< Actes 19 >
1 Or il arriva pendant qu’Apollo était à Corinthe, que Paul, ayant parcouru les provinces supérieures, vint à Ephèse et y trouva quelques disciples,
Wakati Apolo alipokuwa Korintho, Paulo alisafiri sehemu za bara, akafika Efeso ambako aliwakuta wanafunzi kadhaa.
2 Et il leur demanda: Avez-vous reçu l’Esprit-Saint depuis que vous croyez? Ils lui répondirent: S’il y a un Esprit-Saint, nous ne l’avons pas même ouï dire.
Akauliza, “Je, mlipopata kuwa waumini mlipokea Roho Mtakatifu?” Nao wakamjibu, “La! Hata kusikia kwamba kuna Roho Mtakatifu hatujasikia.”
3 Et lui leur repartit: De quel baptême avez-vous donc été baptisés? Ils répondirent; Du baptême de Jean.
Naye akasema, “Sasa mlipata ubatizo wa namna gani?” Wakamjibu, “Ubatizo wa Yohane.”
4 Alors Paul répliqua: Jean a baptisé le peuple du baptême de pénitence, leur disant de croire en celui qui devait venir après lui, c’est-à-dire en Jésus-Christ.
Naye Paulo akasema, “Ubatizo wa Yohane ulikuwa wa kuonyesha kwamba watu wametubu. Yohane aliwaambia watu wamwamini yule ambaye alikuwa anakuja baada yake, yaani Yesu.”
5 Ces paroles entendues, ils furent baptisés au nom du Seigneur Jésus.
Baada ya kusikia hayo, walibatizwa kwa jina la Bwana Yesu.
6 Et après que Paul leur eut imposé les mains, l’Esprit-Saint descendit sur eux, et ils parlaient diverses langues, et prophétisaient.
Basi, Paulo akawawekea mikono, na Roho Mtakatifu akawashukia, wakaanza kusema lugha mbalimbali na kutangaza ujumbe wa Mungu.
7 Ils étaient en tout environ douze.
Wote jumla, walikuwa watu wapatao kumi na wawili.
8 Alors étant entrés dans la synagogue, il y parla avec assurance pendant trois mois, disputant et les persuadant du royaume de Dieu.
Kwa muda wa miezi mitatu Paulo alikuwa akienda katika sunagogi, akawa na majadiliano ya kuvutia sana juu ya Ufalme wa Mungu.
9 Et, comme quelques-uns s’endurcissaient et ne croyaient point, maudissant la voie du Seigneur devant la multitude, il s’éloigna d’eux, et en sépara ses disciples; il disputait tous les jours dans l’école d’un certain Tyran.
Lakini wengine walikuwa wakaidi, wakakataa kuamini, wakaanza kuongea vibaya hadharani juu ya Njia ya Bwana. Hapo Paulo alivunja uhusiano nao, akawachukua pembeni wale wanafunzi wake, akawa anazungumza nao kila siku katika jumba la masomo la Turano.
10 Or c’est ce qui se fit pendant deux ans; de sorte que tous ceux qui demeuraient en Asie, Juifs et gentils, entendirent la parole du Seigneur.
Aliendelea kufanya hivyo kwa muda wa miaka miwili hata wakazi wote wa Asia, Wayahudi na watu wa mataifa mengine, wakaweza kusikia neno la Bwana.
11 Et Dieu faisait, par la main de Paul, des miracles extraordinaires;
Mungu alifanya miujiza ya ajabu kwa mikono ya Paulo.
12 Au point même que l’on mettait sur les malades des mouchoirs et des tabliers qui avaient touché son corps, et ils étaient guéris de leurs maladies, et les esprits mauvais sortaient.
Watu walikuwa wakichukua leso na nguo nyingine za kazi ambazo Paulo alikuwa amezitumia, wakazipeleka kwa wagonjwa, nao wakaponywa magonjwa yao; na wale waliokuwa na pepo wabaya wakatokwa na pepo hao.
13 Or quelques Juifs exorcistes, qui allaient de côté et d’autre, tentèrent d’invoquer le nom de Jésus sur ceux qui avaient en eux des esprits mauvais, disant: Je vous adjure par le Jésus que Paul prêche.
Wayahudi kadhaa wenye kupunga pepo wabaya, walisafiri huko na huko, wakijaribu kulitumia jina la Bwana Yesu kwa wale waliokuwa wamepagawa na pepo wabaya. Walikuwa wakisema: “Ninawaamuru kwa jina la Yesu ambaye Paulo anamhubiri.”
14 C’étaient sept fils de Scéva, Juif et prince des prêtres, qui faisaient cela.
Watoto saba wa Skewa, Kuhani Mkuu wa Kiyahudi, walikuwa miongoni mwa hao waliokuwa wanafanya hivyo.
