< Actes 17 >

1 Après avoir passé par Amphipolis et Apollonie, ils vinrent à Thessalonique, à l’endroit où était la synagogue des Juifs.
Kwa kupitia Amfipoli na Apolonia, walisafiri mpaka Thesalonika ambako kulikuwa na sunagogi la Wayahudi.
2 Or, selon sa coutume, Paul y entra, et pendant trois sabbats, il les entretint des Ecritures,
Paulo alijiunga nao kama ilivyokuwa desturi yake akajadiliana nao Sabato tatu mfululizo, akatumia Maandiko Matakatifu.
3 Leur découvrant et leur faisant voir qu’il a fallu que le Christ souffrît, et qu’il ressuscitât des morts; et ce Christ, disait-il, est Jésus-Christ, que je vous annonce.
Aliyaeleza na kuonyesha kwamba ilimbidi Kristo kuteswa na kufufuka kutoka wafu. Akawaambia, “Yesu ambaye mimi namhubiri kwenu ndiye Kristo.”
4 Quelques-uns d’entre eux crurent, et se joignirent à Paul et à Silas, aussi bien qu’une grande multitude de prosélytes, de gentils, et beaucoup de femmes de qualité.
Baadhi yao walikubali wakajiunga na Paulo na Sila. Kadhalika, idadi kubwa ya Wagiriki waliomcha Mungu pamoja na wanawake wengi wa tabaka la juu, walijiunga nao.
5 Mais les Juifs, poussés par l’envie, prirent avec eux quelques hommes méchants de la lie du peuple, et, les attroupant, ils suscitèrent un mouvement dans la ville; puis, assiégeant la maison de Jason, ils cherchaient Paul et Silas, pour les mener devant le peuple.
Lakini Wayahudi wakaona wivu; wakawakodi wafidhuli sokoni, wakafanya kikundi na kuzusha fujo mjini kote. Wakaivamia nyumba ya Yasoni wakitumaini kuwapata humo Paulo na Sila ili wawalete hadharani.
6 Et ne les ayant point trouvés, ils traînèrent Jason et quelques-uns des frères devant les magistrats de la ville, criant: Voici ceux qui troublent la ville, et qui sont venus ici,
Lakini hawakuwapata na hivyo walimburuta Yasoni pamoja na ndugu wengine mpaka kwa wakuu wa mji, wakapiga kelele: “Watu hawa wamekuwa wakivuruga dunia yote na sasa wako hapa mjini.
7 Ceux que Jason a reçus; or tous sont rebelles aux décrets de César, disant qu’il y a un autre roi, Jésus.
Yasoni amewakaribisha nyumbani kwake. Wote wanafanya kinyume cha amri ya Kaisari wakisema eti Kuna mfalme mwingine aitwaye Yesu.”
8 C’est ainsi qu’ils émurent le peuple et les magistrats de la ville, qui entendirent ce discours.
Kwa maneno hayo waliwatia wasiwasi wakuu wa mji na kundi la watu.
9 Mais Jason et les autres ayant donné caution, ils les renvoyèrent.
Wakawafanya Yasoni na wenzake watoe dhamana, kisha wakawaacha waende zao.
10 Et aussitôt les frères firent partir de nuit pour Bérée, Paul et Silas. Lorsqu’ils y furent arrivés, ils entrèrent dans la synagogue des Juifs.
Usiku, wale ndugu waliwahimiza Paulo na Sila waende Berea. Mara tu walipofika huko, walikwenda katika sunagogi la Wayahudi.
11 Or ceux-ci avaient des sentiments plus nobles que ceux de Thessalonique; ils reçurent la parole avec la plus grande avidité, cherchant tous les jours dans les Ecritures s’il en était ainsi.
Watu wa huko walikuwa wasikivu zaidi kuliko wale wa Thesalonika. Waliupokea ule ujumbe kwa hamu kubwa, wakawa wanayachunguza Maandiko Matakatifu kila siku, ili kuona kama yale waliyosema Paulo na Sila yalikuwa kweli.
12 De sorte que beaucoup d’entre eux crurent, et parmi les gentils, beaucoup de femmes de qualité, et des hommes en assez grand nombre.
