< Jérémie 25 >
1 Parole qui fut adressée à Jérémie touchant tout le peuple de Juda, en la quatrième année de Joakim, fils de Josias, roi de Juda, qui est la première année de Nabuchodonosor, roi de Babylone;
Neno likamjia Yeremia kuhusu watu wote wa Yuda, katika mwaka wa nne wa utawala wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, ambao ulikuwa mwaka wa kwanza wa utawala wa Nebukadneza mfalme wa Babeli.
2 Et que Jérémie, le prophète, annonça à tout le peuple de Juda, et à tous les habitants de Jérusalem, disant:
Hivyo nabii Yeremia akawaambia watu wote wa Yuda na wale wote waishio Yerusalemu:
3 Depuis la treizième année de Josias, fils d’Ammon, roi de Juda, jusqu’à ce jour, c’est la vingt-troisième année; la parole du Seigneur m’a été adressée, et je vous ai parlé, me levant durant la nuit et parlant, et vous ne m’avez pas écouté.
Kwa miaka ishirini na mitatu, kuanzia mwaka wa kumi na tatu wa utawala wa Yosia mwana wa Amoni mfalme wa Yuda, hadi siku hii ya leo, neno la Bwana limekuwa likinijia, nami nimesema nanyi mara kwa mara, lakini hamkusikiliza.
4 Et le Seigneur a envoyé vers vous tous ses serviteurs les prophètes, se levant au point du jour, et les envoyant; et vous n’avez pas écouté, et vous n’avez pas incliné vos oreilles afin d’écouter,
Ingawa Bwana amewatuma watumishi wake wote hao manabii kwenu mara kwa mara, hamkusikiliza wala hamkujali.
5 Lorsqu’il disait: Revenez chacun de votre voie mauvaise, et de vos très mauvaises pensées; et vous habiterez dans la terre que le Seigneur vous a donnée, à vous et à vos pères, de siècle en siècle.
Walisema, “Geukeni sasa, kila mmoja wenu kutoka njia yake mbaya na matendo yake maovu, ndipo mtaweza kukaa katika nchi ambayo Bwana aliwapa ninyi na baba zenu milele.
6 Et n’allez pas à la suite de dieux étrangers, afin de les servir et de les adorer; ne me provoquez pas au courroux par les œuvres de vos mains, et je ne vous affligerai point.
Msiifuate miungu mingine ili kuitumikia na kuiabudu. Msinikasirishe kwa vitu ambavyo mmevitengeneza kwa mikono yenu.”
7 Et vous ne m’avez pas écouté, dit le Seigneur, en sorte que vous m’avez provoqué au courroux par les œuvres de vos mains, pour votre malheur.
“Lakini ninyi hamkunisikiliza mimi, tena mkanikasirisha kwa vitu mlivyovitengeneza kwa mikono yenu, nanyi mmejiletea madhara juu yenu wenyewe,” asema Bwana.
8 À cause de cela, voici ce que dit le Seigneur des armées: À cause de ce que vous n’avez pas écouté mes paroles,
Kwa hiyo Bwana Mwenye Nguvu Zote asema hivi: “Kwa sababu hamkuyasikiliza maneno yangu,
9 Voilà que moi j’enverrai et que je prendrai toutes les familles de l’aquilon, dit le Seigneur, et Nabuchodonosor, roi de Babylone, mon serviteur; et je les amènerai sur cette terre et sur ses habitants, et sur toutes les nations qui sont autour d’elle; et je les perdrai, et j’en ferai un objet de stupeur et de sifflement, et je les réduirai à des solitudes éternelles.
nitayaita mataifa yote ya kaskazini na mtumishi wangu Nebukadneza mfalme wa Babeli,” asema Bwana. “Nitawaleta waishambulie nchi hii na wakazi wake wote, na dhidi ya mataifa yote yanayowazunguka. Nitawaangamiza kabisa na kuwafanya kitu cha kuchukiwa na kudharauliwa, na kuwa magofu daima.
10 Et je ferai cesser parmi eux la voix de la joie et la voix de l’allégresse, la voix de l’époux et la voix de l’épouse, la voix de la meule et la lumière de la lampe.
Nitawaondolea sauti ya shangwe na furaha, sauti ya bibi na bwana arusi, sauti ya mawe ya kusagia, na mwanga wa taa.
11 Et toute cette terre sera une solitude et un objet de stupeur; et toutes ces nations serviront le roi de Babylone durant soixante et dix ans.
Nchi hii yote itakuwa ukiwa na isiyofaa kitu, nayo mataifa haya yatamtumikia mfalme wa Babeli kwa miaka sabini.”
