< Jérémie 14 >

1 Parole du Seigneur qui fut adressée à Jérémie au sujet de la sécheresse.
Hili ndilo neno la Bwana kwa Yeremia kuhusu ukame:
2 La Judée est en deuil, et ses portes sont tombées et ont été obscurcies sur la terre, et le cri de Jérusalem est monté.
“Yuda anaomboleza, miji yake inayodhoofika; wanaomboleza kwa ajili ya nchi, nacho kilio kinapanda kutoka Yerusalemu.
3 Les grands ont envoyé les petits vers l’eau; ils sont venus pour puiser, et ils n’ont pas trouvé d’eau; ils ont rapporté leurs vases vides; ils ont été confondus et affligés, et ils ont couvert leurs têtes.
Wakuu wanawatuma watumishi wao maji; wanakwenda visimani lakini humo hakuna maji. Wanarudi na vyombo bila maji; wakiwa na hofu na kukata tamaa, wanafunika vichwa vyao.
4 À cause du ravage de la terre, parce que la pluie n’est pas venue sur la terre, les laboureurs ont été confondus, ils ont couvert leurs têtes.
Ardhi imepasuka nyufa kwa sababu hakuna mvua katika nchi; wakulima wana hofu na wanafunika vichwa vyao.
5 Car même la biche a mis bas dans la campagne, et elle a abandonné son faon, parce qu’il n’y avait pas d’herbe.
Hata kulungu mashambani anamwacha mtoto wake aliyezaliwa wakati huo huo kwa sababu hakuna majani.
6 Et les onagres se sont tenus sur les rochers, ils ont aspiré l’air comme les dragons, leurs yeux ont défailli, parce qu’il n’y avait pas d’herbe.
Punda-mwitu wanasimama juu ya miinuko iliyo kame na kutweta kama mbweha; macho yao yanakosa nguvu za kuona kwa ajili ya kukosa malisho.”
7 Si nos iniquités nous répondent. Seigneur, agissez en faveur de votre nom, parce que nombreuses sont nos révoltes; c’est contre vous que nous avons péché.
Ingawa dhambi zetu zinashuhudia juu yetu, Ee Bwana, tenda jambo kwa ajili ya jina lako. Kwa kuwa kukengeuka kwetu ni kukubwa, nasi tumetenda dhambi dhidi yako.
8 Attente d’Israël, son sauveur au temps de la tribulation, pourquoi serez-vous comme un étranger dans cette terre, et comme un voyageur qui se détourne pour passer la nuit?
Ee Tumaini la Israeli, Mwokozi wake wakati wa taabu, kwa nini unakuwa kama mgeni katika nchi, kama msafiri anayekaa kwa usiku mmoja tu?
9 Pourquoi serez-vous comme un homme vagabond, comme un homme fort qui ne peut sauver? mais vous, vous êtes au milieu de nous, Seigneur, et votre nom est invoqué sur nous, ne nous abandonnez pas.
Mbona unakuwa kama mtu aliyeshtukizwa, kama shujaa asiye na uwezo wa kuokoa? Wewe uko katikati yetu, Ee Bwana, nasi tunaitwa kwa jina lako; usituache!
10 Voici ce que dit le Seigneur à ce peuple qui a aimé à remuer ses pieds, qui n’est pas demeuré en repos, et qui n’a pas plu au Seigneur: Main tenant il se ressouviendra de leurs iniquités, et il visitera leurs péchés.
Hili ndilo Bwana asemalo kuhusu watu hawa: “Wanapenda sana kutangatanga, hawaizuii miguu yao. Hivyo Bwana hawakubali; sasa ataukumbuka uovu wao na kuwaadhibu kwa ajili ya dhambi zao.”
11 Et le Seigneur me dit: Ne prie pas pour le bien de ce peuple.
Kisha Bwana akaniambia, “Usiombe kwa ajili ya mafanikio ya watu hawa.
12 Lorsqu’ils jeûneront, je n’exaucerai pas leurs prières; et s’ils offrent des holocaustes et des victimes, je ne les recevrai pas, parce que par le glaive, et par la famine, et par la peste, je les consumerai.
Ingawa wanafunga, sitasikiliza kilio chao; hata wakitoa dhabihu za kuteketezwa na dhabihu za nafaka, sitazikubali. Badala yake, nitawaangamiza kwa upanga, njaa na tauni.”
13 Et je dis: A, a, a, Seigneur Dieu, les prophètes leur disent: Vous ne verrez pas le glaive, et la famine ne sera pas parmi vous; mais le Seigneur vous donnera une véritable paix dans ce lieu.
