< Actes 24 >

1 Cinq jours après, le prince des prêtres, Ananie, descendit avec quelques anciens, et un certain Tertullus, orateur: lesquels comparurent contre Paul devant le gouverneur.
Baada ya siku tano, kuhani mkuu Anania akashuka akiwa amefuatana na baadhi ya wazee pamoja na mwanasheria mmoja aitwaye Tertulo, nao wakaleta mashtaka yao dhidi ya Paulo mbele ya mtawala.
2 Or Paul ayant été appelé, Tertullus commença de l’accuser, disant: Jouissant par vous d’une profonde paix, et beaucoup de choses étant redressées par votre prévoyance,
Paulo alipoitwa aingie ndani, Tertulo akaanza kutoa mashtaka akisema, “Mtukufu Feliksi, kwa muda mrefu tumefurahia amani na matengenezo mengi mazuri yamefanywa kwa ajili ya watu hawa kwa sababu ya upeo wako wa kuona mambo ya mbele.
3 Toujours et partout, excellent Félix, nous le reconnaissons, avec toute sorte d’actions de grâces.
Wakati wote na kila mahali, kwa namna yoyote, mtukufu sana Feliksi, tumeyapokea mambo haya yote kwa shukrani nyingi.
4 Mais pour ne point vous retenir plus longtemps, je vous prie de nous écouter un moment avec toute votre bonté.
Lakini nisije nikakuchosha zaidi, ningekuomba kwa hisani yako utusikilize kwa kifupi.
5 Nous avons trouvé que cet homme, vraie peste, excite le trouble parmi les Juifs répandus dans le monde entier, et qu’il est chef de la secte séditieuse des Nazaréens;
“Tumemwona mtu huyu kuwa ni msumbufu, anayechochea ghasia miongoni mwa Wayahudi duniani pote. Yeye ndiye kiongozi wa dhehebu la Wanazarayo,
6 Il a même tenté de profaner le temple; et l’ayant saisi, nous avons voulu le juger suivant notre loi.
na hata amejaribu kulinajisi Hekalu, hivyo tukamkamata; [tukataka kumhukumu kufuatana na sheria zetu.
7 Mais le tribun Lysias survenant, l’a arraché avec une grande violence de nos mains,
Lakini jemadari Lisia alitujia na nguvu nyingi, akamwondoa mikononi mwetu,
8 Ordonnant que ses accusateurs vinssent vers vous; c’est par lui que vous pourrez vous-même, l’interrogeant, vous assurer des choses dont nous l’accusons.
akiwaamuru washtaki wake waje mbele yako: ili] kwa kumchunguza wewe mwenyewe unaweza kujua kutoka kwake mambo yote tunayomshtaki kwayo.”
9 Et les Juifs ajoutèrent que cela était ainsi.
Pia wale Wayahudi wakaunga mkono wakithibitisha kuwa mashtaka yote haya ni kweli.
10 Mais Paul (le gouverneur lui ayant fait signe de parler) répondit: Sachant que depuis plusieurs années, vous êtes établi juge sur ce peuple, je me défendrai avec confiance.
Mtawala Feliksi alipompungia Paulo mkono ili ajitetee, yeye akajibu, “Najua kwamba wewe umekuwa hakimu katika taifa hili kwa miaka mingi, hivyo natoa utetezi wangu kwa furaha.
11 Car vous pouvez savoir qu’il n’y a pas plus de douze jours que je suis monté pour adorer à Jérusalem;
Unaweza kuhakikisha kwa urahisi kuwa hazijapita zaidi ya siku kumi na mbili tangu nilipopanda kwenda Yerusalemu kuabudu.
12 Et ils ne m’ont trouvé disputant avec quelqu’un ou ameutant la foule, ni dans le temple, ni dans la synagogue,
Hawa wanaonishtaki hawakunikuta nikibishana na mtu yeyote Hekaluni au kuchochea umati wa watu katika sinagogi au mahali pengine popote mjini.
13 Ni dans la ville; et ils ne sauraient vous prouver ce dont ils m’accusent maintenant.
Wala hawawezi kabisa kukuthibitishia mashtaka haya wanayonishtaki kwayo.
14 Mais ce que je confesse devant vous, c’est que, suivant la secte qu’ils appellent hérésie, je sers mon Père et mon Dieu, croyant à tout ce qui est écrit dans la loi et dans les prophètes;
Lakini, ninakubali kwamba mimi namwabudu Mungu wa baba zetu, mfuasi wa Njia, ile ambayo wao wanaiita dhehebu. Ninaamini kila kitu kinachokubaliana na Sheria na kile kilichoandikwa katika Manabii,
15 Ayant en Dieu l’espérance qu’il y aura une résurrection, qu’eux aussi attendent, de justes et de méchants.
nami ninalo tumaini kwa Mungu, ambalo hata wao wenyewe wanalikubali kwamba kutakuwa na ufufuo wa wafu, kwa wenye haki na wasio na haki.
