< Aggée 2 >

1 Au septième mois, au vingt-unième jour du mois, la parole du Seigneur fut adressée par l’entremise d’Aggée, le prophète, disant:
Katika siku ya ishirini na moja ya mwezi wa saba, neno la Bwana lilikuja kupitia nabii Hagai, kusema:
2 Parle à Zorobabel, fils de Salathiel, chef de Juda, et à Jésus, fils de Josédec, le grand-prêtre, et à ceux qui sont restés du peuple, en disant:
“Sema na Zerubabeli mwana wa Shealtieli, mtawala wa Yuda, kuhani mkuu Yoshua mwana wa Yehosadaki, na mabaki ya watu. Uwaulize,
3 Qui est celui parmi vous qui, étant resté, a vu cette maison dans sa première gloire? et comment la voyez-vous maintenant? Est-ce qu’elle n’est pas à vos yeux comme si elle n’existait pas?
‘Ni nani miongoni mwenu aliyebaki ambaye aliiona hii nyumba katika utukufu wake wa mwanzo? Sasa inaonekanaje kwenu? Je, haionekani kwenu kama si kitu?
4 Mais maintenant, Zorobabel, prends courage, dit le Seigneur; prends courage, Jésus, fils de Josédec, grand-prêtre; prends courage aussi, peuple entier de la terre, dit le Seigneur des armées; et observez (parce que, moi, je suis avec vous, dit le Seigneur des armées)
Lakini sasa uwe imara, ee Zerubabeli,’ asema Bwana. ‘Kuwa imara, ee kuhani mkuu Yoshua mwana wa Yehosadaki. Mwe imara, enyi watu wote wa nchi,’ asema Bwana, ‘na mfanye kazi. Kwa kuwa mimi nipo pamoja nanyi,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
5 L’alliance que j’ai faite avec vous, lorsque vous êtes sortis de la terre d’Egypte: et mon esprit sera au milieu de vous; ne craignez point.
‘Hili ndilo nililoagana nanyi mlipotoka katika nchi ya Misri. Pia Roho wangu anadumu katikati yenu. Msiogope.’
6 Parce que voici ce que dit le Seigneur des armées: Encore un peu de temps, et j’ébranlerai le ciel, et la terre, et la mer, et la partie aride.
“Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Baada ya muda kidogo kwa mara nyingine nitazitikisa mbingu na nchi, bahari na nchi kavu.
7 Et j’ébranlerai toutes les nations: ET VIENDRÀ LE DÉSIRÉ de toutes les nations; et je remplirai cette maison de gloire, dit le Seigneur des armées.
Nitatikisa mataifa yote, nacho kile kinachotamaniwa na mataifa yote kitakuja, nami nitaujaza utukufu katika nyumba hii,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
8 À moi est l’argent, et à moi est l’or, dit le Seigneur des armées.
‘Fedha ni mali yangu na dhahabu ni mali yangu,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
9 La gloire de cette dernière maison sera plus grande que celle de la première, dit le Seigneur des armées; et en ce lieu je donnerai la paix, dit le Seigneur des armées.
‘Utukufu wa nyumba hii ya sasa utakuwa mkubwa kuliko utukufu wa ile nyumba ya mwanzoni,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. ‘Na mahali hapa nitawapa amani,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.”
10 Au vingt-quatrième jour du neuvième mois, en la seconde année du roi Darius, la parole du Seigneur fut adressée à Aggée, le prophète, disant:
Katika siku ya ishirini na nne ya mwezi wa tisa, katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario, neno la Bwana lilikuja kwa nabii Hagai:
11 Voici ce que dit le Seigneur des armées: Interroge les prêtres sur la loi, en disant:
“Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Ulizeni makuhani jinsi sheria inavyosema:
12 Si un homme porte de la chair sanctifiée dans un coin de son vêtement, et que ce coin de son vêtement touche du pain ou de la viande, ou du vin, ou de l’huile, ou tout autre aliment, ce qu’il aura touché sera-t-il sanctifié? Or, répondant, les prêtres dirent: Non.
Kama mtu akibeba nyama iliyowekwa wakfu katika pindo la vazi lake, kisha lile pindo likagusa mkate au mchuzi, divai, mafuta au chakula kingine, je, kitu hicho kitakuwa kimewekwa wakfu?’” Makuhani wakajibu, “La hasha.”
13 Aggée dit: Si un homme souillé par l’attouchement d’un cadavre touche quelqu’une de toutes ces choses, sera-t-elle souillée? Et les prêtres répondirent et dirent: Elle sera souillée.
