< Genèse 19 >

1 Cependant les deux Anges vinrent à Sodome vers le soir, et Lot étant assis à la porte de la ville. Dès qu’il les eut vus, il se leva et alla au-devant d’eux, et se prosterna, incliné vers la terre.
Malaika wale wawili wakafika Sodoma wakati wa jioni, naye Loti alikuwa ameketi kwenye lango la mji. Wakati alipowaona, aliondoka kwenda kuwalaki na kuwasujudia hadi chini.
2 Et il dit: Je vous conjure, seigneurs, venez dans la maison de votre serviteur, et demeurez-y; lavez vos pieds, et dès le matin vous continuerez votre route. Ils répondirent: Point du tout; mais c’est sur la place que nous demeurerons.
Akasema, “Bwana zangu, tafadhali karibuni kwenye nyumba ya mtumishi wenu. Mnaweza kunawa miguu na kulala hapa kisha asubuhi na mapema mwendelee na safari yenu.” Wakamjibu, “La hasha, tutalala hapa nje uwanjani.”
3 Mais il les força par ses instances de venir chez lui; et lorsqu’ils furent entrés dans sa maison, il leur prépara un repas, et il fit cuire des azymes; et ils mangèrent.
Lakini akasisitiza kwa nguvu kwamba waingie pamoja naye nyumbani kwake. Akawaandalia chakula, mikate isiyotiwa chachu, nao wakala.
4 Mais avant qu’ils allassent se coucher, les hommes de la ville environnèrent la maison, depuis l’enfant jusqu’au vieillard, tout le peuple ensemble.
Kabla hawajaenda kulala, watu wote kutoka kila sehemu ya mji wa Sodoma, vijana kwa wazee, waliizunguka nyumba.
5 Et ils appelèrent Lot et lui dirent: Où sont les hommes qui sont entrés chez toi cette nuit? Amène-les ici, afin que nous les connaissions.
Wakamwita Loti wakisema, “Wako wapi wale watu ambao walikuja kwako jioni hii? Watoe nje kwetu ili tuweze kuwalawiti.”
6 Lot étant sorti vers eux, et ayant fermé derrière lui la porte, dit:
Loti akatoka nje kuonana nao, akaufunga mlango nyuma yake,
7 Ne faites pas, je vous prie, mes frères, ne faites pas ce mal.
akasema, “La hasha, rafiki zangu. Msifanye jambo hili ovu.
8 J’ai deux filles qui n’ont pas encore connu d’hommes: je vous les amènerai, et vous ferez d’elles ce qui vous plaira, pourvu qu’à ces hommes vous ne fassiez aucun mal; car ils sont venus à l’ombre de mon toit.
Tazama, ninao binti wawili ambao kamwe hawajakutana kimwili na mwanaume. Acha niwatoe nje kwenu, nanyi mnaweza kuwafanyia lolote mnalotaka. Lakini msiwafanyie chochote watu hawa, kwa sababu wako kwenye ulinzi chini ya dari langu.”
9 Mais ils répondirent: Retire-toi d’ici. Et de nouveau: Tu es venu ici, dirent-ils, comme étranger; est-ce pour t’ériger en juge. C’est donc toi-même que nous maltraiterons plus qu’eux. Et ils faisaient à Lot la plus grande violence; et déjà ils étaient près d’enfoncer la porte.
Wakamjibu, “Tuondokee mbali.” Wakaendelea kusema, “Huyu mtu alikuja hapa kama mgeni na sasa anataka kuwa mwamuzi wetu! Tutakutenda vibaya kuliko wao.” Waliendelea kumlazimisha Loti na kusonga mbele ili kuvunja mlango.
10 Mais voilà que les hommes avancèrent la main, firent rentrer Lot auprès d’eux et fermèrent la porte;
Lakini watu wale waliokuwa ndani wakanyoosha mkono wakamvuta Loti ndani ya nyumba na kufunga mlango.
11 Et ceux qui étaient dehors, ils les frappèrent d’aveuglement, depuis le plus petit Jusqu’au plus grand, en sorte qu’ils ne pouvaient retrouver la porte.
Kisha wakawapiga kwa upofu wale watu waliokuwa mlangoni mwa ile nyumba, vijana kwa wazee, hivyo hawakuweza kuupata mlango.
