< Ézéchiel 18 >
1 Et la parole du Seigneur me fut adressée, disant:
Neno la Bwana likanijia kusema:
2 D’où vient que parmi vous vous tournez la parole en ce proverbe dans la terre d’Israël, disant: Des pères ont mangé du raisin vert, et les dents des enfants en sont agacées?
“Je, ninyi watu mna maana gani kutumia mithali hii inayohusu nchi ya Israeli: “‘Baba wamekula zabibu zenye chachu, nayo meno ya watoto yametiwa ganzi’?
3 Je vis, moi, dit le Seigneur Dieu, si cette parabole vous sera désormais tournée en proverbe dans Israël.
“Hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, hamtatumia tena mithali hii katika Israeli.
4 Voilà que toutes les âmes sont à moi; comme l’âme du père, ainsi aussi l’âme du fils est à moi; l’âme qui aura péché, mourra elle-même.
Kwa kuwa kila roho ni mali yangu, kama vile ilivyo roho ya baba, vivyo hivyo roho ya mtoto ni mali yangu. Roho itendayo dhambi ndiyo itakayokufa.
5 Et si un homme est juste, et qu’il pratique l’équité et la justice;
“Mtu aweza kuwa ni mwenye haki atendaye yaliyo haki na sawa.
6 Qu’il ne mange point sur les montagnes, et qu’il ne lève point ses yeux vers les idoles de la maison d’Israël; et qu’il ne viole point la femme de son prochain, et qu’il ne s’approche point d’une femme qui est dans ses mois;
Hakula katika mahali pa ibada za miungu kwenye milima wala hakuziinulia macho sanamu za nyumba ya Israeli. Hakumtia unajisi mke wa jirani yake, wala hakukutana kimwili na mwanamke wakati wa siku zake za hedhi.
7 Et qu’il ne contriste personne; qu’il rende le gage à son débiteur; que par violence il ne ravisse rien; qu’il donne de son pain à celui qui a faim, et qu’il couvre d’un vêtement celui qui est nu;
Hamwonei mtu yeyote, bali hurudisha kilichowekwa rehani kwake. Hanyangʼanyi, bali huwapa wenye njaa chakula chake na huwapa nguo walio uchi.
8 Qu’il ne prête point à usure et ne reçoive pas plus qu’il n’a prêté; que de l’iniquité il détourne sa main, et qu’il rende un jugement équitable entre un homme et un homme;
Hakopeshi kwa riba wala hajipatii faida ya ziada. Huuzuia mkono wake usifanye mabaya, naye huhukumu kwa haki kati ya mtu na mtu.
9 Qu’il marche dans mes préceptes, et garde mes ordonnances, afin d’accomplir la vérité; celui-là est juste, il vivra de la vie, dit le Seigneur Dieu.
Huzifuata amri zangu na kuzishika sheria zangu kwa uaminifu. Huyo mtu ni mwenye haki; hakika ataishi, asema Bwana Mwenyezi.
10 Mais s’il engendre un fils voleur, répandant le sang, et qui commette l’une de ces choses,
“Aweza kuwa ana mwana jeuri, amwagaye damu au atendaye mojawapo ya mambo haya
11 Quand il ne les commettrait pas toutes, mais qui mange sur les montagnes, et qui souille la femme de son prochain,
(ingawa baba yake hakufanya mojawapo ya haya): “Hula katika mahali pa ibada za miungu kwenye milima. Humtia unajisi mke wa jirani yake.
12 Et qui contriste l’indigent et le pauvre, qui commette des rapines, qui ne rende point le gage a son débiteur, qui lève ses yeux vers les idoles, qui fasse des abominations,
Huwaonea maskini na wahitaji. Hunyangʼanyana. Harudishi kile kilichowekwa rehani kwake. Huziinulia sanamu macho. Hufanya mambo ya machukizo.
13 Qui prête à usure et qui reçoive plus qu’il n’a prêté; est-ce qu’il vivra? non, il ne vivra point; lorsqu’il aura fait toutes ces choses détestables, il mourra de mort, son sang sera sur lui-même.
