< Ézéchiel 20 >

1 Or il arriva en la septième année, au cinquième mois, au dixième jour du mois, que des hommes d’entre les anciens d’Israël vinrent pour consulter le Seigneur, et qu’ils s’assirent devant moi.
Ikawa ikaja katika mwaka wa saba, siku ya kumi ya mwezi wa tano, wazee wa Israeli wakaja kumuuliza Yahwe na kuketi mbele yangu.
2 Et la parole du Seigneur me fut adressée, disant:
Kisha neno la Yahwe likanijia, kusema,
3 Fils d’un homme, parle aux anciens d’Israël, et tu leur diras: Voici ce que dit le Seigneur Dieu: Est-ce pour me consulter que vous êtes venus, vous? Je vis, moi, je ne vous répondrai point, dit le Seigneur Dieu.
“mwanadamu, tangaza kwa wazee wa Israeli na uwaambie, 'Bwana Yahwe asema hivi: Je! Mmekuja kuniuliza swali? Kama niishivyo, sitaulizwa swali na ninyi! -hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.'
4 Si tu les juges, fils d’un homme, si tu les juges, montre leur les abominations de leurs pères.
Je! Utawahukumu? Utamuhukumu, mwanadamu? Wajulishe kuhusu machukizo ya baba zao.
5 Et tu leur diras: Voici ce que dit le Seigneur Dieu: Au jour où je choisis Israël, et où je levai ma main pour la race de la maison de Jacob, et où je leur apparus dans la terre de l’Egypte, et où je levai ma main pour eux, disant: Je suis le Seigneur votre Dieu;
Waambie, 'Bwana Yahwe asema hivi: Katika siku niliyoichagua Israeli na kuinua mkono wangu kuapa kiapo kwa uzao wa nyumba ya Yakobo, na kufanya kujulikana mimi mwenyewe kwao katika nchi ya Misri, wakati nilipoinua mkono wangu kuapa kiapo kwao. Nalisema, “Mimi ni Yahwe Mungu wenu”-
6 En ce jour-là, je levai ma main pour eux, afin de les conduire de la terre d’Egypte dans une terre que je leur avais destinée, où coulent du lait et du miel, et qui est excellente entre toutes les terres.
siku hiyo niliinua mkono wangu kuapa kiapo kwa ajili yao kwamba nitawatoa kutoka nchi ya Misri kwenye nchi ambayo niliyokuwa nimeichagua kwa umakini kwa ajili yao. Ilikuwa ikitiririka maziwa na asali; ilikuwa nzuri sana utukufu miongoni mwa nchi mbali mbali.
7 Et je leur dis: Que chacun éloigne les scandales de ses yeux, et ne vous souillez point par les idoles de l’Egypte; je suis le Seigneur votre Dieu.
Nikawaambia, “Kila mtu atupilie mabli mambo ya machukizo kutoka mbele ya macho yake na sanamu za Misri. Msijitie unajisi; mimi ni Yahwe Mungu wenu.”
8 Mais ils m’ont irrité, et n’ont pas voulu m’écouler, aucun d’eux n’a rejeté les abominations de leurs yeux, et ils n’ont pas quitté les idoles de l’Egypte; et j’ai dit que je répandrais mon indignation sur eux, et que j’assouvirais ma colère sur eux, au milieu de la terre d’Egypte.
Lakini wameasi juu yangu hawakuwa tayari kunisikiliza. Kila mtu hakutupilia mbali mambo ya machukizo kutoka mbele ya macho yake wala kwa ajili ya sanamu za Misri, hivyo nikaona nimwage ghadhabu yangu juu yao kukamilisha hasira yangu miongoni mwao katikati ya nchi ya Misri.
9 Mais j’ai agi à cause de mon nom, afin qu’il ne fût pas violé devant les nations au milieu desquelles ils étaient, et parmi lesquelles je leur ai apparu, afin de les retirer de la terre d’Egypte.
Nilifanya kwa ajili ya jina langu ili lisinajisiwe katika macho ya mataifa ambao walikaa pamoja nao. Nilijifanya mwenyewe kujulikana kwao, katika macho yao, kwa kuwatoa katika nchi ya Misri.
