< 2 Samuel 2 >

1 Et après cela David consulta le Seigneur, disant: Est-ce que je monterai dans une des villes de Juda? Et le Seigneur lui dit: Monte. Alors David demanda: Où monterai-je? Et le Seigneur lui répondit: À Hébron.
Ikawa baada ya mambo haya, Daudi akamuuliza Bwana, “Je, nipande kwenda katika mojawapo ya miji ya Yuda?” Bwana akasema, “Panda.” Daudi akauliza, “Je, niende wapi?” Bwana akajibu, “Nenda Hebroni.”
2 David donc monta, et ses deux femmes Achinoam, Jezraélite, et Abigaïl, femme de Nabal du Carmel.
Basi Daudi akakwea kwenda huko pamoja na wake zake wawili, Ahinoamu wa Yezreeli na Abigaili, mjane wa Nabali wa Karmeli.
3 Mais David mena aussi les hommes qui étaient avec lui, chacun avec sa maison; et ils demeurèrent dans les villes d’Hébron.
Pia Daudi akawachukua watu waliokuwa pamoja naye, kila mmoja na jamaa yake, nao wakaishi huko Hebroni na miji yake.
4 Alors vinrent les hommes de Juda, et ils oignirent là David, afin qu’il régnât sur la maison de Juda. Et on annonça à David que les hommes de Jabès-Galaad avaient enseveli Saül.
Ndipo watu wa Yuda wakaja Hebroni, huko wakamtia Daudi mafuta awe mfalme juu ya nyumba ya Yuda. Daudi alipoambiwa kuwa ni watu wa Yabeshi-Gileadi waliomzika Sauli,
5 David donc envoya des messagers aux hommes de Jabès-Galaad, et leur dit: Bénis soyez du Seigneur, vous qui avez fait cette miséricorde à votre seigneur Saül, et l’avez enseveli!
akatuma wajumbe kwa watu wa Yabeshi-Gileadi kuwaambia, “Bwana awabariki kwa kuonyesha wema huu kwa kumzika Sauli bwana wenu.
6 Et maintenant le Seigneur vous rendra miséricorde et fidélité; mais moi aussi je vous rendrai grâces de ce que vous avez fait cette action.
Sasa Bwana na awaonyeshe wema na uaminifu, nami pia nitawaonyesha wema ule ule kwa kuwa mmefanya jambo hili.
7 Que vos mains se fortifient, et soyez des fils de courage; car, quoique votre seigneur Saül soit mort, néanmoins la maison de Juda m’a oint pour son roi.
Sasa basi, kuweni hodari na mashujaa, kwa maana bwana wenu Sauli amekufa, nayo nyumba ya Yuda imenitia mafuta niwe mfalme juu yao.”
8 Mais Abner, fils de Ner, prince de l’armée de Saül, prit Isboseth, fils de Saül, et lui fit parcourir le camp.
Wakati huo Abneri mwana wa Neri, jemadari wa jeshi la Sauli, alikuwa amemchukua Ish-Boshethi mwana wa Sauli na kumleta hadi Mahanaimu.
9 Et il l’établit roi sur Galaad, sur Gessuri, sur Jezraël, sur Ephraïm, sur Benjamin et sur tout Israël.
Akamweka awe mfalme juu ya nchi ya Gileadi, Waasheri, Yezreeli, Efraimu, Benyamini na Israeli yote.
10 Isboseth, fils de Saül, avait quarante ans, lorsqu’il commença à régner sur Israël, et il régna deux ans; mais la seule maison de Juda suivait David.
Ish-Boshethi mwana wa Sauli alikuwa na umri wa miaka arobaini alipoanza kutawala Israeli, naye akatawala miaka miwili. Hata hivyo, nyumba ya Yuda ikamfuata Daudi.
11 Et le nombre des jours que David demeura, régnant à Hébron sur la maison de Juda, fut de sept ans et six mois.
Muda ambao Daudi alikuwa mfalme juu ya nyumba ya Yuda huko Hebroni ilikuwa miaka saba na miezi sita.
