< Actes 21 >
1 Or il arriva qu’ayant fait voile, après nous être arrachés d’eux, nous vînmes droit à Cos, et le jour suivant à Rhodes, et de là à Patare.
Wakati tulipokua tumeachana nao, na tunasafiri baharini, tukafika moja kwa moja kwenye mji wa Kosi, na kesho yake tukafika mji wa Rodo, na kutoka huko tukafika mji wa Patara.
2 Et ayant rencontré un vaisseau qui allait en Phénicie, nous y montâmes, et mîmes à la voile.
Tulipopata meli inayovuka kwenda Foinike, tulipanda tukasafiri.
3 Quand nous fûmes en vue de Chypre, la laissant à gauche, nous naviguâmes vers la Syrie et vînmes à Tyr, car c’est là que le vaisseau devait déposer sa charge.
Tulipofika mbele ya kisiwa cha Kipro, tukaiacha upande wa kushoto, tukasafiri hadi Siria, tukaweka nanga katika mji wa Tiro, kwa sababu huko ndiko meli ilikuwa ipakuliwe shehena yake.
4 Or, y ayant trouvé les disciples, nous y demeurâmes sept jours; et les disciples disaient par l’Esprit-Saint à Paul, de ne point monter à Jérusalem.
Baada ya kuwaona wanafunzi, tukakaa huko siku saba. Wanafunzi hawa wakamwambia Paulo kupitia kwa Roho kwamba yeye asikanyage Yerusalemu.
5 Et ces jours écoulés, nous partîmes, et ils vinrent tous, avec leurs femmes et leurs enfants, nous conduire jusque hors de la ville; et nous étant agenouillés sur le rivage, nous priâmes.
Hata tulipotimiza siku zile, sisi tukaondoka tukaenda zetu. Wote pamoja, na wanawake zao na watoto wao, walitusindikiza katika njia zetu hadi tulipotoka nje ya mji. Kisha tukapiga magoti pwani, tukaomba, tukaagana kila mmoja.
6 Et après nous être dit adieu les uns aux autres, nous montâmes sur le vaisseau, et ils s’en retournèrent chez eux.
Tukapanda meli, huku nao wakarudi nyumbani kwao tena.
7 Pour nous, terminant notre navigation de Tyr, nous descendîmes à Ptolémaïde, et, les frères salués, nous demeurâmes un jour avec eux.
Hata tulipomaliza safari yetu kutoka Tiro, tukafika Tolemai. Pale tulisalimia ndugu, na kukakaa nao kwa siku moja.
8 Le lendemain, étant partis, nous vînmes à Césarée; et, entrant dans la maison de Philippe, l’évangéliste, qui était un des sept, nous demeurâmes chez lui.
Kesho yake tuliondoka tukaenda Kaisaria. Sisi tukaingia nyumbani mwa Filipo, mhubiri wa injili, aliyekuwa mmoja wa wale saba, nasi tukakaa pamoja naye.
9 Il avait quatre filles vierges qui prophétisaient.
Mtu huyu alikuwa na mabinti wanne mabikira ambao walitabiri.
10 Et comme nous y demeurâmes quelques jours, il arriva de Judée un prophète nommé Agabus.
Baada ya kukaa huko kwa siku kadhaa, akashuka kutoka Uyahudi nabii mmoja aitwaye Agabo.
11 Or, étant venu nous voir, il prit la ceinture de Paul, et, se liant les pieds et les mains, il dit: Voici ce que dit l’Esprit-Saint: L’homme à qui est cette ceinture, les Juifs le lieront ainsi à Jérusalem, et ils le livreront entre les mains des gentils.
Yeye alikuja kwetu na akautwaa mkanda wa Paulo. kwa huo alijifunga miguu na mikono yake mwenyewe na kusema, “Roho Mtakatifu asema hivi,” “Wayahudi wa Yerusalemu watamfunga mtu anayemiliki mkanda huu, nao watamkabidhi mikononi mwa watu wa mataifa.”
12 Ce qu’ayant entendu, nous conjurions Paul, nous et ceux qui étaient en cet endroit, de ne point monter à Jérusalem.
Tuliposikia mambo hayo, sisi na watu waliokuwa wakiishi mahali pale tulimsihi Paulo asipande kwende Yerusalemu.
13 Alors Paul répondit et dit: Que faites-vous, pleurant et affligeant mon cœur? Car moi, je suis prêt, non seulement à être lié, mais à mourir à Jérusalem pour le nom du Seigneur Jésus.
Ndipo Paulo alijibu, “Mnafanya nini, mnalia na kunivunja moyo wangu? Kwa maana niko tayari, siyo tu kufungwa, lakini pia kufia huko Yerusalemu kwa ajili ya jina la Bwana Yesu.”