10 Je les ai donc fait sortir de la terre d’Egypte, et je les ai conduits dans le désert.
Basi nikawatoa katika nchi ya Misri na kuwaleta kwenye jangwa.
11 Et je leur ai donné mes préceptes, je leur ai fait connaître mes ordonnances, dans lesquelles l’homme qui les accomplira trouvera la vie.
Kisha nikawapa amri zangu na kufanya maagizo yangu kujulikana kwao, kwa kila mwanadamu atakayezishika ataishi.
12 De plus je leur donnai aussi mes sabbats, afin qu’ils fussent un signe entre moi et eux, et qu’ils sussent que je suis le Seigneur qui les sanctifie.
Pia nikawapatia Sabato zangu kama ishara kati yangu na wao, ili wajue kwamba mimi ni Yahwe niwafanyao wawe watakatifu.
13 Mais la maison d’Israël m’a irrité dans le désert; ils n’ont pas marché dans mes préceptes; ils ont rejeté mes ordonnances dans lesquelles l’homme qui les accomplira trouvera la vie, et mes sabbats, ils les ont violés grièvement: j’ai dit donc que je répandrais ma fureur sur eux dans le désert, et que je les exterminerais.
Lakini nyumba ya Israeli imeasi dhidi yangu jangwani. Hawakuenenda katika amri zangu; badala yake, wameyakataa maagizo yangu, ambayo mwanadamu ataishi kama akiyatii. Wamezinajisi Sabato zangu sana, basi nikasema nitamwaga hasira yangu juu yao jangwani ili kuwamalliza.
14 Mais j’ai fait autrement à cause de mon nom, afin qu’il ne fût pas violé devant les nations, d’où je les ai retirés en leur propre présence.
Lakini nilifanya kwa ajili ya jina langu hivyo lisinajisiwe katika macho ya mataifa, ambao niliwatoa mbele ya macho yao kutoka Misri.
15 Moi donc j’ai levé ma main sur eux dans le désert, pour ne les pas faire entrer dans la terre que je leur avais donnée, où coulent du lait et du miel, la principale de toutes les terres;
Basi mimi mwenyewe pia nimeinua mkono wangu kuapa kiapo kwao jangwani sitawarudisha kwenye nchi ile niliyokuwa naenda kuwapatia, nchi inayotiririkayo maziwa na asali, ambayo ilikuwa nzuri sana ambayo ni nzuri kati ya nchi zote.
16 Parce qu’ils ont rejeté mes ordonnances, et qu’ils n’ont pas marché dans mes préceptes, et qu’ils ont violé mes sabbats; car c’est à la suite des idoles que leur cœur allait.
Nimeapa hivi kwa sababu walikataa maagizo yangu na kutotembea katika amri zangu, na wazikufuru Sabato zangu.
17 Et mon œil les a épargnés pour ne pas leur ôter la vie, et je ne les ai pas exterminés dans le désert.
Lakini jicho langu likawahurumia kutokana na uharibifu na sikuwaangamiza jangwani.
18 Mais j’ai dit à leurs enfants dans la solitude: Ne marchez point dans les préceptes de vos pères, ne gardez point leurs coutumes, et ne vous souillez point par leurs idoles.
Nikawaambia watoto wao jangwani, “Msitembee kutokana na amri za wazazi wenu; msiweke maagizo yao au kujinajisi wenyewe kwa sanamu.
19 Je suis le Seigneur votre Dieu; marchez dans mes préceptes, gardez mes ordonnances et pratiquez-les;
Mimi ni Yahwe Mungu wenu, tembeeni katika amri zangu; tunzeni maagizo yangu na kuyatii.
20 Et mes sabbats, sanctifiez-les, afin qu’ils soient un signe entre moi et vous, et que vous sachiez que moi, je suis le Seigneur votre Dieu.
Zitunzeni Sabato zangu takatifu ili kwamba zitakuwa ishara kati yangu na ninyi, hivyo basi mtajua yakwamba mimi ni Yahwe Mungu wenu.”
