< Exode 14 >

1 Or le Seigneur parla à Moïse, disant:
Ndipo Bwana akamwambia Mose,
2 Dis aux enfants d’Israël qu’ils retournent, et qu’ils campent vis-à-vis de Phihahiroth, qui est entre Magdalum et la mer, contre Béelséphon: c’est la vue de ce lieu que vous poserez votre camp, près de la mer.
“Waambie Waisraeli wageuke nyuma na wapige kambi karibu na Pi-Hahirothi, kati ya Migdoli na bahari. Watapiga kambi kando ya bahari, mkabala na Baal-Sefoni.
3 Car Pharaon va dire des enfants d’Israël: Ils sont resserrés dans la terre, le désert les tient enfermés.
Farao atafikiri kwamba, ‘Hao Waisraeli wanatangatanga katika nchi kwa kuchanganyikiwa, nalo jangwa limewafungia.’
4 Et j’endurcirai son cœur, et il les poursuivra; et je serai glorifié en Pharaon et en toute son armée; et les Egyptiens sauront que je suis le Seigneur. Et les enfants d’Israël firent ainsi.
Nami nitaufanya moyo wa Farao mgumu, naye atawafuatilia. Lakini nitajipatia utukufu kwa ajili yangu mwenyewe kupitia Farao na jeshi lake lote, nao Wamisri watajua kuwa mimi ndimi Bwana.” Kwa hiyo Waisraeli wakafanya hivyo.
5 Cependant on annonça au roi des Egyptiens que le peuple s’était enfui, et le cœur de Pharaon et de ses serviteurs fut changé à l’égard du peuple; et ils dirent: Qu’avons-nous voulu faire en laissant aller Israël, pour qu’il ne nous servît plus?
Mfalme wa Misri alipoambiwa kuwa Waisraeli wamekimbia, Farao na maafisa wake wakabadili nia zao kuhusu Waisraeli, wakasema, “Tumefanya nini? Tumewaachia Waisraeli waende zao na tumeukosa utumishi wao!”
6 Il attela donc son char, et prit tout son peuple avec lui.
Kwa hiyo akaandaliwa gari lake la vita, naye akaenda pamoja na jeshi lake.
7 Il emmena aussi, outre six cents chars d’élite, tout ce qu’il y eut de chars dans l’Egypte, et les chefs de toute l’armée.
Akachukua magari bora mia sita, pamoja na magari mengine yote ya Misri, pamoja na maafisa wa magari hayo yote.
8 Et le Seigneur endurcit le cœur de Pharaon, roi d’Egypte, et il poursuivit les enfants d’Israël; mais eux étaient sortis par une main élevée.
Bwana akaufanya mgumu moyo wa Farao, mfalme wa Misri, kwa hiyo akawafuatia Waisraeli, waliokuwa wakiondoka Misri kwa ujasiri.
9 Et comme les Egyptiens suivaient leurs traces de près, ils les trouvèrent dans leur camp près de la mer: toute la cavalerie et les chars de Pharaon et l’armée entière étaient à Phihahiroth contre Béelséphon.
Nao Wamisri, yaani farasi wote wa Farao na magari ya vita, wapanda farasi na vikosi vya askari, wakawafuatia Waisraeli, wakawakuta karibu na Pi-Hahirothi, mkabala na Baal-Sefoni walipokuwa wamepiga kambi kando ya bahari.
10 Et quand Pharaon se fut approché, les enfants d’Israël, levant les yeux, virent les Egyptiens derrière eux, et ils furent saisis d’une grande crainte, et ils crièrent au Seigneur,
Farao alipokaribia, Waisraeli wakainua macho yao, wakawaona Wamisri wakija nyuma yao. Wakashikwa na hofu, wakamlilia Bwana.
11 Et ils dirent à Moïse: Peut-être qu’il n’y avait pas de sépultures en Egypte; c’est pour cela que tu nous a amenés, afin que nous mourions dans le désert: qu’as-tu voulu faire en nous retirant de la terre d’Egypte?
