< 2 Samuel 1 >

1 Or, il arriva, après que Saül fut mort, que David revint de la défaite d’Amalec, et qu’il demeura à Siceleg pendant deux jours.
Baada ya kifo cha Sauli, Daudi alipokuwa amerudi kutoka kuwashinda Waamaleki, Daudi alikaa siku mbili huko Siklagi.
2 Mais au troisième jour, il parut un homme, venant du camp de Saül, le vêtement déchiré et la tête couverte de poussière; et dès qu’il arriva auprès de David, il tomba sur sa face, et se prosterna.
Siku ya tatu akaja mtu mwenye nguo zilizoraruka na mavumbi kichwani mwake kutoka kwenye kambi ya Sauli. Alipomjia Daudi, akajitupa chini ili kumpa heshima.
3 Et David lui demanda: D’où viens-tu? Celui-ci lui répondit: Je me suis échappé du camp d’Israël.
Daudi akamuuliza, “Wewe umetoka wapi?” Akamjibu, “Nimetoroka kutoka kambi ya Waisraeli.”
4 David lui demanda encore: Qu’est-ce qui a été fait? Apprends-le moi. Il répondit: Le peuple s’est enfui de la bataille, et beaucoup d’entre le peuple, ayant succombé, sont morts; et Saül même et Jonathas son fils ont péri.
Daudi akamuuliza, “Ni nini kilichotokea? Niambie.” Akasema, “Watu walikimbia kutoka vitani. Wengi wao walianguka na kufa. Naye Sauli na Yonathani mwanawe wamekufa.”
5 Et David dit au jeune homme qui lui apportait la nouvelle: D’où sais-tu que Saül est mort, et Jonathas son fils?
Ndipo Daudi akamwambia huyo kijana aliyemletea taarifa, “Je, umefahamuje kwamba Sauli na Yonathani mwanawe wamekufa?”
6 Et le jeune homme qui lui apportait la nouvelle lui répondit: Je suis venu par hasard sur la montagne de Gelboé, et Saül était appuyé sur sa lance; or, les chariots et les cavaliers s’avançaient vers lui,
Yule kijana akasema, “Nilijipata huko Mlima Gilboa, naye Sauli alikuwa huko akiegemea mkuki wake, na magari ya vita na wapanda farasi wa upande wa adui wakawa wamemkaribia sana.
7 Et s’étant retourné, et me voyant, il m’a appelé. Et quand je lui eus répondu: Me voici,
Alipogeuka na kuniona, akaniita, nami nikasema, ‘Je, nifanye nini?’
8 Il me demanda: Qui es-tu? Et je lui répondis: Je suis Amalécite.
“Akaniuliza, ‘Wewe ni nani?’ “Nikamjibu, ‘Mimi ni Mwamaleki.’
9 Alors il me dit: Jette-toi sur moi, et tue-moi, parce que je suis en proie aux angoisses, et que toute mon âme est encore en moi.
“Kisha akaniambia, ‘Nikaribie mimi na uniue! Niko katika maumivu makali ya kifo, lakini bado ningali hai.’
10 Me jetant donc sur lui, je le tuai; car je savais qu’il ne pouvait pas vivre après son désastre; alors je pris le diadème qui était sur sa tête, et le bracelet de son bras, et je les apportai ici à vous, mon seigneur.
“Kwa hiyo nikamkaribia nikamuua, kwa sababu nilijua kwamba baada ya kuanguka hangeweza kupona. Nami nikachukua lile taji lililokuwa kichwani mwake na utepe uliokuwa mkononi mwake nami nimevileta hapa kwa bwana wangu.”
11 Mais David prenant ses vêtements, les déchira; ce que firent aussi tous les hommes qui étaient avec lui.
Ndipo Daudi pamoja na watu wote waliokuwa pamoja naye wakazishika nguo zao na kuzirarua.
12 Et ils furent dans le deuil, et ils pleurèrent et ils jeûnèrent jusqu’au soir, au sujet de Saül, de Jonathas, son fils, du peuple du Seigneur et de la maison d’Israël, parce qu’ils avaient succombé au glaive.
Wakaomboleza, wakalia pia na kufunga mpaka jioni kwa ajili ya Sauli na Yonathani mwanawe, kwa ajili ya jeshi la Bwana na nyumba ya Israeli, kwa sababu wameanguka kwa upanga.
13 Et David dit au jeune homme qui lui avait apporté la nouvelle: D’où es-tu? Il répondit: Je suis fils d’un étranger, d’un Amalécite.
Daudi akamwambia yule kijana aliyemletea taarifa, “Wewe ni mwenyeji wa wapi?” Akamjibu, “Mimi ni mwana wa mgeni, Mwamaleki.”