Hukopesha kwa riba na kutafuta faida ya ziada. Je, mtu wa namna hii ataishi? Hapana, hataishi! Kwa sababu amefanya mambo haya yote ya machukizo, hakika atauawa na damu yake itakuwa juu ya kichwa chake mwenyewe.
14 Que s’il engendre un fils qui, voyant tous les péchés que son père a faits, craigne et ne fasse rien de semblable à ces péchés:
“Lakini yawezekana mwana huyo ana mwana aonaye dhambi hizi zote anazofanya baba yake, naye ingawa anaziona, yeye hafanyi mabaya kama haya:
15 Qu’il ne mange point sur les montagnes, et qu’il ne lève point les yeux vers les idoles de la maison d’Israël; qu’il ne viole point la femme de son prochain,
“Hakula katika mahali pa ibada za miungu kwenye milima, wala hainulii macho sanamu za nyumba ya Israeli. Hakumtia unajisi mke wa jirani yake.
16 Et qu’il ne contriste personne; qu’il ne retienne pas le gage à son débiteur, et qu’il ne commette point de rapines; qu’il donne de son pain à celui qui a faim, et qu’il couvre d’un vêtement celui qui est nu;
Hakumwonea mtu yeyote wala hakutaka rehani kwa ajili ya mkopo. Hanyangʼanyi, bali huwapa wenye njaa chakula chake na huwapa nguo walio uchi.
17 Qu’il détourne sa main de toute injustice contre le pauvre; qu’il ne donne point à usure, et ne reçoive rien au-delà de ce qu’il a prêté; qu’il accomplisse mes ordonnances, qu’il marche dans mes préceptes; celui-là ne mourra point dans l’iniquité de son père, mais il vivra de la vie.
Huuzuia mkono wake usitende dhambi, hakopeshi kwa riba wala hajipatii faida ya ziada. Huzishika amri zangu na kuzifuata sheria zangu. Hatakufa kwa ajili ya dhambi za baba yake; hakika ataishi.
18 Son père, qui a calomnié et a fait violence à son frère, et a commis le mal au milieu de son peuple, voilà qu’il est mort dans sa propre iniquité.
Lakini baba yake atakufa kwa ajili ya dhambi yake mwenyewe, kwa sababu alitoza bei isiyo halali kwa nguvu, akamnyangʼanya ndugu yake na kufanya yaliyo mabaya miongoni mwa watu wake.
19 Et vous dites: Pourquoi le fils n’a-t-il point porté l’iniquité de son père? Il est clair que c’est parce que le fils a agi selon l’équité et selon la justice, qu’il a gardé tous mes préceptes, et qu’il les a pratiqués, qu’il vivra de la vie.
“Lakini mnauliza, ‘Kwa nini mwana asiadhibiwe kwa uovu wa baba yake?’ Kwa vile mwana ametenda yaliyo haki na sawa na amekuwa mwangalifu kuzishika amri zangu zote, hakika ataishi.
20 L’âme qui a péché mourra elle-même; un fils ne portera pas l’iniquité de son père, et un père ne portera pas l’iniquité de son fils: la justice du juste sera sur lui et l’impiété de l’impie sera sur lui.
Roho itendayo dhambi ndiyo itakayokufa. Mwana hataadhibiwa kwa ajili ya makosa ya baba yake, wala baba hataadhibiwa kwa ajili ya makosa ya mwanawe. Haki ya mtu mwenye haki itahesabiwa juu yake na uovu wa mtu mwovu utalipizwa juu yake.
21 Mais si l’impie fait pénitence de tous ses péchés qu’il a commis, et qu’il garde tous mes préceptes, et qu’il accomplisse le jugement et la justice, il vivra de la vie et ne mourra point.
“Lakini mtu mwovu akiacha dhambi zake zote alizozitenda na kushika amri zangu zote na kufanya lililo haki na sawa, hakika ataishi, hatakufa.
22 Je ne me souviendrai d’aucune de ses anciennes iniquités; à cause de la justice qu’il a pratiquée, il vivra.
Hakuna kosa lolote alilotenda litakalokumbukwa juu yake. Kwa ajili ya mambo ya haki aliyoyatenda, ataishi.