Kisha Hagai akasema, “Je, kama mtu aliyetiwa unajisi kwa kugusa maiti akigusa mojawapo ya vitu hivi, kitu hicho kitakuwa kimetiwa unajisi?” Makuhani wakajibu, “Ndiyo, huwa kimenajisiwa.”
14 Et Aggée reprit et dit: Ainsi est ce peuple, ainsi est cette nation devant ma face, dit le Seigneur, et ainsi est-il de toute œuvre de leurs mains, et tout ce qu’ils m’ont offert en ce lieu sera souillé.
Kisha Hagai akasema, “‘Basi ndivyo walivyo machoni pangu hawa watu na taifa hili,’ asema Bwana. ‘Lolote wafanyalo na chochote watoacho hapo ni najisi.
15 Et maintenant appliquez vos cœurs à ce qui s’est passé depuis ce jour et au-delà, avant qu’une pierre eût été posée sur une pierre au temple du Seigneur.
“‘Sasa fikirini kwa uangalifu kuanzia leo na kuendelea: tafakarini jinsi mambo yalivyokuwa kabla halijawekwa jiwe moja juu ya lingine katika Hekalu la Bwana.
16 Lorsque vous vous approchiez d’un tas de vingt boisseaux de grains, ils se réduisaient à dix; et lorsque vous entriez au pressoir pour faire cinquante cruches de vin, il s’en faisait vingt.
Wakati mtu alipoendea lundo la nafaka la vipimo ishirini, kulikuwa na vipimo kumi tu. Wakati mtu alipoendea pipa la mvinyo ili kuchota vipimo hamsini, kulikuwa na vipimo ishirini tu.
17 Je vous ai frappés d’un vent brûlant; et j’ai frappé de la nielle et de la grêle tous les travaux de vos mains; et il n’y a eu personne parmi vous qui revînt à moi, dit le Seigneur.
Kazi zenu zote za mikono nilizipiga kwa ukame, ukungu na mvua ya mawe, lakini hata hivyo, hamkunigeukia mimi,’ asema Bwana.
18 Appliquez vos cœurs à ce qui se fera depuis ce jour et à l’avenir, depuis le vingt-quatrième jour du neuvième mois; depuis le jour que les fondements du temple du Seigneur ont été jetés, appliquez votre cœur.
‘Tangu leo na kuendelea, kuanzia siku hii ya ishirini na nne ya mwezi wa tisa, tafakarini siku ambayo msingi wa Hekalu la Bwana uliwekwa. Tafakarini:
19 Est-ce que les grains n’ont déjà pas germé? et la vigne, et le figuier et le grenadier et l’olivier n’ont-ils pas fleuri? Depuis ce jour je bénirai.
Je, bado kuna mbegu iliyobakia ghalani? Mpaka sasa, hakuna mzabibu au mtini, mkomamanga wala mzeituni uliozaa tunda. “‘Kuanzia leo na kuendelea, nitawabariki.’”
20 Et la parole du Seigneur fut adressée une seconde fois à Aggée le vingt-quatrième jour du mois, disant:
Neno la Bwana likamjia Hagai kwa mara ya pili katika siku ya ishirini na nne ya mwezi kusema:
21 Parle à Zorobabel, chef de Juda, en disant: Moi j’ébranlerai à la fois le ciel et la terre.
“Mwambie Zerubabeli mtawala wa Yuda kwamba nitazitikisa mbingu na nchi.
22 Et je renverserai le trône des royaumes, et je briserai la force du règne des nations; et je renverserai le quadrige, et celui qui le monte; les chevaux tomberont ainsi que leurs cavaliers; un homme tombera sous le glaive -de son frère.
Nitapindua viti vya enzi vya falme, na kuziharibu kabisa nguvu za falme za kigeni. Nitapindua magari ya vita pamoja na waendeshaji wake; farasi na wapanda farasi wataanguka, kila mmoja kwa upanga wa ndugu yake.
23 En ce jour-là, dit le Seigneur des armées, je te prendrai, Zorobabel, fils de Salathiel, mon serviteur, dit le Seigneur, et je te poserai comme un sceau, parce que je t’ai choisi, dit le Seigneur des armées.
“‘Katika siku ile,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, ‘nitakuchukua wewe, mtumishi wangu Zerubabeli mwana wa Shealtieli,’ asema Bwana. ‘Nitakufanya kama pete yangu ya muhuri, kwa kuwa nimekuchagua,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.”

< Aggée 2 >