< Colossiens 4 >
1 Maîtres, rendez à vos serviteurs ce qui est juste et équitable, sachant que vous aussi vous avez un maître dans le ciel.
Nanyi wakuu, watendeeni watumwa wenu kwa uadilifu na haki, mkikumbuka kwamba nanyi pia mnaye Bwana mbinguni.
2 Persévérez dans la prière, et veillez-y en action de grâces;
Dumuni katika sala, na mnaposali muwe waangalifu, mkimshukuru Mungu.
3 Priant aussi en même temps pour nous, afin que Dieu ouvre une voie à notre parole, pour publier le mystère du Christ (pour lequel aussi je suis dans les liens),
Vilevile, mtuombee sisi pia ili Mungu atupe fursa ya kuuhubiri ujumbe wake kuhusu siri ya Kristo. Kwa ajili hiyo mimi niko sasa kifungoni.
4 Et que je le manifeste, comme il convient que j’en parle.
Basi, ombeni ili niweze kusema kama inavyonipasa na kwa namna itakayodhihirisha siri hiyo.
5 Conduisez-vous avec sagesse envers ceux qui sont dehors, en rachetant le temps.
Muwe na hekima katika uhusiano wenu na watu wasioamini, mkitumia vizuri kila nafasi mliyo nayo.
6 Que vos paroles soient toujours gracieuses, assaisonnées de sagesse, en sorte que vous sachiez comment il faut que vous répondiez à chacun.
Mazungumzo yenu yanapaswa kuwa daima mema na ya kuvutia, na mnapaswa kujua jinsi ya kumjibu vizuri kila mmoja.
7 Pour ce qui me concerne, Tychique, notre frère bien-aimé, fidèle ministre, et mon compagnon dans le service du Seigneur, vous apprendra toutes choses.
Ndugu yetu mpenzi Tukiko, mfanyakazi mwaminifu na mtumishi mwenzetu katika kazi ya Bwana, atawapeni habari zangu zote.
8 Je l’ai envoyé vers vous exprès, pour qu’il sache ce qui vous concerne, et console vos cœurs;
Ndiyo maana namtuma, ili aichangamshe mioyo yenu kwa kuwaambieni habari zetu.
9 De même qu’Onésime, notre fidèle et bien-aimé frère, qui est votre concitoyen. Pour tout ce qui se passe ici, ils vous le feront connaître.
Anakuja pamoja na Onesimo, ndugu yetu mpenzi na mwaminifu, ambaye ni mwananchi mwenzenu. Watawapeni habari za mambo yote yanayofanyika hapa.
10 Aristarque, mon compagnon de captivité, vous salue, et Marc, cousin de Barnabé, au sujet duquel vous avez reçu des ordres (s’il va chez vous, recevez-le),
Aristarko, ambaye yuko kifungoni pamoja nami, anawasalimuni; hali kadhalika Marko, binamu yake Barnaba, (mmekwisha pata maagizo juu yake; akifika kwenu mkaribisheni).
11 Et Jésus, qui est appelé Juste; lesquels sont de la circoncision: ce sont les seuls qui travaillent avec moi pour le royaume de Dieu, et ils ont été ma consolation.
Naye Yoshua aitwaye Yusto, anawasalimuni. Miongoni mwa Wayahudi waliokwisha pokea imani, hawa tu peke yao, ndio wanaofanya kazi pamoja nami kwa ajili ya Utawala wa Mungu; nao wamekuwa msaada mkubwa kwangu.
12 Epaphras, qui est votre concitoyen, vous salue; serviteur du Christ Jésus, et toujours plein de sollicitude pour vous dans ses prières, afin que vous demeuriez parfaits, et pleins de toutes les volontés de Dieu.
Epafra, mwananchi mwenzenu na mtumishi wa Kristo Yesu anawasalimuni. Daima anawaombeeni ninyi kwa bidii ili mpate kusimama imara, mkomae na kuwa thabiti kabisa katika mambo yote anayotaka Mungu.
13 Car je lui rends ce témoignage, qu’il prend beaucoup de peine pour vous et pour ceux qui sont à Laodicée et à Hiérapolis.
Naweza kushuhudia kwamba anafanya kazi kwa bidii kwa ajili yenu na kwa ajili ya watu wa Laodikea na Hierapoli.
14 Luc, le médecin bien-aimé, vous salue, et Démas.
Luka, daktari wetu mpenzi, na Dema, wanawasalimuni.
15 Saluez nos frères qui sont à Laodicée, et Nymphas, et l’Eglise qui est dans sa maison.
Salamu zetu kwa ndugu zetu wa Laodikea; msalimuni dada Nimfa pamoja na jumuiya yote ya waumini inayokutana nyumbani kwake.
16 Et quand cette lettre aura été lue parmi vous, faites qu’elle soit lue aussi dans l’Eglise de Laodicée; et celle des Laodicéens, lisez-la vous-mêmes.
Mkisha soma barua hii, hakikisheni kwamba inasomwa na Wakristo wa Laodikea; na ninyi fanyeni mpango mpate kuisoma barua waliyoipata kwao.
17 Dites à Archippe: Vois le ministère que tu as reçu dans le Seigneur, afin de le remplir.
Mwambieni Arkipo aitekeleze vizuri ile huduma aliyokabidhiwa na Bwana.
18 La salutation est de moi, Paul. Souvenez-vous de mes liens. Que la grâce soit avec vous. Amen.
Naandika haya kwa mkono wangu mwenyewe: Salamu kutoka kwangu, mimi Paulo. Kumbukeni kwamba niko kifungoni. Neema ya Mungu iwe nanyi.