23 Est-ce que je veux la mort de l’impie, dit le Seigneur Dieu, et non qu’il se détourne de ses voies et qu’il vive?
Je, mimi ninafurahia kifo cha mtu mwovu? Asema Bwana Mwenyezi. Je, si mimi ninafurahi wanapogeuka kutoka njia zao mbaya na kuishi?
24 Mais si le juste se détourne de sa justice, et qu’il fasse l’iniquité selon toutes les abominations que l’impie a coutume de commettre, est-ce qu’il vivra? toutes les œuvres de justice qu’il avait faites seront oubliées, et dans la prévarication par laquelle il a prévariqué, et dans le péché par lequel il a péché, il mourra.
“Lakini kama mtu mwenye haki akiacha haki yake na kutenda dhambi na kufanya mambo ya machukizo ambayo mtu mwovu hufanya, Je, ataishi? Hakuna hata mojawapo ya matendo ya haki aliyotenda litakalokumbukwa. Kwa sababu ya kukosa uaminifu kwake anayo hatia na kwa sababu ya dhambi alizozitenda, atakufa.
25 Et vous avez dit: Elle n’est pas juste, la voie du Seigneur. Ecoutez donc, maison d’Israël: Est-ce ma voie qui n’est pas juste, et ne sont-ce pas plutôt les vôtres qui sont corrompues?
“Lakini mnasema, ‘Njia ya Bwana si ya haki.’ Sikia, ee nyumba ya Israeli: Njia yangu siyo iliyo ya haki? Je, si njia zenu ndizo ambazo si za haki?
26 Car lorsqu’un juste se sera détourné de sa justice, et qu’il aura commis l’iniquité, il y mourra; dans l’injustice qu’il a commise, il mourra.
Kama mtu mwenye haki akiacha haki yake na kutenda dhambi, atakufa kwa ajili ya dhambi yake, kwa sababu ya dhambi alizotenda, atakufa.
27 Et lorsqu’un impie se sera détourné de son impiété qu’il a commise, et qu’il agira selon l’équité et selon la justice, il vivifiera lui-même son âme.
Lakini mtu mwovu akigeuka kutoka maovu aliyoyatenda na kufanya yaliyo haki na sawa, ataokoa maisha yake.
28 Car réfléchissant, et se détournant de toutes ses iniquités, il vivra de la vie, et il ne mourra point.
Kwa kuwa anayafikiria na kugeuka kutoka makosa yake yote aliyoyatenda na kuyaacha, hakika ataishi, hatakufa.
29 Et les enfants d’Israël disent: Elle n’est pas juste, la voie du Seigneur. Sont-ce mes voies qui ne sont pas justes, maison d’Israël, et ne sont-ce pas plutôt les vôtres qui sont corrompues?
Lakini nyumba ya Israeli inasema, ‘Njia za Bwana si haki.’ Je, njia zangu si za haki, ee nyumba ya Israeli? Je, si njia zenu ndizo ambazo si za haki?”
30 C’est pour cela que je jugerai chacun selon ses voies, maison d’Israël, dit le Seigneur Dieu. Convertissez-vous, et faites pénitence de toutes vos iniquités, et l’iniquité ne vous sera pas à ruine.
“Kwa hiyo, ee nyumba ya Israeli, nitawahukumu, kila mmoja sawasawa na njia zake, asema Bwana Mwenyezi. Tubuni! Geukeni kutoka makosa yenu yote, ndipo dhambi haitakuwa anguko lenu.
31 Rejetez loin de vous toutes les prévarications par lesquelles vous avez prévariqué, et faites-vous un cœur nouveau et un esprit nouveau; et pourquoi mourrez-vous, maison d’Israël?
Tupilieni mbali makosa yenu yote mliyoyatenda, nanyi mpate moyo mpya na roho mpya. Kwa nini mfe, ee nyumba ya Israeli?
32 Car je ne veux point la mort de celui qui meurt, dit le Seigneur Dieu; revenez, et vivez.
Kwa maana sifurahii kifo cha mtu awaye yote afaye katika uovu, asema Bwana Mwenyezi. Tubuni basi, mkaishi!