< Exode 36 >

1 Béséléel donc et Ooliab et tous les hommes sages auxquels le Seigneur avait donné la sagesse et l’intelligence, pour qu’ils sussent exécuter habilement, firent ce qui était nécessaire aux usages du sanctuaire, et ce qu’avait ordonné le Seigneur.
Kwa hiyo Bezaleli, Oholiabu na kila mtu Bwana aliyempa ustadi na uwezo wa kujua jinsi ya kufanya kazi zote za kujenga mahali patakatifu wataifanya hiyo kazi kama vile Bwana alivyoagiza.”
2 Car lorsque Moïse les eut appelés avec tous les hommes habiles auxquels le Seigneur avait donné la sagesse et qui de leur propre mouvement s’étaient offerts pour faire l’ouvrage,
Ndipo Mose akawaita Bezaleli na Oholiabu na kila mtu mwenye ustadi ambaye Bwana alikuwa amempa uwezo na mwenye kupenda kuja na kufanya kazi.
3 Il leur livra tous les dons des enfants d’Israël. Pendant qu’ils s’appliquaient avec ardeur à l’ouvrage, chaque jour au matin le peuple offrait des présents votifs.
Wakapokea kutoka kwa Mose sadaka zote ambazo Waisraeli walikuwa wameleta ili kuifanya kazi ya ujenzi wa Mahali Patakatifu. Nao watu wakaendelea kuleta sadaka za hiari kila asubuhi.
4 C’est pourquoi les ouvriers forcés de venir,
Ikafika wakati mafundi wote wenye ujuzi waliokuwa wakiifanya kazi yote ya mahali patakatifu wakasimamisha kazi zao,
5 Dirent à Moïse: Le peuple offre plus qu’il n’est nécessaire.
wakaja na kumwambia Mose, “Watu wanaleta vitu vingi kuliko tunavyohitaji kwa ajili ya kazi hii ambayo Bwana ameagiza ifanyike.”
6 Moïse commanda donc qu’il fût publié par la voix du hérault: Que ni homme ni femme n’offre plus rien pour l’ouvrage du sanctuaire. Et ainsi on cessa d’offrir des présents,
Ndipo Mose akatoa agizo, nao wakapeleka neno hili katika kambi yote: “Mtu yeyote mwanaume au mwanamke asilete tena kitu chochote kwa ajili ya sadaka ya mahali patakatifu.” Hivyo watu wakazuiliwa kuleta zaidi,
7 Parce que ceux qui avaient été offerts suffisaient et surabondaient.
kwa sababu walivyokuwa navyo tayari vilitosha na kuzidi kuifanya kazi yote.
8 Et tous les sages de cœur pour accomplir l’ouvrage du tabernacle, dix rideaux de fin lin retors, d’hyacinthe, de pourpre, d’écarlate deux fois teinte, d’un travail varié, et selon l’art de la tissure en diverses couleurs.
Watu wote wenye ustadi miongoni mwa wafanyakazi wote wakatengeneza maskani kwa mapazia kumi ya kitani iliyosokotwa vizuri, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, naye fundi stadi akatirizi makerubi kwenye mapazia hayo.
9 Un des rideaux avait en longueur vingt-huit coudées, et en largeur quatre; il y avait une seule mesure pour tous les rideaux.
Mapazia yote yalitoshana kwa ukubwa: kila moja lilikuwa na urefu wa dhiraa ishirini na nane, na upana wa dhiraa nne
10 Il joignit cinq rideaux l’un à l’autre, et il attacha les cinq autres ensemble.
Wakayaunganisha mapazia matano pamoja, pia wakafanya vivyo hivyo kwa hayo mengine matano.
11 il fit aussi des lacs d’hyacinthe au bord d’un rideau des deux côtés, et pareillement au bord d’un autre rideau,
Kisha wakatengeneza vitanzi vya kitambaa cha buluu kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu la kwanza, pia wakafanya vivyo hivyo na pazia la fungu la mwisho.
12 Afin que les lacs vinssent l’un contre l’autre, et qu’ils se joignissent ensemble.
Wakatengeneza pia vitanzi hamsini katika pazia mmoja, na vitanzi vingine hamsini kwenye pazia la mwisho la fungu hilo lingine, nazo vitanzi vyote vikaelekeana.
13 C’est pourquoi il fondit aussi cinquante anneaux d’or qui devaient attacher les lacs des rideaux, afin qu’il se fît un seul tabernacle.
Kisha wakatengeneza vifungo hamsini vya dhahabu, na wakavitumia kufunga na kuunganisha zile fungu mbili za mapazia pamoja ili maskani ipate kuwa kitu kimoja.
14 Il fit encore onze couvertures de poils de chèvre pour couvrir le toit du tabernacle.
Wakatengeneza mapazia kumi na moja ya singa za mbuzi kwa ajili ya kufunika maskani.
15 Une couverture avait en longueur trente coudées, et en largeur, quatre coudées: toutes les couvertures étaient d’une seule mesure.
Mapazia hayo kumi na moja yalikuwa na kipimo kimoja, yaani urefu wa dhiraa thelathini, na upana wa dhiraa nne.
16 Il en joignit cinq à part et les six autres séparément;
Wakaunganisha mapazia matano kuwa fungu moja, na hayo mengine sita kuwa fungu lingine.
17 Et il fit cinquante lacs au bord d’une couverture et cinquante au bord d’une autre couverture, afin qu’elles fussent jointes ensemble;
Kisha wakatengeneza vitanzi hamsini kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu moja, na vivyo hivyo kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu hilo lingine.
18 Et de plus cinquante boucles d’airain par lesquelles devait être attaché le toit, afin que de toutes les couvertures, il se fît une seule couverture.
