< Exode 19 >
1 Au troisième mois de la sortie d’Israël de la terre d’Egypte, en ce jour-là, ils vinrent au désert de Sinaï.
Mnamo mwezi wa tatu baada ya Waisraeli kuondoka Misri, siku kama iyo hiyo, wakafika katika Jangwa la Sinai.
2 Car partis de Raphidim et parvenus jusqu’à ce désert, ils campèrent dans le même lieu, et là Israël planta ses tentes vis-à-vis de la montagne de Sinaï.
Baada ya kuondoka Refidimu, waliingia katika Jangwa la Sinai na Israeli wakapiga kambi pale jangwani mbele ya mlima.
3 Or Moïse monta vers Dieu, et le Seigneur l’appela de la montagne, et dit: Voici ce que tu diras à la maison de Jacob, et que tu annonceras aux enfants d’Israël:
Kisha Mose akakwea kwenda kwa Mungu, naye Bwana akamwita kutoka kwenye ule mlima akasema, “Hivi ndivyo utakavyosema na nyumba ya Yakobo na utakachowaambia watu wa Israeli:
4 Vous-mêmes vous avez vu ce que j’ai fait aux Egyptiens, de quelle manière je vous ai portés sur des ailes d’aigles, et que je vous ai pris pour moi.
‘Ninyi wenyewe mmeona nililofanya huko Misri, jinsi nilivyowabeba kwenye mbawa za tai na kuwaleta kwangu.
5 Si donc vous écoutez ma voix, et que vous gardiez mon alliance, vous serez pour moi une portion, choisie d’entre tous les peuples; car toute la terre est à moi.
Sasa kama mkinitii kikamilifu na kutunza Agano langu, basi ninyi mtakuwa mali yangu ya thamani kubwa miongoni mwa mataifa yote. Ijapokuwa dunia yote ni mali yangu,
6 Et vous, vous serez pour moi un royaume sacerdotal, et une nation sainte. Ce sont les paroles que tu diras aux enfants d’Israël.
ninyi mtakuwa kwangu ufalme wa makuhani na taifa takatifu.’ Haya ndiyo maneno utakayosema kwa wana wa Israeli.”
7 Moïse vint, et, les anciens du peuple assemblés, il exposa toutes les paroles qu’avait ordonnées le Seigneur.
Kwa hiyo Mose akarudi, akawaita wazee wa watu na kuwaambia maneno yote ambayo Bwana alikuwa amemwamuru ayaseme.
8 Et tout le peuple répondit ensemble: Tout ce que le Seigneur a dit, nous le ferons. Or, quand Moïse eut rapporté les paroles du peuple au Seigneur,
Watu wote wakajibu kwa pamoja, “Tutafanya kila kitu Bwana alichokisema.” Naye Mose akarudisha majibu yao kwa Bwana.
9 Le Seigneur lui dit: Dès maintenant je viendrai à toi dans l’obscurité de la nuée, afin que le peuple m’entende te parlant, et qu’il te croie pour toujours. Moïse donc annonça les paroles du peuple au Seigneur,
Bwana akamwambia Mose, “Nitakujia katika wingu zito, ili watu wanisikie nikinena nawe na kila mara waweke tumaini lao kwako.” Kisha Mose akamwambia Bwana yale ambayo watu walikuwa wamesema.
10 Qui lui dit: Va vers le peuple, et sanctifie-les aujourd’hui et demain, et qu’ils lavent leurs vêtements.
Naye Bwana akamwambia Mose, “Nenda kwa watu ukawaweke wakfu leo na kesho. Waambie wafue nguo zao
11 Et qu’ils soient prêts pour le troisième jour; car au troisième jour, le Seigneur descendra devant tout le peuple sur la montagne de Sinaï.
na wawe tayari siku ya tatu, kwa sababu siku hiyo, Bwana atashuka juu ya mlima Sinai machoni pa watu wote.
12 Tu fixeras des limites pour le peuple tout autour, et tu leur diras: Gardez-vous de monter sur la montagne et d’en toucher les limites; quiconque touchera la montagne mourra de mort.
Weka mipaka kuzunguka mlima kwa ajili ya watu, uwaambie, ‘Mwe waangalifu, msije mkapanda mlimani au kuugusa. Yeyote atakayeugusa mlima hakika atauawa.
13 Aucune main ne le touchera, mais il sera lapidé, ou percé de traits; soit que ce soit une bête, ou un homme, il ne vivra pas. Quand la trompette commencera à sonner, qu’alors ils montent sur la montagne.
