< Jérémie 11 >
1 Parole qui fut adressée par le Seigneur à Jérémie, disant:
Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Bwana:
2 Ecoutez les paroles de cette alliance, et parlez aux hommes de Juda, et aux habitants de Jérusalem;
“Sikia maneno ya agano hili, nawe uwaambie watu wa Yuda na wale waishio Yerusalemu.
3 Et tu leur diras: Voici ce que dit le Seigneur, le Dieu d’Israël: Maudit l’homme qui n’écoutera pas les paroles de cette alliance,
Waambie kwamba hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli: ‘Amelaaniwa mtu ambaye hatayatii maneno ya agano hili,
4 Que je prescrivis à vos pères, au jour où je les fis sortir de la terre d’Egypte, de la fournaise de fer, disant: Ecoutez ma voix, et faites tout ce que je vous ordonne; et vous serez mon peuple, et moi je serai votre Dieu;
maneno niliyowaamuru baba zenu nilipowatoa katika nchi ya Misri, kutoka tanuru la kuyeyushia vyuma.’ Nilisema, ‘Nitiini mimi na mfanye kila kitu ninachowaamuru, nanyi mtakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wenu.
5 Afin que je fasse revivre le serment que je jurai à vos pères de leur donner une terre où couleraient du lait et du miel, comme c’est en ce jour. Et je répondis et je dis: Amen, Seigneur.
Kisha nitatimiza kiapo nilichowaapia baba zenu, kuwapa nchi itiririkayo maziwa na asali,’ nchi ambayo mnaimiliki leo.” Nikajibu, “Amen, Bwana.”
6 Et le Seigneur me dit: Crie à haute voix ces paroles dans toutes les cités de Juda, et en dehors de Jérusalem, disant: Ecoutez les paroles de cette alliance et observez-les;
Bwana akaniambia, “Tangaza maneno haya yote katika miji ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu: ‘Sikilizeni maneno ya agano hili na kuyafuata.
7 Car prenant à témoin, j’ai pris à témoin vos pères, depuis le jour où je les fis sortir de la terre d’Egypte jusqu’à ce jour; me levant dès le matin, je les ai pris à témoin et j’ai dit: Ecoutez ma voix;
Tangu wakati ule niliwapandisha baba zenu kutoka Misri mpaka leo, niliwaonya tena na tena, nikisema “Nitiini mimi.”
8 Et ils n’ont pas écouté, et ils n’ont pas incliné leur oreille; mais ils ont suivi chacun la dépravation de son cœur mauvais; et j’ai amené sur eux toutes les paroles de cette alliance que je leur ai commandé d’observer, et qu’ils n’ont pas observée.
Lakini hawakusikiliza wala kujali. Badala yake, walifuata ukaidi wa mioyo yao miovu. Hivyo nikaleta juu yao laana zote za agano nililokuwa nimewaamuru wao kulifuata, lakini wao hawakulishika.’”
9 Et le Seigneur me dit: Il a été découvert une conjuration parmi les hommes de Juda et les habitants de Jérusalem.
Kisha Bwana akaniambia, “Kuna shauri baya linaloendelea miongoni mwa watu wa Yuda na wale wanaoishi Yerusalemu.
10 Ils sont revenus aux premières iniquités de leurs pères, qui n’ont pas voulu écouter mes paroles; ceux-ci donc sont allés de même après des dieux étrangers, afin de les servir; la maison d’Israël et la maison de Juda ont rendu vaine l’alliance que j’avais conclue avec leurs pères.
Wamerudia dhambi za baba zao, waliokataa kusikiliza maneno yangu. Wameifuata miungu mingine kuitumikia. Nyumba zote mbili za Israeli na Yuda zimelivunja agano nililofanya na baba zao.
11 À cause de cela, voici ce que dit le Seigneur: Voilà que j’amènerai sur eux des maux dont ils ne pourront sortir; et ils crieront vers moi, et je ne les exaucerai pas.
Kwa hivyo, hili ndilo asemalo Bwana: ‘Nitaleta juu yao maafa ambayo hawawezi kuyakimbia. Hata kama wakinililia, sitawasikiliza.
12 Et les cités de Juda et les habitants de Jérusalem iront et crieront aux dieux auxquels ils font des libations, et ces dieux ne les sauveront pas au temps de leur affliction.
Miji ya Yuda na watu wa Yerusalemu watakwenda kuililia miungu ambayo wameifukizia uvumba, lakini haitawasaidia kamwe wakati maafa yatakapowapiga.
