< 2 Samuel 6 >

1 Or, David rassembla de nouveau tous les hommes choisis d’Israël, au nombre de trente mille.
Tena Daudi akakusanya watu 30,000 wa Israeli waliochaguliwa.
2 Et David se leva et s’en alla, et tout le peuple qui était avec lui d’entre les hommes de Juda, pour amener l’arche de Dieu, sur laquelle fut invoqué le nom du Seigneur des armées, assis entre les chérubins au-dessus d’elle,
Yeye na watu wake wote wakatoka Baala ya Yuda kulipandisha Sanduku la Mungu kutoka huko, linaloitwa kwa Jina, naam, jina la Bwana Mwenye Nguvu Zote, ambaye anaketi katika kiti cha enzi kati ya makerubi walioko juu ya hilo Sanduku.
3 Et ils mirent l’arche de Dieu sur un char neuf; et ils l’enlevèrent de la maison d’Abinadab, qui était à Gabaa; or, Oza et Ahio, fils d’Abinadab, conduisaient le char neuf.
Wakaweka hilo Sanduku la Mungu juu ya gari jipya la kukokotwa na kulileta kutoka nyumba ya Abinadabu, iliyokuwa juu ya kilima. Uza na Ahio, wana wa Abinadabu, walikuwa wakiongoza hilo gari jipya la kukokotwa
4 Et lorsqu’ils l’eurent emportée de la maison d’Abinadab, qui était à Gabaa, gardant l’arche de Dieu, Ahio précédait l’arche.
likiwa na Sanduku la Mungu juu yake, naye Ahio alikuwa anatembea akiwa mbele yake.
5 Mais David et tout Israël jouaient devant le Seigneur de toutes sortes d’instruments, des harpes, des lyres, des tambours, des sistres et des cymbales.
Daudi na nyumba yote ya Israeli walikuwa wanacheza mbele za Bwana kwa nguvu zao zote, kwa nyimbo, vinubi, zeze, matari, kayamba na matoazi.
6 Mais, après qu’ils furent venus à l’aire de Nachon, Oza étendit la main sur l’arche de Dieu et la retint, parce que les bœufs regimbaient et la firent pencher.
Walipofika kwenye uwanja wa kupuria nafaka wa Nakoni, Uza akanyoosha mkono na kulishika Sanduku la Mungu kwa sababu maksai walijikwaa.
7 Et le Seigneur fut irrité d’indignation contre Oza, et le frappa à cause de sa témérité; et il mourut là auprès de l’arche de Dieu.
Hasira ya Bwana ikawaka dhidi ya Uza kwa sababu ya kitendo chake cha kukosa heshima, kwa hiyo Mungu akampiga akafia papo hapo kando ya Sanduku la Mungu.
8 Or, David fut contristé, parce que le Seigneur avait frappé Oza. Et ce lieu a été appelé du nom de Châtiment d’Oza jusqu’à ce jour.
Ndipo Daudi akakasirika kwa sababu ghadhabu ya Bwana ilifurika dhidi ya Uza, hivyo hadi leo mahali hapo panaitwa Peres-Uza.
9 Et David craignit beaucoup le Seigneur en ce jour-là, disant: Comment entrera chez moi l’arche du Seigneur?
Daudi akamwogopa Bwana siku ile, akasema, “Ni jinsi gani Sanduku la Bwana litakavyoweza kunijia?”
10 Et il ne voulut pas faire venir chez lui l’arche du Seigneur dans la cité de David; mais il la fit venir dans la maison d’Obédédom, le Géthéen.
Hakuwa radhi kulichukua Sanduku la Bwana kwake katika Mji wa Daudi. Badala yake akalipeleka kwenye nyumba ya Obed-Edomu, Mgiti.
11 Et l’arche du Seigneur demeura dans la maison d’Obédédom, le Géthéen, durant trois mois, et le Seigneur bénit Obédédom, et toute sa maison.
Sanduku la Bwana likabaki katika nyumba ya Obed-Edomu, Mgiti, kwa miezi mitatu, naye Bwana akambariki pamoja na nyumba yake yote.
12 Et l’on annonça au roi David que le Seigneur avait béni Obédédom et tout ce qui lui appartenait, à cause de l’arche de Dieu. David donc s’en alla, et amena l’arche de Dieu de la maison d’Obédédom en la cité de David avec joie; et David avait avec lui sept chœurs et un veau pour victime.