12 Et lorsque les soixante et dix années seront accomplies, je visiterai le roi de Babylone, et cette nation, dit le Seigneur, et leur iniquité, et la terre des Chaldéens; et j’en ferai des solitudes éternelles.
“Lakini miaka sabini itakapotimia, nitamwadhibu mfalme wa Babeli na taifa lake na nchi ya Wakaldayo kwa ajili ya hatia yao,” asema Bwana. “Nitaifanya kuwa ukiwa milele.
13 Et j’amènerai sur cette terre toutes mes paroles que j’ai dites contre elle, tout ce qui a été écrit dans ce livre, toutes les choses qu’a prophétisées Jérémie contre toutes les nations;
Nitaleta juu ya nchi hiyo mambo yote niliyosema dhidi yake, yote yaliyoandikwa katika kitabu hiki, na kutolewa unabii na Yeremia dhidi ya mataifa yote.
14 Parce qu’elles les ont servis, quoique ce fussent des nations nombreuses et de grands rois; et je leur rendrai selon leurs œuvres, et selon les ouvrages de leurs mains.
Wao wenyewe watakuwa watumwa wa mataifa mengi na wafalme wakuu. Nitawalipizia sawasawa na matendo yao na kazi ya mikono yao.”
15 Parce qu’ainsi dit le Seigneur des armées, Dieu d’Israël: Prends ce calice de vin de fureur de ma main, et tu en feras boire à toutes les nations vers lesquelles moi je t’enverrai.
Hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, aliloniambia: “Chukua kutoka mkononi mwangu kikombe hiki kilichojaa divai ya ghadhabu yangu, na kuyanywesha mataifa yote ambayo ninakutuma kwao.
16 Et elles boiront, et elles seront troublées, et elles perdront le sens à la face du glaive que moi j’enverrai parmi elles.
Watakapoinywa, watapepesuka na kukasirika sana kwa sababu ya upanga nitakaoupeleka katikati yao.”
17 Et je reçus le calice de la main du Seigneur, et j’en fis boire à toutes les nations vers lesquelles m’a envoyé le Seigneur:
Hivyo nikakichukua kikombe kutoka mkononi mwa Bwana, na kuyafanya mataifa yote aliyonituma kwao kukinywa:
18 À Jérusalem et aux cités de Juda, et à ses rois, et à ses princes; afin d’en faire un désert, et un objet de stupeur et de sifflement, et de malédiction, comme c’est en ce jour;
Yaani Yerusalemu na miji ya Yuda, wafalme wake na maafisa wake, kuwafanya magofu na kuwa kitu cha kuchukiza, cha dhihaka na laana, kama walivyo leo;
19 À Pharaon, roi d’Egypte, et à ses serviteurs, et à ses princes, et à tout son peuple;
pia Farao mfalme wa Misri, watumishi wake, maafisa wake na watu wake wote,
20 Et à tous généralement: à tous les rois de la terre d’Ausite, et à tous les rois de la terre des Philistins, et à Ascalon, et à Gaza, et à Accaron, et aux restes d’Azot;
pia wageni wote walioko huko; wafalme wote wa nchi ya Usi; wafalme wote wa Wafilisti (wale wa Ashkeloni, Gaza, Ekroni na watu walioachwa huko Ashdodi);
21 Et à l’Idumée, et à Moab, et aux enfants d’Ammon;
Edomu, Moabu na Amoni;
22 Et à tous les rois de Tyr, et à tous les rois de Sidon, et aux rois de la terre des îles qui sont au-delà de la mer;
wafalme wote wa Tiro na Sidoni; wafalme wa nchi za pwani ngʼambo ya bahari;
23 Et à Dédan, et à Théma, et à Buz, et à tous ceux dont la chevelure est coupée;
Dedani, Tema, Buzi na wote walio maeneo ya mbali;
24 Et à tous les rois d’Arabie, et à tous les rois d’Occident qui habitent dans le désert;
wafalme wote wa Arabuni na wafalme wote wa watu wageni wanaoishi katika jangwa;
25 Et à tous les rois de Zambri, et à tous les rois d’Elam, et à tous les rois des Mèdes;
wafalme wote wa Zimri, Elamu na Umedi;
26 Et aussi à tous les rois de l’aquilon, proches et éloignés, à chacun contre son frère et à tous les royaumes de la terre, qui sont sur sa face; et le roi de Sésach boira après eux.
na wafalme wote wa pande za kaskazini, wa karibu na wa mbali, mmoja baada ya mwingine; yaani falme zote juu ya uso wa dunia. Baada ya hao wote, mfalme wa Sheshaki atakunywa pia.
27 Et tu leur diras: Voici ce que dit le Seigneur des armées, Dieu d’Israël: Buvez et enivrez-vous, et vomissez; et tombez et ne vous relevez pas à la face du glaive que moi j’enverrai parmi vous.