Wakatengeneza vifungo hamsini vya shaba ili kukaza hema pamoja kuwa kitu kimoja.
19 Il fit encore une couverture du tabernacle, de peaux de béliers, teintes en rouge, et par-dessus une autre couverture de peaux violettes.
Kisha wakatengeneza kifuniko cha hema kwa ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu, na juu yake kifuniko cha ngozi za pomboo.
20 Il fit aussi de bois de sétim les ais du tabernacle, qui se tenaient debout.
Wakatengeneza mihimili ya kusimamisha ya mti wa mshita kwa ajili ya maskani.
21 La longueur d’un ais était de dix coudées; et la largeur tenait une coudée et demie,
Kila mhimili ulikuwa na urefu wa dhiraa kumi, na upana wa dhiraa moja na nusu,
22 Il y avait deux emboîtements à chaque ais, afin que l’un fût joint à l’autre. Ainsi fit-il pour tous les ais du tabernacle.
zikiwa na ndimi mbili zilizokuwa sambamba kila mmoja na mwingine. Wakatengeneza mihimili yote ya maskani jinsi hii.
23 De ces ais vingt étaient du côté méridional contre le vent du midi,
Wakatengeneza mihimili ishirini kwa ajili ya upande wa kusini wa maskani,
24 Avec quarante soubassements d’argent. Deux soubassements étaient posés sous un seul ais des deux côtés des angles, où l’emboîtement des côtés se termine dans les angles.
na wakatengeneza vitako arobaini vya fedha vya kuweka chini ya hiyo mihimili, vitako viwili kwa kila mhimili, kimoja chini ya kila ulimi.
25 Et aussi pour le côté du tabernacle, qui regarde l’aquilon, il fit vingt ais,
Kwa upande wa kaskazini wa maskani wakatengeneza mihimili ishirini
26 Avec quarante soubassements d’argent, deux soubassements pour chaque ais,
na vitako arobaini vya fedha, viwili chini ya kila mhimili.
27 Mais contre l’occident, c’est-à-dire, vers cette partie du tabernacle qui regarde la mer, il fit six ais,
Wakatengeneza mihimili sita kwa mwisho ulio mbali, yaani upande wa magharibi wa maskani,
28 Et deux autres à chaque angle du tabernacle, par derrière;
na mihimili miwili ikatengenezwa kwa ajili ya pembe za maskani za upande uliokuwa mbali.
29 Lesquels étaient joints depuis le bas jusqu’au haut, et formaient un seul assemblage. Ainsi fit-il des deux côtés pour chaque angle;
Katika pembe hizi mbili mihimili yake ilikuwa miwili kuanzia chini mpaka juu, na ikaingizwa kwenye pete moja; mihimili ya pembe hizi mbili ilifanana.
30 De manière à ce que huit ais fussent ensemble, et qu’ils eussent seize soubassements d’argent; c’est-à-dire, deux soubassements sous chaque ais.
Kwa hiyo kulikuwa na mihimili minane, na vitako kumi na sita vya fedha, viwili chini ya kila mhimili.
31 Il fit encore des leviers de bois de sétim, cinq pour maintenir les ais d’un côté du tabernacle,
Wakatengeneza pia mataruma kwa mti wa mshita: matano kwa ajili ya mihimili ya upande mmoja wa maskani,
32 Et cinq autres pour assujettir les ais de l’autre côté; et outre ceux-là, cinq autres leviers au côté occidental du tabernacle contre la mer.
matano kwa ajili ya mihimili ya upande mwingine, na matano kwa ajili mihimili ya upande wa magharibi, mwisho kabisa mwa maskani.
33 Il fit aussi un autre levier qui passait par le milieu des ais depuis un angle jusqu’à l’autre angle.
Wakatengeneza taruma la katikati, likapenya katikati ya mihimili kutoka mwisho mmoja hadi mwisho mwingine.
34 Mais les cloisons elles-mêmes des ais, il les dora, leurs soubassements d’argent ayant été fondus. Et il fit leurs cercles d’or, par lesquels les leviers pussent passer, et qu’il couvrit aussi de lames d’or.
Wakaifunika hiyo mihimili kwa dhahabu, na wakatengeneza pete za dhahabu za kushikilia hayo mataruma. Pia wakayafunika hayo mataruma kwa dhahabu.
35 Il fit de plus le voile d’hyacinthe et de pourpre, d’écarlate et de fin Un retors, d’un ouvrage de tisseur en diverses couleurs, varié et parsemé,
Wakatengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa vizuri, naye fundi stadi akatirizi makerubi kwenye hilo pazia.
36 Et quatre colonnes de bois de sétim, lesquelles il dora avec leurs chapiteaux, leurs soubassements d’argent ayant été fondus.
Wakatengeneza nguzo nne za mti wa mshita kwa ajili yake na kuzifunika kwa dhahabu. Wakatengeneza kulabu za dhahabu kwa ajili ya nguzo hizo, na kusubu vitako vinne vya fedha.
37 Il fit encore à l’entrée du tabernacle un voile d’hyacinthe, de pourpre, d’écarlate, de fin lin retors, en ouvrage de brodeur,
Kwa ajili ya ingilio la hema wakatengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa vizuri, kazi ya mtarizi.
38 Et cinq colonnes avec leurs chapiteaux, lesquelles il couvrit d’or, et il fondit leurs bases d’airain.
Pia wakatengeneza nguzo tano zenye kulabu. Wakafunika ncha za juu za hizo nguzo pamoja na tepe zake kwa dhahabu, na pia wakatengeneza vitako vyake vitano vya shaba.

< Exode 36 >