< Deutéronome 23 >

1 Un eunuque dont les parties génératrices auront été froissées, ou amputées, ou arrachées, n’entrera point dans l’assemblée du Seigneur.
Mwanamume aliyejeruhiwa kwa kupondwa au kukatwa haruhusiwi kuingia katika kusanyiko la Yahwe.
2 Un bâtard, c’est-à-dire, un homme né d’une prostituée, n’entrera point dans l’assemblée du Seigneur, jusqu’à la dixième génération.
Mwana haramu haruhusiwi kuwa miongoni mwa kusanyiko la Yahwe; kutoka hadi kizazi cha kumi cha uzao wake, hakuna kati yao anatakiwa kuwa kwenye kusanyiko la Yahwe.
3 L’Ammonite et le Moabite n’entreront point dans l’assemblée du Seigneur, même après la dixième génération, à jamais,
Muamori au Mmoabu haruhusiwi kuwa miongoni mwa kusanyiko la Yahwe; kutoka hadi kizazi cha kumi cha uzao wake, hakuna kati yao anatakiwa kuwa kwenye kusanyiko la Yahwe.
4 Parce qu’ils n’ont pas voulu venir au-devant de vous avec le pain et l’eau, dans le chemin, lorsque vous êtes sortis de l’Egypte; et parce qu’ils ont gagné contre toi Balaam, fils de Béor, de la Mésopotamie de Syrie, afin qu’il te maudît;
Hii ni kwa sababu hawakukutana nanyi kwa mkate na maji barabarani mlipokuwa mmetoka nje ya Misri, na kwa sababu walimkodisha Balaamu mwana wa Beoro kutoka Pethoro kule Aramu Naharaimu, awalaani.
5 Mais le Seigneur ton Dieu ne voulut point écouter Balaam, et il changea sa malédiction en bénédiction pour toi, parce qu’il t’aimait.
Lakini Yahwe Mungu wako hakumsikiliza Balaamu; badala yake, Yahwe Mungu wako aligeuza laana kuwa baraka kwenu, kwa sababu Yahwe Mungu wako aliwapenda.
6 Tu ne feras point de paix avec eux, et tu ne rechercheras aucun bien pour eux durant tous les jours de ta vie, à jamais.
Hamtakiwi kutafuta amani au mafanikio yao, katika siku zenu zote.
7 Tu n’auras point l’Iduméen en abomination, parce qu’il est ton frère; ni l’Egyptien, parce que tu as été étranger dans sa terre.
Hutakiwi kumchukia Muedomi, kwa maana ni kaka yako; hutakiwi kumchukia Mmisri, kwa maana ulikuwa mgeni katika nchi yake.
8 Ceux qui seront nés d’eux, à la troisième génération, entreront dans l’assemblée du Seigneur.
Wazawa wa kizazi cha tatu wanaozaliwa kwao wanaweza kuwa katika kusanyiko la Yahwe.
9 Quand tu sortiras contre tes ennemis pour un combat, tu te garderas de toute chose mauvaise.
Utakapotembea kijeshi dhidi ya maadui zako, basi unapaswa kujitenga na kila aina ya uovu.
10 S’il se trouve parmi vous un homme qui a été souillé dans un songe nocturne, il sortira hors du camp,
Iwapo miongoni mwenu kuna mwanamume ambaye sio msafi kwa sababu ya jambo lililofanyika kwake usiku, basi anatakiwa atoke nje ya kambi ya jeshi; hatakiwi kurudi kambini.
11 Et il n’y reviendra point, avant qu’il ne se soit lavé vers le soir, dans l’eau; et après le coucher du soleil, il reviendra dans le camp.
Jioni ikifika, anatakiwa ajiogeshe kwa maji; na jua likizama atarudi ndani kambini.
12 Tu auras un lieu hors du camp, où tu iras pour les besoins de la nature,
Pia unatakiwa kuwa na eneo nje ya kambi ambayo utakwenda;
13 Portant un pieu à la ceinture; et lorsque tu voudras l’asseoir, tu feras un trou en rond, et tu couvriras de terre ce qui est sorti de toi,
na utakuwa na kitu katika zana zako cha kuchimbia; utakapochuchumaa kujisaidia, unapaswa kuchimbia nacho na kisha kurudishia udongo na kufunika kile kilichotoka kwako.
