< Esdras 7 >

1 Or, après ces choses, sous le règne d’Artaxerxès, roi des Perses, Esdras, fils de Saraïas, fils d’Azarias, fils de Helcias,
Baada ya mambo haya, wakati wa utawala wa Artashasta mfalme wa Uajemi, Ezra mwana wa Seraya, mwana wa Azaria, mwana wa Hilkia,
2 Fils de Sellum, fils de Sadoc, fils d’Achitob,
mwana wa Shalumu, mwana wa Sadoki, mwana wa Ahitubu,
3 Fils d’Amarias, fils d’Azarias, fils de Maraïoth,
mwana wa Amaria, mwana wa Azaria, mwana wa Merayothi,
4 Fils de Zarahias, fils d’Ozi, fils de Bocci,
mwana wa Zerahia, mwana wa Uzi, mwana wa Buki,
5 Fils d’Abisué, fils de Phinéès, fils d’Eléazar, fils d’Aaron, prêtre dès le commencement,
mwana wa Abishua, mwana wa Finehasi, mwana wa Eleazari, mwana wa kuhani mkuu Aroni.
6 Esdras lui-même monta de Babylone, et il était scribe habile dans la loi de Moïse, que le Seigneur Dieu a donnée à Israël; et le roi lui accorda toute sa demande, à cause que la main du Seigneur son Dieu était sur lui.
Huyu Ezra alipanda kutoka Babeli. Alikuwa mwalimu mwenye ujuzi mzuri katika sheria ya Mose, ambayo Bwana, Mungu wa Israeli, alikuwa ametoa. Mfalme alikuwa amempa Ezra kila kitu alichoomba, kwa maana Bwana Mungu wake alikuwa pamoja naye.
7 Or il monta des enfants d’Israël, des fils des prêtres, des fils des Lévites, des chantres, des portiers et des Nathinéens, à Jérusalem, la septième année du roi Artaxerxès.
Pia baadhi ya Waisraeli, wakiwemo makuhani, Walawi, waimbaji, mabawabu na watumishi wa Hekalu, nao walikuja Yerusalemu mwaka wa saba wa utawala wa Mfalme Artashasta.
8 Et ils vinrent à Jérusalem au cinquième mois; c’est la septième année du roi;
Ezra aliwasili Yerusalemu mwezi wa tano wa mwaka wa saba wa utawala wa Mfalme Artashasta.
9 Parce qu’au premier jour du premier mois, Esdras commença à monter de Babylone, et, au premier jour du cinquième mois, il vint à Jérusalem, à cause que la main favorable de son Dieu était sur lui.
Ezra alianza safari yake kutoka Babeli tangu siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, naye akawasili Yerusalemu siku ya kwanza ya mwezi wa tano, kwa maana mkono wa neema wa Mungu wake ulikuwa juu yake.
10 Car Esdras disposa son cœur à rechercher la loi du Seigneur, et à faire et à enseigner en Israël les préceptes et les ordonnances.
Kwa maana Ezra alikuwa amejitoa kwa moyo wote kujifunza na kushika sheria ya Bwana na kuwafundisha watu wa Israeli amri na sheria zake.
11 Or voici la copie de la lettre contenant l’édit que donna le roi Artaxerxès à Esdras, le prêtre instruit dans les paroles et les préceptes du Seigneur et dans ses cérémonies en Israël:
Hii ni nakala ya barua ambayo Mfalme Artashasta alikuwa amempa Ezra aliyekuwa kuhani na mwalimu, mtu aliyeelimika katika mambo yahusuyo maagizo na amri za Bwana kwa Israeli.
12 Artaxerxès, roi des rois, à Esdras, le prêtre, scribe de la loi du Dieu du ciel, très instruit, salut.
Artashasta, mfalme wa wafalme, Kwa Ezra kuhani, mwalimu wa Sheria ya Mungu wa mbinguni: Salamu.
13 Il a été ordonné par moi que quiconque dans mon royaume est du peuple d’Israël, et de ses prêtres et de ses Lévites, et à qui il plaira de monter à Jérusalem, aille avec toi:
Sasa naamuru kwamba mtu yeyote Mwisraeli katika ufalme wangu, pamoja na makuhani na Walawi, ambaye anataka kwenda Yerusalemu pamoja nawe aweza kwenda.
14 Car tu es envoyé de la part du roi et de ses sept conseillers, afin que tu visites la Judée et Jérusalem, selon la loi de ton Dieu, qui est en ta main;
Unatumwa na mfalme na washauri wake saba kuchunguza kuhusu Yuda na Yerusalemu kulingana na Sheria ya Mungu wako, iliyoko mkononi mwako.
15 Et afin que tu portes l’argent et l’or que le roi et ses conseillers ont spontanément offerts au Dieu d’Israël, dont le tabernacle est à Jérusalem!
Zaidi ya hayo, uchukue pamoja nawe fedha na dhahabu ambazo mfalme na washauri wake wamempa Mungu wa Israeli kwa hiari, Mungu ambaye maskani yake yako Yerusalemu,
16 Et tout l’argent et l’or que tu trouveras dans toute la province de Babylone, que le peuple voudra offrir, et ce que quelques-uns d’entre les prêtres auront spontanément offert à la maison de leur Dieu, qui est à Jérusalem,
pia fedha na dhahabu zote unazoweza kupata kutoka jimbo la Babeli, pamoja na sadaka za hiari watakazotoa watu na makuhani kwa ajili ya Hekalu la Mungu wao katika Yerusalemu.