Wakamwambia Mose, “Je, ni kwamba hayakuwako makaburi huko Misri hata umetuleta tufe huku jangwani? Umetufanyia nini kututoa Misri?
12 N’est-ce pas là le langage que nous te tenions en Egypte, disant: Retire-toi de nous, afin que nous servions les Egyptiens? car il valait beaucoup mieux les servir que mourir dans le désert.
Hatukukuambia tulipokuwa huko Misri, tuache tuwatumikie Wamisri? Ingekuwa vyema zaidi kwetu kuwatumikia Wamisri kuliko kufa jangwani!”
13 Or Moïse répondit au peuple: Ne craignez point, demeurez fermes, et voyez les grandes œuvres que le Seigneur va faire aujourd’hui; car les Egyptiens que vous voyez en ce moment, vous ne les verrez plus jamais.
Mose akawajibu Waisraeli, “Msiogope. Simameni imara, nanyi mtauona wokovu Bwana atakaowapatia leo. Hao Wamisri mnaowaona leo kamwe hamtawaona tena.
14 Le Seigneur combattra pour vous, et vous serez dans le silence.
Bwana atawapigania ninyi, nanyi mnatakiwa kutulia tu.”
15 Le Seigneur dit ensuite à Moïse: Pourquoi cries-tu vers moi? Dis aux enfants d’Israël qu’ils partent.
Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Kwa nini wewe unanililia? Waambie Waisraeli waendelee mbele.
16 Mais toi, élève ta verge, et étends ta main sur la mer, et divise-la, afin que les enfants d’Israël marchent au milieu de la mer à sec.
Inua fimbo yako na unyooshe mkono wako juu ya bahari ili kuyagawa maji, hivyo kwamba Waisraeli wapate kupita mahali pakavu baharini.
17 Pour moi, j’endurcirai le cœur des Egyptiens, afin qu’ils vous poursuivent, et je serai glorifié en Pharaon, et en toute son armée, et en ses chars et en ses cavaliers
Nitaifanya mioyo ya Wamisri kuwa migumu kusudi waingie baharini wakiwafuatia. Nami nitajipatia utukufu kupitia Farao pamoja na jeshi lake lote, kupitia magari yake ya vita na wapanda farasi wake.
18 Et les Egyptiens sauront que moi, je suis le Seigneur, quand j’aurai été glorifié en Pharaon, et en ses chars et en ses cavaliers.
Nao Wamisri watajua kwamba Mimi ndimi Bwana nitakapojipatia utukufu kupitia Farao, magari yake ya vita na wapanda farasi wake.”
19 Alors l’ange de Dieu qui précédait le camp d’Israël, alla derrière eux; et ainsi que lui, la colonne de nuée, passant de devant en arrière,
Ndipo malaika wa Mungu, aliyekuwa akisafiri mbele ya jeshi la Israeli, akaondoka akakaa nyuma yao. Pia ile nguzo ya wingu ikaondoka hapo mbele yao na kusimama nyuma,
20 Se tint entre le camp des Egyptiens et le camp d’Israël; or la nuée était ténébreuse, et elle éclairait la nuit; en sorte que durant tout le temps de la nuit, ils ne pouvaient s’approcher l’un de l’autre.
ikakaa kati ya majeshi ya Misri na Israeli. Usiku kucha wingu likaleta giza upande mmoja na nuru kwa upande mwingine, kwa hiyo hakuna aliyemkaribia mwenzake usiku kucha.
21 Lors donc que Moïse eut étendu la main sur la mer, le Seigneur la fit retirer, un vent impétueux et brûlant ayant soufflé toute la nuit, et il la mit à sec, et l’eau fut divisée.