Kisha Mfalme Daudi akaambiwa, “Bwana ameibariki nyumba ya Obed-Edomu pamoja na kila alicho nacho, kwa sababu ya Sanduku la Mungu.” Basi Daudi akateremka na kulipandisha Sanduku la Mungu kutoka nyumba ya Obed-Edomu hadi Mji wa Daudi kwa shangwe.
13 Et lorsque ceux qui portaient l’arche du Seigneur avaient fait six pas, il immolait un bœuf et un bélier.
Wale waliokuwa wamebeba Sanduku la Bwana walipokuwa wametembea hatua sita, Daudi alitoa dhabihu fahali na ndama aliyenoneshwa.
14 Et David dansait de toutes ses forces devant le Seigneur; et il était ceint d’un éphod de lin.
Daudi, akiwa amevaa kisibau cha kitani, alicheza mbele za Bwana kwa nguvu zake zote,
15 Et David et toute la maison d’Israël conduisaient l’arche du testament du Seigneur avec des cris de joie et au son de la trompette.
wakati yeye na nyumba yote ya Israeli walipopandisha Sanduku la Bwana kwa shangwe na sauti za tarumbeta.
16 Et lorsque l’arche du Seigneur fut entrée dans la cité de David, Michol, fille de Saül, regardant par la fenêtre, vit le roi David sautillant et dansant devant le Seigneur; et elle le méprisa en son cœur,
Ikawa Sanduku la Bwana lilipokuwa linaingia katika Mji wa Daudi, Mikali binti Sauli akachungulia dirishani. Naye alipomwona Mfalme Daudi akirukaruka na kucheza mbele za Bwana, akamdharau moyoni mwake.
17 Et ils introduisirent l’arche du Seigneur, et ils la mirent en sa place, au milieu du tabernacle que David avait dressé; et David offrit des holocaustes et des sacrifices pacifiques devant le Seigneur.
Wakaleta Sanduku la Bwana na kuliweka mahali pake ndani ya hema ambalo Daudi alikuwa amelisimamisha kwa ajili yake, naye Daudi akatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani mbele za Bwana.
18 Et quand il eut achevé d’offrir les holocaustes et les sacrifices pacifiques, il bénit le peuple au nom du Seigneur des armées.
Baada ya kumaliza kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani, Daudi akawabariki watu katika jina la Bwana Mwenye Nguvu Zote.
19 Et il distribua à toute la multitude d’Israël, tant aux hommes qu’aux femmes, à chacun une galette de pain, et un morceau de viande de bœuf rôtie, et de la fleur de farine frite dans l’huile; et tout le peuple s’en alla, chacun en sa maison.
Kisha akatoa mkate, andazi la tende na andazi la zabibu kavu kwa kila mtu katika mkutano wote wa Waisraeli, wanaume kwa wanawake. Nao watu wote wakaenda nyumbani kwao.
20 Et David s’en retourna pour bénir sa maison; et Michol, fille de Saül, étant sortie au-devant de David, dit: Qu’il a été glorieux aujourd’hui le roi d’Israël, se découvrant devant les servantes de ses serviteurs! car il s’est dépouillé, comme si un de ses bouffons se dépouillait.
Daudi aliporudi ili kuwabariki watu wa nyumbani mwake, Mikali binti Sauli akatoka nje kumlaki, akamwambia, “Tazama jinsi mfalme wa Israeli alivyojibainisha mwenyewe leo kwa kuvua mavazi yake machoni pa vijakazi wa watumishi wake, kama vile ambavyo mtu asiye na adabu angelifanya!”
21 Et David répondit à Michol: Devant le Seigneur, qui m’a choisi plutôt que ton père et que toute ta maison, et qui m’a ordonné d’être chef sur le peuple du Seigneur en Israël,
Daudi akamwambia Mikali, “Nilifanya hivyo mbele za Bwana ambaye alinichagua mimi badala ya baba yako au mwingine yeyote kutoka nyumba yake wakati aliponiweka niwe mtawala juu ya Israeli, watu wa Bwana. Kwa hiyo nitacheza mbele za Bwana.
22 Je jouerai, et je passerai pour plus vil que je n’ai passé; et je serai humble à mes yeux; et devant les servantes dont tu as parlé, je paraîtrai plus glorieux.
Nitakuwa asiye na heshima zaidi kuliko sasa, nami nitajishusha machoni pangu mwenyewe. Lakini kwa hawa vijakazi uliosema habari zao nitaheshimiwa.”
23 Ainsi, il n’est point né de fils à Michol, fille de Saül, jusqu’au jour de sa mort.
Naye Mikali binti Sauli hakuwa na watoto mpaka siku ya kufa kwake.

< 2 Samuel 6 >