< Ézéchiel 32 >

1 Et il arriva, en la douzième année, au douzième mois, au premier jour du mois, que la parole du Seigneur me fut adressée, disant:
Katika mwaka wa kumi na mbili, mwezi wa kumi na mbili, siku ya kwanza ya mwezi, neno la Bwana likanijia, kusema:
2 Fils d’un homme, fais entendre des lamentations sur Pharaon, roi d’Egypte, et tu lui diras: Tu as été assimilé à un lion de nations et au dragon qui est dans la mer, et tu agitais ta corne dans tes fleuves, et tu troublais les eaux avec tes pieds, et tu foulais leurs fleuves.
“Mwanadamu, fanya maombolezo kwa ajili ya Farao mfalme wa Misri na umwambie: “‘Wewe ni kama simba miongoni mwa mataifa, wewe ni kama joka kubwa baharini, unayevuruga maji kwa miguu yako na kuchafua vijito.
3 À cause de cela, voici ce que dit le Seigneur: J’étendrai sur toi mon filet par une multitude de peuples nombreux, et je t’entraînerai dans mon filet.
“‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Nikiwa pamoja na wingi mkubwa wa watu nitautupa wavu wangu juu yako, nao watakukokota katika wavu wangu.
4 Je te jetterai sur la terre, et je t’étendrai sur la face d’un champ; et je ferai habiter sur toi tous les volatiles du ciel, et je rassasierai de toi toutes les bêtes de la terre.
Nitakutupa nchi kavu na kukuvurumisha uwanjani. Nitawafanya ndege wote wa angani watue juu yako na wanyama wote wa nchi watajishibisha nyama yako.
5 J’exposerai ta chair sur les montagnes, et je remplirai les collines de ta sanie.
Nitatawanya nyama yako juu ya milima na kujaza mabonde kwa mabaki yako.
6 J’arroserai la terre sur les montagnes de ton sang infect; et les vallées seront remplies de toi.
Nitailowanisha nchi kwa damu yako inayotiririka njia yote hadi milimani, nayo mabonde yatajazwa na nyama yako.
7 Et lorsque tu t’éteindras, je couvrirai le ciel, et je ferai noircir ses étoiles; je couvrirai le soleil d’un nuage, et la lune ne donnera pas sa lumière.
Nitakapokuzimisha, nitafunika mbingu na kuzitia nyota zake giza; nitalifunika jua kwa wingu, nao mwezi hautatoa nuru yake.
8 Tous les flambeaux du ciel, je les ferai s’affliger sur toi; et je répandrai des ténèbres sur ta terre, dit le Seigneur Dieu; lorsque tomberont tes blessés sur la terre, dit le Seigneur Dieu.
Mianga yote itoayo nuru angani nitaitia giza juu yako; nitaleta giza juu ya nchi yako, asema Bwana Mwenyezi.
9 Et j’irriterai le cœur de peuples nombreux, lorsque j’apprendrai ta destruction parmi les nations, à des pays que tu ne connais pas.
Nitaifadhaisha mioyo ya mataifa mengi nitakapokuangamiza miongoni mwa mataifa, nikikuleta uhamishoni miongoni mwa nchi ambazo haujapata kuzijua.
10 Et je frapperai de stupeur à ton sujet des peuples nombreux; et leurs rois seront saisis d’effroi et d’une horreur extrême à cause de toi, lorsque mon glaive commencera à voler sur leurs faces, et chacun sera soudainement frappé de stupeur pour son âme au jour de ta ruine.
Nitayafanya mataifa mengi wakustaajabie, wafalme wao watatetemeka kwa hofu kwa ajili yako nitakapotikisa upanga wangu mbele yao. Siku ya anguko lako kila mmoja wao atatetemeka kila dakika kwa ajili ya maisha yake.
11 Parce que voici ce que dit le Seigneur Dieu: Le glaive du roi de Babylone viendra à toi;
“‘Kwa kuwa hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Upanga wa mfalme wa Babeli utakuja dhidi yako.
12 Par les glaives des forts j’abattrai ta multitude; toutes ces nations sont invincibles, et elles détruiront l’orgueil de l’Egypte, et sa multitude sera dissipée.
Nitafanya makundi yako ya wajeuri kuanguka kwa panga za watu mashujaa, taifa katili kuliko mataifa yote. Watakivunjavunja kiburi cha Misri, nayo makundi yake yote ya wajeuri yatashindwa.
13 Et je ferai périr toutes ses bêtes qui étaient le long des grandes eaux; et le pied de l’homme ne les agitera plus, et le sabot des bêtes ne les troublera pas.
