< Exode 3 >

1 Cependant Moïse paissait les brebis de Jéthro son beau-père, prêtre de Madian; or lorsqu’il eut conduit le troupeau dans l’intérieur du désert, il vint à la montagne de Dieu, Horeb.
Basi Mose alikuwa anachunga mifugo ya Yethro mkwewe, kuhani wa Midiani. Mose akapeleka mifugo mbali nyuma ya jangwa, naye akafika Horebu, mlima wa Mungu.
2 Et le Seigneur lui apparut dans une flamme de feu du milieu du buisson; et il voyait que le buisson brûlait et ne se consumait point.
Huko malaika wa Bwana akamtokea Mose katika mwali wa moto kutoka kichakani. Mose akaona kwamba ingawa kile kichaka kilikuwa kinawaka moto, kilikuwa hakiteketei.
3 Moïse dit donc: J’irai, et je verrai cette grande vision, pourquoi le buisson ne se consume point.
Ndipo Mose akawaza, “Nitageuka sasa nione kitu hiki cha ajabu, nami nione ni kwa nini kichaka hiki hakiteketei.”
4 Mais le Seigneur, voyant qu’il s’avançait pour voir, l’appela du milieu du buisson, et dit: Moïse, Moïse. Lequel répondit: Me voici.
Bwana alipoona kuwa amegeuka ili aone, Mungu akamwita kutoka ndani ya kile kichaka, “Mose! Mose!” Naye Mose akajibu, “Mimi hapa.”
5 Et le Seigneur: N’approche point d’ici, dit-il: ôte la chaussure de tes pieds; car le lieu dans lequel tu es est une terre sainte.
Mungu akamwambia, “Usikaribie zaidi. Vua viatu vyako, kwa maana mahali unaposimama ni patakatifu.”
6 Il ajouta: Je suis le Dieu de ton père, le Dieu d’Abraham, le Dieu d’Isaac et le Dieu de Jacob. Moïse cacha sa face, car il n’osait pas regarder vers Dieu.
Kisha akamwambia, “Mimi ni Mungu wa baba yako, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaki, na Mungu wa Yakobo.” Mose aliposikia hayo, akafunika uso wake kwa sababu aliogopa kumtazama Mungu.
7 Le Seigneur lui dit: J’ai vu l’affliction de mon peuple en Egypte, et j’ai entendu sa clameur à cause de la dureté de ceux qui président aux travaux.
Bwana akamwambia, “Hakika nimeona mateso ya watu wangu katika Misri. Nimesikia kilio chao kwa sababu ya wasimamizi wao, nami naguswa na mateso yao.
8 Et sachant sa douleur, je suis descendu pour le délivrer des mains des Egyptiens, et pour le conduire de cette terre dans une autre terre bonne et spacieuse, dans une terre où coulent du lait et du miel, au pays du Chananéen, de l’Héthéen, de l’Amorrhéen, du Phérézéen, de l’Hévéen et du Jébuséen.
Basi nimeshuka niwaokoe kutoka mkono wa Wamisri, niwatoe na kuwapandisha kutoka nchi hiyo, niwapeleke katika nchi nzuri na kubwa, nchi itiririkayo maziwa na asali, nchi ya Wakanaani, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi.
9 La clameur des enfants d’Israël est venue jusqu’à moi, et j’ai vu leur affliction dont ils sont accablés par les Égyptiens.
Sasa kilio cha Waisraeli kimenifikia, nami nimeona jinsi Wamisri wanavyowatesa.
10 Mais viens, et je t’enverrai vers Pharaon, afin que tu retires mon peuple, les enfants d’Israël, de l’Egypte.
Basi, sasa nenda. Ninakutuma kwa Farao ili kuwatoa watu wangu Waisraeli kutoka Misri.”
11 Et Moïse répondit à Dieu: Qui suis-je, moi, pour que j’aille vers Pharaon, et que je retire les enfants d’Israël de l’Egypte?
Lakini Mose akamwambia Mungu, “Mimi ni nani hata niende kwa Farao kuwatoa Waisraeli nchini Misri?”
12 Le Seigneur lui répliqua: Je serai avec toi, et tu auras ceci pour signe que je t’aurai envoyé: Lorsque tu auras retiré mon peuple de l’Egypte, tu immoleras à Dieu sur cette montagne.
Naye Mungu akasema, “Mimi nitakuwa pamoja nawe. Hii itakuwa ishara kwako kwamba ni Mimi nimekutuma: Hapo utakapokuwa umewatoa watu Misri, mtamwabudu Mungu katika mlima huu.”
