< Exode 9 >

1 Mais le Seigneur dit à Moïse: Va vers Pharaon, et dis-lui: Voici ce que dit le Seigneur Dieu des Hébreux: Laisse aller mon peuple, afin qu’il me sacrifie.
Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Nenda kwa Farao ukamwambie, ‘Hili ndilo Bwana, Mungu wa Waebrania asemalo: “Waachie watu wangu waende ili wapate kuniabudu.”
2 Que si tu refuses encore et les retiens,
Kama ukikataa kuwaachia waende, nawe ukiendelea kuwashikilia,
3 Voilà que ma main sera sur tes champs: et sur tes chevaux, et tes ânes, et tes chameaux, et tes bœufs, et tes brebis, une peste très dangereuse.
mkono wa Bwana utaleta pigo baya kwa mifugo yako, juu ya farasi wako, punda, ngamia, ngʼombe wako, kondoo na mbuzi.
4 Et le Seigneur fera une distinction merveilleuse entre les possessions d’Israël et les possessions des Egyptiens; en sorte que rien absolument ne périra de ce qui appartient aux enfants d’Israël.
Lakini Bwana ataweka tofauti kati ya mifugo ya Israeli na ile ya Misri, kwamba hakuna mnyama wa Mwisraeli atakayekufa.’”
5 Et le Seigneur en a marqué le temps, disant: Demain le Seigneur accomplira cette parole en ce pays.
Bwana akaweka wakati na kusema, “Kesho Bwana atalitenda hili katika nchi.”
6 Le Seigneur donc accomplit cette parole le jour suivant: et tous les animaux des Egyptiens moururent; mais parmi les animaux des enfants d’Israël rien absolument ne périt.
Siku iliyofuata Bwana akalitenda: Mifugo yote ya Wamisri ikafa, lakini hakuna hata mnyama mmoja wa wana wa Israeli aliyekufa.
7 Et Pharaon envoya voir: et rien n’était mort de ce que possédait Israël. Et le cœur de Pharaon s’endurcit et il ne laissa pas aller le peuple.
Farao akatuma watu kuchunguza, nao wakakuta kuwa hakuna hata mnyama mmoja wa Waisraeli aliyekufa. Lakini moyo wa Farao haukukubali kuwaachia watu waende.
8 Alors le Seigneur dit à Moïse et à Aaron: Prenez plein vos mains de cendre de foyer, et que Moïse la jette çà et là vers le ciel devant Pharaon;
Kisha Bwana akamwambia Mose na Aroni, “Chukueni majivu ya tanuru, naye Mose ayarushe angani mbele ya Farao.
9 Et qu’il y ait de la poussière sur toute la terre d’Egypte; car il y aura sur les hommes et les bêtes des ulcères, et de grosses tumeurs, dans toute la terre d’Egypte.
Yatakuwa vumbi jepesi juu ya nchi yote ya Misri, pia yatatokea majipu yenye kufura juu ya watu na wanyama katika nchi yote.”
10 Ils prirent donc de la cendre de foyer, et ils se présentèrent devant Pharaon, et Moïse la jeta çà et là vers le ciel, et il se forma des ulcères, de grosses tumeurs sur les hommes et les bêtes.
Basi wakachukua majivu kwenye tanuru na kusimama mbele ya Farao. Mose akayarusha hewani, nayo majipu yenye kufura yakatokea miilini mwa watu na wanyama.
11 Et les magiciens ne pouvaient se tenir devant Moïse, à cause des plaies qui étaient sur eux et dans toute la terre d’Egypte.
Waganga hawakuweza kusimama mbele ya Mose kwa sababu ya majipu yale yaliyokuwa miilini mwao na juu ya miili ya Wamisri wote.
12 Mais le Seigneur endurcit le cœur de Pharaon, et il n’écouta pas Moïse et Aaron, comme l’avait dit le Seigneur à Moïse.
Lakini Bwana akaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu, naye hakuwasikiliza Mose na Aroni, sawasawa kama vile Bwana alivyokuwa amemwambia Mose.
13 Le Seigneur dit encore à Moïse: Lève-toi dès le matin et présente-toi devant Pharaon, et tu lui diras: Voici ce que dit le Seigneur, Dieu des Hébreux: Laisse aller mon peuple, afin qu’il me sacrifie.
