< Deutéronome 2 >

1 Or, partis de là, nous vînmes au désert qui conduit à la mer Rouge, comme m’avait dit le Seigneur, et nous tournâmes autour de la montagne de Séir, durant un long temps.
Kisha tukageuka nyuma na kusafiri kuelekea jangwani kwa njia inayoelekea Bahari ya Shamu, kama Bwana alivyonielekeza. Kwa muda mrefu tulitembea kuzunguka vilima katika nchi ya Seiri.
2 Et le Seigneur me dit:
Kisha Bwana akaniambia,
3 Vous avez suffisamment tourné autour de cette montagne, allez contre l’aquilon:
“Umetembea kuzunguka hii nchi ya vilima kwa muda wa kutosha; sasa geukia kaskazini.
4 Et ordonne au peuple, disant: Vous passerez par les frontières de vos frères, les enfants d’Esaü, qui habitent à Séir, et ils vous craindront.
Wape watu maagizo haya: ‘Mko karibu kupita katikati ya nchi ya ndugu zako ambao ni wazao wa Esau, ambao wanaishi Seiri. Watawaogopa, lakini mwe waangalifu.
5 Voyez avec soin à ne pas vous mettre en mouvement contre eux; car je ne vous donnerai pas de leur terre, et autant que la plante d’un seul pied peut en fouler, parce que j’ai donné en possession à Esaü la montagne de Séir.
Msiwachokoze kwa vita kwa maana sitawapa ninyi sehemu yoyote ya nchi yao, hata sehemu ya kutosha kuweka wayo wenu juu yake. Nimempa Esau nchi ya vilima ya Seiri kama yake mwenyewe.
6 Vous achèterez d’eux des vivres avec de l’argent, et vous mangerez; vous puiserez de l’eau achetée, et vous boirez.
Mtawalipa fedha kwa chakula mtakachokula na maji mtakayokunywa.’”
7 Le Seigneur ton Dieu t’a béni en toute œuvre de tes mains; il connaît ton chemin: comment tu as passé ce grand désert; le Seigneur ton Dieu a habité avec toi pendant quarante ans, et rien ne t’a manqué.
Bwana Mungu wenu amewabariki kwa kazi yote ya mikono yenu. Amewalinda katika safari yenu katikati ya jangwa hili kubwa. Kwa miaka hii arobaini Bwana Mungu wenu amekuwa pamoja nanyi, na hamkupungukiwa na kitu chochote.
8 Lorsque nous eûmes passé à travers nos frères, les enfants d’Esaü, qui habitaient à Séir, nous sommes venus par la voie de la plaine, d’Elath et d’Asiongaber au chemin qui conduit au désert de Moab.
Basi tulipita kwa ndugu zetu wazao wa Esau ambao wanaishi Seiri. Tuligeuka kutoka njia ya Araba ambayo inatokea Elathi na Esion-Geberi, tukasafiri kufuata njia ya jangwa la Moabu.
9 Alors le Seigneur me dit: Ne combats point contre les Moabites, et ne leur livre point bataille; car je ne te donnerai rien de leur terre, parce que c’est aux enfants de Lot que j’ai livré Ar en possession.
Kisha Bwana akaniambia, “Usiwasumbue Wamoabu kwa vita, kwa kuwa sitawapa sehemu yoyote ya nchi yao. Nimetoa nchi ya Ari kwa wazao wa Loti kama milki yao.”
10 Les Emim furent ses premiers habitants, peuple grand et fort, et d’une stature si haute, que la race des Enacim
(Waemi walikuwa wakiishi huko hapo zamani, watu wenye nguvu na wengi, warefu kama Waanaki.
11 Etait regardée comme leur souche, de même que celle des géants, et qu’ils étaient semblables aux enfants d’Enacim. Enfin les Moabites les appellent Emim.
Kama walivyokuwa Waanaki, hao pia walikuwa kama Warefai, lakini Wamoabu waliwaita Waemi.
12 Quant à Séir, les Horrhéens y avaient jadis habité; lesquels chassés et détruits, les enfants d’Esaü y habitèrent, comme a fait Israël dans la terre de sa possession que lui a donnée le Seigneur.
Wahori waliishi Seiri, lakini wazao wa Esau waliwafukuza. Waliwaangamiza Wahori na kukaa mahali pao, kama Waisraeli walivyofanya katika nchi ambayo Bwana aliwapa kama milki yao.)