Ndipo Mose akanyoosha mkono wake juu ya bahari, naye Bwana akayasukuma maji ya bahari nyuma kwa upepo mkali wa mashariki usiku ule wote na kupafanya nchi kavu. Maji yakagawanyika,
22 Ainsi les enfants d’Israël entrèrent au milieu de la mer desséchée; car l’eau était comme un mur à leur droite et à leur gauche.
nao Waisraeli wakapita baharini mahali pakavu, maji yakiwa ukuta upande wao wa kuume na upande wao wa kushoto.
23 Et les poursuivant, les Egyptiens entrèrent après eux au milieu de la mer, ainsi que toute la cavalerie de Pharaon, ses chars et ses cavaliers.
Wamisri wakawafuatia ndani ya bahari, pamoja na farasi wote wa Farao, magari ya vita na wapanda farasi.
24 Et déjà était venue la veille du matin, et voilà que le Seigneur jetant un regard sur le camp des Égyptiens à travers la colonne de feu et de nuée, tua toute leur armée,
Karibia mapambazuko, Bwana akaliangalia jeshi la Wamisri kutoka ile nguzo ya moto na ya wingu, akalifadhaisha.
25 Et renversa les roues des chars, ils furent entraînés au profond de la mer. Les Égyptiens dirent donc: Fuyons Israël, car le Seigneur combat pour eux contre nous.
Mungu akayaondoa magurudumu ya magari yao, kwa hivyo wakayaendesha kwa shida. Nao Wamisri wakasema, “Tuachane na Waisraeli! Bwana anawapigania dhidi ya Misri.”
26 Et le Seigneur dit à Moïse: Étends ta main sur la mer, afin que les eaux retournent vers les Égyptiens, sur leurs chars et leurs cavaliers.
Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Nyoosha mkono wako juu ya bahari ili maji yarudiane yawafunike Wamisri, magari yao ya vita na wapanda farasi wao.”
27 Et lorsque Moïse eut étendu sa main contre la mer, elle retourna au premier point du jour en son premier lieu; et les eaux vinrent à la rencontre des Égyptiens qui s’enfuyaient, et le Seigneur les enveloppa au milieu des flots.
Mose akanyoosha mkono wake juu ya bahari, wakati wa mapambazuko bahari ikarudiana na kuwa kama kawaida. Wamisri wakajaribu kuyakimbia maji, lakini Bwana akawasukumia ndani ya bahari.
28 Ainsi les eaux retournèrent et couvrirent les chars et les cavaliers de toute l’armée de Pharaon, qui poursuivant Israël, étaient entrés dans la mer: et il ne resta pas même un seul d’entre eux.
Maji yakarudiana na kuyafunika magari ya vita na wapanda farasi pamoja na jeshi lote la Farao lililokuwa limewafuata Waisraeli ndani ya bahari. Hakuna hata mmoja wao aliyenusurika.
29 Mais les enfants d’Israël poursuivirent leur chemin au milieu de la mer desséchée, et les eaux étaient pour eux comme un mur à droite et à gauche:
Lakini Waisraeli wakapita baharini mahali pakavu, ukiwepo ukuta wa maji upande wao wa kuume na upande wao wa kushoto.
30 Et le Seigneur délivra en ce jour-là Israël de la main des Egyptiens.
Siku ile Bwana akawaokoa Waisraeli kutoka mikononi mwa Wamisri, nao Waisraeli wakawaona Wamisri wamelala ufuoni mwa bahari wakiwa wamekufa.
31 Et ils virent les Égyptiens morts sur le rivage de la mer, et la main puissante qu’avait étendue le Seigneur contre eux: et le peuple craignit le Seigneur, et ils crurent au Seigneur et à Moïse son serviteur.
Basi Waisraeli walipoona uwezo mkubwa Bwana aliodhihirisha dhidi ya Wamisri, watu wakamwogopa Bwana na wakaweka tumaini lao kwake na kwa Mose mtumishi wake.

< Exode 14 >