< Isaïe 36 >
1 Et il arriva en la quatorzième année du règne du roi Ezéchias, que Sennachérib, roi d’Assyrie, monta contre toutes les villes fortifiées de Juda, et les prit.
Katika mwaka wa kumi na nne wa utawala wa Mfalme Hezekia, Senakeribu mfalme wa Ashuru akaishambulia miji yote ya Yuda yenye ngome na kuiteka.
2 Et le roi des Assyriens envoya Rabsacès, de Lachis à Jérusalem, vers le roi Ezéchias, avec une armée considérable; et il s’arrêta à l’aqueduc de la piscine supérieure, dans la voie du Champ du foulon.
Kisha mfalme wa Ashuru akamtuma jemadari wa jeshi pamoja na jeshi kubwa kutoka Lakishi hadi kwa Mfalme Hezekia huko Yerusalemu. Jemadari wa jeshi akasimama kwenye mfereji wa Bwawa la Juu, lililojengwa katika barabara iendayo kwenye Uwanja wa Dobi.
3 Et sortit vers lui Eliacim, fils d’Helcias, qui était intendant de la maison, ainsi que Sobna, le scribe, et Joahé, fils d’Asaph, qui tenait les registres.
Eliakimu mwana wa Hilkia aliyekuwa msimamizi wa jumba la kifalme, Shebna aliyekuwa katibu, na Yoa mwana wa Asafu mwandishi wakamwendea.
4 Et Rabsacès leur dit: Dites à Ezéchias: Voici ce qu’a dit le grand roi, roi des Assyriens: Quelle est cette confiance dont vous êtes animés?
Jemadari wa jeshi akawaambia, “Mwambieni Hezekia, “‘Hili ndilo asemalo mfalme mkuu, mfalme wa Ashuru: Ni wapi unapoweka hili tumaini lako?
5 Ou par quel conseil ou avec quelle force prétendez-vous vous révolter? en qui avez-vous confiance, pour que vous vous soyez retirés de moi?
Unasema mnayo mikakati na nguvu za kijeshi, lakini unasema maneno matupu tu. Je, wewe unamtegemea nani, hata ukaniasi mimi?
6 Voici que vous vous appuyez sur ce bâton de roseau cassé, l’Egypte; bâton qui, si un homme s’appuie dessus, entrera dans sa main et la percera; ainsi est Pharaon, roi d’Egypte, pour tous ceux qui se confient en lui.
Tazama sasa, unaitegemea Misri, fimbo ile ya mwanzi uliopasuka, ambayo huuchoma na kuujeruhi mkono wa mtu akiiegemea! Hivyo ndivyo alivyo Farao mfalme wa Misri, kwa wote wanaomtegemea.
7 Que si vous me répondez: C’est dans le Seigneur notre Dieu que nous nous confions, n’est-ce pas celui dont Ezéchias a détruit les hauts lieux et les autels, et a dit à Juda et à Jérusalem: C’est devant cet autel que vous adorerez?
Nawe kama ukiniambia, “Tunamtumainia Bwana Mungu wetu”: je, siyo yeye ambaye Hezekia aliondoa mahali pake pa juu pa kuabudia miungu na madhabahu zake, akiwaambia Yuda na Yerusalemu, “Ni lazima mwabudu mbele ya madhabahu haya”?
8 Et maintenant livrez-vous à mon maître, le roi des Assyriens, et je vous donnerai deux mille chevaux, et vous ne pourrez fournir par vous-mêmes des cavaliers pour eux.
“‘Njooni sasa, fanyeni mapatano na bwana wangu, mfalme wa Ashuru: Nitakupa farasi elfu mbili, kama unaweza kuwapandisha waendesha farasi juu yao!
9 Et comment soutiendrez-vous la face du juge d’un seul lieu, d’entre les moindres officiers de mon maître? Que si vous vous confiez dans l’Egypte, dans ses quadriges et dans ses cavaliers,
Utawezaje kumzuia hata afisa mmoja aliye mdogo kati ya maafisa wa bwana wangu, ijapo unategemea Misri kwa magari ya vita na wapanda farasi?
10 Est-ce donc maintenant sans le Seigneur que je suis monté dans cette terre pour la perdre entièrement? Le Seigneur m’a dit: Monte sur cette terre, et perds-la entièrement.
Zaidi ya hayo, je, nimekuja kushambulia na kuangamiza nchi hii bila Bwana? Bwana mwenyewe ndiye aliniambia niishambulie nchi hii na kuiangamiza.’”
11 Et dit Eliacim, ainsi que Sobna et Joahé, à Rabsacès: Parlez à vos serviteurs en langue syriaque; car nous la comprenons; ne nous parlez pas en langue juive aux oreilles du peuple qui est sur le mur.