Wengi wao waliamini na pia wanawake wa Kigiriki wa tabaka la juu na wanaume pia.
13 Mais quand les Juifs de Thessalonique surent que la parole de Dieu était prêchée par Paul à Bérée même, ils y vinrent soulever et troubler la multitude.
Lakini, Wayahudi wa Thesalonika walipogundua kwamba Paulo alikuwa anahubiri neno la Mungu huko Berea, walikwenda huko, wakaanza kufanya fujo na kuchochea makundi ya watu.
14 Aussitôt les frères firent partir Paul, pour qu’il allât jusqu’à la mer; mais Silas et Timothée demeurèrent à Bérée.
Wale ndugu wakamsindikiza haraka aende pwani lakini Sila na Timotheo walibaki Berea.
15 Or ceux qui conduisaient Paul, le menèrent jusqu’à Athènes; et ayant reçu de lui, pour Silas et Timothée, l’ordre de venir le rejoindre au plus vite, ils partirent.
Wale ndugu waliomsindikiza Paulo walikwenda pamoja naye mpaka Athene. Kisha, wakarudi pamoja na maagizo kutoka kwa Paulo kwamba Sila na Timotheo wamfuate upesi iwezekanavyo.
16 Pendant que Paul les attendait à Athènes, son esprit était ému en lui, voyant cette ville livrée à l’idolâtrie.
Paulo alipokuwa anawasubiri Sila na Timotheo huko Athene, moyo wake ulighadhibika sana alipoona jinsi mji huo ulivyokuwa umejaa sanamu za miungu.
17 Il disputait donc dans la synagogue avec les Juifs et les prosélytes, et tous les jours sur la place publique avec ceux qui s’y rencontraient.
Alijadiliana na Wayahudi na watu wengine waliomcha Mungu katika sunagogi; na kila siku alikuwa na majadiliano sokoni pamoja na wowote wale waliojitokeza.
18 Quelques philosophes épicuriens et stoïciens discouraient aussi avec lui, et plusieurs disaient: Que veut dire ce semeur de paroles? Et d’autres: Il paraît annoncer des dieux nouveaux; parce qu’il leur annonçait Jésus et la résurrection.
Wengine waliofuata falsafa ya Epikuro na Stoiki walibishana naye. Wengine walisema, “Anataka kusema nini huyu bwanamaneno?” Kwa kuwa Paulo alikuwa anahubiri juu ya Yesu na juu ya ufufuo, wengine walisema, “Inaonekana kama anahubiri juu ya miungu ya kigeni.”
19 Et, l’ayant pris, ils le conduisirent devant l’Aréopage, disant: Pouvons-nous savoir quelle est cette nouvelle doctrine que tu publies?
Hivyo walimchukua Paulo, wakampeleka Areopago, wakasema, “Tunataka kujua jambo hili jipya ulilokuwa unazungumzia.
20 Car tu portes à nos oreilles de certaines choses nouvelles; nous voudrions donc savoir ce que ce peut être.
Vitu vingine tulivyosikia kwa masikio yetu vinaonekana kuwa viroja kwetu. Tungependa kujua mambo haya yana maana gani.”
21 (Or tous les Athéniens et les étrangers demeurant à Athènes ne s’occupaient qu’à dire ou à entendre quelque chose de nouveau.)
Wananchi wa Athene na wakazi wengine wa huko walikuwa wanatumia wakati wao wote kuhadithiana na kusikiliza habari mpyampya.
22 Ainsi, étant au milieu de l’Aréopage, Paul dit: Athéniens, je vous vois, en toutes choses, religieux presque jusqu’à l’excès.
Basi, Paulo alisimama mbele ya baraza la Areopago, akasema, “Wananchi wa Athene! Ninaona kwamba ninyi, kwa vyovyote, ni watu wa dini sana.
23 Car, passant, et voyant vos simulacres, j’ai trouvé même un autel où il était écrit: Au Dieu INCONNU. Or ce que vous adorez sans le connaître, moi, je vous l’annonce.
