< Actes 11 >
1 Or les apôtres et les frères, qui étaient en Judée, apprirent que les gentils aussi avaient reçu la parole de Dieu.
Mitume na ndugu kule Yudea walisikia kwamba watu wa mataifa mengine pia walikuwa wamelipokea neno la Mungu.
2 Et, lorsque Pierre fut revenu à Jérusalem, ceux de la circoncision disputaient contre lui,
Basi, Petro aliporudi Yerusalemu, wale Wayahudi waumini waliopendelea watu wa mataifa mengine watahiriwe, walimlaumu wakisema:
3 Disant: Pourquoi es-tu entré chez des hommes incirconcis, et as-tu mangé avec eux?
“Wewe umekwenda kukaa na watu wasiotahiriwa na hata umekula pamoja nao!
4 Et Pierre commença à leur exposer les choses par ordre, disant:
Hapo Petro akawaeleza kinaganaga juu ya yale yaliyotendeka tangu mwanzo:
5 J’étais dans la ville de Joppé, priant, et dans un ravissement d’esprit, je vis comme une grande nappe suspendue par les quatre coins, qu’on abaissait du ciel, et qui vint jusqu’à moi.
“Siku moja nikiwa nasali mjini Yopa, niliona maono; niliona kitu kama shuka kubwa likishushwa chini kutoka mbinguni likiwa limeshikwa pembe zake nne, likawekwa kando yangu.
6 En la considérant attentivement, je vis les quadrupèdes de la terre, et les bêtes sauvages, et les reptiles, et les oiseaux du ciel.
Nilichungulia ndani kwa makini nikaona wanyama wenye miguu minne, wanyama wa mwituni, wanyama watambaao na ndege wa angani.
7 Et j’entendis une voix qui me disait: Tue et mange.
Kisha nikasikia sauti ikiniambia: Petro amka, chinja, ule.
8 Et je répondis: Nullement, Seigneur; car jamais rien d’impur ou de souillé n’entra dans ma bouche.
Lakini mimi nikasema: La, Bwana; maana chochote kilicho najisi au kichafu hakijapata kamwe kuingia kinywani mwangu.
9 Et la voix du ciel me dit une seconde fois: Ce que Dieu a purifié, ne l’appelle pas impur.
Ile sauti ikasikika tena kutoka mbinguni: Usiviite najisi vitu ambavyo Mungu amevitakasa.
10 Cela fut fait par trois fois, et tout rentra dans le ciel.
Jambo hilo lilifanyika mara tatu, na mwishowe vyote vilirudishwa juu mbinguni.
11 Et voilà qu’aussitôt trois hommes, envoyés vers moi de Césarée, s’arrêtèrent devant la maison où j’étais.
Ghafla, watu watatu waliokuwa wametumwa kwangu kutoka Kaisarea waliwasili kwenye nyumba niliyokuwa nakaa.
12 Et l’Esprit me dit d’aller avec eux sans hésiter. Les six frères que voici vinrent avec moi, et nous entrâmes dans la maison de cet homme.
Roho aliniambia niende pamoja nao bila kusita. Hawa ndugu sita waliandamana nami pia kwenda Kaisarea na huko tuliingia nyumbani mwa Kornelio.
13 Or il nous raconta comment il avait vu dans sa maison un ange qui s’était présenté et lui avait dit: Envoie à Joppé et fais venir Simon, qui est surnommé Pierre;
Yeye alitueleza jinsi alivyokuwa amemwona malaika amesimama nyumbani mwake na kumwambia: Mtume mtu Yopa akamwite mtu mmoja aitwaye Simoni, kwa jina lingine Petro.
14 Il le dira des paroles par lesquelles tu seras sauvé, toi et toute ta maison.
Yeye atakuambia maneno ambayo kwayo wewe na jamaa yako yote mtaokolewa.
15 Lorsque j’eus commencé de parler, l’Esprit descendit sur eux comme sur nous au commencement.
Na nilipoanza tu kuongea, Roho Mtakatifu aliwashukia kama alivyotushukia sisi pale awali.
16 Alors je me souvins de la parole du Seigneur, lorsqu’il disait: Jean a baptisé dans l’eau; mais vous, vous serez baptisés dans l’Esprit-Saint.
Hapo nilikumbuka yale maneno Bwana aliyosema: Yohane alibatiza kwa maji, lakini ninyi mtabatizwa kwa Roho Mtakatifu.
17 Si donc Dieu leur a donné la même grâce qu’à nous, qui avons cru au Seigneur Jésus-Christ; qui étais-je, moi, pour m’opposer à Dieu?