13 Nous levant donc pour passer le torrent de Zared, nous vînmes auprès.
Bwana akasema, “Sasa ondokeni mvuke Bonde la Zeredi.” Hivyo tukavuka bonde.
14 Or, le temps pendant lequel nous marchâmes de Cadesbarné jusqu’au passage du torrent de Zared, fut de trente-huit ans, jusqu’à ce que toute la génération des hommes combattants eut été exterminée du camp, comme l’avait juré le Seigneur,
Miaka thelathini na minane ilipita tangu wakati tulipoondoka Kadesh-Barnea mpaka tulipovuka Bonde la Zeredi. Kwa wakati huo kile kizazi chote cha wanaume kuanzia wale wawezao kwenda vitani kilikuwa kimekufa, kama Bwana alivyokuwa amewaapia.
15 Dont la main fut contre eux, pour qu’ils périssent du milieu du camp.
Mkono wa Bwana uliwakabili hadi alipowaangamiza wote huko kambini.
16 Or, après que tous les combattants furent tombés,
Ikawa baada ya mtu wa mwisho kuanzia wale wawezao kwenda vitani kufa,
17 Le Seigneur me parla, disant:
Bwana akaniambia,
18 Tu franchiras aujourd’hui les frontières de Moab, la ville du nom d’Ar:
“Leo utapita katika nchi ya Moabu huko Ari.
19 Et t’approchant des lieux voisins des enfants d’Ammon, garde-toi de combattre contre eux, et de les provoquer au combat; car je ne te donnerai point de la terre des enfants d’Ammon, parce que c’est aux enfants de Lot que je l’ai donnée en possession.
Utakapokuja kwa Waamoni, msiwasumbue wala kuwachokoza kwa vita, kwa kuwa sitawapa ardhi yoyote iliyo ya Waamoni kuwa milki yenu. Nimeitoa kama milki ya wazao wa Loti.”
20 Elle a été réputée terre des géants, et en elle autrefois ont habité des géants que les Ammonites appellent Zomzommim,
(Hiyo pia ilidhaniwa kuwa nchi ya Warefai waliokuwa wakiishi huko, lakini Waamoni waliwaita Wazamzumi.
21 Peuple grand et nombreux, et d’une haute taille comme les Enacim, et que le Seigneur détruisit devant les Ammonites qu’il fit habiter en leur place,
Walikuwa watu wenye nguvu na wengi, warefu kama Waanaki. Bwana akawaangamiza kutoka mbele ya Waamoni, ambao waliwafukuza na kukaa mahali pao.
22 Comme il avait fait pour les enfants d’Esaü qui habitent à Séir, détruisant les Horrhéens, et leur livrant leur terre qu’ils possèdent jusqu’à présent.
Bwana alikuwa amefanya vivyo hivyo kwa wazao wa Esau, ambao waliishi Seiri, wakati alipowaangamiza Wahori watoke mbele yao. Waliwafukuza na wao wakaishi mahali pao mpaka leo.
23 Les Hévéens aussi qui habitaient à Hasérim jusqu’à Gaza, furent chassés par les Cappadociens, qui, sortis de Cappadoce, les détruisirent et habitèrent en leur place.
Nao Waavi ambao waliishi katika vijiji mpaka Gaza, Wakaftori waliokuja kutoka Kaftori waliwaangamiza na kukaa mahali pao.)
24 Levez-vous et passez le torrent d’Arnon: voilà que j’ai livré en ta main Séhon, roi d’Hésébon, l’Amorrhéen, et commence à posséder sa terre, et engage un combat contre lui.
“Ondoka sasa na uvuke Bonde la Arnoni. Tazama, nimemweka mikononi mwako Sihoni Mwamori, mfalme wa Heshboni na nchi yake. Anza kuimiliki nchi hiyo na umwingize katika vita.
25 Aujourd’hui je commencerai à envoyer la terreur et l’effroi aux peuples qui sont sous le ciel entier, afin que, ton nom ouï, ils tremblent, et que, comme les femmes qui enfantent, ils frémissent, et soient saisis par la douleur.
Siku hii ya leo nitaanza kuwatia hofu na woga mataifa yote chini ya mbingu wawaogope ninyi. Watakaposikia taarifa zenu, watatetemeka na kufadhaika kwa sababu yenu.”
