< Actes 26 >

1 Alors Agrippa dit à Paul: On te permet de parler pour te défendre. Paul aussitôt, étendant la main, commença sa justification.
Ndipo Agripa akamwambia Paulo, “Unayo ruhusa kujitetea.” Hivyo Paulo akawaashiria kwa mkono wake, akaanza kujitetea, akasema:
2 Roi Agrippa, je m’estime heureux d’avoir, sur toutes les choses dont les Juifs m’accusent, à me défendre aujourd’hui devant vous,
“Mfalme Agripa, najiona kuwa na heri kusimama mbele yako leo ninapojitetea kuhusu mashtaka yote ya Wayahudi,
3 Surtout, vous connaissant toutes choses, et les coutumes et les questions qui existent parmi les Juifs. C’est pourquoi je vous supplie de m’écouter avec patience.
hasa kwa sababu unajua vyema desturi zote za Kiyahudi na ya kuwa wewe unajua kwa undani mila na masuala ya mabishano. Kwa hiyo, nakusihi unisikilize kwa uvumilivu.
4 Et d’abord ma vie qui, depuis le commencement, s’est passée au milieu de ma nation à Jérusalem, tous les Juifs la connaissent,
“Wayahudi wote wanajua jinsi nilivyoishi tangu nilipokuwa mtoto, kuanzia mwanzo wa maisha yangu katika nchi yangu na pia huko Yerusalemu.
5 Sachant d’avance (s’ils veulent rendre témoignage), que, dès le commencement, j’ai vécu pharisien, selon la secte la mieux fondée de notre religion.
Wao wamefahamu kwa muda mrefu na wanaweza kushuhudia kama wakipenda, ya kwamba kutokana na misimamo mikali sana ya dhehebu letu kwenye dini yetu, niliishi nikiwa Farisayo.
6 Et cependant me voici soumis à un jugement au sujet de l’espérance en la promesse qui a été faite par Dieu à nos pères,
Nami sasa ni kwa sababu ya tumaini langu katika kile ambacho Mungu aliwaahidi baba zetu, ninashtakiwa leo.
7 Et dont nos douze tribus, servant Dieu nuit et jour, espèrent entrer en possession. Ainsi, c’est au sujet de cette espérance, ô roi, que je suis accusé par les Juifs.
Hii ndiyo ahadi ambayo makabila yetu kumi na mawili yanatarajia kuiona ikitimizwa wanapomtumikia Mungu kwa bidii usiku na mchana. Ee mfalme, ninashtakiwa na Wayahudi kwa ajili ya tumaini hili.
8 Juge-t-on incroyable parmi vous que Dieu ressuscite les morts?
Kwa nini yeyote miongoni mwenu afikiri kwamba ni jambo lisilosadikika Mungu kufufua wafu?
9 Pour moi, j’avais pensé que je devais par mille moyens agir contre le nom de Jésus de Nazareth;
“Mimi pia nilikuwa nimeshawishika kwamba imenipasa kufanya yote yale yaliyowezekana kupinga Jina la Yesu wa Nazareti.
10 Et c’est ce que j’ai fait à Jérusalem; j’ai jeté en prison un grand nombre de saints, en ayant reçu le pouvoir des princes des prêtres; et, lorsqu’on les faisait mourir, j’ai donné mon suffrage.
Nami hayo ndiyo niliyoyafanya huko Yerusalemu. Kwa mamlaka ya viongozi wa makuhani, niliwatia wengi wa watakatifu gerezani na walipokuwa wakiuawa, nilipiga kura yangu kuunga mkono.
11 Et parcourant souvent toutes les synagogues pour les tourmenter, je les forçais de blasphémer; et, de plus en plus furieux contre eux, je les poursuivais jusque dans les villes étrangères.
Mara nyingi nilikwenda kutoka sinagogi moja hadi ingine nikiamuru waadhibiwe, nami nilijaribu kuwalazimisha wakufuru. Katika shauku yangu dhidi yao, hata nilikwenda miji ya kigeni ili kuwatesa.
12 Comme j’allais dans ces dispositions à Damas, avec pouvoir et permission des princes des prêtres,
“Siku moja nilipokuwa katika mojawapo ya safari hizi nikiwa ninakwenda Dameski, nilikuwa na mamlaka na agizo kutoka kwa kiongozi wa makuhani.
13 Je vis, ô roi, au milieu du jour, dans le chemin, qu’une lumière du ciel, surpassant l’éclat du soleil, brillait autour de moi et de ceux qui étaient avec moi.
Ilikuwa yapata adhuhuri, ee mfalme, nilipokuwa njiani, niliona nuru kutoka mbinguni kali kuliko jua, ikingʼaa kunizunguka pande zote mimi na wale niliokuwa pamoja nao.
14 Et, étant tous tombés par terre, j’entendis une voix qui me disait en langue hébraïque: Saul, Saul, pourquoi me persécutes-tu? Il t’est dur de regimber contre l’aiguillon.
Wote tulipokuwa tumeanguka chini, nikasikia sauti ikisema nami kwa lugha ya Kiebrania, ‘Sauli, Sauli, mbona unanitesa? Ni vigumu kwako kuupiga teke mchokoo.’
15 Et moi, je demandai: Qui êtes-vous, Seigneur? Et le Seigneur répondit: Je suis Jésus que tu persécutes.
“Nikauliza, ‘Ni nani wewe, Bwana?’ “Naye Bwana akajibu, ‘Ni Mimi Yesu unayemtesa.
