< Jérémie 29 >

1 Et voici les paroles de la lettre que Jérémie le prophète envoya de Jérusalem aux restes des anciens de la transmigration, et aux prêtres, et aux prophètes, et à tout le peuple que Nabuchodonosor avait fait passer de Jérusalem à Babylone.
Haya ndiyo maneno ya ile barua ambayo nabii Yeremia aliituma kutoka Yerusalemu kwenda kwa wazee waliobaki miongoni mwa wale waliohamishwa, na kwa makuhani, manabii na watu wengine wote ambao Nebukadneza alikuwa amewachukua kwenda uhamishoni Babeli kutoka Yerusalemu.
2 Après que le roi Jéchonias fut sorti de Jérusalem, ainsi que la reine, et les eunuques, et les princes de Juda et de Jérusalem, et l’artisan, et le lapidaire;
(Hii ilikuwa ni baada ya Mfalme Yekonia na malkia mamaye, maafisa wa mahakama, viongozi wa Yuda na wa Yerusalemu, mafundi na wahunzi kwenda uhamishoni kutoka Yerusalemu.)
3 Par l’entremise d’Elasa, fils de Saphan, et par Gamarias, fils d’Helcias, que Sédécias, roi de Juda, envoya à Nabuchodonosor, roi de Babylone, à Babylone, Jérémie, disait:
Barua ilikabidhiwa kwa Elasa mwana wa Shafani, na kwa Gemaria mwana wa Hilkia, ambao Sedekia mfalme wa Yuda aliwatuma kwa Mfalme Nebukadneza huko Babeli. Barua yenyewe ilisema:
4 Voici ce que dit le Seigneur des armées, Dieu d’Israël, à tous les fils de la transmigration que j’ai transférés de Jérusalem à Babylone:
Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, awaambialo wale wote niliowapeleka kutoka Yerusalemu kwenda uhamishoni Babeli:
5 Bâtissez des maisons, et habitez-les; plantez des jardins et mangez-en les fruits;
“Jengeni nyumba na mstarehe, pandeni bustani na mle mazao yake.
6 Prenez des femmes, et engendrez des fils et des filles; donnez à vos fils des femmes, et donnez vos filles à des maris, et qu’elles enfantent des fils et des filles; et multipliez-vous là, et ne soyez pas en petit nombre.
Oeni wake na mzae wana na binti, waozeni wana wenu wake, nanyi watoeni binti zenu waolewe, ili nao pia wazae wana na binti. Ongezekeni idadi yenu huko, wala msipungue.
7 Et recherchez la paix de la cité dans laquelle je vous ai fait émigrer, et priez pour elle le Seigneur, parce que dans sa paix sera votre paix.
Pia tafuteni amani na mafanikio ya mji ambamo nimewapeleka uhamishoni. Mwombeni Bwana kwa ajili ya mji huo, kwa sababu ukistawi, ninyi pia mtastawi.”
8 Car voici ce que dit le Seigneur des armées. Dieu d’Israël: Qu’ils ne vous séduisent pas, vos prophètes qui sont au milieu de vous, et vos devins; et ne faites pas attention aux songes que vous songez;
Naam, hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: “Msikubali manabii na wabashiri walioko miongoni mwenu wawadanganye. Msisikilize ndoto ambazo mmewatia moyo kuota.
9 Parce que c’est faussement qu’eux vous prophétisent en mon nom, et je ne les ai point envoyés, dit le Seigneur,
Wanawatabiria ninyi uongo kwa jina langu. Sikuwatuma,” asema Bwana.
10 Parce que voici ce que dit le Seigneur: Lorsque soixante-dix ans auront commencé d’être accomplis à Babylone, je vous visiterai; et je réaliserai pour vous ma bonne parole en vous ramenant en ce lieu.
Hili ndilo asemalo Bwana: “Miaka sabini itakapotimia kwa ajili ya Babeli, nitakuja kwenu na kutimiza ahadi yangu ya rehema ya kuwarudisha mahali hapa.
11 Car moi, je sais les pensées que je pense sur vous, dit le Seigneur, pensées de paix et non d’affliction: c’est de vous accorder la fin de vos maux et la patience.
Kwa maana ninajua mipango niliyo nayo kwa ajili yenu,” asema Bwana, “ni mipango ya kuwafanikisha na wala si ya kuwadhuru, ni mipango ya kuwapa tumaini katika siku zijazo.