Kisha Bwana akamwambia Mose, “Amka mapema asubuhi, usimame mbele ya Farao, umwambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Waebrania: Waachie watu wangu waende, ili kwamba waweze kuniabudu,
14 Parce que, pour cette fois, j’enverrai toutes mes plaies sur ton cœur, et sur tes serviteurs, et sur ton peuple, afin que tu saches que nul n’est semblable à moi dans toute la terre.
au wakati huu nitaleta mapigo yangu yenye nguvu dhidi yako, maafisa wako na watu wako, ili upate kujua kuwa hakuna mwingine kama Mimi katika dunia yote.
15 C’est maintenant, en effet, qu’étendant la main, je frapperai toi et ton peuple de la peste, et tu périras de dessus la terre.
Kwa kuwa mpaka sasa ningelikuwa nimenyoosha mkono wangu na kukupiga wewe na watu wako kwa pigo ambalo lingekufutilia mbali juu ya nchi.
16 Car je t’ai établi pour montrer en toi ma puissance, et pour que mon nom soit publié dans toute la terre.
Lakini nimekuinua wewe kwa kusudi hili hasa, ili nipate kukuonyesha uwezo wangu, na ili Jina langu lipate kutangazwa duniani yote.
17 Tu retiens encore mon peuple, et tu ne veux pas le laisser aller?
Bado unaendelea kujiinua juu ya watu wangu, wala hutaki kuwaachia waende.
18 Voilà que je ferai pleuvoir demain à cette même heure une grêle extrêmement abondante, telle qu’il n’y en a point eu en Egypte, du jour où elle a été fondée, jusqu’au temps présent.
Kwa hiyo, kesho wakati kama huu nitaleta mvua mbaya sana ya mawe ambayo haijapata kunyesha katika nchi ya Misri, tangu siku ilipoumbwa mpaka leo.
19 Envoie donc dès maintenant, et rassemble tes bêtes et tout ce que tu as dans la campagne; car les hommes et les bêtes et toutes les choses qui se trouvent dehors, n’ayant pas été retirées des champs, et sur lesquelles sera tombée la grêle, mourront.
Sasa toa amri urudishe wanyama wote watoke malishoni na chochote ambacho kipo mashambani waje mpaka mahali pa usalama, kwa sababu mvua ya mawe itanyesha juu ya kila mtu na kila mnyama ambaye hajaletwa ndani ambao bado wako nje mashambani, nao watakufa.’”
20 Celui qui d’entre les serviteurs de Pharaon craignit la parole du Seigneur, fit retirer ses serviteurs et ses bêtes dans les maisons;
Wale maafisa wa Farao ambao waliliogopa neno la Bwana wakafanya haraka kuwaleta watumwa wao na mifugo yao ndani.
21 Mais celui qui négligea le discours du Seigneur laissa ses serviteurs et ses bêtes dans les champs.
Lakini wale waliopuuza neno la Bwana wakawaacha watumwa wao na mifugo yao shambani.
22 Alors le Seigneur dit à Moïse: Etends ta main vers le ciel, afin qu’il fasse de la grêle dans toute la terre d’Egypte, sur les hommes, et sur les bêtes et sur toute l’herbe de la campagne dans la terre d’Egypte.
Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Nyoosha mkono wako kuelekea angani ili kwamba mvua ya mawe inyeshe juu ya Misri yote, juu ya watu, wanyama na juu ya kila kitu kiotacho katika mashamba ya Misri.”
23 Et Moïse étendit sa verge vers le ciel, et le Seigneur donna des tonnerres et de la grêle et des éclairs qui couraient de toutes parts sur la terre: c’est ainsi que le Seigneur fit pleuvoir de la grêle sur la terre d’Egypte.
Mose alipoinyoosha fimbo yake kuelekea angani, Bwana akatuma ngurumo na mvua ya mawe, umeme wa radi ulimulika hadi nchi. Kwa hiyo Bwana akaifanya mvua ya mawe kunyesha juu ya nchi ya Misri,
24 Et la grêle et le feu mêlés tombaient ensemble, et la grêle fut d’une telle grosseur, que jamais pareille ne parut dans toute la terre d’Egypte, depuis que cette nation a été fondée.
mvua ya mawe ikanyesha na radi ikamulika pote. Ikawa dhoruba ya kutisha ambayo haijakuwako katika nchi ya Misri, tangu nchi hiyo iwe taifa.
