< Exode 12 >

1 Le Seigneur dit aussi à Moïse et à Aaron dans la terre d’Egypte:
Yahweh akasema na Musa na Aruni katika nchi ya Misri. Alisema,
2 Ce mois sera pour vous le commencement des mois: il sera le premier dans les mois de l’année.
“Kwako wewe, mwezi huu utakuwa mwanzo wa miezi, mwezi wa kwanza wa mwaka kwako.
3 Parlez à toute l’assemblée des enfants d’Israël, et dites-leur: Au dixième jour de ce mois, que chacun prenne un agneau par chacune de ses familles et de ses maisons.
Liambie kusanyiko la Israeli, 'Siku ya kumi mwezi huu kila mtu lazima achukuwe mwana kondoo au mbuzi mdogo wa kwake, kila familia ifanye hivi, mwana kondoo kwa kila nyumba.
4 Mais si le nombre est trop petit pour qu’il puisse suffire à manger l’agneau, il prendra son voisin qui est proche de sa maison, selon le nombre des âmes qui peuvent suffire à manger l’agneau.
Kama hiyo nyumba ni ndogo sana kwa mwana kondoo, mwanaume na jirani yake wachukuwe mwana kondoo au nyama ya mbuzi mdogo ambayo itatosha watu. Lazima iwe yatosha kwa kila mtu kula, kwaiyo lazima wachukuwe nyama ya kutosha kulisha wote.
5 Or l’agneau sera sans tache, mâle, ayant un an. Conformément à ce rite vous prendrez aussi un chevreau.
Mwana kondoo wako au mbuzi wako mdogo lazima asiwe na upungufu, dume mwenye mwaka mmoja. Unaweza kuchukuwa mmoja wa kondoo au mbuzi.
6 Et vous le garderez jusqu’au quatorzième jour de ce mois; et toute la multitude des enfants d’Israël l’immolera vers le soir.
Lazima umtunze mpaka siku ya kumi na nne ya huo mwezi. Kisha kusanyiko lote la Israeli lazima liwaue hawa wanyama jioni.
7 Ils prendront de son sang, et ils en mettront sur les deux poteaux et sur les linteaux des maisons, en lesquelles ils les mangeront.
Lazima uchukuwe baadhi ya damu na uweke kwenye sehemu mbili za mihimili ya milango na juu ya fremu za milango ambapo utalia hizo nyama.
8 Et ils mangeront cette nuit-là les chairs rôties au feu avec des pains azymes et avec des laitues sauvages.
Lazima ule hizo nyama usiku, baada ya kuchoma kwenye moto. Kula na mkate ulio andaliwa kwa hamira, pamoja na mimea michungu.
9 Vous n’en mangerez rien cru, ni cuit dans l’eau, mais seulement rôti au feu; vous en mangerez la tête avec les pieds et les intestins.
Usiile mbichi au imechemshwa kwenye maji. Badala yake, choma kwenye moto na kichwa chake, miguu na sehemu za ndani.
10 Il n’en demeurera rien jusqu’au matin: s’il y a quelque reste, vous le brûlerez au feu.
Usiache ata kidogo kubaki mpaka asubui. Lazima uchome chochote kilicho baki asubui.
11 Or c’est ainsi que vous le mangerez: Vous ceindrez vos reins; et vous aurez votre chaussure à vos pieds, tenant un bâton en vos mains, et vous mangerez à la hâte; car c’est la Pâque, (c’est-à-dire) le passage du Seigneur.
Hivi ndivyo wa paswa kula: ukiwa umefunga mkanda wako, umevaa viatu vyako, na gongo lako mkononi mwako. Lazima ule kwa haraka. Ni Pasaka ya Yahweh.
12 Et je passerai par la terre d’Egypte cette nuit-là, et je frapperai tout premier-né dans la terre d’Egypte, depuis l’homme jusqu’au bétail, et sur tous les dieux de l’Egypte j’exercerai des jugements, moi le Seigneur.
Yahweh anasema hili: Nitaenda katika nchi ya Misri usiku na kushambulia wazaliwa wote wa kwanza wa wanadamu na wanyama katika nchi ya Misri. Nitaleta pigo kwa miungu yote ya Misri. Mimi ni Yahweh.
13 Or le sang sera un signe en votre faveur dans les maisons où vous serez; car je verrai le sang, et je passerai au-delà de vous; et la plaie de destruction ne vous atteindra pas lorsque je frapperai la terre d’Egypte.
