< Colossiens 1 >

1 Paul, apôtre de Jésus-Christ par la volonté de Dieu, et Timothée son frère;
Mimi Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, na ndugu Timotheo,
2 Aux saints et aux frères fidèles en Jésus-Christ qui sont à Colosse,
tunawaandikia ninyi watu wa Mungu huko Kolosai, ndugu zetu waaminifu katika kuungana na Kristo. Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu.
3 Grâce à vous et paix par Dieu notre Père, et par Notre Seigneur Jésus-Christ. Nous rendons grâces à Dieu le Père de Notre Seigneur Jésus-Christ, priant sans cesse pour vous;
Daima tunamshukuru Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, wakati tunapowaombea.
4 Depuis que nous avons appris votre foi dans le Christ Jésus, et la charité que vous avez pour tous les saints,
Maana tumesikia juu ya imani yenu katika Kristo Yesu na juu ya upendo wenu kwa watu wote wa Mungu.
5 À cause de l’espérance qui vous est réservée dans les cieux, et dont vous avez eu connaissance par la parole de la vérité de l’Evangile,
Wakati ujumbe ule wa kweli, yaani Habari Njema, ilipowafikieni kwa mara ya kwanza, mlipata kusikia juu ya lile tumaini linalopatikana kwake. Kwa sababu hiyo imani na upendo wenu vinategemea jambo lile mnalotumainia ambalo mmewekewa salama mbinguni.
6 Qui vous est parvenu, comme il est aussi répandu dans le monde entier, où il fructifie et croît, ainsi qu’en vous, depuis le jour où vous l’avez entendu, et où vous avez connu la grâce de Dieu dans la vérité;
Habari Njema inazidi kuzaa matunda na kuenea ulimwenguni kote kama vile ilivyofanya kwenu ninyi tangu siku ile mliposikia juu ya neema ya Mungu na kuitambua ilivyo kweli.
7 Selon que vous l’avez appris du très cher Epaphras, notre compagnon dans le service de Dieu et ministre fidèle du Christ Jésus à votre égard;
Mlijifunza juu ya neema ya Mungu kutoka kwa Epafra, mtumishi mwenzetu, ambaye ni mfanyakazi mwaminifu wa Kristo kwa niaba yetu.
8 Lequel nous a fait connaître aussi votre charité toute spirituelle.
Yeye alitupa habari za upendo wenu mliojaliwa na Roho.
9 C’est pourquoi, du jour où nous l’avons appris, nous ne cessons de prier pour vous, et de demander à Dieu que vous soyez remplis de la connaissance de sa volonté, en toute sagesse et intelligence spirituelle;
Kwa sababu hiyo tumekuwa tukiwaombeeni daima tangu tulipopata habari zenu. Tunamwomba Mungu awajazeni ujuzi kamili wa mapenzi yake, awajazeni hekima yote na elimu iletwayo na Roho wake.
10 Afin que vous marchiez d une manière digne de Dieu, lui plaisant en toutes choses, fructifiant en toutes sortes de bonnes œuvres, et croissant dans la science de Dieu;
Hapo mtaweza kuishi kama anavyotaka Bwana na kutenda daima yanayompendeza. Maisha yenu yatakuwa yenye matunda ya kila namna ya matendo mema na mtazidi kukua katika kumjua Mungu.
11 Corroborés de toute force par la puissance de sa gloire, de toute patience et de toute longanimité accompagnée de joie;
Mungu awajalieni nguvu kwa uwezo wake mtukufu ili mweze kustahimili kila kitu kwa uvumilivu.
12 Rendant grâces à Dieu le Père qui nous a fait dignes d’avoir part à l’héritage des saints dans la lumière;
Na kwa furaha, mshukuruni Baba aliyewawezesha ninyi kuwa na sehemu yenu katika mambo yale Mungu aliyowawekea watu wake katika utawala wa mwanga.
13 Qui nous a arrachés de la puissance des ténèbres, et transférés dans le royaume du Fils de sa dilection,
Yeye alituokoa katika nguvu ya giza, akatuleta salama katika ufalme wa Mwanae mpenzi,
14 En qui nous avons la rédemption par son sang, la rémission des péchés;
ambaye kwa njia yake tunakombolewa, yaani dhambi zetu zinaondolewa.
15 Qui est l’image du Dieu invisible, le premier-né de toute créature.
Kristo ni mfano wa Mungu asiyeonekana; ni mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote.
16 Car c’est par lui que toutes choses ont été créées dans les cieux et sur la terre, les visibles et les invisibles, soit trônes, soit dominations, soit principautés, soit puissances: tout a été créé par lui et en lui;
Maana kwa njia yake vitu vyote viliumbwa duniani na mbinguni, vitu vinavyoonekana na visivyoonekana: wenye enzi, watawala, wakuu na wenye mamlaka. Vyote viliumbwa kwa njia yake na kwa ajili yake.