16 C’est pourquoi je m’efforce d’avoir toujours ma conscience sans reproche devant Dieu et devant les hommes.
Kwa hiyo ninajitahidi siku zote kuwa na dhamiri safi mbele za Mungu na mbele za wanadamu.
17 Mais après plusieurs années, je suis venu pour faire des aumônes à ma nation, et à Dieu des offrandes et des vœux.
“Basi, baada ya kutokuwepo kwa miaka mingi nilikuja Yerusalemu ili kuwaletea watu wangu msaada kwa ajili ya maskini na kutoa dhabihu.
18 C’est dans ces exercices qu’ils m’ont trouvé dans le temple, sans concours ni tumulte.
Nilikuwa nimeshatakaswa kwa taratibu za kiibada waliponikuta Hekaluni nikifanya mambo haya. Hapakuwa na umati wa watu, pamoja nami wala aliyehusika kwenye fujo yoyote.
19 Et ce sont certains Juifs d’Asie, lesquels auraient dû se présenter devant vous et m’accuser, s’ils avaient quelque chose contre moi;
Lakini kulikuwa na baadhi ya Wayahudi kutoka Asia, ambao wangelazimika wawepo hapa mbele yako ili watoe mashtaka kama wanalo jambo lolote dhidi yangu.
20 Ou bien que ceux-ci disent s’ils ont trouvé en moi quelque iniquité, quand j’ai comparu devant le conseil;
Au, watu hawa walioko hapa waseme ni uhalifu gani walioniona nao waliponisimamisha mbele ya baraza,
21 Si ce n’est à l’égard de cette seule parole que j’ai prononcée hautement étant au milieu d’eux: C’est à cause de la résurrection des morts, que suis aujourd’hui jugé par vous.
isipokuwa ni kuhusu jambo hili moja nililopiga kelele mbele yao kwamba, ‘Mimi nashtakiwa mbele yenu leo kwa sababu ya ufufuo wa wafu.’”
22 Mais Félix qui connaissait très bien cette voie, les remit, disant: Quand le tribun Lysias sera venu, je vous écouterai.
Basi Feliksi ambaye alikuwa anafahamu vizuri habari za Njia ile, akaahirisha shauri lile kwa maelezo yake akisema, “Wakati jemadari Lisia atakapoteremka huku, nitaamua shauri lako.”
23 Et il commanda au centurion de garder Paul, mais de lui laisser du repos, et de n’empêcher aucun des siens de le servir.
Ndipo akaamuru kiongozi wa askari amweke chini ya ulinzi lakini ampe uhuru na kuwaruhusu rafiki zake wamhudumie.
24 Or quelques jours après, Félix venant avec Drusille, sa femme, qui était Juive, appela Paul, et l’entendit sur ce qui touche la foi dans le Christ-Jésus.
Baada ya siku kadhaa, Feliksi alikuja pamoja na Drusila mkewe, ambaye alikuwa Myahudi. Alituma aitiwe Paulo, naye akamsikiliza alipokuwa akinena juu ya imani katika Kristo Yesu.
25 Mais Paul discourant sur la justice, la chasteté, et le jugement futur, Félix effrayé, répondit: Quant à présent, retire-toi; je te manderai en temps opportun;
Naye Paulo alipokuwa akinena juu ya haki, kuwa na kiasi na juu ya hukumu ijayo, Feliksi aliingiwa na hofu na kusema, “Hiyo yatosha sasa! Waweza kuondoka. Nitakapokuwa na wasaa nitakuita.”
26 Il espérait en même temps que Paul lui donnerait de l’argent; c’est pourquoi, le faisant souvent venir, il s’entretenait avec lui.
Wakati huo Feliksi alitazamia kwamba Paulo angempa rushwa. Hivyo akawa anamwita mara kwa mara na kuzungumza naye.
27 Deux années s’étant écoulées, Félix eut pour successeur Portius Festus. Or Félix, voulant faire plaisir aux Juifs, laissa Paul en prison.
Baada ya miaka miwili kupita, Porkio Festo akaingia kwenye utawala mahali pa Feliksi, lakini kwa kuwa Feliksi alitaka kuwapendeza Wayahudi, akamwacha Paulo gerezani.

< Actes 24 >