21 Mais les enfants m’ont aigri, ils n’ont pas marché dans mes préceptes, et ils n’ont pas gardé mes ordonnances, de manière à accomplir les choses par lesquelles l’homme qui les aura accomplies vivra; et mes sabbats, ils les ont violés; et j’ai menacé de répandre ma fureur sur eux, et d’assouvir ma colère sur eux dans le désert.
Lakini watoto wao waliniasi. Hawakutembea kwenye sheria zangu au kushika maagizo yangu, ambazo mwanadamu ataishi kama akizitii. Wamezinajisi Sabato zangu, hivyo nimeamua kumwaga ghadhabu yangu juu yao kutimiza ghadhabu yangu dhidi yao katika jangwa.
22 Mais j’ai détourné ma main, et j’ai agi à cause de mon nom, afin qu’il ne fût pas violé devant les nations, d’où je les ai retirés sous leurs propres yeux.
Lakini niliurudisha mkono wangu na kutenda kwa ajili ya jina langu, hivyo lisitiwe unajisi katika macho ya mataifa ambao mbele ya macho yao niliwatoa Waisraeli.
23 De nouveau j’ai levé ma main sur eux dans la solitude, afin de les disperser parmi les nations et de les jeter au vent dans les divers pays;
Mimi mwenyewe pia nimeuinua mkono wangu kuapa juu yao jangwani, kwamba nitawatawanya kati ya maifa na kuwatawanya miongoni mwa nchi mabali mbali.
24 Parce qu’ils n’avaient pas observé mes ordonnances, et qu’ils avaient rejeté mes préceptes, et violé mes sabbats, et que leurs yeux s’étaient portés sur les idoles de leurs pères.
Nimeamua kufanya hivi kwa kuwa hawakuzitii amri zangu, na tangu walipo zikataa sheria zangu na kuzinajisi Sabato zangu. Macho yao yalizitamani sanamu za baba zao.
25 Moi donc aussi je leur ai donné des préceptes qui n’étaient pas bons, et des ordonnances dans lesquelles ils ne trouveront pas la vie.
Kisha niliwapa amri ambazo hazikuwa nzuri, na maagizo ambayo hawakuweza kuishi kwayo.
26 Je les ai souillés dans leurs présents, lorsqu’ils offraient tout ce qui ouvre un sein, pour leurs péchés; et ils sauront que je suis le Seigneur.
Nikawafanya unajisi kwa zawadi zao wakati walipofanya dhabihu za kila limbuko la tumbo la uzazi na kutupa kwenye moto. Nalifanya hivi ili kuwaogofya hivyo wangeweza kujua kwamba mimi ni Yahwe!'
27 C’est pourquoi parle à la maison d’Israël, fils d’un homme, et tu leur diras: Voici ce que dit le Seigneur Dieu: Vos pères m’ont encore outragé en cela, qu’après qu’ils m’avaient dédaigné par leur mépris,
Kwa hiyo, mwanadamu, waambie nyumba ya Israeli na waambie, 'Bwana Yahwe asema hivi: Katika hili pia baba zenu walinikufuru wakati walipokuwa sio waaminifu kwangu.
28 Et que je les avais fait entrer dans la terre que j’avais juré de leur donner, ils ont vu toute colline élevée et tout arbre touffu, et là ils ont immolé leurs victimes, et là ils m’ont donné un sujet d’irritation par leurs oblations, là ils ont consumé leurs parfums de suavité, et ils ont fait leurs nombreuses libations.
Wakati nilipowaleta kwenye nchi ambayo niliyokuwa nimewaapia kuwapatia, na kisha popote walipoona jiwe lolote refu na mti wenye majani, walitoa sadaka zao, walinikasirisha kwa sadaka zao, na huko pia walichoma ubani wao wa kunukia na kumwaga sadaka zao za kinywaji.
29 Et je leur ai dit: Quel est ce haut lieu où vous allez? et on a appelé son nom Haut lieu jusqu’à ce jour.
Kisha nikawaambia, “Nini maana ya mahali palipoinuka ambapo mmeleta sadaka huko?” Hivyo jina lake linaitwa Bana hata leo.'
