< Éphésiens 3 >
1 C’est pour cela que moi, Paul, je suis le prisonnier du Christ Jésus, pour vous gentils;
Kutokana na hayo, mimi Paulo, mfungwa wa Kristo Yesu kwa ajili yenu, namwomba Mungu.
2 Car vous avez appris sans doute que Dieu m’a confié la dispensation de sa grâce en votre faveur;
Bila shaka mmekwisha sikia kwamba Mungu, kwa neema yake, alinikabidhi kazi hii niifanye kwa faida yenu.
3 Puisque, par révélation, il m’a fait connaître ce mystère, comme je vous l’ai écrit plus haut en peu de mots;
Mimi nilijulishwa kwa njia ya ufunuo mpango wake uliofichika. (Nimeandika kwa ufupi juu ya jambo hili,
4 De sorte que lisant, vous pouvez comprendre l’intelligence que j’ai du mystère du Christ,
nanyi mkiyasoma maneno yangu mtaweza kujua jinsi ninavyoielewa siri hiyo ya Kristo.)
5 Mystère qui, dans les autres générations, n’a pas été découvert aux enfants des hommes, comme il est maintenant révélé par l’Esprit aux saints apôtres et aux prophètes,
Zamani watu hawakujulishwa siri hiyo; lakini sasa Mungu amewajulisha mitume na manabii wake watakatifu kwa njia ya Roho.
6 Que les gentils sont cohéritiers, membres d’un même corps, et participants avec eux de sa promesse en Jésus-Christ par l’Evangile,
Siri yenyewe ni hii: kwa njia ya Habari Njema watu wa mataifa mengine wanapata sehemu yao pamoja na Wayahudi katika zile baraka za Mungu; wao ni viungo vya mwili uleule, na wanashiriki ahadi ileile aliyofanya Mungu kwa njia ya Kristo Yesu.
7 Dont j’ai été fait le ministre, en vertu du don de la grâce de Dieu, qui m’a été donnée par l’opération de sa vertu.
Mimi nimefanywa kuwa mtumishi wa Habari Njema kwa neema ya pekee aliyonijalia Mungu kwa uwezo wake mkuu.
8 À moi, le moindre des saints, a été donnée cette grâce d’annoncer parmi les gentils les richesses incompréhensibles du Christ,
Mimi ni mdogo kuliko watu wote wa Mungu; lakini amenijalia neema yake, ili niwahubirie watu wa mataifa utajiri wake Kristo usiopimika,
9 Et d’éclairer tous les hommes touchant la dispensation du mystère caché, dès l’origine des siècles, en Dieu qui a créé toutes choses; (aiōn )
tena niwaangazie watu wote waone jinsi mpango wa Mungu uliofichika unavyotekelezwa. Mungu aliye Muumba wa vitu vyote alificha siri hiyo yake tangu milele, (aiōn )
10 Afin que les principautés et les puissances qui sont dans les cieux connussent par l’Eglise la sagesse multiforme de Dieu,
kusudi, sasa kwa njia ya kanisa, wakuu na wenye enzi wa mbinguni wapate kuitambua hekima ya Mungu iliyo ya namna nyingi.
11 Selon le décret éternel qu’il a accompli dans le Christ Jésus Notre Seigneur, (aiōn )
Mungu alifanya jambo hilo kufuatana na azimio lake la milele ambalo amelifanya kwa njia ya Kristo Bwana wetu. (aiōn )
12 En qui nous avons la liberté et l’accès auprès de Dieu, avec confiance par la foi en lui.
Basi, katika kuungana na Kristo, na kwa njia ya imani katika Kristo, sisi tunathubutu kumkaribia Mungu kwa uhodari.
13 Aussi je vous demande de ne vous point laisser abattre à cause de mes tribulations pour vous, car c’est votre gloire.
Kwa hiyo, nawaombeni msife moyo kwa sababu ya mateso ninayopata kwa ajili yenu, maana hayo ni kwa ajili ya utukufu wenu.
14 C’est pour cela que je fléchis les genoux devant le Père de Notre Seigneur Jésus-Christ,
Kwa sababu hiyo, nampigia magoti Baba,
15 De qui toute paternité tire son nom au ciel et sur la terre;
aliye asili ya jamaa zote duniani na mbinguni.
16 Afin qu’il vous accorde, selon les richesses de sa gloire, que vous soyez puissamment fortifiés par son Esprit dans l’homme intérieur;
Namwomba Mungu, kadiri ya utajiri wa utukufu wake, awajalieni kwa uwezo wa Roho wake, nguvu ya kuwa imara ndani yenu,
17 Que le Christ habite par la foi dans vos cœurs, et qu’enracinés et fondés dans la charité,
naye Kristo akae mioyoni mwenu kwa imani. Namwomba mpate kuwa na mzizi na msingi katika mapendo
18 Vous puissiez comprendre avec tous les saints, quelle est la largeur et la longueur, la hauteur et la profondeur,
kusudi muweze kufahamu pamoja na watu wote wa Mungu jinsi upendo wa Kristo ueneavyo kwa mapana na marefu, kwa kimo na kina.
19 Et connaître aussi la charité du Christ, qui surpasse toute science, afin que vous soyez remplis de toute la plénitude de Dieu.
Naam, mpate kujua upendo wa Kristo upitao elimu yote, mjazwe kabisa utimilifu wote wa Mungu.
20 Mais à celui qui est puissant pour tout faire bien au-delà de ce que nous demandons ou concevons, selon la vertu qui opère en nous,
Kwake yeye ambaye kwa nguvu yake ifanyayo kazi ndani yetu, aweza kufanya mambo makuu zaidi ya yale tuwezayo kuomba au kufikiria;
21 À lui la gloire dans l’Eglise et dans le Christ Jésus, dans toutes les générations du siècle des siècles! Amen. (aiōn )
kwake Mungu uwe utukufu katika kanisa na katika Kristo Yesu, nyakati zote, milele na milele! Amina. (aiōn )