12 Et Abner, fils de Ner, sortit du camp, et les serviteurs d’Isboseth, fils de Saül, pour venir à Gabaon.
Abneri mwana wa Neri, pamoja na watu wa Ish-Boshethi mwana wa Sauli, wakatoka Mahanaimu kwenda Gibeoni.
13 Mais Joab, fils de Sarvia, et les serviteurs de David sortirent, et les rencontrèrent près de la piscine de Gabaon. Et lorsqu’ils se furent assemblés, ils se postèrent en droite ligne, ceux-ci d’un côté de la piscine, et ceux-là de l’autre.
Yoabu mwana wa Seruya na watu wa Daudi wakatoka na kukutana nao kwenye bwawa la Gibeoni. Kikundi kimoja kiliketi upande mmoja wa bwawa, na kikundi kingine upande wa pili.
14 Alors Abner dit à Joab: Que les jeunes hommes se lèvent, et qu’ils escarmouchent devant nous. Et Joab répondit: Qu’ils se lèvent.
Ndipo Abneri akamwambia Yoabu, “Tuwaweke baadhi ya vijana wasimame na wapigane ana kwa ana mbele yetu.” Yoabu akasema, “Sawa, na wafanye hivyo.”
15 Ils se levèrent donc, et ils passèrent au nombre de douze de Benjamin, du côté d’Isboseth, fils de Saül, et de douze d’entre les serviteurs de David.
Kwa hiyo vijana wakasimama, wakahesabiwa: watu wa Benyamini na wa Ish-Boshethi mwana wa Sauli kumi na wawili, na upande wa Daudi kumi na wawili.
16 Et chacun, ayant pris par la tête son concurrent, enfonça son glaive dans le côté de son adversaire, et ils tombèrent ensemble; et on appela ce lieu du nom de Champ des forts à Gabaon.
Kisha kila mtu akakamatana na mpinzani wake kichwani na kuchomana kwa upanga, nao wakaanguka chini pamoja. Kwa hiyo mahali pale katika Gibeoni pakaitwa Helkath-Hasurimu.
17 Et il s’éleva une guerre très violente en ce jour-là; et Abner fut mis en fuite et les hommes d’Israël par les serviteurs de David.
Siku hiyo vita vilikuwa vikali sana, naye Abneri na watu wa Israeli wakashindwa na watu wa Daudi.
18 Or étaient là les trois fils de Sarvia, Joab, Abisaï et Asaël; et Asaël fut un coureur très agile, comme un des chevreuils qui demeurent dans les forêts.
Wana watatu wa Seruya walikuwako huko: nao ni Yoabu, Abishai na Asaheli. Basi huyo Asaheli alikuwa na mbio kama paa.
19 Aussi Asaël poursuivait Abner, et il ne se détourna ni à droite ni à gauche, ne cessant de poursuivre Abner.
Asaheli akamfukuza Abneri, pasipo kugeuka kulia wala kushoto wakati akimfuata.
20 C’est pourquoi Abner regarda derrière lui, et dit: Es-tu Asaël, toi? Et il répondit: Oui, je le suis.
Abneri akaangalia nyuma na kumuuliza, “Ni wewe, Asaheli?” Akamjibu, “Ndiyo.”
21 Et Abner lui dit: Va à droite ou à gauche, et saisis un de ces jeunes hommes et prends pour toi ses dépouilles. Mais Asaël ne voulut pas cesser de le poursuivre.
Ndipo Abneri akamwambia, “Geuka upande wa kulia au kushoto. Mchukue mmoja wa vijana wa kiume na umvue silaha zake.” Lakini Asaheli hakuacha kumfukuza.
22 Et Abner parla de nouveau à Asaël: Retire-toi, ne me suis point, pour ne pas que je sois forcé de te percer contre la terre; car je ne pourrai lever ma face du côté de Joab ton frère.
Abneri akamwonya tena Asaheli akimwambia, “Acha kunifukuza! Kwa nini nikuue? Je, nitawezaje kumtazama ndugu yako Yoabu usoni?”