Lakini nikasema, “Aa, Bwana Mwenyezi, manabii wanaendelea kuwaambia, ‘Hamtaona upanga wala kukabiliwa na njaa. Naam, nitawapa amani ya kudumu mahali hapa.’”
14 Et le Seigneur me dit: C’est faussement que ces prophètes prophétisent en mon nom; je ne les ai point envoyés, et je ne leur ai rien ordonné, et je ne leur ai pas parlé; c’est une vision mensongère, et de la divination, et de la fraude, et la séduction de leur cœur qu’ils vous prophétisent.
Ndipo Bwana akaniambia, “Manabii wanatabiri uongo kwa jina langu. Sikuwatuma, wala sikuwaweka, wala sikusema nao. Wanawatabiria maono ya uongo, maaguzi, maono ya sanamu zisizofaa kitu, na madanganyo ya mawazo yao wenyewe.
15 C’est pourquoi voici ce que dit le Seigneur, des prophètes qui prophétisent en mon nom, que moi je n’ai point envoyés, et qui disent: Le glaive et la faim ne seront pas sur cette terre: Par le glaive et par la famine seront consumés ces prophètes.
Kwa hiyo, hili ndilo Bwana asemalo kuhusu manabii wanaotabiri kwa jina langu: Mimi sikuwatuma, lakini wanasema, ‘Hakuna upanga wala njaa itakayoigusa nchi hii.’ Manabii hao hao watakufa kwa upanga na njaa.
16 Et les peuples pour lesquels ils prophétisent seront jetés sur les voies de Jérusalem, par la famine, et par le glaive, et il n’y aura personne qui les ensevelisse, eux et leurs femmes, leurs fils et leurs filles; et je répandrai sur eux leur propre mal.
Nao watu hao wanaowatabiria watatupwa nje katika barabara za Yerusalemu kwa sababu ya njaa na upanga. Hapatakuwepo yeyote wa kuwazika wao au wake zao, wana wao au binti zao. Nitawamwagia maafa wanayostahili.
17 Et tu leur diras cette parole: Que mes yeux fassent couler des larmes durant la nuit et le jour, et qu’ils ne se taisent pas; parce que la vierge, fille de mon peuple, a été brisée d’un grand brisement, frappée d’une plaie extrêmement grave.
“Nena nao neno hili: “‘Macho yangu na yatiririkwe na machozi usiku na mchana bila kukoma; kwa kuwa binti yangu aliye bikira, yaani watu wangu, amepata jeraha baya, pigo la kuangamiza.
18 Si je sors dans les champs, voici des tués par le glaive, et si j’entre dans la cité, voici des exténués de faim. Le prophète même et le prêtre sont allés dans une terre qu’ils ignoraient.
Kama nikienda mashambani, ninaona wale waliouawa kwa upanga; kama nikienda mjini, ninaona maangamizi ya njaa. Nabii na kuhani kwa pamoja wamekwenda katika nchi wasiyoijua.’”
19 Est-ce que rejetant, vous avez rejeté Juda? ou votre âme a-t-elle abominé Sion? pourquoi donc nous avez-vous frappés de telle sorte qu’il n’y a aucune guérison? Nous avons attendu la paix, et nul bien n’est venu; le temps de la guérison, et voici la perturbation.
Je, umemkataa Yuda kabisa? Umemchukia Sayuni kabisa? Kwa nini umetuumiza hata hatuwezi kuponyeka? Tulitarajia amani, lakini hakuna jema lililotujia; tulitarajia wakati wa kupona lakini kuna hofu kuu tu.
20 Seigneur, nous avons connu nos impiétés, et les iniquités de nos pères, parce que nous avons péché contre vous.
Ee Bwana, tunatambua uovu wetu na kosa la baba zetu; kweli tumetenda dhambi dhidi yako.
21 Ne nous livrez pas à l’opprobre à cause de votre nom, et ne nous faites pas d’affront touchant le trône de votre gloire; souvenez-vous de ne pas rendre vaine votre alliance avec nous.
Kwa ajili ya jina lako usituchukie kabisa; usikidharau kiti chako cha enzi kilichotukuka. Kumbuka agano lako nasi na usilivunje.
22 Est-ce que parmi les idoles des nations, il en est qui fassent pleuvoir? ou les cieux peuvent-ils donner des pluies? N’est-ce pas vous, Seigneur notre Dieu, vous que nous avons attendu? car c’est vous qui avez fait toutes ces choses.
Je, kuna sanamu yoyote isiyofaa kitu ya mataifa iwezayo kuleta mvua? Je, anga peke yake zaweza kutoa mvua? La hasha, ni wewe peke yako, Ee Bwana, Mungu wetu. Kwa hiyo tumaini letu liko kwako, kwa kuwa wewe ndiwe ufanyaye haya yote.

< Jérémie 14 >