< Jérémie 24 >
1 Le Seigneur me fit voir, et voici deux paniers pleins de figues, placés devant le temple du Seigneur, après que Nabuchodonosor, roi de Babylone, eut transféré Jéchonias, fils de Joakim, roi de Juda, et ses princes, et l’artisan, et le lapidaire, loin de Jérusalem, et qu’il les eut emmenés à Babylone.
Bwana alinionyeshea kitu. Tazama, vikapu viwili vya tini viliwekwa mbele ya hekalu la Bwana. (Maono haya yalitokea baada ya Nebukadreza, mfalme wa Babeli, kumchukua mateka Yekonia mwana wa Yehoyakimu, mfalme wa Yuda, maofisa wa Yuda, mafundi na wafua vyuma kutoka Yerusalemu na kuwapeleka Babeli.)
2 L’un de ces paniers contenait des figues très bonnes, comme ont coutume d’être les figues de la première saison, et l’autre panier contenait des figues très mauvaises, qu’on ne pouvait manger, parce qu’elles étaient mauvaises.
Kikapu kimoja cha tini kilikuwa nzuri sana, kama tini za kwanza zilizoiva, lakini kikapu kingine cha tini zilizokuwa mbaya sana zisizoweza kuliwa.
3 Et le Seigneur me dit: Que vois-tu, Jérémie? Et je dis: Je vois des figues bonnes, très bonnes; et des mauvaises, très mauvaises, qui ne peuvent être mangées, parce qu’elles sont mauvaises.
Bwana akaniambia, “Unaona nini Yeremia?” Nikasema, “Tini. Tini ambazo ni nzuri sana na tini ambazo ni mbaya sana haziwezi kuliwa.”
4 Et la parole du Seigneur me fut adressée, disant:
Ndipo neno la Bwana likanijia, kusema,
5 Voici ce que dit le Seigneur, Dieu d’Israël: Comme ces figues sont bonnes, ainsi je traiterai bien les fils de la transmigration que j’ai envoyés de ce lieu dans la terre des Chaldéens.
“Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi: nitawaangalia mateka wa Yuda kwa manufaa yao, kama vile tini hizi nzuri, nilipowatoa mateka kutoka hapa mpaka nchi ya Wakaldayo.
6 Et je porterai sur eux un regard favorable, et je les ramènerai dans cette terre; je les rétablirai, et je ne les détruirai pas; je les planterai, et je ne les arracherai pas.
Nitaweka macho yangu kwao wapate mema na kuwarejeshea nchi hii. Nitawajenga, wala sitawaangamiza.
7 Et je leur donnerai un cœur, afin qu’ils me connaissent, parce que moi je suis le Seigneur; et ils seront mon peuple, et je serai leur Dieu, parce qu’ils reviendront à moi en tout leur cœur.
Nitawapanda, wala sitawang'oa. Ndipo nitawapa moyo wa kunijua; kwa kuwa mimi ndimi Bwana. Watakuwa watu wangu na mimi nitakuwa Mungu wao, hivyo watanirudia kwa moyo wao yote.
8 Quant à ces figues très mauvaises, qui ne peuvent être mangées, parce qu’elles sont mauvaises, voici ce que dit le Seigneur: Ainsi je traiterai Sédécias, roi de Juda, et ses princes, et les restes de Jérusalem qui sont demeurés dans cette ville, et ceux qui habitent dans la terre d’Egypte.
Lakini kama vile tini mbaya ambazo ni hazifai kuliwa - asema Bwana - nitatenda hivi kwa Sedekia, mfalme wa Yuda, pamoja na viongozi wake, na pamoja na wengine wa Yerusalemu ambao wanabaki katika nchi hii au kwenda kukaa katika nchi ya Misri.
9 Je les livrerai en vexation et en affliction, dans tous les royaumes de la terre; en opprobre et en parabole, et en proverbe, et en malédiction dans tous les lieux dans lesquels je les aurai jetés.
Nitawafanya kuwa kitu cha kutisha, wapate maafa, mbele ya falme zote duniani, aibu na somo kwa mithali, matusi, na laana mahali pote nitakapowafukuza.
10 Et j’enverrai contre eux le glaive, et la famine, et la peste, jusqu’à ce qu’ils soient exterminés de la terre que je leur ai donnée, à eux et à leurs pères.
Nitatuma upanga, njaa, na tauni dhidi yao watapotelea mbali kutoka kwenye nchi niliyowapa wao na baba zao.”