Sababu yenyewe ni kwamba katika pitapita yangu niliangalia sanamu zenu za ibada nikakuta madhabahu moja ambayo imeandikwa: Kwa ajili ya Mungu yule Asiyejulikana. Basi, huyo mnayemwabudu bila kujua, ndiye ninayemhubiri kwenu.
24 Le Dieu qui a fait le monde, et tout ce qui est dans le monde, ce Dieu, étant le Seigneur du ciel et de la terre, n’habite point en des temples faits de la main des hommes,
Mungu, aliyeumba ulimwengu na vyote vilivyomo, ni Bwana wa mbingu na nchi; yeye hakai katika hekalu zilizojengwa na watu.
25 Et n’est point honoré par les ouvrages des mains des hommes, comme s’il avait besoin de quelque chose, puisqu’il donne lui-même à tous la vie, la respiration et toutes choses;
Wala hatumikiwi kwa mikono ya watu kana kwamba anahitaji chochote kile, kwa maana yeye mwenyewe ndiye anayewapa watu uhai, anawawezesha kupumua na anawapa kila kitu.
26 Il a fait que d’un seul toute la race des hommes habite sur toute la face de la terre, déterminant les temps de leur durée et les limites de leur demeure;
Kutokana na mtu mmoja aliumba mataifa yote na kuyawezesha kuishi duniani kote. Aliamua na kupanga kabla kabisa lini na wapi mataifa hayo yangeishi.
27 Afin qu’ils cherchent Dieu, et s’efforcent de le trouver comme à tâtons, quoiqu’il ne soit pas loin de chacun de nous.
Alifanya hivyo, ili mataifa hayo yapate kumfuata, na kama vile kwa kupapasapapasa, yapate kumfikia. Hata hivyo lakini, Mungu hayuko mbali na kila mmoja wetu.
28 Car ces en lui que nous vivons, et que nous nous mouvons et que nous sommes; comme quelques-uns assurément de vos poètes l’ont dit: nous sommes même de sa race.
Kama alivyosema mtu mmoja: Ndani yake yeye sisi tunaishi, tunajimudu, na tuko! Ni kama washairi wenu wengine walivyosema: Sisi ni watoto wake.
29 Puisque donc nous sommes la race de Dieu, nous ne devons pas estimer que l’être divin soit semblable à de l’or, ou à de l’argent, ou à de la pierre sculptée par l’art et l’industrie de l’homme.
Ikiwa basi, sisi ni watoto wa Mungu, haifai kumfikiria Mungu kuwa kama dhahabu, fedha au hata jiwe lililochongwa na kutiwa nakshi na binadamu.
30 Mais, fermant les yeux sur les temps d’une telle ignorance, Dieu annonce maintenant aux hommes que tous, en tous lieux, fassent pénitence;
Mungu alifanya kama kwamba haoni nyakati zile watu walipokuwa wajinga. Lakini sasa, anaamuru watu wote kila mahali watubu.
31 Parce qu’il a fixé un jour auquel il doit juger le monde avec équité par l’homme qu’il a établi, comme il en a donné la preuve à tous, en le ressuscitant d’entre les morts.
Kwa maana amekwisha weka siku ambayo atauhukumu ulimwengu kwa haki kwa njia ya mtu mmoja aliyemteua. Mungu amewathibitishia wote jambo hili kwa kumfufua mtu huyo kutoka wafu!”
32 Mais lorsqu’ils entendirent parler de résurrection de morts, les uns se moquaient, et les autres dirent: Nous t’entendrons là-dessus une autre fois.
Walipomsikia Paulo anasema juu ya jambo la kufufuka kwa wafu, wengine wao waliangua kicheko; lakini wengine walisema, “Tunataka kukusikia tena juu ya jambo hili!”
33 C’est ainsi que Paul sortit d’au milieu d’eux.
Hivyo, Paulo aliwaacha, akatoka barazani.
34 Quelques-uns cependant, s’attachant à lui, crurent: entre lesquels, Denys l’aréopagite, et une femme du nom de Damaris, et d’autres avec eux.
Lakini watu kadhaa waliandamana naye, wakawa waumini. Miongoni mwao walikuwa Dionisio wa Areopago, mwanamke mmoja aitwaye Damari na wengineo.

< Actes 17 >