14 Et David lui dit: Pourquoi n’as-tu pas craint de lever ta main, pour tuer le christ du Seigneur?
Daudi akamuuliza, “Kwa nini hukuogopa kuinua mkono wako ili kumwangamiza mpakwa mafuta wa Bwana?”
15 Et David appelant un de ses serviteurs, dit: Approche-toi, jette-toi sur lui. Le serviteur le frappa, et il mourut,
Kisha Daudi akamwita mmoja wa watu wake na kumwambia, “Nenda ukamuue!” Kwa hiyo akampiga, naye akafa.
16 Et David ajouta: Ton sang sur ta tête! car ta bouche a parlé contre toi, disant: C’est moi qui ai tué le christ du Seigneur.
Kwa maana Daudi alikuwa amemwambia, “Damu yako iwe juu ya kichwa chako mwenyewe. Kinywa chako mwenyewe kimeshuhudia dhidi yako uliposema, ‘Nilimuua mpakwa mafuta wa Bwana.’”
17 Alors David fit entendre cette complainte sur Saül et sur Jonathas, son fils
Daudi akafanya maombolezo haya kuhusu Sauli na Yonathani mwanawe,
18 (Et il ordonna qu’on enseignât l’arc aux enfants de Juda, comme il est écrit dans le Livre des Justes), et il dit: Considère, ô Israël, ceux qui sont morts sur tes hauts lieux, couverts de blessures.
naye akaagiza kwamba watu wa Yuda wafundishwe ombolezo hili la upinde (ambalo limeandikwa katika Kitabu cha Yashari):
19 Les illustres, ô Israël, ont été tués sur tes montagnes: comment des forts sont-ils tombés?
“Walio fahari yako, ee Israeli, wameuawa juu ya mahali pako palipoinuka. Jinsi wenye nguvu walivyoanguka!
20 Ne l’annoncez pas dans Geth, ne l’annoncez pas dans les carrefours d’Ascalon, de peur que les filles des Philistins ne se livrent à la joie, et que les filles des incirconcis ne bondissent d’allégresse.
“Msilisimulie hili katika Gathi, msilitangaze hili katika barabara za Ashkeloni, binti za Wafilisti wasije wakafurahia, binti za hao wasiotahiriwa wasije wakashangilia.
21 Montagnes de Gelboé, que ni pluie, ni rosée ne viennent sur vous: qu’il n’y ait point de champs de prémices, parce que là a été jeté un bouclier de forts, le bouclier de Saül, comme s’il n’avait pas été oint avec l’huile.
“Enyi milima ya Gilboa, msipate umande wala mvua, wala mashamba yazaayo sadaka ya nafaka. Kwa maana huko ndiko ngao ya mwenye nguvu iliponajisiwa, ngao ya Sauli haitapakwa tena mafuta.
22 La flèche de Jonathas n’est jamais retournée en arrière, sans avoir du sang de ceux qui ont été tués, et de la graisse des forts, et le glaive de Saül n’est pas revenu en vain.
Kutokana na damu ya waliouawa, kutokana na miili ya wenye nguvu, ule upinde wa Yonathani haukugeuka nyuma. Upanga wa Sauli haukurudi bure.
23 Saül et Jonathas, aimables et beaux dans leur vie, même à leur mort, n’ont pas été séparés; plus rapides que des aigles, plus forts que des lions.
“Sauli na Yonathani, maishani walipendwa na kuneemeka, na katika kifo hawakutengana. Walikuwa wepesi kuliko tai, walikuwa na nguvu kuliko simba.
24 Filles d’Israël, pleurez sur Saül, qui vous revêtait d’écarlate au milieu des délices, et vous fournissait de l’or pour votre parure.
“Enyi binti za Israeli, lieni kwa ajili ya Sauli, ambaye aliwavika nguo nyekundu na maridadi, ambaye aliremba mavazi yenu kwa mapambo ya dhahabu.
25 Comment des forts sont-ils tombés dans la bataille? Jonathas a été tué sur tes hauteurs.
“Tazama jinsi mashujaa walivyoanguka vitani! Yonathani ameuawa mahali pako palipoinuka.
26 Je pleure sur toi, mon frère, Jonathas, de la plus grande beauté, aimable au-dessus de l’amour des femmes. Comme une mère aime son fils unique, ainsi moi je te chérissais.
Nahuzunika kwa ajili yako, Yonathani ndugu yangu, kwangu ulikuwa mpendwa sana. Upendo wako kwangu ulikuwa wa ajabu, wa ajabu zaidi kuliko ule wa wanawake.
27 Comment des forts sont-ils tombés, et des armes guerrières ont-elles péri?
“Tazama jinsi mashujaa walivyoanguka! Silaha za vita zimeangamia!”

< 2 Samuel 1 >