Damu itakuwa ishara kwenye nyumba zenu ya kuja kwangu. Nitakapo ona damu, nitapita nitakapo shambulia nchi ya Misri. Ili pigo halitawajia na kuwaharibu.
14 Ce jour sera pour vous un monument, et vous le célébrerez dans vos générations comme consacré au Seigneur par un culte éternel.
Hii siku itakuwa kumbukumbu kwenu, ambayo lazima muadhimishe kama sherehe ya Yahweh. Itakuwa sheria kwenu pia, kwenye vizazi vyote vya watu wenu, ambayo mwapaswa kuadhimisha leo.
15 Pendant sept jours vous mangerez des azymes: dès le premier jour il n’y aura point de levain dans vos maisons; quiconque mangera du pain levé, depuis le premier jour jusqu’au septième jour, son âme périra du milieu d’Israël.
Utakula mkate bila hamira wakati wa siku saba. Siku ya kwanza utaondoa hamira kwenye nyumba zenu. Yeyote atakaye kula mkate uliyotiwa chachu kwanzia siku ya kwanza mpaka siku ya saba, huyo mtu lazima akatwe kutoka Israeli.
16 Le premier jour sera saint et solennel, et le septième jour sera vénérable par la même solennité: vous ne ferez aucun travail en ces jours-là, excepté ce qui regarde la nourriture.
Siku ya kwanza kutakuwa na kusanyiko lililo tengwa kwa ajili yangu, na siku ya saba kutakuwa na kusanyiko kama hilo. Hakuna kazi itakayo fanywa hizi siku, zaidi ya kupika kila mmoja ale. Hiyo ndio kazi pekee itakayo fanywa na wewe.
17 Vous observerez donc la fête des Azymes; car c’est en ce même jour que je conduirai votre armée hors de la terre d’Egypte: ainsi vous garderez ce jour en vos générations par un rite perpétuel.
Lazima uadhimishe hii Sherehe ya Mkate Usiotiwa Chachu kwasababu ni siku hii ambayo nitawaleta watu wako, makundi yaliyo na silaha, kwa makundi yaliyo na silaha, kutoka nchi ya Misri. Lazima uadhimishe hii siku kwa vizazi vyote vya watu wako. Hii itakuwa sheria kwako.
18 Au premier mois, le quatorzième jour du mois, vers le soir, vous mangerez des azymes jusqu’au vingt-unième jour du même mois, vers le soir.
Lazima ule mkate usiotiwa chachu kuanzia jioni ya siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza wa mwaka, mpaka jioni ya siku ya ishirini na moja ya mwezi.
19 Sept jours durant, on ne trouvera point de levain dans vos maisons: celui qui mangera du pain levé, son âme périra du milieu de l’assemblée d’Israël, qu’il soit étranger ou naturel du pays.
Wakati wa hizi siku, nyumbani mwenu kusipatikane na hamira. Yeyote atakaye kula mkate ulio andaliwa na hamira lazima akatwe kutoka jamii ya Israeli, huyo mtu awe ni mgeni au mtu aliye zaliwa nchini mwenu.
20 Vous ne mangerez rien de fermenté; dans toutes vos habitations vous mangerez des azymes.
Hautakula chochote kilicho andaliwa na hamira. Popote utapo ishi, lazima ule mkate usio na hamira.”'
21 Or Moïse appela tous les anciens des enfants d’Israël et leur dit: Allez, et prenez un animal par chacune de vos familles, et immolez la Pâque.
Kisha Musa akawaita viongozi wote wa Israeli na kuwaambia, “Nendeni na mchague mwana kondoo au mbuzi watakao tosha kulisha familia zenu na muue mwana kondoo wa pasaka.
22 Trempez un bouquet d’hysope dans le sang qui est sur le seuil de la porte, et vous en aspergerez le linteau et les deux poteaux, et que nul de vous ne sorte hors de la porte de sa maison jusqu’au matin.
Kisha chukua jani la hisopu na uchovye kwenye damu itakayo kuwa kwenye beseni. Paka damu iliyo kwenye beseni juu ya fremu ya mlango na kwenye mihimili miwili ya mlango. Hakuna ata mmoja atakaye toka nje ya mlango wake mpaka asubui.
23 Car le Seigneur passera frappant les Egyptiens; et lorsqu’il verra le sang sur le linteau et sur les poteaux, il passera au-delà de la porte de la maison, et il ne permettra pas que le destructeur entre dans vos maisons et vous frappe.
Kwa kuwa Yahweh atapita kushambulia Wamisri. Atakapo ona damu juu ya fremu ya mlango na kwenye mihimili miwili ya mlango, atapita mlango wako na ata ruhusu mharibifu kuja nyumbani kwenu kuwashambulia.
