< Ézéchiel 45 >

1 Et lorsque vous commencerez à diviser la terre par le sort, séparez les prémices pour le Seigneur; un lieu de la terre sanctifié, d’une longueur de vingt-cinq mille coudées, et d’une largeur de dix mille; il sera sanctifié dans toute sa limite autour.
“‘Mtakapogawa nchi kuwa urithi, mtaitoa sehemu ya nchi kwa Bwana kuwa eneo takatifu, urefu wake dhiraa 25,000, upana wake dhiraa 20,000 eneo hili lote litakuwa takatifu.
2 Et il y aura de sanctifié de tout côté cinq cents coudées en carré tout autour, et cinquante coudées encore pour ses faubourgs aux environs.
Katika hiyo, itakuwepo sehemu mraba ambayo ni mahali patakatifu kila upande dhiraa 500 ikiwa imezungukwa na eneo la wazi lenye upana wa dhiraa hamsini.
3 Et d’après cette mesure, tu mesureras une longueur de vingt-cinq mille coudées, et une largeur de dix mille, et dans ce lieu même sera le temple, et le saint des saints.
Katika eneo takatifu, pima sehemu yenye urefu wa dhiraa 25,000 na upana wa dhiraa 10,000. Ndani ya hilo eneo kutakuwa mahali patakatifu, Patakatifu pa Patakatifu.
4 Ce qu’il y aura de sanctifié de cette terre sera pour les prêtres, ministres du sanctuaire, qui s’approchent du ministère du Seigneur; et ce lieu sera pour leurs maisons, et pour le sanctuaire de sainteté.
Itakuwa sehemu takatifu ya nchi kwa ajili ya makuhani, wale wanaohudumu ndani ya mahali patakatifu na ambao hukaribia ili kuhudumu mbele za Bwana. Patakuwa mahali pa nyumba zao pamoja na sehemu kwa ajili ya mahali patakatifu.
5 Or, vingt-cinq mille coudées de longueur et dix mille de largeur seront pour les Lévites qui servent dans la maison; ils posséderont aussi eux-mêmes vingt chambres.
Eneo la urefu wa dhiraa 25,000 na upana wa dhiraa 10,000 litakuwa la Walawi wale wanaotumika hekaluni, kama milki yao kwa ajili ya miji ya kuishi.
6 Et pour la possession de la cité, vous donnerez cinq mille coudées de largeur, et de longueur vingt-cinq mille, selon ce qui est séparé pour le sanctuaire; et ce sera pour toute la maison d’Israël.
“‘Utatoa mji kama mali yao wenye upana wa dhiraa 5,000 na urefu wa dhiraa 25,000, karibu na sehemu takatifu, itakuwa mali ya nyumba yote ya Israeli.
7 Au prince aussi vous donnerez ce qui s’étendra de part et d’autre, le long de ce qui a été séparé pour le sanctuaire et pour la possession de la cité, vis-à-vis de ce qui a été séparé pour le sanctuaire, et vis-à-vis de la possession de la ville; depuis le côté de la mer jusqu’à la mer, et depuis le côté de l’orient jusqu’à l’orient; or la longueur de sa possession sera égale dans chacune de ses portions, depuis les bornes de l’occident jusqu’aux bornes de l’orient.
“‘Mkuu anayetawala atakuwa na lile eneo linalopakana na lile eneo lililowekwa wakfu upande huu na upande huu na eneo la mji. Eneo la mji litaenea upande wa magharibi kuanzia upande wa magharibi na upande wa mashariki kuanzia upande wa mashariki, likiendelea kwa urefu kutoka magharibi hadi mpaka wa mashariki sambamba na mojawapo ya sehemu za makabila.
8 Il aura une possession de la terre dans Israël, et les princes ne dépouilleront plus mon peuple, mais ils donneront la terre à la maison d’Israël, selon leurs tribus.
Nchi hii itakuwa milki yake katika Israeli. Nao wakuu wangu hawataonea tena watu wangu bali watairuhusu nyumba ya Israeli kuimiliki nchi kulingana na makabila yao.
9 Voici ce que dit le Seigneur Dieu: Que cela vous suffise, princes d’Israël; cessez l’iniquité et les rapines; faites jugement et justice; séparez vos confins de ceux de mon peuple, dit le Seigneur Dieu.
“‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Yatosha, enyi wakuu wa Israeli! Acheni mbali ukatili wenu na uonevu wenu mkafanye lile lililo haki na sawa. Acheni kuwatoza watu wangu isivyo haki, asema Bwana Mwenyezi.
10 Vous aurez une balance juste, et un éphi juste, et un bat juste.
Tumieni mizani sahihi na vipimo sahihi vya efa na bathi.
11 L’éphi et le bat seront égaux, et d’une même mesure; en sorte que le bat tiendra la dixième partie du cor, et l’éphi la dixième partie du cor; leur poids sera égal, par rapport à la mesure du cor.
Efa na bathi viwe sawa, bathi iwe sehemu ya kumi ya homeri na efa iwe sehemu ya kumi ya homeri, homeri itakuwa ndicho kiwango cha kukubalika kwa vyote viwili.
12 Mais le sicle a vingt oboles. Or vingt sicles, et vingt-cinq sicles, et quinze sicles, font la mine.
Shekeli moja itakuwa gera ishirini. Shekeli ishirini, jumlisha na shekeli ishirini na tano, jumlisha na shekeli kumi na tano zitakuwa mina moja.
