< Hébreux 8 >

1 Mais voici l’abrégé de ce que je dis: Nous avons un pontife tel, qu’il est assis à la droite du trône de la Majesté dans les cieux.
Basi jambo tunalotaka kulisema ni hili: Tunaye Kuhani Mkuu ambaye ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Aliye Mkuu mbinguni,
2 Ministre du sanctuaire et du vrai tabernacle, que le Seigneur a dressé, et non pas un homme.
yeye ahudumuye katika patakatifu, hema la kweli lililowekwa na Bwana, wala si na mwanadamu.
3 Car tout pontife est établi pour offrir des dons et des victimes; d’où il est nécessaire que celui-ci ait aussi quelque chose à offrir.
Kila kuhani mkuu huwekwa ili atoe sadaka na dhabihu. Vivyo hivyo, ilikuwa jambo muhimu kwa huyu Kuhani naye awe na kitu cha kutoa.
4 Si donc il était sur la terre, il ne serait pas même prêtre, y en ayant déjà pour offrir les dons selon la loi,
Kama angekuwa duniani, hangekuwa kuhani, kwa sababu tayari wapo watu watoao sadaka kama ilivyoelekezwa na sheria.
5 Qui sont ministres d’un culte, modèle et ombre des choses célestes; comme il fut répondu à Moïse, lorsqu’il devait dresser le tabernacle: Vois [dit Dieu), et fais toutes choses selon le modèle qui t’a été montré sur la montagne.
Wanahudumu katika patakatifu palipo mfano na kivuli cha mambo ya mbinguni. Hii ndiyo sababu Mose alionywa alipokaribia kujenga hema, akiambiwa: “Hakikisha kuwa unavitengeneza vitu vyote kwa mfano ulioonyeshwa kule mlimani.”
6 Mais celui-ci a été investi d’un ministère d’autant plus excellent, qu’il est médiateur d’une alliance plus parfaite, établie sur de meilleures promesses.
Lakini huduma aliyopewa Yesu ni bora zaidi kuliko yao, kama vile agano ambalo yeye ni mpatanishi wake lilivyo bora zaidi kuliko lile la zamani, nalo limewekwa misingi wa ahadi zilizo bora zaidi.
7 Car si la première eût été sans imperfection, il n’y aurait certainement pas eu lieu d’en rechercher une seconde.
Kwa maana kama hapakuwa na kasoro katika lile agano la kwanza, pasingekuwa na haja ya kutafuta nafasi kwa ajili ya jingine.
8 Or, se plaignant d’eux. Dieu dit: Voici venir des jours, dit le Seigneur, où j’accomplirai avec la maison d’Israël et avec la maison de Juda une nouvelle alliance;
Lakini Mungu aliona kosa kwa watu, naye akasema: “Siku zinakuja, asema Bwana, nitakapofanya agano jipya na nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda.
9 Non selon l’alliance que j’ai faite avec leurs pères, au jour où je les pris par la main pour les tirer de la terre d’Egypte: parce qu’ils n’ont point eux-mêmes persévéré dans mon alliance, moi aussi je les ai délaissés, dit le Seigneur.
Agano langu halitakuwa kama lile nililofanya na baba zao nilipowashika mkono kuwaongoza watoke nchi ya Misri, kwa sababu hawakuendelea kuwa waaminifu katika agano langu, nami nikawaacha, asema Bwana.
10 Et voici l’alliance que je ferai avec la maison d’Israël après ces jours, dit le Seigneur: Je mettrai mes lois dans leur esprit, et je les écrirai dans leur cœur; et je serai leur Dieu, et eux seront mon peuple;
Hili ndilo agano nitakalofanya na nyumba ya Israeli baada ya siku zile, asema Bwana. Nitaziweka sheria zangu katika nia zao na kuziandika mioyoni mwao. Nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.
11 Et chacun n’enseignera plus son prochain, ni chacun son frère, disant: Connais le Seigneur; parce que tous me connaîtront depuis le plus petit jusqu’au plus grand;
Mtu hatamfundisha tena jirani yake, wala mtu kumfundisha ndugu yake akisema, ‘Mjue Bwana,’ kwa sababu wote watanijua mimi, tangu aliye mdogo kabisa kwao, hadi aliye mkuu sana.
12 Car je pardonnerai leurs iniquités, et je ne me souviendrai plus de leurs péchés.
Kwa sababu nitasamehe uovu wao, wala sitazikumbuka dhambi zao tena!”
13 Mais en disant une nouvelle alliance, il a déclaré la première vieillie. Or ce qui devient ancien et vieillit est près de sa fin.
Kwa kuliita agano hili “jipya,” Mungu amefanya lile agano la kwanza kuwa kuukuu; nacho kitu kinachoanza kuchakaa na kuwa kikuukuu kiko karibu kutoweka.

< Hébreux 8 >