12 Alors ils dirent à Lot: As-tu ici quelqu’un des tiens, un gendre, ou des fils, ou des filles? tous ceux qui sont à toi, fais-les sortir de cette ville;
Wale watu wawili wakamwambia Loti, “Una mtu mwingine yeyote hapa, wakwe zako, wana au binti, ama yeyote mwingine aliye wako katika mji huu? Waondoe hapa,
13 Car nous détruirons ce lieu, parce que leur clameur s’est élevée de plus en plus devant le Seigneur qui nous a envoyés pour les perdre.
kwa sababu tunapaangamiza mahali hapa. Kilio kwa Bwana dhidi ya watu wa hapa ni kikubwa kiasi kwamba ametutuma kupaangamiza.”
14 Lot étant donc sorti, parla à ses gendres, qui devaient épouser ses filles, et dit: Levez-vous, sortez de ce lieu; parce que le Seigneur détruira cette ville. Et il leur sembla parler comme en se jouant.
Kwa hiyo Loti alitoka ili kuzungumza na wakwe zake, waliokuwa wamewaposa binti zake. Akawaambia, “Fanyeni haraka kuondoka mahali hapa, kwa kuwa Bwana yu karibu kuangamiza mji huu!” Lakini wakwe zake walifikiri kwamba alikuwa akitania.
15 Mais lorsqu’il fut matin, les Anges le pressaient, disant: Lève-toi, prends ta femme, et les deux filles que tu as, afin que tu ne périsses pas, toi aussi, dans le châtiment de la ville.
Kunako mapambazuko, malaika wakamhimiza Loti, wakamwambia, “Fanya haraka! Mchukue mke wako na binti zako wawili walioko hapa, la sivyo utaangamizwa wakati mji utakapoadhibiwa.”
16 Mais lui différant, ils prirent sa main et la main de sa femme et de ses deux filles, parce que le Seigneur lui faisait grâce.
Alipositasita, wale watu wakamshika mkono wake na mikono ya mke wake na binti zake wawili na kuwaongoza salama nje ya mji, kwa kuwa Bwana alikuwa na huruma kwao.
17 Et ils l’emmenèrent, le mirent hors de la ville: et là, ils lui parlèrent, disant: Sauve ton âme; ne regarde point derrière toi, et ne t’arrête dans aucune contrée d’alentour; mais sauve-toi sur la montagne, de peur que tu ne périsses toi aussi avec les autres.
Mara walipokwisha kuwatoa nje, mmoja wao akawaambia, “Mkimbie kwa usalama wenu! Msitazame nyuma, wala msisimame popote katika nchi tambarare! Kimbilieni milimani, ama sivyo mtaangamizwa!”
18 Et Lot leur répondit: Je vous prie, mon Seigneur,
Lakini Loti akawajibu, “La hasha, bwana zangu, tafadhalini!
19 Puisque votre serviteur a trouvé grâce devant vous et que vous avez signalé la miséricorde que vous m’avez faite, pour sauver mon âme, non, je ne puis être sauvé sur la montagne; il est à craindre que le mal ne m’atteigne, et que je ne meure.
Mtumishi wenu amepata kibali mbele ya macho yenu, nanyi mmeonyesha wema mkubwa kwangu kwa kuokoa maisha yangu. Lakini siwezi kukimbilia milimani, janga hili litanikumba, nami nitakufa.
20 Cette ville ici près, où je puis m’enfuir, est petite et j’y serai sauvé; n’est-elle pas de peu d’étendue? et mon âme n’y vivra-t-elle pas?
Tazama, hapa kuna mji karibu wa kukimbilia, nao ni mdogo. Niruhusuni nikimbilie humo, ni mdogo sana, ama sivyo? Ndipo maisha yangu yatasalimika.”
21 Et il lui répondit: Voici que même en cela, j’ai accueilli ta prière, de ne pas détruire la ville pour laquelle tu m’as parlé.
Akamwambia, “Vema sana, nitalikubali hili ombi pia, sitauangamiza mji ulioutaja.
22 Hâte-toi, et tu y seras sauvé; car je ne pourrai rien faire jusqu’à ce que tu y sois entré. C’est pourquoi cette ville fut appelée du nom de Ségor.
Lakini ukimbilie huko haraka, kwa sababu sitaweza kufanya lolote mpaka ufike huko.” (Ndiyo maana mji huo ukaitwa Soari.)
23 Le soleil se leva sur la terre, et Lot entra dans Ségor.
Wakati Loti alipofika Soari, jua lilikuwa limechomoza katika nchi.
24 Le Seigneur donc fit pleuvoir sur Sodome et Gomorrhe du soufre et du feu venus du ciel d’auprès du Seigneur;
Ndipo Bwana akanyesha moto wa kiberiti uliotoka mbinguni kwa Bwana juu ya Sodoma na Gomora.
25 Et il détruisit ces villes, et toute la contrée d’alentour, et tous les habitants des villes, et toutes les plantes de la terre.