14 Après que tu te seras relevé de là (car le Seigneur ton Dieu marche au milieu de ton camp, pour te délivrer, et te livrer tes ennemis); ainsi, que ton camp soit saint, et qu’il n’y paraisse aucune saleté, de peur qu’il ne t’abandonne.
Kwa maana Yahwe Mungu wako anatembea miongoni mwa kambi yenu kuwapa ushindi na kuwapa maadui zenu mkononi mwenu. Kwa hiyo kambi yenu lazima iwe takatifu, ili kwamba asione kitu chochote kichafu miongoni mwenu na kuwaacha.
15 Tu ne livreras point à son maître l’esclave qui se sera réfugié près de toi;
Hutakiwi kumrudishia bwana mtumwa aliyetoroka kwake.
16 Il habitera avec toi dans le lieu qui lui plaira, et il se reposera dans une de tes villes; ne le contriste pas.
Mruhusu aishi pamoja nawe, katika mji wowote atakaochagua. Usimuonee.
17 Il n’y aura point de femme publique d’entre les filles d’Israël, ni de prostitué d’entre les enfants d’Israël.
Hapatakiwi kuwa na kahaba wa kidhehebu miongoni mwa mabinti wa Israeli, na wala hapatakiwi kuwa na kahaba wa kidhehebu miongoni mwa wana wa kiume wa Israeli.
18 Tu n’offriras point la récompense de la prostitution, ni le prix d’un chien, dans la maison du Seigneur ton Dieu, quoi que ce soit que tu aies voué, parce que l’un et l’autre est une abomination auprès du Seigneur ton Dieu.
Hautakiwi kuleta mshahara wa kahaba au mshahara wa mbwa katika nyumba ya Yahwe Mungu wako kwa kiapo chochote; kwa maana vyote hivi na machukizo mbele ya Yahwe Mungu wako.
19 Tu ne prêteras à usure à ton frère, ni argent, ni grains, ni quelque autre chose que ce soit;
Hutakiwi kumkopesha Muisraeli mwenzako kwa riba – riba ya fedha, riba ya chakula, au riba ya kitu chochote kinachokopeshwa kwa riba.
20 Mais à l’étranger. Quant à ton frère, ce sera sans usure, que tu lui prêteras ce dont il aura besoin, afin que le Seigneur ton Dieu te bénisse en toutes tes œuvres, dans la terre dans laquelle tu entreras pour la posséder.
Kwa mgeni unaweza kukopesha kwa riba; lakini kwa Muisraeli mwenzako haupaswi kukopesha kwa riba, ili kwamba Yahwe Mungu wako aweze kukubariki katika kila jambo uwekalo mkono wako, katika nchi ambayo mnaenda kumiliki.
21 Lorsque tu auras voué un vœu au Seigneur ton Dieu, tu ne tarderas point à l’acquitter, parce que le Seigneur ton Dieu te le redemandera; et si tu diffères il te sera imputé à péché.
Unapofanya kiapo kwa Yahwe Mungu wako, haupaswi kukawia kuikamilsha, kwa maana Yahwe Mungu wako hakika atadai kiapo hicho; itakuwa dhambi kako usipokamilisha.
22 Si tu ne veux point promettre, tu seras sans péché.
Lakini iwapo utajizuia kutoa kiapo, haitakuwa dhambi kwako.
23 Mais ce qui une fois est sorti de tes lèvres, tu l’observeras, et tu feras comme tu as promis au Seigneur ton Dieu; car tu as parlé par ta propre volonté et par ta bouche.
Kile ambacho kimetoka kinywani mwako unapaswa kukifuata na kukitekeleza; kulingana na kiapo ulichotamka kwa Yahwe Mungu wako, chochote ulichotamka kwa hiari kwa kinywa chako.
24 Entré dans la vigne de ton prochain, mange des raisins autant qu’il te plaira; mais n’en emporte point dehors avec toi.
Utakapokwenda katika shamba la mizabibu la jirani yako, unatakiwa kula mizabibu idadi yoyote unayotaka, lakini hautakiwi kuhifadhi yoyote katika kikapu chako.
25 Si tu entres dans les blés de ton ami, tu cueilleras des épis et tu les broieras avec la main; mais tu n’en couperas pas avec la faux.
Utakapokwenda katika shamba la zao lililoiva la jirani yako, unaweza kuvuna kichwa cha mavuno kwa mkono wako, lakini haupaswi kutumia mundu kuvuna zao lililoiva la jirani yako.

< Deutéronome 23 >