Nitaangamiza mifugo yake yote wanaojilisha kando ya maji mengi, hayatavurugwa tena kwa mguu wa mwanadamu wala kwato za mnyama hazitayachafua tena.
14 Alors je rendrai leurs eaux très pures, et je ferai couler leurs fleuves comme l’huile, dit le Seigneur Dieu,
Kisha nitafanya maji yake yatulie na kufanya vijito vyake vitiririke kama mafuta, asema Bwana Mwenyezi.
15 Lorsque j’aurai livré la terre d’Egypte à la désolation; mais la terre sera dénuée de ce qui la remplissait, quand j’aurai frappé tous ses habitants; et ils sauront que je suis le Seigneur.
Nitakapoifanya Misri kuwa ukiwa na kuiondolea nchi kila kitu kilichomo ndani yake, nitakapowapiga wote waishio humo, ndipo watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.’
16 Voici un cantique de deuil, et on le chantera; les filles des nations le chanteront; c’est sur l’Egypte et sur sa multitude qu’elles le chanteront, dit le Seigneur Dieu.
“Hili ndilo ombolezo watakalomwimbia. Binti za mataifa wataliimba, kwa kuwa Misri na makundi yake yote ya wajeuri wataliimba, asema Bwana Mwenyezi.”
17 Et il arriva, en la douzième année, au quinzième jour du mois, que la parole du Seigneur me fut adressée, disant:
Katika mwaka wa kumi na mbili, mwezi wa kwanza, siku ya kumi na tano ya mwezi, neno la Bwana likanijia kusema:
18 Fils d’un homme, chante un cantique lugubre sur la multitude de l’Egypte; et précipite-la, elle-même et les filles des nations puissantes, au fond de la terre, avec ceux qui descendent dans la fosse.
“Mwanadamu, omboleza kwa ajili ya makundi ya wajeuri wa Misri na uwatupe kuzimu yeye na binti za mataifa yenye nguvu, waende huko pamoja nao washukao shimoni. (questioned)
19 Que qui es-tu plus belle? descends, et dors avec les incirconcis.
Je, ninyi mnamzidi nani kwa uzuri? Shukeni chini! Nanyi mkalazwe pamoja na hao wasiotahiriwa!
20 C’est au milieu des tués par le glaive qu’ils tomberont, le glaive a été livré, ils l’ont attirée ainsi que tous ses peuples.
Wataanguka miongoni mwa wale waliouawa kwa upanga. Upanga umefutwa, mwache aburutwe mbali pamoja na hao wajeuri wake wote.
21 Ils lui parleront du milieu de l’enfer, les plus puissants d’entre les forts qui sont descendus avec ses auxiliaires, et qui dorment incirconcis, tués par le glaive. (Sheol h7585)
Kutoka kuzimu viongozi hodari watanena kuhusu Misri pamoja na wale walioungana nao, ‘Wameshuka chini, nao wamelala kimya pamoja na hao wasiotahiriwa, pamoja na wale waliouawa kwa upanga.’ (Sheol h7585)
22 Là est Assur et toute sa multitude; autour de lui sont ses sépulcres, tous les tués, et ceux qui sont tombés sous le glaive;
“Ashuru yuko huko pamoja na jeshi lake lote, amezungukwa na makaburi ya watu wake wote waliouawa, wale wote walioanguka kwa upanga.
23 Dont les sépulcres ont été placés au plus profond d’une fosse; et sa multitude se trouve autour de son tombeau; tous tués et tombés sous le glaive, qui autrefois avaient répandu la frayeur dans la terre des vivants.
Makaburi yao yako kwenye kina cha chini cha shimo na jeshi lake limelala kulizunguka kaburi lake. Wote waliokuwa wameeneza hofu kuu katika nchi ya walio hai wameuawa, wameanguka kwa upanga.
24 Là est Elam, et toute sa multitude autour de son sépulcre; tous ceux-ci tués et tombés sous le glaive; qui sont descendus incirconcis au fond de la terre, qui ont jeté la terreur dans la terre des vivants, et ont porté leur ignominie avec ceux qui descendent dans la fosse.