25 Ainsi la grêle frappa dans toute la terre d’Egypte tout ce qui s’était trouvé dans les champs, depuis l’homme jusqu’à la bête; elle frappa aussi toute l’herbe de la campagne, et elle brisa tout arbre de la contrée.
Mvua ya mawe ikaharibu kila kitu katika nchi ya Misri kilichokuwa katika mashamba, watu na wanyama, ikaharibu kila kitu kinachoota mashambani na kuvunja kila mti.
26 Seulement dans la terre de Gessen, où étaient les enfants d’Israël, la grêle ne tomba pas.
Mahali pekee ambapo mvua ya mawe haikunyesha ni nchi ya Gosheni, ambako Waisraeli waliishi.
27 Alors Pharaon envoya et appela Moïse et Aaron, leur disant: J’ai encore péché, maintenant: le Seigneur est juste; moi et mon peuple nous sommes les impies.
Ndipo Farao akawaita Mose na Aroni akawaambia, “Wakati huu nimetenda dhambi. Bwana ni mwenye haki, mimi na watu wangu ni wakosaji.
28 Priez le Seigneur que ces tonnerres de Dieu et la grêle cessent, afin que je vous laisse aller, et, qu’en aucune manière, vous ne demeuriez ici davantage.
Mwombeni Bwana, kwa kuwa tumepata ngurumo na mvua za mawe za kututosha. Nitawaachia mwondoke; hamtahitaji kungoja zaidi.”
29 Moïse répondit: Quand je serai sorti de la ville, j’étendrai mes mains vers le Seigneur, et les tonnerres cesseront, et il n’y aura plus de grêle; afin que tu saches qu’au Seigneur est la terre.
Mose akamjibu, “Nitakapokuwa nimetoka nje ya mji, nitanyoosha mikono yangu juu kumwomba Bwana. Ngurumo zitakoma na hapatakuwepo mvua ya mawe tena, ili upate kujua kuwa, nchi ni mali ya Bwana.
30 Or je sais que toi-même et tes serviteurs ne craignez pas encore le Seigneur Dieu.
Lakini ninajua kuwa wewe na maafisa wako bado hammwogopi Bwana Mungu.”
31 Ainsi le lin et l’orge furent gâtés, parce que l’orge était verte, et que le fin poussait déjà ses balles.
(Kitani na shayiri viliharibiwa, kwa kuwa shayiri ilikuwa na masuke, na kitani ilikuwa katika kutoa maua.
32 Mais le froment et l’épeautre ne furent point gâtés, parce qu’ils étaient tardifs.
Hata hivyo, ngano na jamii nyingine ya ngano hazikuharibiwa kwa sababu zilikuwa hazijakomaa bado.)
33 Moïse donc, sorti d’avec Pharaon et de la ville, étendit ses mains vers le Seigneur, et les tonnerres et la grêle cessèrent, et il ne tomba plus une goutte d’eau sur la terre.
Kisha Mose akaondoka kwa Farao akaenda nje ya mji. Mose akanyoosha mikono yake kuelekea kwa Bwana, ngurumo na mvua ya mawe vikakoma, mvua haikuendelea tena kunyesha nchini.
34 Or Pharaon, voyant que la pluie, la grêle et les tonnerres avaient cessé, aggrava son péché;
Farao alipoona kwamba mvua ya mawe na ngurumo zimekoma, akafanya dhambi tena. Yeye na maafisa wake wakafanya mioyo yao kuwa migumu.
35 Et son cœur et celui de ses serviteurs s’appesantirent et s’endurcirent extrêmement; et il ne laissa point aller les enfants d’Israël, comme avait ordonné le Seigneur par l’entremise de Moïse.
Kwa hiyo moyo wa Farao ukawa mgumu, wala hakuwaachia Waisraeli waende, kama vile Bwana alivyokuwa amesema kupitia Mose.

< Exode 9 >