Ndipo Eliakimu, Shebna na Yoa wakamwambia yule jemadari wa jeshi, “Tafadhali zungumza na watumishi wako kwa lugha ya Kiaramu, kwa kuwa tunaifahamu. Usiseme nasi kwa Kiebrania watu walioko juu ya ukuta wakiwa wanasikia.”
12 Et Rabsacès leur dit: Est-ce donc vers ton maître et vers toi que m’a envoyé mon maître, pour dire toutes ces paroles, et non pas plutôt vers les hommes qui sont sur le mur, pour qu’ils mangent leurs excréments et boivent leur urine avec vous?
Lakini yule jemadari wa jeshi akajibu, “Je, bwana wangu amenituma kutoa ujumbe huu kwa bwana wenu na kwenu tu? Je, hakunituma pia kwa watu walioketi ukutani, ambao, kama ninyi, itawabidi kula mavi yao na kunywa mikojo yao wenyewe?”
13 Et Rabsacès se tint debout et cria d’une voix forte en hébreu: Ecoutez les paroles du grand roi, du roi des Assyriens.
Kisha yule jemadari wa jeshi akasimama na kuita kwa lugha ya Kiebrania, akasema: “Sikieni maneno ya mfalme mkuu, mfalme wa Ashuru!
14 Voici ce que dit le roi: Qu’Ezéchias ne vous séduise point; parce qu’il ne pourra vous arracher à ma main.
Hili ndilo asemalo mfalme: Msikubali Hezekia awadanganye. Hawezi kuwaokoa!
15 Et qu’Ezéchias ne vous donne point de confiance dans le Seigneur, disant: Le Seigneur nous délivrera certainement; cette cité ne sera pas livrée à la main du roi des Assyriens.
Msikubali Hezekia awashawishi kumtumaini Bwana kwa kuwaambia, ‘Hakika Bwana atatuokoa. Mji huu hautaangukia mikononi mwa mfalme wa Ashuru.’
16 N’écoutez point Ezéchias; car voici ce que dit le roi des Assyriens: Faites la paix avec moi, et sortez vers moi, et vous mangerez chacun de votre vigne et chacun de votre figuier, vous boirez chacun de l’eau de votre citerne,
“Msimsikilize Hezekia. Hili ndilo mfalme wa Ashuru asemalo: Fanyeni amani nami na mje kwangu. Kisha kila mmoja wenu atakula kutoka kwa mzabibu wake na mtini wake mwenyewe, na kunywa maji kutoka kisima chake mwenyewe,
17 Jusqu’à ce que je vienne et que je vous transporte dans une terre qui est comme votre terre, une terre de blé et de vin, une terre de pains et de vignes.
mpaka nije nikawapeleke katika nchi iliyo kama nchi yenu wenyewe, nchi ya nafaka na divai mpya, nchi ya mkate na ya mashamba ya mizabibu.
18 Qu’Ezéchias ne vous déconcerte pas, disant: Le Seigneur nous délivrera. Est-ce que les dieux des nations ont délivré chacun sa terre de la main du roi des Assyriens?
“Msikubali Hezekia awapotoshe asemapo, ‘Bwana atatuokoa.’ Je, yuko mungu wa taifa lolote aliyewahi kuokoa nchi yake kutoka mkononi mwa mfalme wa Ashuru?
19 Où est le Dieu d’Emath et d’Arphad? où est le Dieu de Sépharvaïm? est-ce qu’ils ont délivré Samarie de ma main?
Iko wapi miungu ya Hamathi na ya Arpadi? Iko wapi miungu ya Sefarvaimu? Je, imeokoa Samaria kutoka mkononi mwangu?
20 Quel est celui de tous les dieux de ces terres qui a arraché sa terre à ma main, pour que le Seigneur arrache Jérusalem de ma main?
Ni yupi miongoni mwa miungu yote ya nchi hizi ameweza kuokoa nchi yake mkononi mwangu? Inawezekanaje basi Bwana aiokoe Yerusalemu mkononi mwangu?”
21 Et ils gardèrent le silence, et ils ne lui répondirent pas un mot. Le roi en effet l’avait commandé, disant: Ne lui répondez pas.
Lakini wale watu wakakaa kimya, wala hawakujibu lolote, kwa kuwa mfalme alikuwa amewaamuru, “Msimjibu lolote.”
22 Et Eliacim, fils d’Helcias, qui était intendant de la maison, et Sobna, le scribe, et Joahé, fils d’Asaph, qui tenait les registres, entrèrent auprès d’ Ezéchias, leurs vêlements déchirés, et ils lui rapportèrent les paroles de Rabsacès.
Kisha Eliakimu mwana wa Hilkia msimamizi wa jumba la kifalme, Shebna katibu, na Yoa mwana wa Asafu, mwandishi wakamwendea Hezekia, nguo zao zikiwa zimeraruliwa, na kumwambia yale jemadari wa jeshi aliyoyasema.