13 Et voici quelles seront les prémices que vous prendrez: la sixième partie de l’éphi sur un cor de froment; et la sixième partie de l’éphi sur un cor d’orge.
“‘Hili ndilo toleo maalum mtakalotoa: moja ya sita ya efa kutoka kila homeri ya ngano na moja ya sita ya efa kutoka kila homeri ya shayiri.
14 Voici aussi la mesure de l’huile: le bat d’huile est la dixième partie du cor; et les dix bats font un cor, parce que les dix bats remplissent un cor.
Sehemu ya mafuta iliyoamriwa, yaliyopimwa kwa bathi, ni sehemu ya kumi ya bathi kutoka kila kori moja (ambayo ina bathi kumi au homeri moja.)
15 Et ils offriront un bélier d’un troupeau de deux cents bêtes de celles que le peuple d’Israël nourrit pour le sacrifice, et pour l’holocauste, et pour les oblations pacifiques, afin d’expier leurs fautes, dit le Seigneur Dieu.
Pia kondoo mmoja atachukuliwa kutoka kwenye kila kundi la kondoo mia mbili kutoka kwenye malisho yaliyonyeshewa vizuri ya Israeli. Hivi vitatumika kwa ajili ya sadaka ya nafaka, sadaka ya kuteketezwa na sadaka za amani ili kufanya upatanisho kwa ajili ya watu, asema Bwana Mwenyezi.
16 Tout le peuple du pays sera obligé à ces prémices pour le prince en Israël.
Watu wote wa nchi wataungana pamoja na mkuu anayetawala Israeli ili kutoa hii sadaka maalum.
17 Et à la charge du prince seront les holocaustes, et le sacrifice, et les libations dans les solennités, et dans les calendes et dans les sabbats, et dans toutes les solennités de la maison d’Israël; c’est lui qui offrira le sacrifice pour le péché, l’holocauste et les victimes pacifiques pour l’expiation de la maison d’Israël.
Huu utakuwa ndio wajibu wa mkuu anayetawala kutoa sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya nafaka na sadaka ya kinywaji kwenye sikukuu, Mwezi Mwandamo na Sabato, kwenye sikukuu zote zilizoamriwa za nyumba ya Israeli. Atatoa sadaka za dhambi, sadaka za nafaka, sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani ili kufanya upatanisho kwa ajili ya nyumba ya Israeli.
18 Voici ce que dit le Seigneur Dieu: Au premier mois, et au premier jour de ce mois, tu prendras d’un troupeau un veau sans tache, et tu expieras le sanctuaire.
“‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika mwezi wa kwanza, siku ya kwanza ya huo mwezi utamchukua fahali mchanga asiye na dosari na kutakasa mahali patakatifu.
19 Et le prêtre prendra du sang qui sera pour le péché, et il en mettra aux poteaux de la maison, aux quatre coins du rebord de l’autel, et aux poteaux de la porte du parvis intérieur.
Kuhani itampasa achukue sehemu ya hiyo damu ya sadaka ya dhambi na kuipaka kwenye miimo ya Hekalu, kwenye pembe nne za juu za ukingo wa hayo madhabahu na juu ya miimo ya lango la ukumbi wa ndani.
20 Et ainsi tu feras au septième jour du mois pour quiconque a péché par ignorance, et a été trompé par une erreur humaine, et tu expieras ainsi la maison.
Itakupasa kufanya vivyo hivyo katika siku ya saba ya mwezi huo kwa ajili ya mtu yeyote ambaye hutenda dhambi bila kukusudia au bila kujua, hivyo utafanya upatanisho kwa ajili ya Hekalu.
21 Au premier mois, et au quatorzième jour de ce mois, sera pour vous la solennité de la Pâque; sept jours durant, on mangera des azymes.
“‘Katika mwezi wa kwanza siku ya kumi na nne utaadhimisha Pasaka. Sikukuu itaendelea kwa siku saba, wakati huo wa hizo siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu.
22 Et le prince offrira en ce jour-là pour lui-même et pour tout le peuple du pays, un veau en sacrifice pour le péché;
Katika siku hiyo mkuu anayetawala atatoa fahali kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili yake mwenyewe na kwa ajili ya watu wote wa nchi.
23 Et pendant la solennité des sept jours, il offrira en holocauste au Seigneur sept veaux et sept béliers sans tache, chaque jour durant les sept jours, et pour le péché, un bouc de chèvres chaque jour.
Kila siku wakati wa hizo siku saba za sikukuu atatoa mafahali saba na kondoo dume saba wasio na dosari kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana na beberu kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
24 Et il offrira en sacrifice un éphi de farine par veau, et un éphi par bélier, et un hin d’huile par chaque éphi.
Pia atatoa sadaka ya nafaka efa moja kwa kila fahali na efa moja kwa kila kondoo dume, pamoja na hini moja ya mafuta kwa kila efa.
25 Au septième mois, au quinzième jour de ce mois, pendant la solennité, il fera sept jours de suite les mêmes choses qui ont été dites auparavant, tant pour l’expiation du péché, que pour l’holocauste, et pour le sacrifice des oblations et pour l’huile.
“‘Wakati wa hizo siku saba za sikukuu, ambayo huanza katika mwezi wa saba kwenye siku ya kumi na tano, mkuu anayetawala atatoa mahitaji yale yale kwa ajili ya sadaka za dhambi, sadaka za kuteketezwa, sadaka za nafaka na mafuta.

< Ézéchiel 45 >