Hivyo akaiteketeza miji ile na eneo lote la tambarare, pamoja na wote waliokuwa wanaishi katika miji, hata pia mimea yote katika nchi.
26 Et la femme de Lot, regardant derrière elle, fut changée en une statue de sel.
Lakini mke wa Loti akatazama nyuma, hivyo akawa nguzo ya chumvi.
27 Or Abraham se levant le matin, et venant où il avait été auparavant avec le Seigneur,
Asubuhi na mapema siku iliyofuata, Abrahamu akaamka na kurudi mahali pale aliposimama mbele za Bwana.
28 Regarda Sodome et Gomorrhe, et toute la terre de cette contrée, et il vit une fumée qui montait de la terre, comme la fumée d’une fournaise.
Akatazama upande wa Sodoma na Gomora, kuelekea nchi yote ya tambarare, akaona moshi mzito ukipanda kutoka kwenye nchi, kama moshi utokao kwenye tanuru.
29 Mais, lorsque le Seigneur détruisait les villes de cette contrée, s’étant souvenu d’Abraham, il sauva Lot de la ruine de ces villes dans lesquelles il avait habité.
Kwa hiyo Mungu alipoiangamiza miji ya tambarare alimkumbuka Abrahamu, akamtoa Loti kutoka kwenye lile janga lililoharibu miji ile ambamo Loti alikuwa ameishi.
30 Et Lot sortit de Ségor; il se retira sur la montagne, et ses deux filles avec lui (car il craignait de demeurer dans Ségor), et il demeura dans la caverne, lui et ses deux filles avec lui.
Loti na binti zake wawili waliondoka Soari na kufanya makao yao kule milimani, kwa maana aliogopa kukaa Soari. Yeye na binti zake wawili waliishi katika pango.
31 Or l’aînée dit à la plus jeune: Notre père est vieux, et il n’est resté sur la terre aucun homme qui puisse nous épouser selon la coutume de toute la terre.
Siku moja binti mkubwa akamwambia yule mdogo, “Baba yetu ni mzee na hakuna mwanaume mahali hapa atakayekutana na sisi kimwili, kama ilivyo desturi ya mahali pote duniani.
32 Viens, et enivrons-le de vin, et dormons avec lui, afin que nous puissions par notre père conserver une postérité.
Tumnyweshe baba yetu mvinyo kisha tukutane naye kimwili ili tuhifadhi uzao wetu kupitia baba yetu.”
33 Elles donnèrent donc à leur père du vin à boire cette nuit-là; et l’aînée vint et dormit avec son père; mais celui-ci ne s’aperçut, ni quand sa fille se coucha, ni quand elle se leva.
Usiku ule walimnywesha baba yao mvinyo, alipolewa binti yake mkubwa akaingia na kukutana naye kimwili. Baba yao hakujua wakati binti yake alipoingia kulala naye wala alipotoka.
34 Et le lendemain, l’aînée dit à la plus jeune: Voilà que j’ai dormi hier avec mon père; donnons-lui à boire du vin encore cette nuit, et tu dormiras avec lui, afin que nous conservions une postérité de notre père.
Siku iliyofuata binti mkubwa akamwambia yule mdogo, “Usiku uliopita mimi nilikutana kimwili na baba yangu. Tumnyweshe divai tena, usiku huu nawe ukutane naye kimwili ili tuweze kuhifadhi uzao wetu kupitia baba yetu.”
35 Et elles donnèrent encore cette nuit-là à leur père du vin à boire; et la plus jeune fille dormit avec lui; et encore cette fois, il ne s’aperçut pas quand elle se coucha, ou quand elle se leva.
Kwa hiyo wakamnywesha baba yao mvinyo tena usiku ule, naye binti yake mdogo akaingia, akakutana naye kimwili. Kwa mara nyingine baba yao hakujua binti yake alipolala naye wala alipoondoka.
36 Ainsi les deux filles de Lot conçurent de leur père.
Hivyo binti wawili wa Loti wakapata mimba kwa baba yao.
37 L’aînée enfanta un fils, et l’appela du nom de Moab; c’est le père des Moabites, jusqu’au présent jour.
Binti mkubwa akamzaa mwana, akamwita jina lake Moabu; ndio baba wa Wamoabu hata leo.
38 La plus jeune aussi enfanta un fils, et l’appela du nom d’Ammon, c’est-à-dire le fils de mon peuple; c’est le père des Ammonites, jusqu’aujourd’hui.
Binti mdogo naye pia akamzaa mwana, naye akamwita Benami; ndiye baba wa Waamoni hata leo.

< Genèse 19 >