13 Car selon le nombre de tes cités étaient tes dieux, ô Juda, et selon le nombre de tes rues, ô Jérusalem, tu as élevé des autels de confusion, des autels pour faire des libations aux Baalim.
Mnayo miungu mingi kama miji mliyo nayo, ee Yuda, nazo madhabahu mlizozijenga za kufukizia uvumba huyo mungu wa aibu Baali ni nyingi kama barabara za Yerusalemu.’
14 Toi donc, ne prie pas pour ce peuple, et ne m’adresse pour eux ni louange, ni prière, parce que je ne les exaucerai pas au temps de leur cri vers moi, au temps de leur affliction.
“Wewe usiwaombee watu hawa wala kufanya maombezi yoyote au kunisihi kwa ajili yao, kwa sababu sitawasikiliza watakaponiita wakati wa taabu yao.
15 Pourquoi est-ce que mon bien-aimé a dans ma maison commis beaucoup de crimes? est-ce que des chairs saintes ôteront de toi tes méchancetés dont tu t’es glorifiée?
“Mpenzi wangu anafanya nini hekaluni mwangu, anapofanya mashauri yake maovu na wengi? Je, nyama iliyowekwa wakfu yaweza kuondolea mbali adhabu yako? Unapojiingiza katika ubaya wako, ndipo unashangilia.”
16 Olivier fertile, beau, chargé de fruits, superbe, le Seigneur t’a appelée de ce nom; à la voix de sa parole, un grand feu s’est allumé dans cet olivier, et ses rameaux ont été brûlés.
Bwana alikuita mti wa mzeituni uliostawi ulio na matunda mazuri kwa sura. Lakini kwa ngurumo ya mawimbi makuu atautia moto, nayo matawi yake yatavunjika.
17 Et le Seigneur des armées qui t’a planté, a prononcé le mal sur toi, à cause des maux de la maison d’Israël et de la maison de Juda, qu’elles se sont faits à elles-mêmes pour m’irriter en faisant des libations aux Baalim.
Bwana Mwenye Nguvu Zote, aliyekupanda, ametamka maafa kwa ajili yako, kwa sababu nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda mmefanya maovu na kunikasirisha kwa kumfukizia Baali uvumba.
18 Mais vous. Seigneur, vous m’avez fait voir leurs pensées, et je les ai connues; alors vous m’avez montré leurs œuvres.
Kwa sababu Bwana alinifunulia hila zao mbaya, nilizifahamu, kwa kuwa wakati ule alinionyesha yale waliyokuwa wanayafanya.
19 Et moi, j’ai été comme un agneau plein de douceur que l’on porte pour en faire une victime; et je n’ai pas su qu’ils formaient contre moi des projets, disant: Mettons du bois dans son pain, rayons-le de la terre des vivants, et que son nom ne soit plus rappelé dans la mémoire.
Nilikuwa kama mwana-kondoo mpole aliyeongozwa machinjoni; mimi sikutambua kwamba walikuwa wamefanya shauri baya dhidi yangu, wakisema, “Sisi na tuuangamize mti na matunda yake; nasi tumkatilie mbali kutoka nchi ya walio hai, ili jina lake lisikumbukwe tena.”
20 Mais vous, Seigneur Sabaoth, vous qui jugez justement et qui éprouvez les reins et les cœurs, que je voie votre vengeance sur eux; car je vous ai révélé ma cause.
Lakini, Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, wewe uhukumuye kwa haki, nawe uchunguzaye moyo na akili, wacha nione ukiwalipiza wao kisasi, kwa maana kwako nimeweka shauri langu.
21 À cause de cela, voici ce que dit le Seigneur aux hommes d’Anathoth, qui cherchent mon âme, et disent: Tu ne prophétiseras pas au nom du Seigneur, et tu ne mourras pas de nos mains.
“Kwa hiyo hili ndilo Bwana asemalo kuhusu watu wa Anathothi wale wanaotafuta uhai wako wakisema, ‘Usitoe unabii kwa jina la Bwana, la sivyo utakufa kwa mikono yetu’:
22 C’est pourquoi voici ce que dit le Seigneur des armées: Voilà que moi je les visiterai; les jeunes hommes mourront par le glaive, leurs fils et leurs filles mourront de faim.
kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: ‘Nitawaadhibu. Vijana wao waume watakufa kwa upanga, wana wao na binti zao kwa njaa.
23 Et rien ne restera d’eux; car j’amènerai le mal sur les hommes d’Anathoth, l’année de leur visite.
Hawatasaziwa hata mabaki kwao, kwa sababu nitaleta maafa kwa watu wa Anathothi katika mwaka wa adhabu yao.’”