< Amos 6 >
1 Malheur à vous qui êtes opulents dans Sion, et qui vous confiez en la montagne de Samarie; grands, chefs des peuples, qui entrez avec pompe dans la maison d’Israël.
Ole wenu ninyi mnaostarehe na kuridhika katika Sayuni, na ninyi mnaojisikia salama juu ya Mlima Samaria, ninyi watu mashuhuri wa taifa lililoendelea kuliko mataifa mengine, ambao watu wa Israeli wanawategemea!
2 Passez à Chalanée, et voyez, allez de là à Emath la grande, et descendez à Geth des Philistins et dans tous leurs plus beaux, royaumes, pour voir si leurs limites sont plus étendues que vos limites.
Nendeni Kalne mkaone kutoka huko; mwende hadi Hamathi iliyo kuu, kisha mshuke hadi Gathi ya Wafilisti. Je, wao ni bora kuliko falme zenu mbili? Je, nchi yao ni kubwa kuliko yenu?
3 Vous qui êtes réservés pour un jour mauvais, et qui vous avancez vers un trône d’iniquité;
Mnaiweka mbali siku iliyo mbaya na kuleta karibu utawala wa kuogofya.
4 Qui dormez sur des lits d’ivoire, et vous étendez mollement sur vos couches; qui mangez l’agneau du premier bétail et les veaux tirés du milieu du gros bétail;
Ninyi mnalala juu ya vitanda vilivyofunikwa kwa pembe za ndovu, na kujinyoosha juu ya viti vya fahari. Mnajilisha kwa wana-kondoo wazuri na ndama walionenepeshwa.
5 Qui chantez aux accords du psaltérion; ils ont pensé qu’ils avaient des instruments pour les cantiques comme David;
Ninyi mnapiga vinubi kama Daudi, huku mkitunga nyimbo za vinanda mbalimbali.
6 Ils buvaient du vin dans des coupes, se parfumaient de la meilleure huile de senteur et étaient insensibles à la ruine de Joseph.
Mnakunywa mvinyo kwa bakuli zilizojazwa, na mnajipaka mafuta mazuri, lakini hamhuzuniki kwa maangamizi ya Yosefu.
7 À cause de quoi, ils transmigreront à la tête des exilés, et cette troupe d’efféminés sera emportée.
Kwa hiyo mtakuwa miongoni mwa watu wa kwanza kwenda uhamishoni; karamu zenu na kustarehe kutakoma.
8 Le Seigneur Dieu a juré par son âme; le Seigneur Dieu des armées dit: Je déteste l’orgueil de Jacob, et je hais ses maisons; et je livrerai la cité avec ses habitants.
Bwana Mwenyezi ameapa kwa nafsi yake mwenyewe: Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote asema: “Nachukia kiburi cha Yakobo, nachukia ngome zake; nitautoa mji wao na kila kitu kilichomo ndani mwake.”
9 Que s’il reste dix hommes dans une seule maison, eux-mêmes aussi mourront.
Kama watu kumi watabaki katika nyumba moja, wao pia watakufa.
10 Et le parent de l’un l’enlèvera et le brûlera, afin d’emporter ses os de la maison, et il dira à celui qui est au fond de la maison: Est-ce qu’il y a encore quelqu’un chez toi? Et il répondra: C’est la fin. Et l’autre lui dira: Tais-toi, et ne te souviens pas du nom du Seigneur.
Kama jamaa ambaye atachoma miili akija ili kuitoa nje ya nyumba, na kumuuliza yeyote ambaye bado anajificha humo, “Je, yuko mtu yeyote pamoja nawe?” Naye akisema, “Hapana,” ndipo atakaposema, “Nyamaza kimya! Haturuhusiwi kutaja jina la Bwana.”
11 Parce que voici que le Seigneur commandera, et il frappera la grande maison de ruines, et la petite maison de déchirements.
Kwa kuwa Bwana ameamuru, naye atabomoa jumba kubwa vipande vipande na nyumba ndogo vipande vidogo vidogo.
12 Est-ce que des chevaux peuvent courir au milieu des rochers, ou peut-on labourer avec les buffles? C’est pourtant ce que vous avez fait vous-mêmes, puisque vous avez changé le jugement en amertume, et le fruit de la justice en absinthe.
Je, farasi waweza kukimbia kwenye miamba mikali? Je, aweza mtu kulima huko kwa maksai? Lakini mmegeuza haki kuwa sumu na matunda ya uadilifu kuwa uchungu:
13 Vous qui vous réjouissez dans le néant, qui dites: N’est-ce point par notre propre force que nous avons établi notre puissance?
ninyi mnaoshangilia kushindwa kwa Lo-Debari na kusema, “Je, hatukuteka Karnaimu kwa nguvu zetu wenyewe?”
14 Maison d’Israël, voici que je susciterai contre vous une nation, dit le Seigneur Dieu des armées, et elle vous brisera depuis l’entrée d’Emath jusqu’au torrent du désert.
Maana Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote asema, “Nitainua taifa dhidi yenu, ee nyumba ya Israeli, nalo litawatesa kuanzia Lebo-Hamathi hadi Bonde la Araba.”