< Ecclésiaste 7 >
1 Mieux vaut une bonne réputation que les parfums précieux; et le jour de la mort que le jour de la naissance.
Jina zuri ni bora kuliko manukato ya gharama, na siku ya kufa ni bora kuliko siku ya kuzaliwa.
2 Mieux vaut aller dans une maison de deuil que dans une maison de festin; car dans celle-là on est averti de la fin de tous les hommes, et le vivant pense à ce qui doit arriver.
Ni bora kwenda kwenye nyumba ya maombolezo kuliko nyumba ya karamu, kwa kuwa maombolezo huja kwa watu wote wakati wa mwisho wa uhai, kwa hiyo watu wanaoishi ni lazima waweke hili moyoni.
3 Mieux vaut la colère que le rire, parce que par la tristesse du visage est corrigé le cœur de celui qui pèche.
Huzuni ni bora kuliko kicheko, kwa kuwa baada ya uso wa huzuni huja furaha ya moyo.
4 Le cœur des sages est où est la tristesse; et le cœur des insensés où est la joie.
Moyo wa mwenye hekima uko katika nyumba ya maombolezo, lakini moyo wa wapumbavu uko katika nyumba ya karamu.
5 Mieux vaut être repris par un sage que d’être trompé par les flatteries des insensés;
Ni bora kusikiliza maonyo ya mtu mwenye hekima kuliko kusikiliza wimbo wa wapumbavu.
6 Parce que, comme est le pétillement des épines qui brûlent sous une marmite, ainsi est le rire de l’insensé; mais cela même est vanité.
Kwa kuwa kama mlio wa miiba chini ya chungu, ndivyo kilivyo kicheko cha wapumbavu. Huu pia ni mvuke.
7 L’oppression trouble le sage, et elle détruira la force de son cœur.
kweli jeuri humfanya mtu mwenye hekima kuwa mpumbavu, na rusha huharibu moyo.
8 Mieux vaut la fin d’un discours que le commencement. Mieux vaut un homme patient qu’un arrogant.
Ni heri mwisho wa jambo kuliko mwanzo; na watu wenye uvumilivu ni bora kuliko wenye majivuno rohoni.
9 Ne sois pas prompt à te mettre en colère; parce que la colère repose dans le sein de l’insensé.
Usikasirike haraka rohoni mwako, kwa sababu hasira hukaa katika mioyo ya wapumbavu.
10 Ne dis pas: Quelle est la cause, penses-tu, que les temps anciens furent meilleurs qu’ils ne sont maintenant? car insensée est une question de ce genre.
Usiseme, “Kwa nini siku za zamani zilikuwa bora kuliko siku hizi?” Kwa kuwa sio kwa sababu ya hekima kwamba unauliza swali hili.
11 La sagesse est plus utile avec les richesses, et elle sert davantage à ceux qui voient le soleil.
Hekima ni njema kama vitu vya thamani tunavyorithi kutoka kwa wazazi wetu. Inatoa faida kwa wale wanaoliona jua.
12 Car comme la sagesse protège, l’argent protège aussi; mais l’instruction a cela de plus, ainsi que la sagesse, qu’elles donnent la vie à leur possesseur.
Kwa kuwa hekima hutoa ulinzi kama vile fedha inavyoweza kutoa ulinzi, lakini faida ya maarifa ni kwamba hekima humpa uhai kwa yeyote aliye nayo.
13 Considère les œuvres de Dieu: personne ne peut corriger celui qu’il méprise.
Tafakaria matendo ya Mungu: Ni nani awezaye kuimarisha chochote alichokipindisha?
14 Au jour heureux, jouis des biens, et précautionne-toi contre le mauvais jour; car comme l’un, ainsi il a fait l’autre, sans que l’homme trouve contre lui de justes plaintes.
Wakati nyakati vinakuwa njema, ishi kwa furaha katika hali hiyo, lakini wakati unapokuwa mbaya, tafakari hili: Mungu ameruhusu hali zote ziwepo, Kwa sababu hii, hakuna mwanadamu yeyote atakaye fahamu chochote kinacho kuja baada yake.
15 J’ai encore vu ceci dans les jours de ma vanité: le juste périt dans sa justice, et l’impie vit longtemps dans sa malice.