12 Et vous m’invoquerez, et vous partirez; vous me prierez, et moi je vous exaucerai.
Kisha mtaniita, na mtakuja na kuniomba, nami nitawasikiliza.
13 Vous me chercherez et vous me trouverez, lorsque vous m’aurez cherché de tout votre cœur.
Mtanitafuta na kuniona, mtakaponitafuta kwa moyo wenu wote.
14 Et je serai trouvé par vous, dit le Seigneur; et je vous ramènerai vos captifs, et je vous rassemblerai du milieu de toutes les nations et de tous les lieux dans lesquels je vous ai chassés, dit le Seigneur; et je vous ferai revenir du lieu dans lequel je vous ai fait émigrer,
Nitaonekana kwenu,” asema Bwana, “nami nitawarudisha watu wenu waliotekwa. Nitawakusanya kutoka mataifa yote na mahali pote nilipokuwa nimewafukuzia, nami nitawarudisha mahali ambapo nilikuwa nimewatoa walipochukuliwa uhamishoni,” asema Bwana.
15 Parce que vous avez dit: Le Seigneur a suscité pour nous des prophètes à Babylone.
Mnaweza mkasema, “Bwana ameinua manabii kwa ajili yetu huku Babeli,”
16 Parce que voici ce que dit le Seigneur au roi qui est assis sur le trône de David, et à tout le peuple habitant de cette ville, à vos frères qui ne sont pas allés avec vous en captivité.
lakini hili ndilo asemalo Bwana kuhusu mfalme aketiaye kiti cha enzi cha Daudi, na watu wa kwenu wote wanaobaki katika mji huu, ndugu zenu ambao hawakwenda pamoja nanyi uhamishoni.
17 Voici ce que dit le Seigneur des armées: Voilà, j’enverrai contre eux le glaive, la famine et la peste, et je les rendrai comme des figues mauvaises, qui ne peuvent être mangées, parce qu’elles sont très mauvaises.
Naam, hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Nitatuma upanga, njaa na tauni dhidi yao, nami nitawafanya kuwa kama tini dhaifu zile ambazo ni mbovu sana zisizofaa kuliwa.
18 Et je les poursuivrai par le glaive, et par la famine, et par la peste; et je les livrerai en vexation à tous les royaumes de la terre; en malédiction, et en stupeur, et en sifflement, et en opprobre, à toutes les nations chez lesquelles moi-même je les ai chassés;
Nitawafukuza kwa upanga, kwa njaa na kwa tauni, nami nitawafanya kitu cha kuchukiza sana kwa falme zote za dunia, na kuwa kitu cha laana na cha kuogofya, cha dharau na kukemewa, miongoni mwa mataifa yote nitakakowafukuzia.
19 Parce qu’ils n’ont pas écouté mes paroles, dit le Seigneur, que je leur ai adressées par mes serviteurs les prophètes, me levant durant la nuit, et les envoyant; et vous ne m’avez pas écouté, dit le Seigneur.
Kwa kuwa hawakuyasikiliza maneno yangu,” asema Bwana, “maneno ambayo niliwatumia tena na tena kupitia watumishi wangu manabii. Wala ninyi watu wa uhamisho hamkusikiliza pia,” asema Bwana.
20 Vous donc, écoutez la parole du Seigneur, vous tous, fils de la transmigration, que j’ai envoyés de Jérusalem à Babylone.
Kwa hiyo, sikieni neno la Bwana, enyi nyote mlio uhamishoni, niliowapeleka Babeli kutoka Yerusalemu.
21 Voici ce que dit le Seigneur des armées. Dieu d’Israël, à Achab, fils de Colias, et à Sédécias, fils de Maasias, qui vous prophétisent en mon nom le mensonge: Voilà que moi je les livrerai aux mains de Nabuchodonosor, roi de Babylone, et il les frappera sous vos yeux.
Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo kuhusu Ahabu mwana wa Kolaya, na Sedekia mwana wa Maaseya, wanaowatabiria uongo kwa jina langu: “Nitawatia mikononi mwa Nebukadneza mfalme wa Babeli, naye atawaua mbele ya macho yenu hasa.