23 Asaël dédaigna de l’entendre, et ne voulut pas se détourner. Abner donc, retournant sa lance, le frappa dans l’aîne, le transperça, et il mourut dans le même lieu; et tous ceux qui passaient par ce lieu dans lequel Asaël était tombé et était mort, s’arrêtaient.
Lakini Asaheli alikataa kuacha kumfuatia, kwa hiyo Abneri akamchoma Asaheli tumboni kwa ncha butu ya mkuki wake, mkuki ukamtoboa ukatokea mgongoni mwake. Akaanguka na kufa papo hapo. Ikawa kila mtu alisimama alipofika mahali pale Asaheli alipoanguka na kufa.
24 Or, Joab et Abisaï poursuivant Abner qui s’enfuyait, le soleil se coucha; et ils vinrent jusqu’à la colline de l’aqueduc, qui est vis-à-vis de la vallée, sur le chemin du désert de Gabaon.
Lakini Yoabu na Abishai walimfuata Abneri, na jua lilipokuwa linatua, wakafika kwenye kilima cha Ama, karibu na Gia kwenye njia ya kuelekea kwenye nyika ya Gibeoni.
25 Et les enfants de Benjamin s’assemblèrent auprès d’Abner; et réunis en un seul bataillon, ils s’arrêtèrent sur le haut d’un tertre.
Ndipo watu wa kabila la Benyamini wakakusanyika tena nyuma ya Abneri. Wakaunda kikosi na kujiimarisha juu ya kilima.
26 Alors Abner cria à Joab, et dit: Est-ce jusqu’à la dernière extermination que ton glaive tranchant sévira? Ignores-tu que le désespoir est dangereux? Jusqu’à quand ne diras-tu pas au peuple, qu’il cesse de poursuivre ses frères?
Abneri akamwita Yoabu, akamwambia, “Je, ni lazima upanga uendelee kuangamiza milele? Hutambui kwamba jambo hili litaishia katika uchungu? Utaacha kuwaagiza watu wako waache kuwafuatilia ndugu zao hata lini?”
27 Et Joab lui répondit: Le Seigneur vit! si tu avais parlé, ce matin se serait retiré le peuple qui poursuit son frère.
Yoabu akajibu, “Hakika kama aishivyo Mungu, kama hukusema, hawa watu wangeendelea kuwafuatia ndugu zao mpaka asubuhi.”
28 Joab donc sonna de la trompette, et toute l’armée s’arrêta; et ils ne poursuivirent plus Israël, et ils n’engagèrent pas le combat.
Basi Yoabu akapiga tarumbeta, nao watu wote wakasimama, hawakuwafuata Israeli tena, wala hawakuwapiga tena.
29 Or, Abner et ses hommes s’en allèrent à travers les plaines, pendant toute cette nuit-là, et ils passèrent le Jourdain, et, tout Béthoron traversé, ils vinrent au camp.
Usiku ule wote Abneri na watu wake wakatembea kupitia Araba. Wakavuka Mto Yordani, wakaendelea wakipitia nchi yote ya Bithroni wakafika Mahanaimu.
30 Quant à Joab, étant revenu, après avoir laissé Abner de côté, il assembla tout le peuple; et il manqua des serviteurs de David dix-neuf hommes, sans compter Asaël.
Basi Yoabu akarudi kutoka kumfuatia Abneri, na kuwakusanya watu wake wote. Pamoja na Asaheli, watu kumi na tisa wa Daudi walikuwa wamepotea.
31 Mais les serviteurs de David frappèrent de Benjamin et des hommes qui étaient avec Abner trois cent soixante, qui même moururent.
Lakini watu wa Daudi walikuwa wamewaua watu wa kabila la Benyamini 360 waliokuwa pamoja na Abneri.
32 Et ils emportèrent Asaël, et l’ensevelirent dans le sépulcre de son père à Bethléhem; et Joab et les hommes qui étaient avec lui marchèrent pendant toute la nuit, et au point du jour ils parvinrent à Hébron.
Wakamchukua Asaheli, wakamzika katika kaburi la baba yake huko Bethlehemu. Kisha Yoabu na watu wake wakatembea usiku kucha na kufika huko Hebroni wakati wa mapambazuko.

< 2 Samuel 2 >