Basi, kama Mungu amewapa pia watu wa mataifa mengine zawadi ileile aliyotupa sisi tulipomwamini Bwana Yesu Kristo, je, mimi ni nani hata nijaribu kumpinga Mungu?”
18 Ces choses entendues, ils se turent, et glorifièrent Dieu, disant: Dieu a donc accordé la pénitence aux gentils aussi, pour qu’ils aient la vie.
Waliposikia hayo, waliacha ubishi, wakamtukuza Mungu wakisema, “Mungu amewapa watu wa mataifa mengine nafasi ya kutubu na kuwa na uzima!”
19 Cependant ceux qui avaient été dispersés par la persécution qui s’était élevée au temps d’Etienne, avaient passé jusqu’en Phénicie, en Chypre, et à Antioche, n’annonçant la parole qu’aux Juifs seulement.
Kutokana na mateso yaliyotokea wakati Stefano alipouawa, waumini walitawanyika. Wengine walikwenda mpaka Foinike, Kupro na Antiokia wakihubiri ule ujumbe kwa Wayahudi tu.
20 Mais il y avait parmi eux quelques hommes de Chypre et de Cyrène, qui, étant entrés dans Antioche, parlaient aux Grecs, leur annonçant le Seigneur Jésus.
Lakini baadhi ya waumini waliotoka Kupro na Kurene, walikwenda Antiokia wakautangaza huo ujumbe kwa watu wa mataifa mengine wakiwahubiria ile Habari Njema juu ya Bwana Yesu.
21 Et la main du Seigneur était avec eux; et un grand nombre crurent et se convertirent au Seigneur.
Bwana aliwasaidia na idadi kubwa ya watu iliamini na kumgeukia Bwana.
22 Or, lorsque le bruit en fut venu jusqu’aux oreilles de l’Eglise de Jérusalem, ils envoyèrent Barnabé à Antioche,
Habari ya jambo hilo ikasikika kwa lile kanisa la Yerusalemu. Hivyo wakamtuma Barnaba aende Antiokia.
23 Lequel, lorsqu’il fut arrivé et qu’il eut vu la grâce de Dieu, se réjouit; et il les exhortait tous à persévérer, d’un cœur ferme, dans le Seigneur;
Alipofika huko na kuona jinsi Mungu alivyowaneemesha wale watu, alifurahi na kuwahimiza wote wadumu katika uaminifu wao kwa Bwana.
24 Car c’était un homme bon, plein de l’Esprit-Saint et de foi. Ainsi une grande multitude s’attacha au Seigneur.
Barnaba alikuwa mtu mwema na mwenye kujaa Roho Mtakatifu na imani. Kundi kubwa la watu lilivutwa kwa Bwana.
25 Barnabé partit ensuite pour Tarse, afin de chercher Paul; et, l’ayant trouvé, il l’amena à Antioche.
Kisha, Barnaba alikwenda Tarso kumtafuta Saulo
26 Et pendant une année entière ils demeurèrent dans cette Eglise, et y enseignèrent une foule nombreuse; en sorte que ce fut à Antioche que les disciples reçurent pour la première fois le nom de Chrétiens.
Alipompata, alimleta Antiokia. Nao wote wawili walikaa na lile kanisa kwa mwaka wote mzima wakifundisha kundi kubwa la watu. Huko Antiokia, ndiko, kwa mara ya kwanza, wafuasi waliitwa Wakristo.
27 Or, en ces jours-là, des prophètes vinrent de Jérusalem à Antioche;
Wakati huohuo, manabii kadhaa walikuja Antiokia kutoka Yerusalemu.
28 Et l’un d’eux, du nom d’Agabus, se levant, annonçait, par l’Esprit-Saint, qu’il y aurait une grande famine dans tout l’univers; laquelle, en effet, arriva sous Claude.
Basi, mmoja wao aitwaye Agabo alisimama, na kwa uwezo wa Roho akabashiri kwamba kutakuwa na njaa kubwa katika nchi yote (Njaa hiyo ilitokea wakati Klaudio alipokuwa akitawala).
29 Et les disciples résolurent d’envoyer, chacun suivant ce qu’il possédait, des aumônes aux frères qui habitaient dans la Judée;
Wale wanafunzi waliamua kila mmoja kwa kadiri ya uwezo wake apeleke chochote ili kuwasaidia wale ndugu waliokuwa wanaishi Yudea.
30 Ce qu’ils firent, en effet, les envoyant aux anciens par les mains de Barnabé et de Saul.
Basi, wakafanya hivyo na kupeleka mchango wao kwa wazee wa kanisa kwa mikono ya Barnaba na Saulo.