24 Garde cette parole comme une loi éternelle pour toi et pour tes enfants.
Lazima uadhimishe hili tukio. Hili litakuwa daima sheria kwako na kwa uzao wenu.
25 Et lorsque vous serez entrés dans le pays que le Seigneur doit vous donner, comme il a promis, vous observerez ces cérémonies.
Utakapo ingia nchi Yahweh atakayo kupa, kama alivyo ahidi kufanya, lazima uadhimishe hili tendo la ibada.
26 Et quand vos enfants vous demanderont: Quel est ce culte religieux?
Watoto wako watakapo kuuliza, 'Hili tendo la ibada lina maana gani?'
27 Vous leur direz: C’est la victime du passage du Seigneur, quand il passa par-dessus les maisons des enfants d’Israël en Egypte, frappant les Egyptiens, et préservant nos maisons. Alors le peuple profondément incliné adora.
kisha lazima useme, 'Ni sadaka ya Pasaka ya Yahweh, kwasababu Yahweh kapita nyumba za Waisraeli Misri alipo washambulia Wamisri. Aliweka nyumba zetu huru.”' Kisha watu wakamsujudia Yahweh.
28 Et étant sortis, les enfants d’Israël firent comme le Seigneur avait ordonné à Moïse et à Aaron.
Waisraeli wakaenda na kufanya kama Yahweh alivyo waamuru Musa na Aruni.
29 Or il arriva au milieu de la nuit que le Seigneur frappa tous les premiers-nés dans la terre d’Egypte, depuis le premier-né de Pharaon qui était assis sur son trône, jusqu’au premier-né de la captive qui était en prison, et tout premier-né des bêtes.
Ikawa usiku wa manane kuwa Yahweh akawashambulia wazaliwa wote wa kwanza wa nchi ya Misri, kuanzia mzaliwa wa kwanza wa Farao, aliye keti kiti chake cha enzi, mzaliwa wa kwanza wa mtu aliye gerezani na wazaliwa wote wa kwanza wa mifugo.
30 Et Pharaon se leva la nuit, et tous ses serviteurs et tout son peuple, et il s’éleva un grand cri en Egypte, car il n’était pas de maison dans laquelle ne gésît un mort.
Farao akaamka usiku - yeye, watumishi wake, na Wamisri. Palikuwa na kelele za maombolezo Misri, kwa kuwa hakukuwa na nyumba ambayo hamna mtu hakufa.
31 Pharaon ayant donc appelé Moïse et Aaron pendant la nuit, leur dit: Levez-vous, et sortez du milieu de mon peuple, vous et les enfants d’Israël; allez, sacrifiez au Seigneur, comme vous dites.
Farao akamuita Musa na Aruni usiku na kusema, “Inuka, tokeni miongoni mwa watu wangu, nyie pamoja na Waisraeli. Nenda, mmuabudu Yahweh, kama mlivyo sema mnataka kufanya.
32 Prenez aussi vos brebis et votre gros bétail, comme vous aviez demandé, et vous en allant, bénissez-moi.
Chukuweni ng'ombe zenu na kondoo zenu, kama mlivyo sema, na muende, na pia mnibariki.”
33 Et les Egyptiens pressaient le peuple de sortir de leur pays promptement, disant; Nous mourrons tous.
Wamisri walikuwa na haraka ya kuwa ondoa nchini, kwa kuwa walisema, “Sisi ni watu tuliokufa.”
34 Le peuple prit donc de la farine pétrie avant qu’elle fût levée, et la liant dans les manteaux, il la mit sur ses épaules.
Watu wakachukuwa ngano yao pasipo kuongeza hamira yeyote. Bakuli zao zakukandia ngano zilifungiwa kwenye nguo zao na kwenye mabega yao.
35 Alors les enfants d’Israël firent comme avait ordonné Moïse; et ils demandèrent aux Egyptiens des vases d’argent et d’or et beaucoup de vêtements.
Watu Waisraeli walifanya kama Musa alivyo waambia. Waliwaomba Wamisri vitu vya fedha, vitu vya dhahabu, na nguo.
36 Or le Seigneur fit trouver grâce au peuple devant les Egyptiens, pour qu’ils les leur prêtassent; et ils dépouillèrent les Egyptiens.
Yahweh aliwafanya Wamisri na shauku ya kuwapendeza Waisraeli. Hivyo Wamisri waliwapa chochote walicho waomba. Katika hili, Waisraeli waliwachukulia vingi Wamisri.