16 Mais lève-toi et tiens-toi sur tes pieds; car je ne t’ai apparu que pour t’établir ministre et témoin des choses que tu as vues, et de celles pour lesquelles je t’apparaîtrai encore,
Sasa inuka usimame kwa miguu yako. Nimekutokea ili nikuteue uwe mtumishi na shahidi wa mambo ambayo umeyaona, na yale nitakayokuonyesha.
17 Te délivrant des mains du peuple et de celles des gentils vers lesquels je t’envoie maintenant,
Nitakuokoa kutoka kwa watu wako na watu wa Mataifa ambao ninakutuma kwao,
18 Pour ouvrir leurs yeux, afin qu’ils se convertissent des ténèbres à la lumière, et de la puissance de Satan à Dieu, et qu’ils reçoivent la rémission des péchés, et une part entre les saints, par la foi en moi.
uyafumbue macho yao ili wageuke kutoka gizani waingie nuruni, na kutoka kwenye nguvu za Shetani wamgeukie Mungu, ili wapate msamaha wa dhambi na sehemu miongoni mwa wale waliotakaswa kwa kuniamini mimi.’
19 Ainsi, roi Agrippa, je ne fus pas incrédule à la vision céleste;
“Hivyo basi, Mfalme Agripa, sikuacha kuyatii yale maono yaliyotoka mbinguni,
20 Mais à ceux de Damas, d’abord, puis à Jérusalem, dans tout le pays de Judée, et aux gentils, j’annonçais qu’ils fissent pénitence, et qu’ils se convertissent à Dieu, faisant de dignes œuvres de pénitence.
bali niliyatangaza kwanza kwa wale wa Dameski, kisha Yerusalemu na katika vijiji vyote vya Uyahudi na pia kwa watu wa Mataifa, kwamba inawapasa kutubu na kumgeukia Mungu na kuthibitisha toba yao kwa matendo yao.
21 Voilà pourquoi les Juifs; s’étant saisis de moi lorsque j’étais dans le temple, cherchaient à me tuer.
Ni kwa sababu hii Wayahudi walinikamata nilipokuwa Hekaluni, wakataka kuniua.
22 Mais, assisté du secours de Dieu, jusqu’à ce jour je suis demeuré ferme, rendant témoignage aux petits et aux grands, ne disant rien que ce que les prophètes et Moïse ont prédit devoir arriver:
Hadi leo nimepata msaada kutoka kwa Mungu, na hivyo nasimama hapa nikishuhudia kwa wakubwa na wadogo. Sisemi chochote zaidi ya yale ambayo manabii na Mose walisema yatatukia:
23 Que le Christ souffrirait, qu’il serait le premier dans la résurrection des morts, et qu’il devait annoncer la lumière à ce peuple et aux gentils.
kwamba Kristo atateswa, na kwamba yeye atakuwa wa kwanza kufufuka kutoka kwa wafu, na atatangaza nuru kwa watu wake na kwa watu wa Mataifa.”
24 Comme il parlait ainsi, exposant sa défense, Festus, d’une voix forte, dit: Tu es fou, Paul; ton grand savoir te fait perdre le sens.
Paulo alipokuwa akifanya utetezi huu, Festo akasema kwa sauti kubwa, “Paulo, wewe umerukwa na akili! Kusoma kwingi kunakufanya uwe kichaa!”
25 Et Paul: Je ne suis point fou (dit-il), ô excellent Festus; mais je dis des paroles de sagesse et de vérité.
Lakini Paulo akajibu, “Mimi sijarukwa na akili, mtukufu sana Festo, bali nanena kweli nikiwa na akili zangu timamu.
26 Et il sait bien ces choses, le roi devant qui je parle avec tant d’assurance; car je pense qu’il n’ignore rien de cela, aucune de ces choses ne s’étant passée dans un coin.
Naam, Mfalme anajua kuhusu mambo haya yote, nami nasema naye kwa uhuru. Kwa sababu nina hakika kwamba hakuna hata mojawapo ya mambo haya asilolijua, kwa kuwa hayakufanyika mafichoni.
27 Croyez-vous aux prophètes, roi Agrippa? Je sais que vous y croyez.
Mfalme Agripa, je, unaamini manabii? Najua kuwa unaamini.”
28 Et Agrippa à Paul: Peu s’en faut que tu ne me persuades d’être chrétien.
Agripa akamwambia Paulo, “Je, unanishawishi kwa haraka namna hii niwe Mkristo?”
29 Mais Paul: Plaise à Dieu qu’il ne s’en faille ni peu ni beaucoup; que non seulement vous, mais encore tous ceux qui m’écoutent, deveniez aujourd’hui tels que je suis moi-même, à l’exception de ces liens.
Paulo akasema, “Ikiwa ni kwa haraka au la, namwomba Mungu, si wewe peke yako bali pia wale wote wanaonisikiliza leo, wawe kama mimi nilivyo, kasoro minyororo hii.”
30 Alors le roi, le gouverneur, Bérénice, et tous ceux qui étaient assis avec eux se levèrent.
Baada ya kusema hayo, mfalme akainuka pamoja na mtawala na Bernike na wale waliokuwa wameketi pamoja nao.
31 Et s’étant retirés à part, ils se parlaient l’un à l’autre, disant: Cet homme n’a rien fait qui mérite la mort ou les liens.
Walipokuwa wakiondoka, wakaambiana, “Mtu huyu hafanyi jambo lolote linalostahili kufa au kufungwa.”
32 Aussi Agrippa dit à Festus: Cet homme pourrait être renvoyé, s’il n’en avait appelé à César.
Agripa akamwambia Festo, “Mtu huyu angeachwa huru kama hangekuwa amekata rufaa kwa Kaisari.”

< Actes 26 >