14 Mais ne pouvant le persuader, nous nous tînmes en repos, disant: Que la volonté du Seigneur soit faite.
Kwa vile Paulo hakutaka kushawishiwa, tuliacha na kusema, “Basi mapenzi ya Bwana yafanyike.”
15 Après ces jours, ayant fait nos préparatifs, nous partîmes pour Jérusalem.
Baada ya siku hizi, tulichukua mifuko yetu na tukapanda Yerusalemu.
16 Or avec nous vinrent aussi quelques disciples de Césarée, amenant avec eux un certain Mnason, de Chypre, ancien disciple, chez qui nous devions loger.
Baadhi ya wanafunzi kutoka Kaisaria pia walifuatana nasi. Wakamleta mtu mmoja aitwaye Mnasoni, mtu wa Kipro, mwanafunzi wa zamani, ambaye tulikaa naye.
17 Quand nous fûmes arrivés à Jérusalem, les frères nous reçurent avec joie.
Tulipofika Yerusalemu, ndugu walitukaribisha kwa furaha.
18 Le jour suivant, Paul entrait avec nous chez Jacques, et tous les anciens s’assemblèrent.
Kesho yake Paulo alienda pamoja nasi kwa Yakobo, na wazee wote walikuwepo.
19 Après les avoir salués, il racontait en détail ce que Dieu avait fait pour les gentils par son ministère.
Baada ya kuwasalimu, aliwapa taarifa moja baada ya nyingine ya mambo ambayo Mungu aliyotenda miongoni mwa mataifa kwa kupitia huduma yake.
20 Or eux, l’ayant entendu, glorifiaient Dieu; et ils lui dirent: Tu vois, mon frère, combien de milliers de Juifs ont cru; cependant tous sont zélés pour la loi.
Wakati waliposikia hayo, wakamsifu Mungu, na wakamwambia, “Unaona, ndugu, kuna maelfu wangapi wameamini miongoni mwa Wayahudi. Wao wote wana nia ya kushika sheria.
21 Or ils ont ouï dire de toi que tu enseignes aux Juifs qui sont parmi les gentils, d’abandonner Moïse, disant qu’ils ne doivent point circoncire leurs fils, ni marcher selon les coutumes.
Wameambiwa kuhusu wewe, kwamba unafundisha Wayahudi wanaoishi kati ya mataifa kuachana na Musa, na kwamba unawaambia wasiwatahiri watoto wao, na wasifuate desturi za zamani.
22 Que faire donc? Certainement la multitude devra s’assembler, car ils apprendront que tu es arrivé.
Tunapaswa tufanye nini? Bila shaka watasikia kwamba wewe umekuja.
23 Fais donc ce que nous te disons: Nous avons ici quatre hommes qui sont liés par un vœu.
Hivyo fanya kile sisi tunachokuambia sasa: tunao watu wanne ambao wameweka nadhiri.
24 Prends-les avec toi, purifie-toi avec eux, et paie pour eux, afin qu’ils se rasent la tête, et tous sauront que ce qu’ils ont entendu dire de toi est faux; mais que toi aussi tu marches observant la loi.
Wachukue watu hawa na ujitakase mwenyewe pamoja nao, na uwalipie gharama zao, ili waweze kunyoa vichwa vyao. Hivyo kila mmoja apate kujua kwamba mambo waliyoambiwa kuhusu wewe ni ya uongo. Watajifunza kwamba wewe pia unafuata sheria.
25 Quant à ceux qui ont cru d’entre les gentils, nous avons écrit qu’ils devaient s’abstenir de ce qui a été immolé aux idoles, du sang, des animaux étouffés et de la fornication.
Lakini kwa habari za mataifa ambao wamekuwa waumini, tuliandika na kutoa maagizo kwamba wanapaswa kujiepusha na vitu vilivyotolewa dhabihu kwa sanamu, na damu, kutokana na kile kilichonyongwa, na wajiepushe na uasherati.”
26 Alors Paul ayant pris ces hommes, et s’étant le lendemain purifié avec eux, entra dans le temple, indiquant les jours où s’accomplirait la purification, et quand l’offrande serait présentée pour chacun d’eux.
Ndipo, Paulo aliwatwaa wanaume, na siku ya pili, akajitakasa mwenyewe pamoja nao, akaingia Hekaluni, kutangaza kipindi cha siku za kujitakasa, hadi sadaka itolewa kwa ajili ya kila mmoja wao.
27 Mais comme les sept jours s’écoulaient, les Juifs d’Asie l’ayant vu dans le temple, émurent tout le peuple, et mirent la main sur lui, criant:
Siku hizo saba zilipokaribia kumalizika, baadhi ya Wayahudi kutoka Asia wakamuona Paulo Hekaluni, na makutano wakakasirika, na wakamnyoshea mikono.