17 Prends-le librement, et achète soigneusement avec cet argent des veaux, des béliers, des agneaux, des sacrifices et leurs libations, et offre-les sur l’autel du temple de votre Dieu, qui est à Jérusalem.
Hakikisha kwamba fedha hizi zimetumika kununua mafahali, kondoo dume na wana-kondoo pamoja na sadaka za nafaka na sadaka za vinywaji, uvitoe dhabihu juu ya madhabahu ya Hekalu la Mungu wenu katika Yerusalemu.
18 Mais de plus, s’il te plaît, à toi et à tes frères, de faire quelque chose avec le reste de l’argent et de l’or, faites-le selon la volonté de Dieu.
Kisha wewe na Wayahudi ndugu zako mnaweza kufanya lolote linaloonekana jema sana kwa fedha na dhahabu zilizosalia, kulingana na mapenzi ya Mungu wenu.
19 Les vases aussi qui te sont donnés pour le service de la maison de ton Dieu, mets-les en la présence de Dieu à Jérusalem;
Uvitoe kwa Mungu wa Yerusalemu vyombo vyote ulivyokabidhiwa kwa ajili ya ibada katika Hekalu la Mungu wako.
20 Mais quant à toutes les autres choses dont on a besoin pour la maison de ton Dieu, quelque considérable que soit ce qu’il sera nécessaire que tu dépenses, il te sera donné du trésor et du fisc du roi,
Kitu kingine chochote kinachohitajika kwa ajili ya Hekalu la Mungu wenu ambacho unatakiwa kukitoa, waweza kukitoa kutoka hazina ya mfalme.
21 Et par moi. Moi, Artaxerxès, le roi, j’ai établi et j’ai ordonné à tous les gardes du trésor public qui sont au-delà du fleuve, disant: Que tout ce que vous demandera Esdras, le prêtre, le scribe de la loi du Dieu du ciel, vous le donniez sans délai,
Mimi, Mfalme Artashasta, sasa naagiza watunza hazina wote wa Ngʼambo ya Mto Frati kutoa kwa bidii chochote kwa Ezra kuhani na mwalimu wa Sheria ya Mungu wa mbinguni atakachohitaji kwenu,
22 Jusqu’à cent talents d’argent, et jusqu’à cent cors de froment, et jusqu’à cent bats de vin, et jusqu’à cent bats d’huile: mais du sel sans mesure.
talanta 100 za fedha, ngano kori 100, divai bathi 100, mafuta ya zeituni bathi 100, na chumvi kiasi chochote.
23 Que tout ce qui appartient au culte du Dieu du ciel soit fourni soigneusement dans la maison du Dieu du ciel, de peur qu’il ne s’irrite contre le royaume du roi et de ses fils.
Chochote ambacho Mungu wa mbinguni ameagiza, kifanyike kwa ukamilifu kwa ajili ya Hekalu la Mungu wa mbinguni. Kwa nini pawepo ghadhabu dhidi ya utawala wa mfalme na wanawe?
24 À vous aussi nous faisons savoir, par rapport à tous les prêtres, Lévites, chantres, portiers, Nathinéens et ministres de cette maison de Dieu, que vous n’avez le pouvoir d’imposer sur eux ni impôts, ni tribut, ni vivres.
Pia ninyi fahamuni kuwa hamna mamlaka ya kuwatoza kodi, ushuru au ada makuhani, Walawi, waimbaji, mabawabu, watumishi wa Hekalu au wafanyakazi wengine kwenye nyumba ya Mungu.
25 Or toi, Esdras, selon la sagesse de ton Dieu laquelle est en ta main, établis des juges, et des présidents, afin qu’ils jugent tout le peuple qui est au-delà du fleuve, c’est-à-dire ceux qui connaissent la loi de ton Dieu; mais les ignorants, enseigne-les librement.
Nawe Ezra, kufuatana na hekima ya Mungu wenu uliyo nayo, weka mahakimu na waamuzi wote wanaozifahamu sheria za Mungu wenu ili watoe haki kwa watu wote wa Ngʼambo ya Mto Frati. Nawe inakupasa umfundishe yeyote ambaye hazifahamu.
26 Et quiconque n’observera point la loi de ton Dieu, et la loi du roi soigneusement, il y aura contre lui une condamnation, soit à la mort, soit à l’exil, soit à la confiscation de ses biens, ou certainement à la prison.
Yeyote ambaye hataitii sheria ya Mungu wenu pia sheria ya mfalme, hakika lazima aadhibiwe kwa kuuawa, kuhamishwa, kunyangʼanywa mali au kufungwa gerezani.
27 Béni le Seigneur, Dieu de nos pères, qui a mis dans le cœur du roi de glorifier la maison du Seigneur qui est à Jérusalem,
Sifa ziwe kwa Bwana, Mungu wa baba zetu, Mungu ambaye kwa njia hii ameweka ndani ya moyo wa mfalme kuipa heshima nyumba ya Bwana iliyoko Yerusalemu, kwa namna hii
28 Et qui a incliné sa miséricorde vers moi devant le roi et ses conseillers, et devant tous les puissants princes du roi! Et moi, fortifié par la main du Seigneur mon Dieu, laquelle était sur moi, j’ai assemblé les princes d’Israël pour monter avec moi.
ambaye ameniongezea kibali chake mbele ya mfalme, washauri wake na maafisa wote wa mfalme wenye uwezo. Kwa kuwa mkono wa Bwana Mungu wangu ulikuwa pamoja nami, nilijipa moyo nikakusanya watu walio viongozi kutoka Israeli wakwee pamoja nami.

< Esdras 7 >