“Kisha uwaambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: Kunyweni, mlewe na mtapike; angukeni, wala msiinuke tena kwa sababu ya upanga nitakaotuma miongoni mwenu.’
28 Que s’ils ne veulent pas recevoir de ta main le calice pour boire, tu leur diras: Voici ce que dit le Seigneur des armées: Buvant, vous boirez;
Lakini kama wakikataa kupokea kikombe kutoka mikononi mwako na kunywa, waambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: Ni lazima mnywe!
29 Parce que voilà que dans la cité dans laquelle mon nom a été invoqué, moi je commencerai à affliger, et vous, vous serez comme des innocents et exempts de châtiment? Vous n’en serez pas exempts; car moi j’appelle le glaive sur tous les habitants de la terre, dit le Seigneur des armées.
Tazama, nimeanza kuleta maafa juu ya mji ulio na Jina langu, na je, kweli ninyi mtaepuka kuadhibiwa? Hamwezi kuepuka kuadhibiwa, kwa maana nitaleta vita juu ya wote waishio duniani, asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.’
30 Et toi, tu leur prophétiseras toutes ces choses et tu leur diras: Le Seigneur d’en haut rugira, et de son habitacle saint il fera entendre sa voix; rugissant il rugira contre le lieu même de sa gloire, et un cri, comme les cris de ceux qui foulent le pressoir, retentira contre tous les habitants de la terre.
“Basi sasa toa unabii kwa maneno haya yote dhidi yao, uwaambie: “‘Bwana atanguruma kutoka juu; atatoa sauti ya ngurumo kutoka makao yake matakatifu na kunguruma kwa nguvu sana dhidi ya nchi yake. Atapiga kelele kama wao wakanyagao zabibu, atapiga kelele dhidi ya wote waishio duniani.
31 Le bruit en est parvenu jusqu’aux extrémités de la terre, parce que le Seigneur entre en jugement avec toutes les nations; il est lui-même en contestation avec toute chair: j’ai livré les impies au glaive, dit le Seigneur.
Ghasia zitasikika hadi miisho ya dunia, kwa maana Bwana ataleta mashtaka dhidi ya mataifa; ataleta hukumu juu ya wanadamu wote na kuwaua waovu wote,’” asema Bwana.
32 Voici ce que dit le Seigneur des armées: Voilà que l’affliction passera d’une nation sur une nation, et une grande tempête sortira des extrémités de la terre.
Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: “Tazama! Maafa yanaenea kutoka taifa moja hadi jingine; tufani kubwa inainuka kutoka miisho ya dunia.”
33 Et les tués par le Seigneur seront en ce jour-là d’un bout de la terre à son autre bout; ils ne seront pas pleures, et ils ne seront pas recueillis, ni ensevelis, mais comme un fumier sur la face de la terre, ils seront étendus.
Wakati huo, hao waliouawa na Bwana watatapakaa kila mahali, kuanzia mwisho mmoja wa dunia hadi mwisho mwingine. Hawataombolezewa wala kukusanywa au kuzikwa, lakini watakuwa kama mavi yaliyoenea juu ya ardhi.
34 Hurlez, pasteurs, et criez; couvrez-vous de cendres, vous les chefs du troupeau, parce que sont remplis les jours après lesquels vous devez être tués; vous serez dispersés, et vous tomberez comme des vases précieux.
Lieni na kuomboleza, enyi wachungaji, mgaagae mavumbini, ninyi viongozi wa kundi. Kwa maana wakati wenu wa kuchinjwa umewadia; mtaanguka na kuvunjavunjwa kama vyombo vizuri vya udongo.
35 Et la fuite sera enlevée aux pasteurs, et le salut aux chefs du troupeau.
Wachungaji hawatakuwa na mahali pa kukimbilia, viongozi wa kundi hawatapata mahali pa kutorokea.
36 La voix de la clameur des pasteurs, et les hurlements des chefs du troupeau se feront entendre, parce que le Seigneur a dévasté leurs pâturages.
Sikia kilio cha wachungaji, maombolezo ya viongozi wa kundi, kwa maana Bwana anayaharibu malisho yao.
37 Et les champs de la paix sont dans le silence, à la face de la colère de la fureur du Seigneur.
Makao yao ya amani yataharibiwa kwa sababu ya hasira kali ya Bwana.
38 Il a abandonné, comme le lion, sa retraite, et leur terre a été désolée à la face de la colère de la colombe, et à la face de la colère de la fureur du Seigneur.
Kama simba ataacha pango lake, nchi yao itakuwa ukiwa kwa sababu ya upanga wa mdhalimu, na kwa sababu ya hasira kali ya Bwana Mungu.