30 À cause de cela, dis à la maison d’Israël: Voici ce que dit le Seigneur Dieu: Certainement vous vous souillez vous-mêmes dans la voie de vos pères, et vous forniquez à la suite de leurs pierres d’achoppement;
Kwa hiyo waambie nyumba ya Israeli, 'Bwana Yahwe asema hivi: Je! Kwa nini unajinajisi mwenyewe kwa njia za baba zako? Kwahiyo kwa nini unatenda kama makahaba, kutafuta kwa ajili ya mambo ya machukizo?
31 Et par l’oblation de vos dons, vous vous souillez, lorsque vous faites passer vos enfants au feu, et par toutes vos idoles jusqu’à ce jour; et moi je vous répondrai, maison d’Israël? Je vis, moi, dit le Seigneur Dieu, je ne vous répondrai point.
Kwa kuwa wakati mtoapo zawadi zenu na kuwaweka watoto wenu kwenye moto, siku hii mnajitia unajisi pamoja na sanamu zenu zote. Kwa hiyo kwa nini niwaache mniulize mimi, nyumba ya Israeli? Kama niishivyo-Hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-Sitawaacha mniulize swali.
32 Et la pensée de votre esprit ne s’accomplira pas, lorsque vous dites: Nous serons comme les nations et comme les familles de la terre, nous adorerons comme eux du bois et de la pierre.
Mawazo yanayoumbika kwenye moyo wako hayatatokea kamwe. Mmesema, “Ngoja tuwe kama mataifa mengine, kama koo za nchi nyingine waabuduo mti na jiwe.”
33 Je vis, moi, dit le Seigneur Dieu, avec une main forte, et avec un bras étendu, et dans ma fureur épanchée je régnerai sur vous.
Kama niishivyo-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-Nitatawala hakika juu yenu kwa mkono wenye nguvu, mkono ulionyooshwa, na ghadhabu itakayomwagwa juu yenu.
34 Et je vous ferai sortir du milieu des peuples, et je vous rassemblerai des pays dans lesquels vous avez été dispersés, avec une main forte, et avec un bras étendu, et dans ma fureur épanchée je régnerai sur vous.
Nitawatoa kutoka kwa watu wengine na kuwakusanya kutoka kwenye nchi mlizotawanyika ndani mwao. Nitafanya hivi kwa mkono hodari na kwa ghadhabu iliyomwagika.
35 Et je vous amènerai dans le désert des peuples, et là j’entrerai en jugement avec vous, face à face.
Kisha nitawaleta kwenye jangwa la watu, na huko nitawahukumu uso kwa uso.
36 Comme j’ai disputé en jugement contre vos pères dans le désert de l’Egypte, ainsi je vous jugerai, dit le Seigneur Dieu.
Kama nilivyo wahukumu baba zenu katika jangwa la nchi ya Misri, hivyo pia nitawahukumu-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
37 Et je vous assujettirai à mon sceptre, et je vous ferai entrer dans les liens de mon alliance.
Nitawafanya mpite chini ya fimbo yangu, na nitawafanya kutii maagizo yangu ya agano.
38 Et je séparerai de vous les transgresseurs et les impies; et je les ferai sortir du pays où ils demeuraient comme étrangers; mais dans la terre d’Israël ils n’entreront pas, et vous saurez que je suis le Seigneur.
Nitawasafisha kutoka miongoni mwenu maasi na wale ambao walionichukiza. Nitawatoa kutoka nchi ambayo wanayoishi kama wageni, lakini hawataingia kwenye nchi ya Israeli. Kisha mtajua yakwamba mimi ni Yahwe.
39 Et vous, maison d’Israël, voici ce que dit le Seigneur Dieu: Suivez chacun vos idoles et les servez. Que si en cela même vous ne m’écoutez pas, et que vous souilliez encore mon nom saint par vos présents et par vos idoles,
Basi kwenu, nyumba ya Israeli, Bwana Yahwe asema hivi: Kila mmoja wenu ataenda kwa sanamu zake mwenyewe. Muwaabudu kama mtakataa kunisikiliza, lakini hamtalikufuru tena jina langu takatifu kwa zawadi zenu na sanamu zenu.