13 Moïse dit à Dieu: Voici que j’irai vers les enfants d’Israël, et je leur dirai: Le Dieu de vos pères m’a envoyé vers vous. S’ils me demandent: Quel est son nom? que leur dirai-je?
Mose akamwambia Mungu, “Ikiwa nitawaendea Waisraeli na kuwaambia, ‘Mungu wa baba zenu amenituma kwenu,’ nao wakiniuliza, ‘Jina lake ni nani?’ Nitawaambia nini?”
14 Dieu dit à Moïse: Je suis CELUI QUI SUIS. Il ajouta: Tu diras ainsi aux enfants d’Israël: CELUI QUI EST m’a envoyé vers vous.
Mungu akamwambia Mose, “Mimi niko ambaye niko. Hivyo ndivyo utakavyowaambia Waisraeli: ‘Mimi niko amenituma kwenu.’”
15 Et Dieu dit encore à Moïse: Tu diras ceci aux enfants d’Israël: Le Seigneur Dieu de vos pères, le Dieu d’Abraham, le Dieu d’Isaac et le Dieu de Jacob m’a envoyé vers vous: c’est là mon nom pour l’éternité, et c’est celui qui doit me rappeler à la mémoire de génération en génération.
Vilevile Mungu akamwambia Mose, “Waambie Waisraeli, ‘Bwana, Mungu wa baba zenu, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaki, na Mungu wa Yakobo amenituma kwenu.’ Hili ndilo Jina langu milele, Jina ambalo mtanikumbuka kwalo kutoka kizazi hadi kizazi.
16 Va et assemble les anciens d’Israël, et tu leur diras: Le Seigneur Dieu de vos pères m’a apparu, le Dieu d’Abraham, le Dieu d’Isaac et le Dieu de Jacob, disant: Visitant, je vous ai visités, et j’ai vu tout ce qui vous est arrivé en Egypte.
“Nenda, ukawakusanye wazee wa Israeli, uwaambie, ‘Bwana, Mungu wa baba zenu, Mungu wa Abrahamu, Isaki na Yakobo, alinitokea akaniambia: Nimewatazama, nami nimeona mliyofanyiwa katika Misri.
17 Et j’ai dit que je vous retirerai de l’affliction de l’Egypte pour vous conduire dans la terre du Chananéen, de l’Héthéen, de l’Amorrhéen, du Phérézéen, de l’Hévéen et du Jébuséen, terre où coulent du lait et du miel.
Nami nimeahidi kuwapandisha kutoka mateso yenu katika nchi ya Misri, niwapeleke nchi ya Wakanaani, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi, nchi itiririkayo maziwa na asali.’
18 Et ils entendront ta voix; et tu entreras, toi et les anciens d’Israël, auprès du roi d’Egypte, et tu lui diras: Le Seigneur Dieu des Hébreux nous a appelés: nous ferons le chemin de trois journées dans le désert, afin que nous immolions au Seigneur notre Dieu.
“Wazee wa Israeli watakusikiliza. Kisha wewe na wazee mtakwenda kwa mfalme wa Misri na kumwambia, ‘Bwana, Mungu wa Waebrania ametutokea. Turuhusu twende safari ya siku tatu huko jangwani kutoa dhabihu kwa Bwana Mungu wetu.’
19 Mais moi, je sais que le roi d’Egypte ne vous laissera pas aller, si ce n’est par une main puissante.
Lakini nafahamu kwamba mfalme wa Misri hatawaruhusu kwenda, mpaka mkono wenye nguvu umlazimishe.
20 Aussi j’étendrai ma main, et je frapperai l’Egypte de toute sorte de prodiges que je vais faire au milieu d’eux: après cela il vous laissera aller.
Kwa hiyo nitaunyoosha mkono wangu na kuwapiga Wamisri kwa maajabu yote nitakayofanya miongoni mwao. Baada ya hayo, atawaruhusu mwondoke.
21 Et je ferai que ce peuple trouvera grâce aux yeux des Egyptiens; et quand vous sortirez, vous ne vous en irez pas dépourvus.
“Nami nitawapa hawa watu upendeleo mbele ya Wamisri, kwa hiyo mtakapoondoka nchini hamtaondoka mikono mitupu.
22 Mais chaque femme demandera à sa voisine et à son hôtesse des vases d’argent et dor, et des vêtements, que vous mettrez, sur vos fils et vos filles, et vous dépouillerez l’Egypte.
Kila mwanamke Mwisraeli atamwomba jirani yake Mmisri na mwanamke yeyote anayeishi nyumbani kwake ampe vyombo vya fedha, dhahabu na nguo, ambavyo mtawavika wana wenu na binti zenu. Hivyo mtawateka nyara Wamisri.”

< Exode 3 >