Nimeona mambo mengi katika siku zangu za ubatili. Kuna watu wenye haki ambao wanaangamia licha ya kwamba wana haki, na kuna watu waovu wanaoishi maisha marefu licha ya kwamba ni waovu.
16 Ne sois point juste à l’excès, ni plus sage qu’il n’est nécessaire, pour que tu ne deviennes pas insensible.
Usiwe mwenye haki katika macho yako mwenyewe. Kwa nini kujiharibu mwenyewe?
17 N’agis pas en impie à l’excès; et ne sois pas insensé, afin que tu ne meures pas dans un temps qui n’est pas le tien.
Usiwe mwovu sana au mpumbavu. Kwa nini ufe kabla ya wakati wako?
18 Il est bon que tu soutiennes le juste; mais même ne retire pas de celui-là ta main, parce que celui qui craint Dieu ne néglige rien.
Ni vyema kwamba ushike hekima hii, na kwamba usiache haki iende zake. Kwa kuwa mtu amchae Mungu atatimiza ahadi zake zote.
19 La sagesse a rendu le sage plus fort que dix princes d’une cité.
Hekima ina nguvu ndani ya mwenye hekima, zaidi ya watawala kumi katika mji.
20 Car il n’est pas d’homme juste sur la terre qui fasse le bien et ne pèche point.
Hakuna mtu mwenye haki juu ya nchi anayefanya mema na hatendi dhambi.
21 Mais surtout, à toutes les paroles qui se disent, ne prête pas ton cœur; de peur que tu n’entendes ton serviteur te maudire;
Usisikilize kila neno linaongelewa, kwa sababu unaweza kusikia mtumishi wako anakulaani.
22 Car ta conscience sait que toi-même tu as fréquemment maudit les autres.
Vivyo hivyo unafahamu mwenyewe ndani ya moyo wako umewalaani wengine mara kadhaa.
23 J’ai tout tenté avec la sagesse. J’ai dit: Je deviendrai sage, et la sagesse s’est retirée bien loin de moi
Haya yote nimeyathibitisha kwa hekima. Nikasema, “nitakuwa mwenye hekima,” lakini zaidi ambavyo ningekuwa.
24 Beaucoup plus loin qu’elle n’était, et grande est sa profondeur; qui la trouvera?
Hekima i mbali na kina sana. Ni nani awezaye kuipata?
25 J’ai parcouru toutes choses avec mon esprit, afin de savoir, de considérer, et de chercher la sagesse et la raison des choses, et de connaître l’impiété de l’insensé et l’erreur des imprudents:
Nikageuza moyo wangu kujifunza kuchunguza na kutafuta hekima na ufafanuzi wa ukweli, na kufahamu kwamba ubaya ni ujinga na kwamba upumbavu ni wazimu.
26 Et j’ai trouvé la femme plus amère que la mort; elle est un lacs de chasseur, son cœur est un filet, ses mains sont des chaînes. Celui qui plaît à Dieu lui échappera; mais celui qui est pécheur sera pris par elle.
Nikapata kufahamu kwamba uchungu kuliko kifo, ndivo alivyo mwanamke yeyote ambaye moyo wake umejaa mitego, na nyavu, na ambaye mikono yake ni minyororo. Yeyote ampendezaye Mungu ataponyoka kutoka kwake, lakini mwenye dhambi atachukuliwa naye.
27 Voilà ce que j’ai trouvé, dit l’Ecclésiaste, une chose et une autre, afin de trouver une raison,
“Tafakari kile nilichovumbua,” asema Mwalimu. “Nimekuwa nikiongeza uvumbuzi mmoja hadi mwingine ili kwamba nipate ufafanuzi wa ukweli.
28 Que cherche encore mon âme, et que je n’ai pas trouvée. J’ai trouvé un homme entre mille; une femme entre toutes, je ne l’ai pas trouvée.
Hii ndiyo bado natafuta, lakini bado sijapata. Sikupata mwanamme mmoja mwenye haki miongoni mwa elfu, lakini sikupata mwanamke miongoni mwa wale wote.
29 J’ai trouvé cela seulement, que Dieu a fait l’homme droit, et que celui-ci s’est embarrassé lui-même dans des questions infinies.
Nimegundua hili: kwamba Mungu alimuumba binadamu akiwa mnyoofu, lakini wametoka katika hali ya unyofu wakitafuta magumu mengi.