront très mauvaises.
“Sauti ya kilio chao inapanda kutoka Heshboni hadi Eleale na Yahazi, kutoka Soari hadi Horonaimu na Eglath-Shelishiya, kwa kuwa hata maji ya Nimrimu yamekauka.
35 Et j’ôterai de Moab, dit le Seigneur, et celui qui fait des oblations sur les hauteurs, et celui qui sacrifie à ses dieux.
Nitakomesha wale wote katika Moabu watoao sadaka mahali pa juu, na kufukiza uvumba kwa miungu yao,” asema Bwana.
36 C’est pour cela que mon cœur sur Moab retentira comme une flûte; et mon cœur sur les hommes de mur de briques donnera un son de flûte; parce qu’il a fait plus qu’il ne pouvait, c’est pour cela qu’ils ont péri.
“Kwa hiyo moyo wangu unaomboleza kwa ajili ya Moabu kama filimbi; unaomboleza kama filimbi kwa ajili ya watu wa Kir-Haresethi. Utajiri waliojipatia umetoweka.
37 Car toute tête sera chauve, et toute barbe sera rasée; à toutes les mains il y aura un lien, et sur tout dos un cilice.
Kila kichwa kimenyolewa na kila mwenye ndevu zimekatwa; kila mkono umekatwa na kila kiuno kimefunikwa kwa nguo ya gunia.
38 Sur tous les toits de Moab, et dans toutes ses places, on entendra toute sorte de pleurs, parce que j’ai brisé Moab comme un vase inutile, dit le Seigneur.
Juu ya mapaa yote katika Moabu na katika viwanja hakuna kitu chochote isipokuwa maombolezo, kwa kuwa nimemvunja Moabu kama gudulia ambalo hakuna mtu yeyote anayelitaka,” asema Bwana.
39 Comment a-t-elle été vaincue, et ont-ils poussé des hurlements? comment Moab a-t-il baissé la tête et a-t-il été couvert de confusion? Et Moab sera un objet de dérision et un exemple pour tous autour de lui.
“Tazama jinsi alivyovunjikavunjika! Jinsi wanavyolia kwa huzuni! Tazama jinsi Moabu anavyogeuka kwa aibu! Moabu amekuwa kitu cha kudhihakiwa, kitu cha kutisha kwa wale wote wanaomzunguka.”
40 Voici ce que dit le Seigneur: Comme l’aigle il volera, et il étendra ses ailes vers Moab.
Hili ndilo asemalo Bwana: “Tazama! Tai anashuka chini, akitanda mabawa yake juu ya Moabu.
41 Carioth a été prise, les fortifications ont été emportées; et le cœur des forts de Moab sera en ce jour-là comme le cœur d’une femme en travail.
Miji itatekwa na ngome zake zitatwaliwa. Katika siku hiyo, mioyo ya mashujaa wa Moabu itakuwa kama moyo wa mwanamke katika utungu wa kuzaa.
42 Et Moab cessera d’être un peuple, parce que contre le Seigneur il s’est glorifié.
Moabu ataangamizwa kama taifa kwa sababu amemdharau Bwana.
43 L’effroi, et la fosse, et le lacs pour toi, ô habitant de Moab, dit le Seigneur.
Hofu kuu, shimo na mtego vinawangojea, enyi watu wa Moabu,” asema Bwana.
44 Qui aura fui à la face de l’effroi tombera dans la fosse, et qui sera monté de la fosse sera pris dans le lacs; car j’amènerai sur Moab l’année de leur visite, dit le Seigneur.
“Yeyote atakayeikimbia hiyo hofu kuu ataanguka ndani ya shimo, yeyote atakayepanda kutoka shimoni, atanaswa katika mtego, kwa sababu nitaletea Moabu mwaka wa adhabu yake,” asema Bwana.
45 À l’ombre d’Hésébon se sont arrêtés ceux qui fuyaient le lacs; mais un feu est sorti d’Hésébon, et une flamme du milieu de Séhon, et elle a dévoré une partie de Moab, et le sommet des fils du tumulte.
“Katika kivuli cha Heshboni, wakimbizi wamesimama pasipo msaada, kwa kuwa moto umezimika huko Heshboni, mwali wa moto kutoka katikati ya Sihoni; unaunguza vipaji vya nyuso za Moabu, mafuvu yao wenye kujivuna kwa kelele.
46 Malheur à toi, Moab! tu as péri, peuple de Chamos: tes fils ont été pris, ainsi que tes filles, pour la captivité.
Ole wako, ee Moabu! Watu wa Kemoshi wameangamizwa; wana wako wamepelekwa uhamishoni na binti zako wamechukuliwa mateka.
47 Mais je ramènerai les captifs de Moab dans les derniers jours, dit le Seigneur. Jusqu’ici les jugements contre Moab.
“Lakini nitarudisha mateka wa Moabu, katika siku zijazo,” asema Bwana. Huu ndio mwisho wa hukumu juu ya Moabu.

< Jérémie 48 >