“Elamu yuko huko, pamoja na makundi yake yote ya wajeuri wakiwa wamelizunguka kaburi lake. Wote wameuawa, wameanguka kwa upanga. Wote waliokuwa wameeneza hofu katika nchi ya walio hai walishuka kuzimu bila kutahiriwa. Wanaichukua aibu yao pamoja na wale washukao shimoni. (questioned)
25 Au milieu des tués on a placé son lit parmi tous ses peuples; autour de lui est son sépulcre; tous ceux-ci sont des incirconcis et des tués par le glaive; car ils jetèrent la terreur dans la terre des vivants, et ils ont porté leur ignominie avec ceux qui descendent dans la fosse; c’est au milieu des tués qu’ils ont été placés.
Kitanda kimetandikwa kwa ajili yake miongoni mwa waliouawa, pamoja na makundi yake yote ya wajeuri wakiwa wamelizunguka kaburi lake. Wote ni watu wasiotahiriwa, wameuawa kwa upanga. Kwa sababu vitisho vyao vilienea katika nchi ya walio hai, wameichukua aibu yao pamoja na wale washukao shimoni, nao wamewekwa miongoni mwa waliouawa.
26 Là est Mosoch, et Thubal, et toute sa multitude; autour de lui sont ses sépulcres; tous ceux-ci sont des incirconcis, et des tués, et des tombés sous le glaive, parce qu’ils jetèrent la frayeur dans la terre des vivants.
“Mesheki na Tubali wako humo, pamoja na makundi yao ya wajeuri wakiwa wameyazunguka makaburi yao. Wote hawakutahiriwa, wameuawa kwa upanga kwa sababu walieneza vitisho vyao katika nchi ya walio hai.
27 Et ils ne dormiront pas avec les forts, et ceux qui sont tombés, et les incirconcis descendus dans l’enfer avec leurs armes, et qui ont mis leurs glaives sous leurs têtes; et leurs iniquités ont pénétré dans leurs os, parce qu’ils sont devenus la terreur des forts dans la terre des vivants. (Sheol h7585)
Je, hawakulala na mashujaa wengine wasiotahiriwa waliouawa, ambao wameshuka kaburini wakiwa na silaha zao za vita, ambao panga zao ziliwekwa chini ya vichwa vyao na uovu wao juu ya mifupa yao? Adhabu kwa ajili ya dhambi zao ilikuwa juu ya mifupa yao, ingawa vitisho vya mashujaa hawa vilikuwa vimeenea hadi kwenye nchi ya walio hai. (Sheol h7585)
28 Et toi donc, au milieu des incirconcis tu seras brisé, et tu dormiras avec les tués par le glaive.
“Wewe pia, ee Farao, utavunjwa nawe utalala miongoni mwa wasiotahiriwa, pamoja na wale waliouawa kwa upanga.
29 Là est l’Idumée, et ses rois et tous ses chefs, qui ont été mis avec leur armée parmi les tués par le glaive, et qui ont dormi avec les incirconcis et avec ceux qui descendent dans la fosse.
“Edomu yuko humo, wafalme wake wote na wakuu wake wote, ambao ijapokuwa wana nguvu, wamelazwa pamoja na wale waliouawa kwa upanga. Wamelala pamoja na wasiotahiriwa, pamoja na wale washukao shimoni.
30 Là sont tous les princes de l’aquilon et tous les chasseurs qui ont été amenés avec les tués, tremblants et confondus dans leur force; qui ont dormi incirconcis avec les tués par le glaive, et ont porté leur confusion avec ceux qui descendent dans la fosse.
“Wakuu wote wa kaskazini na Wasidoni wote wako huko, wameshuka chini pamoja na waliouawa kwa aibu ijapokuwa kuna vitisho vilivyosababishwa na nguvu zao. Wamelala bila kutahiriwa pamoja na wale waliouawa kwa upanga na kuchukua aibu yao pamoja na wale washukao chini shimoni.
31 Pharaon les a vus, et il s’est consolé de toute sa multitude qui a été tuée par le glaive; Pharaon et toute son armée, dit le Seigneur Dieu,
“Farao, yeye pamoja na jeshi lake lote, atakapowaona atafarijiwa kwa ajili ya makundi yake yote ya wajeuri, wale waliouawa kwa upanga, asema Bwana Mwenyezi.
32 Parce que j’ai répandu ma terreur dans la terre des vivants, et il a dormi au milieu des incirconcis avec les tués par le glaive; Pharaon et toute sa multitude, dit le Seigneur Dieu.
Ingawa nilimfanya Farao aeneze vitisho vyake katika nchi ya walio hai, Farao pamoja na makundi yake yote ya wajeuri watalazwa miongoni mwa wasiotahiriwa, pamoja na wale waliouawa kwa upanga, asema Bwana Mwenyezi.”

< Ézéchiel 32 >