< Esdras 5 >

1 Or Aggée, le prophète, et Zacharie, fils d’Addo, prophétisèrent, prophétisant aux Juifs qui étaient en Judée et à Jérusalem, au nom du Dieu d’Israël.
Ndipo Hagai nabii na Zakaria mtoto wa Ido nabii wakatabiri kwa jina la Mungu wa Israel kwa wayahudi wa Yuda na Yerusalem.
2 Alors se levèrent Zorobabel, fils de Salathiel, et Josué, fils de Josédec, et ils commencèrent à bâtir le temple de Dieu à Jérusalem, et avec eux les prophètes de Dieu qui les aidaient.
Zerubabeli mtoto wa Shealtieli na Yoshua mtoto wa Yosadaki wakainuka na kuanza kujenga nyumba ya Mungu Yerusalem pamoja na manabii ambao waliwahamasisha wao.
3 Or, en ce temps-là, vinrent vers eux Thathanaï, qui était chef au-delà du fleuve, et Stharbuzanaï, et leurs conseillers, et c’est ainsi qu’ils leur dirent: Qui vous a donné le conseil de bâtir cette maison et de restaurer ses murs?
Ndipo Tatenai Mkuu wa mji ngambo ya mto, Shethar - Bozenai, na mshirika wao, wakaja na kusema kwao, “Nani aliyewapa agizo la kujenga nyumba hii na kukamilisha ukuta?”
4 À quoi nous répondîmes en leur disant quels étaient les noms des hommes auteurs de cette construction.
Vilevile walisema, “Ni majina ya watu gani wanaoshughulika na ujenzi huu?”
5 Or l’œil de leur Dieu fut sur les anciens des Juifs, et ils ne purent les empêcher. Et il leur plut que l’affaire fût renvoyée à Darius, et qu’alors ils répondraient à cette accusation.
Lakini jicho la Mungu lilikuwa pamoja na viongozi wa Wayahudi na maadui wao hawakuweza kuwazuia. Walikuwa wakisubiri barua kutumwa kwa mfalme na amri kurudi kwao kwa ajili ya suala hili.
6 Copie de la lettre que Thathanaï, chef de la contrée au-delà du fleuve, et Stharbuzanaï et ses conseillers Arphasachéens, qui étaient au-delà du fleuve, envoyèrent à Darius, le roi.
Hii ni nakala ya barua kwa Tatenai, mkuu wa mji ngambo ya mto, na Shethar - Bozenai na wenzao katika mji ngambo ya Mto, ambao waliwatuma kwa mfalme Dario.
7 La parole qu’ils lui avaient envoyée était écrite ainsi: À Darius, le roi, toute paix.
Wakatuma ujumbe, wakiandika kwa mfalme Dario, “Amani tele iwe kwako”
8 Qu’il soit connu du roi que nous sommes allés dans la province de Judée, dans la maison du grand Dieu que l’on bâtit de pierres non polies et dont on pose les bois sur les murailles. Or cet ouvrage s’élève avec diligence et s’accroît entre leurs mains.
Mfalme atambue kwamba tulikwenda Yuda kwenye nyumba ya Mungu Mkuu. Imeshajengwa kwa mawe makubwa na mbao zimewekwa katika kuta. Hii kazi inafanyika kwa utaratibu na inaendelea vizuri kwa mikono yao.
9 Nous avons donc interrogé les vieillards, et c’est ainsi que nous leur avons dit: Qui vous a donné le pouvoir de bâtir cette maison et de rétablir ces murs?
Tukawauliza wazee, ni nani aliyewapa agizo la kujenga nyumba na ukuta?'
10 Mais nous leur avons aussi demandé leurs noms, afin de vous les indiquer, et nous avons écrit les noms des hommes qui sont les princes parmi eux.
Pia tuliwauliza majina yao ili kwamba ujue majina ya kila mtu ambaye aliwaongoza.
11 Or ils nous ont répondu ces paroles, disant: Nous sommes serviteurs du Dieu du ciel et de la terre; nous bâtissons le temple qui était construit beaucoup d’années avant celles-ci, et que le grand roi d’Israël avait bâti et construit.
Nao wakatujibu na kusema, “Sisi tu watumishi wa Mungu wa mbingu na nchi na sisi tunaijenga nyumba hii ambayo ilijengwa miaka mingi iliyopita wakati mfalme mkuu wa Israel alijenga na kuikamisha.
12 Mais après que nos pères eurent provoqué au courroux le Dieu au ciel, il les livra entre les mains de Nabuchodonosor, roi de Babylone, Chaldéen; et il détruisit même cette maison, et transporta son peuple à Babylone.
Ingawa, watangulizi wetu walipomchukiza Mungu wa mbinguni, Mungu akawatia katika mikono ya mfalme wa Babeli Nebukadineza, ambaye alivunja nyumba na kuwachukua watu mateka Babeli.
13 Or, à la première année de Cyrus, roi de Babylone, le roi Cyrus publia un édit afin que cette maison de Dieu fût bâtie.
Pia, katika mwaka wa kwanza wa kutawala Koreshi mfalme wa Babeli, Koreshi aliamuru nyumba ya Mungu kujengwa.
14 Et même les vases d’or et d’argent du temple de Dieu, que Nabuchodonosor avait enlevés du temple qui était à Jérusalem, et qu’il avait apportés dans le temple de Babylone, le roi Cyrus les tira du temple de Babylone, et ils furent donnés à un nommé Sassabasar, qu’il établit même prince.
Mfalme Koreshi pia alirudisha vitu vya dhahabu na fedha vya nyumba ya Mungu ambavyo Nebukadineza alivichukua kwenye hekalu Yerusalem na kuvipeleka kwenye hekalu Babeli. Naye akavitunza kwa Sheshbaza, ambaye alimchagua kuwa kiongozi.
15 Et il lui dit: Prends ces vases, et va, et mets-les dans le temple qui est à Jérusalem, et que la maison de Dieu soit bâtie en son lieu.
Naye akamwambia, “Chukua hivi vitu. Uondoke na kuviweka kwenye Hekalu Yerusalem. Na nyumba ya Mungu ijengwe kule.”
16 Alors donc ce Sassabasar vint, et posa les fondements du temple de Dieu à Jérusalem, et, depuis ce temps-là jusqu’à présent, on le bâtit, et il n’est pas encore achevé.
Ndipo huyu Sheshbaza akaja na kuweka msingi kwa nyumba ya Mungu katika Yerusalem: na ikaendelea kujengwa, lakini bado haijakamilika
17 Maintenant donc, s’il semble bon au roi, qu’il recherche dans la bibliothèque du roi, qui est à Babylone, s’il a été ordonné par le roi Cyrus que la maison de Dieu serait rebâtie à Jérusalem, et qu’il nous envoie la volonté du roi sur cela.
Sasa ikiwa itampendeza mfalme, na uchunguzi ufanyike kwenye nyumba ya ukumbusho Babeli Ikiwapo hukumu ya mfalme wa Koreshi ya kujenga nyumba ya Mungu Yerusalem. Na mfalme anaweza kutuma uamuzi wake kwetu.

< Esdras 5 >