17 Et lui-même est avant tous, et tout subsiste en lui.
Kristo alikuwako kabla ya vitu vyote; kwa kuungana naye, vyote vyadumu mahali pake.
18 Et lui-même est le chef du corps de l’Eglise; il est le principe, le premier-né d’entre les morts, afin qu’en toutes choses il garde la primauté.
Yeye ni kichwa cha mwili wake, yaani kanisa; yeye ni chanzo cha uhai wa huo mwili. Yeye ndiye mwanzo, mzaliwa wa kwanza aliyefufuliwa kutoka wafu, ili awe na nafasi ya kwanza katika vitu vyote.
19 Parce qu’il a plu an Père que toute plénitude habitât en lui;
Maana Mungu alipenda utimilifu wote uwe ndani yake.
20 Et par lui de se réconcilier toutes choses, pacifiant par le sang de sa croix, soit ce qui est sur la terre, soit ce qui est dans les cieux.
Kwa njia yake Mungu alivipatanisha naye vitu vyote naam, viumbe vyote mbinguni na duniania; alileta amani kwa damu ya Kristo msalabani.
21 Et vous, qui autrefois étiez adversaires et ennemis en esprit par vos œuvres mauvaises,
Hapo kwanza ninyi pia mlikuwa mbali na Mungu na mlikuwa adui zake kwa sababu ya fikira zenu na matendo yenu maovu.
22 Il vous a maintenant réconciliés dans le corps de sa chair par la mort, pour vous rendre saints, purs et irrépréhensibles devant lui;
Lakini sasa, kwa kifo cha Mwanae aliyeishi hapa duniani, Mungu amewapatanisha naye, kusudi awalete mbele yake mkiwa watakatifu, safi na bila lawama.
23 Si toutefois vous demeurez fondés et affermis dans la foi, et inébranlables dans l’espérance de l’Evangile que vous avez entendu, qui a été prêché à toute créature qui est sous le ciel, et dont j’ai été fait ministre, moi Paul,
Mnapaswa, lakini kuendelea kuwa imara na thabiti katika imani hiyo, na msikubali kusukumwa mbali na tumaini lile mlilopata wakati mlipoisikia Habari Njema. Mimi Paulo nimekuwa mtumishi wa hiyo Habari Njema ambayo imekwisha hubiriwa kila kiumbe duniani.
24 Qui maintenant me réjouis dans mes souffrances pour vous, et accomplis dans ma chair ce qui manque aux souffrances du Christ, pour son corps qui est l’Eglise,
Na sasa nafurahi kuteseka kwa ajili yenu, maana kwa mateso yangu hapa duniani, nasaidia kukamilisha kile kilichopungua bado katika mateso ya Kristo kwa ajili ya mwili wake, yaani kanisa.
25 Dont j’ai été fait ministre, selon la dispensation de Dieu, qui m’a été confiée pour que je vous annonce complètement la parole de Dieu;
Nami nimefanywa kuwa mtumishi wa kanisa kufuatana na mpango wake Mungu ambao alinikabidhi kwa faida yenu. Mpango wenyewe ni kuutangaza kwa ukamilifu ujumbe wake,
26 Le mystère qui a été caché dès l’origine des siècles et des générations, et qui est maintenant révélé à ses saints, (aiōn g165)
ambao ni siri aliyowaficha binadamu wote tangu milele, lakini sasa amewajulisha watu wake. (aiōn g165)
27 Auxquels Dieu a voulu faire connaître quelles sont les richesses de la gloire de ce mystère parmi les nations, lequel est le Christ, pour vous l’espérance de la gloire,
Mpango wa Mungu ni kuwajulisha watu wake siri hii kuu na tukufu ambayo ni kwa ajili ya watu wote. Na, siri yenyewe ndiyo hii: Kristo yuko ndani yenu, na jambo hilo lamaanisha kwamba ninyi mtaushiriki utukufu wa Mungu.
28 Christ que nous vous annonçons, reprenant tout homme, et enseignant à tout homme toute sagesse, afin de rendre tout homme parfait dans le Christ Jésus:
Kwa sababu hiyo tunamhubiri Kristo kwa watu wote; tunawaonya na kuwafundisha wote kwa hekima yote, ili tuweze kumleta kila mmoja mbele ya Mungu akiwa amekomaa katika kuungana na Kristo.
29 Ce à quoi je travaille en combattant selon l’énergie qu’il produit puissamment en moi.
Kwa madhumuni hayo mimi nafanya kazi na kujitahidi nikiitumia nguvu kuu ya Kristo ifanyayo kazi ndani yangu.

< Colossiens 1 >