Hakika atapigwa mawe au kupigwa mishale; mkono wa mtu hautamgusa. Akiwa mwanadamu au mnyama, hataruhusiwa kuishi.’ Ila tu wakati baragumu itakapopigwa kwa mfululizo, ndipo watu wote watakapopanda mlimani.”
14 Et Moïse descendit de la montagne vers le peuple, et le sanctifia. Et quand ils eurent lavé leurs vêtements,
Baada ya Mose kushuka kutoka mlimani akawaendea watu na kuwaweka wakfu, wakafua nguo zao.
15 Il leur dit: Soyez prêts pour le troisième jour, et ne vous approchez point de vos femmes.
Kisha akawaambia watu, “Jitayarisheni kwa ajili ya siku ya tatu. Mwanaume yeyote asimkaribie mwanamke.”
16 Et déjà le troisième jour était venu, et le matin avait répandu sa lumière, et voilà que des tonnerres commencèrent à se faire entendre, des éclairs à briller et une nuée très épaisse à couvrir la montagne, et le son d’une trompette retentissait très fortement, et la peur saisit le peuple qui était dans le camp.
Asubuhi ya siku ya tatu kulikuwa na ngurumo na radi pamoja na wingu nene juu ya mlima na mlio mkubwa sana wa tarumbeta. Kila mmoja aliyekuwa kambini akatetemeka.
17 Et lorsque Moïse les eut conduits du lieu où était le camp à la rencontre de Dieu, ils s’arrêtèrent au pied de la montagne.
Kisha Mose akawaongoza watu kutoka kambini kukutana na Mungu, nao wakasimama chini ya mlima.
18 Or toute la montagne de Sinaï fumait, parce que le Seigneur y était descendu au milieu du feu, et la fumée en montait comme une fournaise; aussi, toute la montagne inspirait la terreur.
Mlima Sinai ulikuwa umefunikwa na moshi, kwa sababu Bwana alishuka juu yake katika moto. Moshi wa moto huo ulipanda juu kama moshi kutoka kwenye tanuru kubwa na mlima wote ukatetemeka kwa nguvu nyingi,
19 Et le son de la trompette augmentait insensiblement de plus en plus et se répandait plus au loin. Moïse parlait, et Dieu lui répondait.
nayo sauti ya tarumbeta ikawa kubwa zaidi na zaidi. Kisha Mose akazungumza na sauti ya Bwana ikamjibu.
20 Et le Seigneur descendit sur la montagne de Sinaï, sur le sommet même de la montagne, et il appela Moïse sur son faîte. Lors qu’il y fut monté,
Bwana akashuka juu ya Mlima Sinai na akamwita Mose apande juu mlimani. Kwa hiyo Mose akapanda juu,
21 Il lui dit: Descends, et adjure le peuple, de peur qu’il ne veuille dépasser les limites pour voir le Seigneur et qu’il n’en périsse une grande multitude.
naye Bwana akamwambia Mose, “Shuka ukawaonye watu ili wasijipenyeze kutafuta kumwona Bwana na wengi wao wakafa.
22 Que les prêtres aussi qui s’approchent du Seigneur soient sanctifiés, pour ne pas qu’il les frappe.
Hata makuhani, watakaomkaribia Bwana ni lazima wajiweke wakfu, la sivyo Bwana atawaadhibu.”
23 Et Moïse répondit au Seigneur: Le peuple ne pourra pas monter sur la montagne de Sinaï; car vous même vous l’avez assuré et ordonné, disant: Mets des limites autour de la montagne, et sanctifie-la.
Mose akamwambia Bwana, “Watu hawawezi kupanda mlima Sinai kwa sababu wewe mwenyewe ulituonya ukisema, ‘Wekeni mipaka kuuzunguka mlima na kuutenga kama patakatifu.’”
24 Et le Seigneur lui dit: Va, descends; et tu monteras toi et Aaron avec toi; mais que les prêtres et le peuple ne passent point les limites, et ne montent point vers le Seigneur, de peur qu’il ne les fasse mourir.
Bwana akajibu, “Shuka ukamlete Aroni pamoja nawe. Lakini makuhani pamoja na watu wasije wakalazimisha kuja kwa Bwana, nisije nikawaadhibu.”
25 Moïse descendit donc vers le peuple et il leur raconta toutes ces choses.
Basi Mose akashuka kwa watu na kuwaambia lile aliloambiwa.