40 Sur ma montagne sainte, sur la montagne élevée d’Israël, dit le Seigneur Dieu, là me servira toute la maison d’Israël; tous, dis-je, me serviront dans la terre en laquelle ils me seront agréables; et là je demanderai vos prémices et vos premières dîmes, dans tout ce que vous me consacrerez.
Kwa kuwa juu ya mlima wangu mtakatifu, juu ya kilele cha mlima wa Israeli-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-wote wa nyumba ya Israeli mtaniabudu huko katika nchi. Nitabarikiwa kwa kutaka sadaka zenu huko, na pia malimbuko yenu ya shukrani pamoja na vitu vyenu vyote vitakatifu.
41 Comme une odeur de suavité je vous recevrai, lorsque je vous aurai retirés d’entre les peuples, et que je vous aurai rassemblés des pays où vous avez été dispersés, et je serai sanctifié parmi vous aux yeux des nations.
Nitawapokea kama harufu nzuri ya ubani wakati nitakapowatoa kutoka wale watu na kuwakusanya toka nchi ambazo mlizotawanyika. Nitajifunua mimi mwenyewe kama mtakatifu ndani yenu kwa ajili ya mataifa waone.
42 Et vous saurez que je suis le Seigneur, lorsque je vous aurai fait rentrer dans la terre d’Israël, dans la terre pour laquelle j’ai levé ma main que je la donnerais à vos pères.
Kisha, wakati nitakapowaleta katika nchi ya Israeli, kwenye nchi ambayo niliuinulia mkono wangu kuapa kuwapatia baba zenu, mtajua yakwamba mimi ni Yahwe.
43 Et là vous vous souviendrez de vos voies, et de tous vos crimes dont vous vous êtes souillés; et vous vous déplairez à vous-mêmes à vos propres yeux, à cause de toutes les méchancetés que vous avez commises.
Kisha mtazikumbuka njia zenu mbaya huko, na matendo yenu yote machafu mliyoyafanya wenyewe, na mtajichukia wenyewe katika macho yenu kwa matendo yenu yote maovu mliyoyafanya.
44 Et vous saurez que je suis le Seigneur, lorsque je vous aurai fait du bien à cause de mon nom, et non point selon vos voies mauvaises, ni selon vos crimes détestables, ô maison d’Israël, dit le Seigneur Dieu.
Hivyo mtajua kwamba mimi ni Yahwe nifanyapo haya kwenu kwa ajili ya jina langu, sio kwa njia zenu mbaya au matendo yenu mabovu, nyumba ya Israeli-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”'
45 Et la parole du Seigneur me fut adressée, disant:
Kisha neno la Yahwe likanijia, kusema,
46 Fils d’un homme, tourne la face contre la voie du midi; et répands tes paroles vers l’Africus, et prophétise à la forêt du champ du midi.
“Mwanadamu, weka uso wako kuelekea nchi za kusini, na kuongea juu ya kusini; tabiri juu ya msitu wa Negebu.
47 Et tu diras à la forêt du midi: Ecoute la parole du Seigneur; voici ce que dit le Seigneur: Voici que moi j’allumerai en toi un feu, et je brûlerai en toi tout arbre vert et tout arbre aride; la flamme de l’embrasement ne s’éteindra pas; et par elle toute face sera brûlée, depuis le midi jusqu’à l’aquilon.
Uuambie msitu wa Negebu, 'Hivi ndivyo Yahwe asemavyo-Bwana Yahwe asema hivi: Tazama, nitaweka moto ndani yako. Utakula kila mti mbichi na kila mti mkavu ndani yako. Miali ya moto haitazimika; na kila uso utokao kusini hata kaskazini utateketezwa kwa moto.
48 Et toute chair verra que moi, le Seigneur, j’ai allumé la flamme, et elle ne s’éteindra pas.
Kisha watu wote wenye mwili watajua yakwamba mimi ni Yahwe nimeuwasha moto, na hautazimika.”'
49 Et j’ai dit: Ah! ah! ah! Seigneur Dieu; eux disent de moi: Est-ce qu’il ne parle pas en paraboles, celui-ci?
Kisha nimesema, Ee! Bwana Yahwe, Wananisema mimi, 'Je! yeye sio mwenye kusema mafumbo?”'

< Ézéchiel 20 >