15 Mais l’esprit mauvais, répondant, leur dit: Je connais Jésus, et je sais qui est Paul; mais vous, qui êtes-vous?
Lakini pepo mbaya aliwajibu, “Ninamfahamu Yesu, ninamjua pia Paulo, lakini ninyi ni nani?”
16 Et l’homme en qui était le plus mauvais démon s’élança sur eux, et, s’étant rendu maître de deux d’entre eux, il les maltraita de telle sorte, qu’ils s’enfuirent de cette maison, nus et blessés.
Kisha yule mtu aliyepagawa aliwarukia wote kwa kishindo, akawashinda nguvu. Na hao watoto wa Skewa wakakimbia kutoka ile nyumba wakiwa uchi na wamejaa majeraha.
17 Cela fut connu de tous les Juifs et gentils qui habitaient Ephèse; et la crainte s’empara d’eux tous, et le nom du Seigneur Jésus était glorifié.
Kila mtu huko Efeso, Myahudi na asiye Myahudi, alisikia juu ya tukio hilo. Wote waliingiwa na hofu, wakalitukuza jina la Bwana Yesu.
18 Beaucoup d’entre les croyants venaient, confessant, et déclarant ce qu’ils avaient fait.
Waumini wengi walijitokeza wakakiri hadharani mambo waliyokuwa wametenda.
19 Et beaucoup aussi de ceux qui avaient exercé les arts curieux, apportèrent leurs livres, et les brûlèrent en présence de tous; et le prix en ayant été supputé, on trouva la somme de cinquante mille deniers.
Wengine waliokuwa wameshughulikia mambo ya uchawi hapo awali, walikusanya vitabu vyao, wakavichoma mbele ya wote. Walikisia gharama ya vitabu hivyo, wakaona yafikia vipande vya fedha elfu hamsini.
20 Ainsi croissait et s’affermissait puissamment la parole de Dieu.
Kwa namna hiyo, neno la Bwana lilizidi kuenea na kuwa na nguvu zaidi.
21 Ces choses accomplies, Paul résolut, par un mouvement de l’Esprit-Saint, la Macédoine et l’Achaïe traversées, d’aller à Jérusalem, disant: Après que j’aurai été là, il faut que je voie Rome aussi.
Baada ya mambo hayo, Paulo aliamua kwenda Yerusalemu kwa kupitia Makedonia na Akaya. Alisema, “Baada ya kufika huko, itanilazimu kuona Roma pia.”
22 Et envoyant en Macédoine deux de ceux qui l’assistaient, Timothée et Eraste, il demeura lui-même quelque temps en Asie.
Hivyo, aliwatuma wawili wa wasaidizi wake, Timotheo na Erasto, wamtangulie kwenda Makedonia, naye akabaki kwa muda huko Asia.
23 Mais il survint en ce temps-là, un grand trouble au sujet de la voie du Seigneur.
Wakati huo ndipo kulipotokea ghasia kubwa huko Efeso kwa sababu ya hiyo Njia ya Bwana.
24 Car un certain orfèvre, du nom de Démétrius, qui, faisant en argent de petits temples de Diane, procurait un gain considérable aux ouvriers,
Kulikuwa na mfua fedha mmoja aitwaye Demetrio, ambaye alikuwa na kazi ya kutengeneza sanamu za nyumba ya mungu wa kike aitwaye Artemi. Shughuli hiyo iliwapatia mafundi faida kubwa.
25 Les ayant assemblés, avec d’autres qui faisaient de ces sortes d’ouvrages, il dit: Hommes, vous savez que c’est de cette industrie que vient notre gain;
Demetrio aliwakusanya hao wafanyakazi pamoja na wengine waliokuwa na kazi kama hiyo, akawaambia, “Wananchi, mnafahamu kwamba kipato chetu kinatokana na biashara hii.
26 Et vous voyez et entendez dire que ce Paul ayant persuadé non seulement Ephèse, mais presque toute l’Asie, il a détourné une grande multitude, disant: Ils ne sont pas dieux ceux qui sont faits par des mains.
Sasa, mnaweza kusikia na kujionea wenyewe mambo Paulo anayofanya, si tu hapa Efeso, ila pia kote katika Asia. Yeye amewashawishi na kuwageuza watu wakakubali kwamba miungu ile iliyotengenezwa na watu si miungu hata kidogo.
27 Or, non seulement nous courons risque que notre métier soit décrié, mais que le temple même de la grande Diane tombe dans le mépris, et que s’anéantisse insensiblement la majesté de celle que toute l’Asie et le monde entier révère.
Hivyo iko hatari kwamba biashara yetu itakuwa na jina baya. Si hivyo tu, bali pia jambo hilo linaweza kuifanya nyumba ya mungu Artemi kuwa si kitu cha maana. Hatimaye sifa zake huyo ambaye Asia na dunia yote inamwabudu, zitakwisha.”