37 Et les enfants d’Israël partirent de Ramessès pour Socoth, environ six cent mille hommes de pied, sans les petits enfants.
Waisraeli wakasafiri kutoka Ramesi kwenda Sakothi. Walikuwa na idadi ya wanaume 600, 000 kwa miguu, kuongezea kwa wanawake na watoto.
38 Mais une foule innombrable de gens de toute espèce monta avec eux, ainsi que des brebis, du gros bétail et des animaux de divers genres en très grand nombre.
Mchanganyiko wa kundi la wasio Waisraeli pia walienda nao, pamoja na ng'ombe na kondoo, idadi kumbwa ya mifugo.
39 Ils firent cuire aussi la farine qu’ils avaient apportée d’Egypte déjà toute pétrie, et firent des pains azymes cuits sous la cendre; car il? ne pouvaient fermenter, les Egyptiens les forçant de partir, et ne leur permettant de prendre aucun délai; et ils n’avaient pas eu la facilité d’apprêter aucun aliment.
Walioka mikate na unga wa ngano wenye hamira walio utoa Misri. Ulikuwa hauna hamira kwasababu waliondolewa Misri na hawakuweza chelewa kuandaa chakula.
40 Or l’habitation des enfants d’Israël pendant qu’ils demeurèrent en Egypte, fut de quatre cent trente ans.
Waisraeli waliishi Misri kwa miaka 430.
41 Lesquels accomplis, toute l’armée du Seigneur sortit le même jour de la terre d’Egypte.
Baada ya miaka 430, siku hiyo hiyo, majeshi yote ya Yahweh yalio jiami waliondoka kutoka nchi ya Misri.
42 Cette nuit doit être observée en l’honneur du Seigneur, quand il les retira de la terre d’Egypte, et tous les enfants d’Israël doivent l’observer dans leurs générations.
Huu ulikuwa usiku wakuwa macho, ili Yahweh awatoe kutoka nchi ya Misri. Huu ulikuwa usiku wa Yahweh wa kuadhimishwa na Waisraeli wote na watu wa vizazi vyao vyote.
43 Et le Seigneur dit à Moïse et à Aaron: Voici le rite de la Pâque: Aucun étranger n’en mangera.
Yahweh akamwambia Musa na Aruni, “Hii ni sheria ya Pasaka: hakuna mgeni anaye ruhusiwa kuila.
44 Mais tout esclave acheté sera circoncis, et alors il en mangera.
Walakini, kila mtumwa wa Misraeli, aliye nunuliwa kwa pesa, anaeza kula baada ya kutahiriwa.
45 L’étranger et le mercenaire n’en mangeront point.
Wageni na watumishi waajiriwa hawapaswi kula chakula chochote.
46 C’est dans une même maison qu’on la mangera; et vous ne porterez point de sa chair au dehors, et vous n’en romprez aucun os.
Chakula chapaswa kuliwa ndani ya nyumba moja. Hauruhusiwi kubeba nyama yeyote nje ya nyumba, na hauruhusiwi kuvunja mfumba wowote.
47 Toute l’assemblée d’Israël la fera.
Jamii zote za Israeli za paswa kuadhimisha sherehe.
48 Que si quelqu’un des étrangers veut entrer dans votre colonie et faire la Pâque du Seigneur, tous ses enfants mâles seront circoncis auparavant, et alors il la célébrera selon le rite; et il sera comme un naturel du pays; mais si quelqu’un n’a pas été circoncis, il n’en mangera pas.
Kama mgeni anaishi na wewe na anataka kuadhimisha Pasaka kwa Yahweh, ndugu zake wote wa kiume wapaswa kutahiriwa. Kisha anaeza kuja na kuadhimisha. Atakuwa kama watu walio zaliwa kwenye nchi. Walakini, hakuna mtu asiye tahiriwa anaruhusiwa kula chakula chochote.
49 La même loi sera pour l’indigène et pour le colon qui séjournent chez vous.
Sheria hii hii itahusika kwa mzaliwa wa asili na mgeni anayeishi miongoni mwenu.”
50 Et tous les enfants d’Israël firent comme avait ordonné le Seigneur à Moïse et à Aaron.
Waisraeli wote walifanya kama Yahweh alivyo waamuru Musa na Aruni.
51 Et le même jour le Seigneur retira les enfants d’Israël de la terre d’Egypte, selon leurs bandes.
Ikaja kuwa siku hiyo Yahweh akawaleta Israeli kutoka nchi ya Misri kwa makundi yalio jiami.

< Exode 12 >