28 Hommes d’Israël, au secours! Voici l’homme qui enseigne partout contre le peuple, contre la loi, et contre ce lieu; et qui, de plus, a introduit des gentils dans le temple, et a ainsi violé le saint lieu.
Walikuwa wanapiga kelele, “Watu wa Israeli, tusaidieni. Huyu ni yule mtu anayewafundisha watu kila mahali mambo ambayo ni kinyume na watu, sheria, na mahali hapa. Pia amewaleta Wayunani katika Hekalu na kupanajisi mahali hapa patakatifu.”
29 Ils avaient vu, en effet, Trophime, d’Ephèse, dans la ville avec Paul, et ils pensèrent que Paul l’avait introduit dans le temple.
Kwa kuwa mwanzoni walikuwa wamemwona Trofimo Muefeso akiwa pamoja naye mjini, nao walidhani kwamba Paulo alimleta hekaluni.
30 Aussitôt toute la ville s’émut, et il se fit un grand concours de peuple. S’étant donc saisis de Paul, ils l’entraînèrent hors du temple; et aussitôt les portes furent fermées.
Mji wote ulikuwa na taharuki, na watu wakakimbia pamoja na kumkamata Paulo. Wakamtoa nje ya Hekalu, na milango mara ikafungwa.
31 Comme ils cherchaient à la tuer, on vint dire au tribun de la cohorte: Tout Jérusalem est en confusion.
Walipokuwa wakijaribu kumuua, habari zilimfikia mkuu wa jeshi la walinzi kuwa Yerusalemu yote ilikuwa imejaa ghasia.
32 Celui-ci ayant pris, sur le champ, des soldats et des centurions, courut à eux. Dès qu’ils virent le tribun et les soldats, ils cessèrent de frapper Paul.
Mara hiyo akawachukua askari na jemadari akaukimbilia umati. Wakati Watu walipomwona mkuu wa jeshi na askari, wakaacha kumpiga Paulo.
33 Alors s’approchant, le tribun le prit, et le fit lier de deux chaînes; et il demandait qui il était, et ce qu’il avait fait.
Kisha mkuu wa jeshi alimkaribia na akamshika Paulo, na akaamuru afungwe minyororo miwili. Akamuuliza yeye ni nani na amefanya nini.
34 Mais, dans la foule, l’un criait une chose, l’autre une autre. Ne pouvant rien savoir de certain à cause du tumulte, il le fit conduire au camp.
Baadhi ya watu kwenye umati walikuwa wanapayuka kitu hiki na wengine kingine. Kwa kuwa jemadari hakuweza kuwaambia chochote kwa sababu ya zile kelele, akaamuru Paulo aletwe ndani ya ngome.
35 Lorsque Paul fut arrivé sur les degrés, les soldats le portèrent, à cause de la violence du peuple.
Basi alipofika kwenye ngazi, akachukuliwa na askari kwa sababu ya ghasia za umati.
36 Car une multitude de peuple le suivait, criant: Ôte-le du monde.
Maana umati wa watu walimfuata na waliendelea kupiga kelele, “Mwondoeni huyu!”
37 Comme il allait entrer dans le camp, Paul demanda au tribun: M’est-il permis de vous dire quelque chose? Le tribun lui répondit: Sais-tu le grec?
Paulo alipokuwa analetwa ndani ya ngome, alimwambia mkuu wa jeshi, “Naweza kukwambia kitu?” Yule mkuu wa jeshi akasema, “Je unaongea Kiyunani?
38 N’es-tu pas cet Egyptien qui a excité, il y a quelques jours, une sédition, et qui a conduit au désert quatre mille sicaires?
Je, wewe si yule Mmisri ambaye awali aliongoza uasi na alichukua magaidi elfu nne nyikani?”
39 Et Paul lui répondit: Je vous assure que je suis Juif, de Tarse en Cilicie, et citoyen de cette ville qui n’est pas inconnue. Permettez-moi, je vous prie, de parler au peuple.
Paulo akasema, “Mimi ni Myahudi, kutoka mji wa Tarso ya Kilikia. Mimi ni raia wa mji maarufu. Nawaomba, mniruhusu nizungumze na watu.”
40 Le tribun l’ayant permis, Paul se tenant debout sur les degrés, fit signe de la main au peuple, et en grand silence s’étant fait, il leur parla en langue hébraïque, disant:
Wakati jemadari alipompa ruhusa, Paulo akasimama penye ngazi na akatoa ishara kwa watu kwa mkono wake. Wakati kulipokuwa na ukimya sana, akaongea nao kwa Kihebrania. Akasema,