< Isaïe 34 >

1 Approchez, nations, et écoutez; peuples, soyez attentifs: que la terre écoute, ainsi que sa plénitude, le globe et tout ce qu’il produit.
Njooni karibu, enyi mataifa, nanyi msikilize; sikilizeni kwa makini, enyi kabila za watu! Dunia na isikie, navyo vyote vilivyo ndani yake, ulimwengu na vyote vitokavyo ndani yake!
2 Parce que l’indignation du Seigneur est sur toutes les nations, et sa fureur sur leur milice entière; il les a tués et les a livrés au carnage.
Bwana ameyakasirikia mataifa yote; ghadhabu yake ni juu ya majeshi yao yote. Atawaangamiza kabisa, atawatia mikononi mwa wachinjaji.
3 Ceux qui leur ont été tués seront jetés dehors, et de leurs cadavres s’élèvera une odeur fétide, et des montagnes se liquéfieront par leur sang.
Waliouawa watatupwa nje, maiti zao zitatoa uvundo, milima itatota kwa damu zao.
4 Et toute la milice des cieux se liquéfiera; et les cieux se rouleront comme un livre; et toute leur milice tombera comme tombe une feuille d’une vigne et d’un figuier.
Nyota zote za mbinguni zitayeyuka na anga litasokotwa kama kitabu, jeshi lote la angani litaanguka kama majani yaliyonyauka kutoka kwenye mzabibu, kama tini iliyonyauka kutoka kwenye mtini.
5 Parce que mon glaive s’est enivré de sang dans le ciel; voici qu’il descendra sur l’Idumée, et sur un peuple que j’ai voué à la mort, pour le juger.
Upanga wangu umekunywa na kushiba huko mbinguni, tazama, unashuka katika hukumu juu ya Edomu, wale watu ambao nimeshawahukumu, kuwaangamiza kabisa.
6 Le glaive du Seigneur est plein de sang, il est couvert de graisse; du sang des agneaux et des boucs, du sang des béliers les plus gras; car il y a une victime du Seigneur à Bosra, et un grand carnage dans la terre d’Edom.
Upanga wa Bwana umeoga katika damu, umefunikwa na mafuta ya nyama: damu ya kondoo na mbuzi, mafuta kutoka figo za kondoo dume. Kwa maana Bwana ana dhabihu huko Bosra, na machinjo makuu huko Edomu.
7 Et des licornes descendront avec eux, et des taureaux avec les puissants d’entre eux: leur terre sera enivrée de sang, et leur sol de la graisse des gras;
Nyati wataanguka pamoja nao, ndama waume na mafahali wakubwa. Nchi yao italowana kwa damu, nayo mavumbi yataloa mafuta ya nyama.
8 Parce que c’est le jour de la vengeance du Seigneur, l’année des rétributions dans le jugement de Sion.
Kwa sababu Bwana anayo siku ya kulipiza kisasi, mwaka wa malipo, siku ya kushindania shauri la Sayuni.
9 Et ses torrents seront convertis en poix, et son sol en soufre, et sa terre deviendra une poix brûlante.
Vijito vya Edomu vitageuka kuwa lami, mavumbi yake yatakuwa kiberiti kiunguzacho, nchi yake itakuwa lami iwakayo!
10 Ni nuit ni jour le feu ne s’éteindra, à jamais s’élèvera sa fumée; de génération en génération elle sera désolée; dans les siècles des siècles personne n’y passera.
Haitazimishwa usiku wala mchana, moshi wake utapaa juu milele. Kutoka kizazi hadi kizazi itakuwa ukiwa, hakuna mtu yeyote atakayepita huko tena.
11 Et l’onocrotale et le hérisson la posséderont; l’ibis et le corbeau y habiteront; et le cordeau sera étendu sur elle, afin qu’elle soit réduite au néant, et le niveau pour sa ruine.
Bundi wa jangwani na bundi mwenye sauti nyembamba wataimiliki, bundi wakubwa na kunguru wataweka viota humo. Mungu atanyoosha juu ya Edomu kamba ya kupimia ya machafuko matupu, na timazi ya ukiwa.
12 Ses nobles ne seront pas là; ils invoqueront un roi, et tous ses princes seront anéantis.
Watu wake wa kuheshimiwa hawatakuwa na chochote kitakachoitwa ufalme huko, nao wakuu wao wote watatoweka.
13 Et les épines et les orties croîtront dans ses maisons, et le paliure dans ses forteresses; et elle sera le repaire des dragons et le pâturage des autruches.
Miiba itaenea katika ngome za ndani, viwawi na michongoma itaota kwenye ngome zake. Itakuwa maskani ya mbweha, makao ya bundi.
14 Les démons y rencontreront les onocentaures, et le bouc criera, l’un à l’autre; là s’est couchée la lamie, et elle y a trouvé son repos.
Viumbe vya jangwani vitakutana na fisi, nao mbuzi-mwitu watalia wakiitana; huko viumbe vya usiku vitastarehe pia na kujitafutia mahali pa kupumzika.
15 Le hérisson a eu une tanière, et a nourri ses petits, et il a creusé tout autour, et il les a réchauffés sous son ombre; là se sont assemblés les milans, l’un près de l’autre.
Bundi wataweka viota huko na kutaga mayai, atayaangua na kutunza makinda yake chini ya uvuli wa mabawa yake; pia huko vipanga watakusanyika, kila mmoja na mwenzi wake.
16 Recherchez dans le livre du Seigneur, et lisez; une seule de ces choses n’a pas manqué; l’un n’a pas cherché l’autre; parce que ce qui procède de ma bouche, c’est lui qui l’a commandé, et que son esprit lui-même a rassemblé ces choses.
Angalieni katika gombo la Bwana na msome: Hakuna hata mmoja katika hawa atakayekosekana, hakuna hata mmoja atakayemkosa mwenzi wake. Kwa kuwa ni kinywa chake Mungu kimeagiza, na Roho wake atawakusanya pamoja.
17 Et lui-même a jeté pour eux le sort, et sa main a divisé leur part au cordeau; jusqu’à l’éternité ils la posséderont, et dans toutes les générations ils y habiteront.
Huwagawia sehemu zao, mkono wake huwagawanyia kwa kipimo. Wataimiliki hata milele na kuishi humo kutoka kizazi hadi kizazi.

< Isaïe 34 >