28 Ce discours entendu, ils furent remplis de colère, et ils s’écrièrent, disant: Grande est la Diane des Ephésiens!
Waliposikia hayo, waliwaka hasira, wakaanza kupiga kelele: “Mkuu ni Artemi, wa Efeso!”
29 La ville fut aussitôt remplie de confusion, et ils firent irruption dans le théâtre, y entraînant Gaïus et Aristarque, macédoniens, compagnons de voyage de Paul.
Mji wote ukajaa ghasia. Wakawavamia Gayo na Aristarko, wenyeji wa Makedonia, ambao walikuwa wasafiri wenzake Paulo, wakakimbia nao mpaka kwenye ukumbi wa michezo.
30 Or Paul, voulant pénétrer au milieu du peuple, les disciples ne le permirent pas.
Paulo mwenyewe alitaka kuukabili huo umati wa watu, lakini wale waumini walimzuia.
31 Quelques-uns aussi des Asiarques, qui étaient ses amis, envoyèrent vers lui, le priant de ne pas se présenter au théâtre;
Maofisa wengine wa huo mkoa wa Asia, waliokuwa rafiki zake, walimtumia Paulo ujumbe wakimsihi asijihatarishe kwa kwenda kwenye ukumbi wa michezo.
32 Cependant les uns criaient une chose, les autres une autre. Car c’était une réunion confuse, et la plupart ne savaient pourquoi ils étaient assemblés.
Wakati huo, kila mtu alikuwa anapayuka; wengine hili na wengine lile, mpaka hata ule mkutano ukavurugika. Wengi hawakujua hata sababu ya kukutana kwao.
33 Cependant on dégagea Alexandre de la foule, à l’aide des Juifs qui le poussaient devant eux. Or Alexandre demanda de la main qu’on fît silence, voulant se défendre devant le peuple.
Kwa vile Wayahudi walimfanya Aleksanda ajitokeze mbele, baadhi ya watu katika ule umati walidhani kuwa ndiye. Basi, Aleksanda aliwaashiria watu kwa mkono akitaka kujitetea mbele ya ule umati wa watu.
34 Mais, dès qu’il eut été reconnu pour Juif, tous, d’une seule voix, crièrent pendant environ deux heures: Grande est la Diane des Ephésiens!
Lakini walipotambua kuwa yeye ni Myahudi, wote kwa sauti moja walipiga kelele: “Mkuu ni Artemi wa Efeso!” Wakaendelea kupayukapayuka hivyo kwa muda wa saa mbili.
35 Alors le scribe ayant apaisé la foule, dit: Ephésiens, quel est l’homme qui ignore que la ville d’Ephèse rend un culte à la grande Diane, fille de Jupiter?
Hatimaye karani wa mji alifaulu kuwanyamazisha, akawaambia, “Wananchi wa Efeso, kila mtu anajua kwamba mji huu wa Efeso ni mlinzi wa nyumba ya mungu Artemi na mlinzi wa ile sanamu iliyoanguka kutoka mbinguni.
36 Puisque donc on ne peut le contester, il faut que vous soyez calmes, et que vous ne fassiez rien témérairement.
Hakuna anayeweza kukana mambo haya. Hivyo basi, tulieni; msifanye chochote bila hadhari.
37 Car vous avez amené ces hommes, qui ne sont ni sacrilèges, ni blasphémateurs de votre déesse.
Mmewaita watu hawa hapa ingawaje hawakuikufuru nyumba ya mungu wala kumtukana mungu wetu wa kike.
38 Que si Démétrius et les ouvriers qui sont avec lui ont à se plaindre de quelqu’un, il y a des audiences publiques, il existe des proconsuls; qu’ils s’accusent les uns les autres.
Kama, basi Demetrio na wafanyakazi wake wana mashtaka yao kuhusu watu hawa, yapo mahakama na wakuu wa mikoa; wanaweza kushtakiana huko.
39 Mais si vous avez quelque autre affaire à proposer, elle pourra se terminer dans une assemblée régulière.
Kama mna matatizo mengine, yapelekeni katika kikao halali.
40 Car nous courons risque d’être accusés de sédition sur ce qui s’est passé aujourd’hui, n’y ayant personne qui donne un motif (que nous puissions justifier) de cet attroupement. Et lorsqu’il eut dit cela, il congédia l’assemblée.
Kwa maana tungaliweza kushtakiwa kwa kusababisha ghasia kutokana na vituko vya leo. Ghasia hii haina msingi halali na hatungeweza kutoa sababu za kuridhisha za ghasia hiyo.”
Baada ya kusema hayo aliuvunja mkutano.