22 Et ils seront pris comme exemple de malédiction par tous les fils de la transmigration de Juda qui sont à Babylone, et qui diront: Que le Seigneur te traite comme Sédécias et comme Achab, que le roi de Babylone a fait griller au feu,
Kwa ajili yao, watu wote wa uhamisho kutoka Yuda walioko Babeli watatumia laana hii: ‘Bwana na akutendee kama Sedekia na Ahabu, ambao mfalme wa Babeli aliwachoma kwa moto.’
23 Parce qu’ils ont fait une folie dans Israël, et qu’ils ont commis l’adultère avec les femmes de leurs amis, et qu’ils ont dit faussement en mon nom ce que je ne leur ai pas commandé; c’est moi qui suis le juge et le témoin, dit le Seigneur.
Kwa kuwa wamefanya mambo maovu kabisa katika Israeli, wamezini na wake za majirani zao, tena kwa Jina langu wamesema uongo, mambo ambayo sikuwaambia kuyafanya. Nami nayajua haya, na ni shahidi wa jambo hilo,” asema Bwana.
24 Et tu diras à Séméias, le Néhélamite:
Mwambie Shemaya Mnehelami,
25 Voici ce que dit le Seigneur des armées, Dieu d’Israël: Parce que tu as envoyé des lettres en ton nom à tout le peuple qui est dans Jérusalem et à Sophonias, fils de Maasias et prêtre, et à tous les prêtres, disant:
“Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: Ulituma barua kwa jina lako mwenyewe kwa watu wote wa Yerusalemu, kwa Sefania mwana wa kuhani Maaseya na kwa makuhani wengine wote. Ulimwambia Sefania,
26 Le Seigneur t’a établi prêtre à la place du pontife Joïada, afin que tu sois chef dans la maison du Seigneur, ayant autorité sur tout, homme saisi d’une fureur prophétique, et prophétisant, afin que tu le mettes dans les fers et dans la prison.
‘Bwana amekuweka wewe uwe kuhani badala ya Yehoyada ili uwe msimamizi wa nyumba ya Bwana. Unapaswa kufunga kwa mikatale na mnyororo wa shingoni mwendawazimu yeyote anayejifanya nabii.
27 Et maintenant pourquoi n’as-lu pas repris Jérémie, l’Anathothite, qui vous prophétise?
Kwa nini basi hukumkemea Yeremia Mwanathothi, aliyejifanya kama nabii miongoni mwenu?
28 Parce qu’outre cela, il a envoyé vers nous à Babylone, disant: C’est long; bâtissez des maisons et habitez-les, et plantez des jardins, et mangez-en les fruits.
Ametutumia ujumbe huu huku Babeli: Mtakuwako huko muda mrefu. Kwa hiyo jengeni nyumba mkakae; pandeni mashamba na mle mazao yake.’”
29 Sophonias le prêtre lut donc cette lettre aux oreilles de Jérémie le prophète.
Kuhani Sefania, hata hivyo, akamsomea nabii Yeremia ile barua.
30 Et la parole du Seigneur fut adressée à Jérémie, disant:
Ndipo neno la Bwana likamjia Yeremia kusema:
31 Envoie vers tous les fils de la transmigration, disant: Voici ce que dit le Seigneur à Séméias, le Néhélamite: Parce que Séméias a prophétisé, et que moi je ne l’ai pas envoyé; et qu’il vous a fait vous confier dans un mensonge;
“Tuma ujumbe huu kwa watu wote walio uhamishoni: ‘Hili ndilo Bwana asemalo kuhusu Shemaya Mnehelami: Kwa sababu Shemaya amewatabiria ninyi, hata ingawa sikumtuma, naye amewafanya kuamini uongo,
32 C’est pour cela que voici ce que dit le Seigneur: Voilà que moi je visiterai Séméias le Néhélamite et sa race; il n’aura pas d’homme de sa race assis au milieu de ce peuple, et il ne verra pas le bien que moi je ferai à mon peuple, dit le Seigneur, parce qu’il a proféré des paroles de prévarication contre le Seigneur.
hili ndilo Bwana asemalo: Hakika nitamwadhibu Shemaya Mnehelami pamoja na uzao wake. Hapatakuwa na yeyote atakayebaki miongoni mwa watu hawa, wala hataona mema nitakayowatendea watu wangu, asema Bwana, kwa sababu ametangaza uasi dhidi yangu.’”

< Jérémie 29 >