< 2 Samuel 8 >

1 Or, il arriva après cela que [David battit les Philistins et les humilia; et David ôta le frein du tribut de la main des Philistins.
ikawa baada ya haya Daudi aliwashambulia Wafilisti na kuwashinda. Hivyo Daudi akaichukua Gathi na vijiji vyake kutoka katika mamlaka ya wafilisti.
2 Il battit aussi Moab et les mesura au cordeau, les faisant coucher par terre; or, il en mesura deux cordeaux, l’un pour les tuer, l’autre pour leur conserver la vie; et Moab fut assujetti à David lui payant tribut.
Kisha akaishinda Moabu na akawapima watu wake kwa mstari kwa kuwafanya walale chini juu ya ardhi. Alipima mistari miwili ya kuua, na mstari mmoja kamili kuwahifadhi hai. Hivyo Wamoabu wakawa watumishi wa Daudi na wakaanza kumlipa kodi.
3 De plus, David battit Adarézer, fils de Rohob, roi de Soba, quand il partit pour dominer sur le fleuve d’Euphrate.
Kisha Daudi akamshinda Hadadezeri mwana wa Rehobu, mfalme wa Soba, Hadadezeri aliposafiri kuurudisha ufalme wake katika mto Frati.
4 Et David, après lui avoir pris mille sept cents cavaliers et vingt mille hommes de pied, coupa les nerfs des jambes à tous les chevaux des chariots; mais il en laissa pour cent chariots.
Daudi aliteka magari 1, 700 ya farasi na askari ishirini elfu waendao kwa miguu. Daudi akawakata miguu farasi wa magari, lakini akahifadhi wakutosha magari mia moja.
5 Vint aussi la Syrie de Damas, pour porter secours à Adarézer, roi de Soba; et David tua vingt-deux mille hommes de la Syrie.
Wakati Washami wa Dameski walipokuja kumsaidia Hadadeziri mfalme wa Soba, Daudi akaua katika Washami watu ishirini na mbili elfu.
6 Et David mit une garnison dans la Syrie de Damas; et la Syrie devint tributaire de David; et le Seigneur conserva David dans tous les lieux où il alla.
Daudi akaweka ngome huko Shamu ya Dameski, na Washami wakawa watumishi wake na wakaleta kodi. Yahwe akampa Daudi ushindi kila alikokwenda.
7 Et David enleva les armes d’or qu’avaient les serviteurs d’Adarézer, et les porta à Jérusalem.
Daudi akachukua ngao za dhahabu walizokuwa nazo watumishi wa Hadadezeri naye akazileta Yerusalemu.
8 Et de Beté et de Béroth, villes d’Adarézer, le roi David enleva une très grande quantité d’airain.
Mfalme Daudi akachukua shaba nyingi kutoka Beta na Berosai, miji ya Hadadezeri.
9 Or, Thoü, roi d’Emath, apprit que David avait battu toutes les forces d’Adarézer;
Wakati Tou, mfalme wa Hamathi, aliposikia kwamba Daudi amelishinda jeshi lote la Hadadezeri,
10 Alors il envoya Joram son fils vers le roi David, pour le saluer, en le félicitant, et lui rendre grâce de ce qu’il avait vivement attaqué Adarézer, et l’avait battu; car Thoü était ennemi d’Adarézer; et dans la main de Joram étaient des vases d’or, des vases d’argent et des vases d’airain,
Tou akamtuma Hadoramu mwanawe kwa mfalme Daudi kumpa salamu na kumbariki, kwa kuwa Daudi alikuwa amepigana na Hadadezeri na kumshinda, maana Hadadezeri alikuwa amepiga vita dhidi ya Tou. Hadoramu akaja pamoja na vitu vya fedha, dhahabu, na shaba.
11 Que le roi David consacra aussi au Seigneur, avec l’argent et l’or qu’il avait consacrés de toutes les nations qu’il avait soumises,
Mfalme Daudi akaviweka wakfu vitu hivi kwa ajili ya Yahwe, pamoja na fedha na dhahabu kutoka katika mataifa yote aliyokuwa ameyashinda-
12 De la Syrie, de Moab, des enfants d’Ammon, des Philistins, d’Amalec et des dépouilles d’Adarézer, fils de Rohob, roi de Soba.
kutoka Shamu, Moabu, Waamoni, Wafilist, Waamaleki, pamoja na nyara zote alizoziteka kutoka kwa Hadadezeri mwana wa Rehobu, mfalme wa Soba.
13 David se fit encore un nom, lorsque, la Syrie prise, il fut revenu dans la vallée des Salines, où il tailla en pièces dix-huit mille hommes.
Jina la Daudi likajulikana sana alipowashinda washami katika bonde la Chumvi, pamoja na watu wao wapatao elfu kumi na nane.
14 Et il mit des gardes dans l’Idumée, et il établit une garnison; et toute l’Idumée devint assujettie à David; et le Seigneur conserva David dans tous les lieux où il alla.
Akaweka ngome katika Edomu yote, na Waedomu wote wakawa watumishi wake. Yahwe akampa Daudi ushindi kila alipokwenda.
15 Ainsi David régna sur tout Israël; il rendait aussi des jugements et la justice à tout son peuple.
Daudi akatawala juu ya Israeli yote, naye akatenda kwa haki na usawa kwa watu wote.
16 Mais Joab, fils de Sarvia, commandait l’armée, et Josaphat, fils d’Ahilud, tenait les registres;
Yoabu mwana wa Seruya alikuwa mkuu wa jeshi, na Yehoshafati mwana wa Ahiludi alikuwa mwenye kuandika taarifa.
17 Et Sadoc, fils d’Achitob, et Achimélech, fils d’Abiathar, étaient prêtres, et Saraïas, scribe;
Sadoki mwana wa Ahitubu na Ahimeleki mwana wa Abiathari walikuwa makuhani, na Seraya alikuwa mwandishi.
18 Mais Banaïas, fils de Joïada, commandait les Céréthiens et les Phéléthiens; mais les fils de David étaient prêtres.
Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa juu ya Wakerethi na Wapelethi, na wana wa Daudi walikuwa washauri wa mfalme.

< 2 Samuel 8 >