26 J’envoyai donc des messagers du désert de Cadémoth vers Séhon, roi d’Hésébon, avec des paroles de paix, disant:
Kutoka jangwa la Kedemothi nilituma wajumbe wenye maneno ya amani kwa Sihoni mfalme wa Heshboni kusema,
27 Nous passerons à travers ta terre; nous marcherons par la voie publique; nous ne nous détournerons ni à droite ni à gauche.
“Turuhusu tupite katika nchi yako. Tutapita katika barabara kuu, hatutageuka kuume wala kushoto.
28 Vends-nous des vivres selon le prix, afin que nous mangions: donne-nous de l’eau pour de l’argent, et ainsi nous boirons. Le tout est que tu nous accordes le passage,
Tuuzie chakula tule na maji tunywe kwa thamani yake katika fedha. Turuhusu tu tupite kwa miguu,
29 Comme ont fait les enfants d’Esaü qui habitent à Séir, et les Moabites qui demeurent à Ar, jusqu’à ce que nous arrivions au Jourdain, et que nous passions dans la terre que le Seigneur notre Dieu doit nous accorder.
kama wazao wa Esau ambao wanaishi Seiri na Wamoabu ambao wanaishi Ari walivyotufanyia, mpaka tuvuke Yordani kuingia nchi ambayo Bwana Mungu wetu anatupatia.”
30 Mais Séhon, roi d’Hésébon, ne voulut point nous donner le passage, parce que le Seigneur ton Dieu avait endurci son esprit et fermé son cœur, afin qu’il fût livré en tes mains, comme tu vois maintenant.
Lakini Sihoni mfalme wa Heshboni alikataa kuturuhusu kupita. Kwa kuwa Bwana Mungu wako alikuwa ameifanya roho yake kuwa ngumu na moyo wake kuwa mkaidi ili amweke kwenye mikono yenu, kama alivyofanya sasa.
31 Alors le Seigneur me dit: Voilà que j’ai commencé à te livrer Séhon et sa terre: commence à la posséder.
Bwana akaniambia, “Tazama, nimeanza kuwapa Mfalme Sihoni na nchi yake kwako. Sasa anzeni kuishinda na kuimiliki nchi yake.”
32 Et Séhon sortit au-devant de nous avec tout son peuple pour nous combattre à Jasa;
Wakati Sihoni pamoja na jeshi lake lote walipokuja kukutana nasi katika vita huko Yahazi,
33 Et le Seigneur notre Dieu nous le livra, et nous le battîmes avec ses fils et tout son peuple.
Bwana Mungu wetu alimweka mikononi mwetu, nasi tukamwangamiza pamoja na wanawe na jeshi lake lote.
34 Nous prîmes en ce temps-là toutes ses villes, nous tuâmes les habitants, hommes, femmes et petits enfants, et nous n’y laissâmes rien,
Kwa wakati ule tuliteka miji yake yote na kuiangamiza kabisa: wanaume, wanawake na watoto. Hatukumwacha yeyote.
35 Excepté les bestiaux, qui devinrent la part de ceux qui les pillèrent, et les dépouilles des villes que nous prîmes.
Lakini mifugo na nyara tulizoziteka kutoka ile miji tulijichukulia wenyewe.
36 Depuis Aroër, qui est sur le bord du torrent d’Arnon, ville qui est située dans la vallée, jusqu’à Galaad, il n’y eut point de bourg ni de ville qui échappât à nos mains; le Seigneur notre Dieu nous les livra toutes,
Kutoka Aroeri kwenye ukingo wa Bonde la Arnoni, kutoka mji ulio ndani ya bonde, hata mpaka Gileadi, hapakuwa na mji hata mmoja uliokuwa na nguvu kutushinda. Bwana Mungu wetu alitupa yote.
37 Excepté la terre des enfants d’Ammon, dont nous n’avons pas approché, et tout ce qui se trouve auprès du torrent de Jéboc, et les villes des montagnes, et tous les lieux que le Seigneur notre Dieu nous a interdits.
Lakini kulingana na amri ya Bwana Mungu wetu, hamkujiingiza katika nchi yoyote ya Waamoni, wala katika sehemu yoyote iliyo kandokando ya Mto Yaboki, wala katika miji iliyoko katika vilima.

< Deutéronome 2 >